Hadithi: Mpangaji

MPANGAJI 22
By CK Allan

“Mshtakiwa tafadhali jibu, unaweza kutaja majina ya hao watu waliokuwa kwenye hii video?” hakimu sasa aliingilia kati baada ya kuona ukimya usiokuwa wa kawaida kutoka kwa mama Joan
“aah mmmh ah sio mimi na hao watu siwajui!” alisema tena mama Joan na kupelekea watu pale mahakamani kuangua kicheko
“haya tuambie unamfahamu Yule pale?” Mwendesha mashtaka alisema sasa akimnyoshea mkono Fred
“ahhh ndio, Hapana!” alisema mama Joan kwa kusita sita
“Hapana au ndio ?” aliuliza tena
“aaaah, mmhhh” aliongea mama Joan kisha akaanguka chini, hakimu aliahirisha kesi tena na mama Joan akakimbizwa Hospitali huku akisisitiza Mzee Kidude na Sele wasitoke nje Ya jiji la Dar es salaam wakati wote kesi ikiwa inaendelea

“asante sana Baba, sikujua utafanya hivyo! Alisema Doreen sasa walipokuwa nyumbani kwa Mr K kuangaliwa mwenendo wa kesi yao
“kwasasa kesi ya msingi tunakaribia kuimaliza, mzizi wa yote haya ni hii kesi ya msingi, kama mambo yakienda hivi tunashinda hii kesi asubuhi sana” alisema Rapha huku akimalizia soda yake kwenye glas
“unadhani wanaweza kuja na hoja gani?” aliuliza Sele
“hawana hoja zaidi watang’ang’ania validility tu” alisema Rapha
“ndio nini iyo validility?”aliuliza Doreen
“ni muda wa huu ushahidi , kuwa ulikaa muda mrefu bila kutolewa, lakini hoja hii inakufa kwa kuzingia sheria ya ushahidi namba 213 ya mwaka 2005 kuwa ushahidi utaendelea kutumika na kuhesabika ni hai kuanzia siku shauri lilipofunguliwa hadi mwisho wa kesi” alisema Rapha
“hivi kwasasa Mama Joan atakuwa chini ya ulinzi wa Polisi ama bado hajapatikana na hatia?” aliuliza Sele
“Yule ni mtuhumiwa na kutokana na kilichotokea pale lazima atakuwa chini ya ulinzi ili asiharibu upelelezi, lakini tu hatalazimika kutoa ushahidi mpaka daktari athibitishe kwa maandishi kuwa anaweza kufanya hivyo” alisema Rapha
‘oooohoo basi kama ni hivyo mambo ni tofauti na tunavyofikiria” alisema Sele akisimama huku wenzake wakimshangaa tu
“huyu mama anafanya mchezo hizo siku kadhaa za kuwa hospitali inaweza kuwa ni janja yake kufanya jambo Fulani” alisema Sele akijishika shika ndevu zake
“kwani yupo hospitali gani?” alisema Mr K
“Hatujui ngoja tupeleleze mpaka jioni tutakuwa tumepata jibu” alisema Rapha huku akisimama na kuaga wenzake na kutoka nje ya nyumba ya Mr K,
Ni kweli majira ya jioni Sele alipata kujua kuwa mama Joan alikuwa amelazwa katika hospitali ya Mtakatifu Emmaus iliyokuwa kigamboni, Sele alichukua simu yake kisha akaingia kwenye mtandao na kutafuta taarifa za hospitali hiyo pamoja na kuangalia mazingira yake jinsi yalivyo
“naona kuwa kuna jambo haliko sawa kuhusu mama Joan ni kama anaficha kitu Fulani hivi na hata kule kuumwa sidhani kama ni kwa kawaida” alisema Esta sasa akimstua Sele katika mawazo yake hayo
“ah Yule haumwi ninachofikiria ni kuwa anajaribu kwenda kupanga mikakati yake zaidi ili kwamba aweze kutoka katika kesi inayomkabili” alisema Sele
Hata hivyo baada ya siku kadhaa waliitwa tena mahakamani na kuelezwa kuwa kesi yao inaahirishwa tena kwakuwa mama Joan, bado alikua hayupo katika hali nzuri ya kiafya
Hata hivyo baada ya siku chache tu wakili wa utetezi wa mama Joan na mzee Kidude alijitoa kwenye Kesi! Na hivyo ikabidi mzee Kidude ajitafutie wakili wake,
Siku hiyo mzee Kidude akiwa anatoka hospitali kumjulia hali mama Joan akiwa na derava wake ghafla gari moja ilikatisha mbele yake na kusimama kwa ghafla, kitu ambacho kilisababisha kidude kushtuka ghafla na derava wake kufunga breki za papo kwa papo, wakati wakiwa wanashangaa walishuka watu wanne haraka haraka wakiwa na bunduki na kumtoa mzee kidude na kumuingiza kwenye gari yao halafu mmoja wao akaenda kuendesha ile gari na kutokomea, kilikuwa ni kitendo cha dakika mbili tu na sekunde kadhaa,
“semeni jamani mnataka kiasi gani cha pesa semeni jamani!” alisema mzee Kidude
“kaa kimya mzee” walisema wale vijana na sasa safari ikaendelea na kisha wakamfunika kitambaa na kuingia nae kwenye “nyumba yao” ya siku zote, baada ya dakika kadhaa sasa walimfungua kitambaa mzee Kidude

Sasa mzee Kidude aliomba bora awe anaota kuliko kutazamana uso kwa uso na Yule mtu aliyekuwa mbele yake
“pole mzee Kidude naona vijana wamekusumbua kidogo, karibu tuketi rafiki yangu!” alisema mzee Tupa
“kumbe, kumbe, ku-mbe,ni, we-we,’ alisema Mzee Kidude kwa tabu
“usijali,” aliongea mzee Tupa huku akitabasamu kisha akakonyeza walinzi wake ambao waliondoka na kuwaacha wenyewe
“haya mbona hutaki kuniua, niue sasa” alisema mzee Kidude
“mimi sio muuaji , ningetaka kukuaa ningekuwa kule kule bagamoyo, tangu siku ile umelala na mke wangu!” alisema Mzee Tupa na kumuacha mzee Kidude akitapata kutafuta maneno
“usihangaike nisikilize” alianza mzee Tupa
“najua ni wewe unasababisha kesi isisomwe mpaka sasa ukidhani kwamba utaweza kuwanunua mahakimu na hivyo unamuambiaYule shetani mwenzako kuwa azidi kujifanyisha huko hsopitali, sasa nisikilize unatakiwa ufanye mambo mawili tu,
Jambo la kwanza
Upeleke taarifa rasmi kuwa mko tayari kwa kesi kesho kutwa, halafu jambo la pili eleza pesa za Gift ulitoa wapi, na eleza ukweli mahakamani, ni hayo tu, najua unajua nitakachokufanya endapo hutafanya kama ninavyokulekeza” alisema mzee Tupa sasa akimkonyeza Mlinzi wake ambaye alikua mbali kidogo na hapo
“haya warudisheni” aliwaambia
“mpaka kesho asubuhi nitaona uaminifu wako mzee Kidude” alisema mzee Tupa
Sasa mzee Kidude alijikuta akipagawa, kabisa sasa alianza kuamini akili zake zile za mwanzo wakati anatamani kujiingiza katika mchezo huyu, mara kadhaa alikua anajiambia kuwa anacheza na kifo chake mwenyewe “unacheza na mke wa raisi Kidude” ni maneno ambayo yalikua yanamjia mara kwa mara kichwani kwake kabla hajaanza huu ujasiri wake wa kipumbavu
“bossi uko sawa?’ sasa dereva wake alikua akijaribu kumuongelesha bosi wake huyo
“twende nyumbani” alisema tu bila kujibu swali

Walifika na moja kwa moja mzee Kidude alifungua friji na kutoa kilevi na kujimiminia
“kwa mara nyingine tena umalaya umeniponza” alijisemea kidude
Sasa alikua na saa 13 tu kuamua hatima yake,

Mzee tupa alikua amepata simu kutoka kwa Raisi , kama angehitaji msaada wake bila kutambulikana, Mzee Tupa hakutaka msaada uliopilitiliza zaidi tu alitaka kujua mwenendo wa kesi na jinsi mkewe anavyojaribu kujitoa , angekuwa na uwezo hata wa kuomba kesi hiyo ifutwe ama apangiwe hakimu yoyote amtakaye lakini mzee Tupa alisema haki itendeke kwa asilimia mia
Na hivyo siku hiyo ndipo alipopata taarifa kuwa mama Joan alikuwa haumwi bali alikua anavuta muda ili kununua mahakimu na kuweka mambo mengine sawa, na tayari mzee Kidude alipokuwa kule hospitali sasa aliweza kujulishwa kila hatua na kuamua kumchukua jioni ile, mzee Tupa alikuwa na video kadhaa na mauza uza ya mkewe na Bwana Kidude, hakutaka zisambae haraka kwani zilikua zinamchafua yeye pia na sasa akafikiri njia pekee ni kumkaanga mama Joan na mafuta yake mwenyewe, ilikua kazi ndogo tu kumshawishi wakili wake kujitoa na sasa ilikua ni zamu ya Mzee Kidude
Kesho yake hakimu alipokea taarifa kuwa mama Joan anaweza kuendelea na kesi baada ya kupona na hivyo ikapangwa wiki iliyofuata huku wote wakisisitizwa waje na vielelezo vya msingi
Siku hiyo ya hukumu,
Kama kawaida siku hiyo mahakama ilikua imefurika watu kutoka sehemu mbali mbali kwani tayari kesi hiyo ilikua miongoni mwa kesi maarufu sana zilizovutia
Upekee wa siku hiyo mzee Tupa pamoja na watoto wake walikuwepo kushuhudia hukumu ya kesi hiyo
Baada ya kusoma utangulizi na maelezo ya msingi sasa hakimu aliwapa tena nafasi ya pande zote mbili kutoa hoja zao za kuhitimisha na kisha mzee Kidude akapewa nafasi na kutoa ushahidi wake,
Wakati anaingia kizimbani macho yake yalitazamana na mzee Tupa ambaye alimkonyeza na yeye akamkonyeza kisha akaanza kutoa ushahidi wake
“mheshimiwa hakimu, zile pesa nilipewa na mama Joan kuwa niziweke kwenye Gari la Sele kusudi kwamba tumtengenezee kesi ya uhujumu uchumi na ndio nasikitika sana nimedanganya mahakama
Hii story ni fire 🔥 sio ya kukosa kabisa
Missy Gf
Nourhan
Analyse
Half american
Watu8
Dr Restart
baby zu
Depal
Kalpana
Lovelovie
Glenn
Demi
Binadamu Mtakatifu
Darlin
Lloyd Munroe mshamba_hachekwi
moneytalk
Dahan
Johnnie Walker
Leejay49
Amehlo
Palina
am 4 real
Shunie
Numbisa
Bantu Lady
charlote
Kalpana
Luv
masai dada
Tayukwa
Kelsea
Antennah
Cee
Litro
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom