Hadi Juni 2024, zimeripotiwa taarifa za watu zaidi ya 50 waliotekwa na kupotezwa kabisa

DR Mambo Jambo

JF-Expert Member
May 10, 2012
9,892
20,998
"Uchambuzi huu Kwa hisani ya Boniyai"

Mwaka huu 2024 pekee yake binafsi nime’ ripoti taarifa za watu zaidi ya 50 waliotekwa na kupotezwa kabisa.

Hawa ni baadhi tu ya watu waliopotea kwa kutekwa na kisha taarifa zao kutopatikana mahala popote ikiwemo vituo vya Polisi na Hospitali katika vyumba vya kuhifadhia maiti.

1. Herman William
2. David Gasper Lema
3. Ridhiwani Hemed Msangi
4. ⁠Hamza Said
5. ⁠Paul Jerome Kisoka
6. ⁠Gidion Michael Mwihumbo
7. Kelvin Sebastian Mkabai
8. Benson Erasto Arbogast Ishungisa
9. Casian Mazambo
10. Charles Aden Mwampyate na wengine zaidi ya 40

Tofauti na tulivyozoea kuona matukio ya Jinai mengine ambapo mtu akiuwawa au Kutekwa baada ya muda ndugu na jamaa zake wanaweza kuokota mwili au mabaki ya mwili baada ya kuuwawa.

Miaka ya hivi karibuni imekuwa ni tofauti kidogo, ndugu au Jamaa yako akitekwa akapotea na kuuwawa

Basi uwezekano wa kupata taarifa juu ya kifo cha ndugu yenu ni mdogo sana

Na uwezekano hata wa kupatikana kwa mwili au mabaki ya mwili umekuwa ni mgumu sana.

Bila shaka wauaji wameacha ile mbinu ya zamani ya kuua na kupeleka maiti vyumba vya kuhifadhia maiti

Kuua na kuteleleza mwili barabarani, kuua na kutupa mwili ukiwa katika mifuko ya sandarusi au viroba.Kuua na Kutupa mwili katika bahari au mito

Kwa tukio hili la Edger Edson Mwakabela (Sativa) limetufundisha kuwa watekaji na wauwaji wana mbinu mpya ambayo inapoteza ushahidi kwa 100%.

Mbinu hii ni ya kupeleka watu matika mbuga za wanyama au hifadhi za taifa zenye wanyama wakali, ili baada ya kukuua mwili wako utafunwe na wanyama wa porini.

Edger Edson Mwakabela (SATIVA ) anasema watesi wake walio mteka siku ya tarehe 23 June 2024 walimchukua Dar es saalam kisha kumpaki katika karakana za Kituo cha polisi Oysterbay, Mkoa wa kipolisi wa Kinondoni na baadae kuanza kuelekea naye mkoani Arusha.

Kwanini Arusha? Kwa akili za haraka utagundua walielekea mkoa wenye Mbuga nyingi za Jirani za Wanyama wakali wenye uwezo wa kula mwili na mifupa yake kama Serengeti, Ngorongoro,Manyara na Tarangire.

Lakini huenda kwa sababu ya msimu wa watalii na ubize wa wageni katika mbuga hizi,Wauwaji wa Edger Edson Mwakabela waliamua kuchagua eneo lingine mbali kabisa baada yabkuona mbuga za Arusha hazina utulivu nyakati hizi

Wakaanza safari ya masaa 15 yenye umbali wa Kilomita 1091 ya kutoka Arusha kuelekea huko hifadhi ya ya Taifa ya Katavi wilaya ya Mlele

Sababu ni moja tu.Walifuata Fisi wenye madoa madoa (Spotted hyena) ambao wanasifa ya kunusa mzoga kuutafuna wote hadi mifupa ikaisha

Hifadhi ya Taifa ya Katavi ina ukubwa wa kilomita za mraba 4,471 (maili za mraba 1,727) ipo Kusini Magharibi mwa Tanzania,kaskazini mwa ziwa Tanganyika, Kilomita 40 kutoka Mji wa mpanda.

"an estimated 4,000 elephants might converge on the area,together with several herds of 1,000-plus buffalo, while an abundance of giraffe, zebra,impala and reedbuck provide easy pickings for the numerous lion prides and spotted hyena clans."

Spotted hyena ndiyo siri ya wauaji ya Edger Edson Mwakabela kutembea umbali wa Kilomita 1,091 kutafuta hifadhi ya Taifa ya Katavi wanakopatika Fisi wa aina hiyo.

Walikuwa wana uhakika wa kuua na kupoteza ushahidi kwa haraka sana, ndani ya masaa 12 tu pasingebaki mabaki ya mwili.

Na ili wasibahatishe kazi yao wakahakikisha wanatekeleza mauaji pembeni ya Mto Ikuu unaosifika kwa Mamba wakali sana pamoja viboko wengi.

Kwa mujibu wa wenyeji wanaoishi pembezoni mwa msitu wa hifadhi wa Katavi wanashangaa imekuwaje mtu huyo ameweza kupatikana akiwa hai bila kutafunwa na fisi au Mamba

Wenyeji wanasema Jamaa ana bahati sana,aende akatoe sadaka,ule msitu nusu saa tu ni nyingi sana sana kuishi,wanyama wanakutafuna

Sasa nimejiridhisha kwa mbinu hii miili ya watu waliopotea kwa miaka ya hivi karibuni tusiwe na matumaini ya kuja kupatikana.

Au kupata ushahidi wa mabaki yao, kama wauaji wanatumia mbinu ya Kuua ndani ya hifadhi na kutelekeza mwili wako ili utafunwe na wanyama.

20240628_151113.jpg 20240628_151109.jpg 20240628_151117.jpg
 
"Uchambuzi huu Kwa hisani ya Boniyai"

Mwaka huu 2024 pekee yake binafsi nime’ ripoti taarifa za watu zaidi ya 50 waliotekwa na kupotezwa kabisa.

Hawa ni baadhi tu ya watu waliopotea kwa kutekwa na kisha taarifa zao kutopatikana mahala popote ikiwemo vituo vya Polisi na Hospitali katika vyumba vya kuhifadhia maiti.

1. Herman William
2. David Gasper Lema
3. Ridhiwani Hemed Msangi
4. ⁠Hamza Said
5. ⁠Paul Jerome Kisoka
6. ⁠Gidion Michael Mwihumbo
7. Kelvin Sebastian Mkabai
8. Benson Erasto Arbogast Ishungisa
9. Casian Mazambo
10. Charles Aden Mwampyate na wengine zaidi ya 40

Tofauti na tulivyozoea kuona matukio ya Jinai mengine ambapo mtu akiuwawa au Kutekwa baada ya muda ndugu na jamaa zake wanaweza kuokota mwili au mabaki ya mwili baada ya kuuwawa.

Miaka ya hivi karibuni imekuwa ni tofauti kidogo, ndugu au Jamaa yako akitekwa akapotea na kuuwawa

Basi uwezekano wa kupata taarifa juu ya kifo cha ndugu yenu ni mdogo sana

Na uwezekano hata wa kupatikana kwa mwili au mabaki ya mwili umekuwa ni mgumu sana.

Bila shaka wauaji wameacha ile mbinu ya zamani ya kuua na kupeleka maiti vyumba vya kuhifadhia maiti

Kuua na kuteleleza mwili barabarani, kuua na kutupa mwili ukiwa katika mifuko ya sandarusi au viroba.Kuua na Kutupa mwili katika bahari au mito

Kwa tukio hili la Edger Edson Mwakabela (Sativa) limetufundisha kuwa watekaji na wauwaji wana mbinu mpya ambayo inapoteza ushahidi kwa 100%.

Mbinu hii ni ya kupeleka watu matika mbuga za wanyama au hifadhi za taifa zenye wanyama wakali, ili baada ya kukuua mwili wako utafunwe na wanyama wa porini.

Edger Edson Mwakabela (SATIVA ) anasema watesi wake walio mteka siku ya tarehe 23 June 2024 walimchukua Dar es saalam kisha kumpaki katika karakana za Kituo cha polisi Oysterbay, Mkoa wa kipolisi wa Kinondoni na baadae kuanza kuelekea naye mkoani Arusha.

Kwanini Arusha? Kwa akili za haraka utagundua walielekea mkoa wenye Mbuga nyingi za Jirani za Wanyama wakali wenye uwezo wa kula mwili na mifupa yake kama Serengeti, Ngorongoro,Manyara na Tarangire.

Lakini huenda kwa sababu ya msimu wa watalii na ubize wa wageni katika mbuga hizi,Wauwaji wa Edger Edson Mwakabela waliamua kuchagua eneo lingine mbali kabisa baada yabkuona mbuga za Arusha hazina utulivu nyakati hizi

Wakaanza safari ya masaa 15 yenye umbali wa Kilomita 1091 ya kutoka Arusha kuelekea huko hifadhi ya ya Taifa ya Katavi wilaya ya Mlele

Sababu ni moja tu.Walifuata Fisi wenye madoa madoa (Spotted hyena) ambao wanasifa ya kunusa mzoga kuutafuna wote hadi mifupa ikaisha

Hifadhi ya Taifa ya Katavi ina ukubwa wa kilomita za mraba 4,471 (maili za mraba 1,727) ipo Kusini Magharibi mwa Tanzania,kaskazini mwa ziwa Tanganyika, Kilomita 40 kutoka Mji wa mpanda.

"an estimated 4,000 elephants might converge on the area,together with several herds of 1,000-plus buffalo, while an abundance of giraffe, zebra,impala and reedbuck provide easy pickings for the numerous lion prides and spotted hyena clans."

Spotted hyena ndiyo siri ya wauaji ya Edger Edson Mwakabela kutembea umbali wa Kilomita 1,091 kutafuta hifadhi ya Taifa ya Katavi wanakopatika Fisi wa aina hiyo.

Walikuwa wana uhakika wa kuua na kupoteza ushahidi kwa haraka sana, ndani ya masaa 12 tu pasingebaki mabaki ya mwili.

Na ili wasibahatishe kazi yao wakahakikisha wanatekeleza mauaji pembeni ya Mto Ikuu unaosifika kwa Mamba wakali sana pamoja viboko wengi.

Kwa mujibu wa wenyeji wanaoishi pembezoni mwa msitu wa hifadhi wa Katavi wanashangaa imekuwaje mtu huyo ameweza kupatikana akiwa hai bila kutafunwa na fisi au Mamba

Wenyeji wanasema Jamaa ana bahati sana,aende akatoe sadaka,ule msitu nusu saa tu ni nyingi sana sana kuishi,wanyama wanakutafuna

Sasa nimejiridhisha kwa mbinu hii miili ya watu waliopotea kwa miaka ya hivi karibuni tusiwe na matumaini ya kuja kupatikana.

Au kupata ushahidi wa mabaki yao, kama wauaji wanatumia mbinu ya Kuua ndani ya hifadhi na kutelekeza mwili wako ili utafunwe na wanyama.

View attachment 3028293View attachment 3028294View attachment 3028295
Muwe mnawaambia hao wasishindane na wenye Nguvu kama hawawezi kujitetea.

Hapo ashukuru karma imemstahi na kupotea mazima.

Mwisho hivi Huwa anajuaje kwmaba nimepelekwa.pale,mda Fulani ikawa hivi na vile afu nikapigwa na hiki,nini kinamjulisha yote hayo kwenye mazingira ya kutekwa?

Pole yake.
 
Muwe mnawaambia hao wasishindane na wenye Nguvu kama hawawezi kujitetea.

Hapo ashukuru karma imemstahi na kupotea mazima.

Mwisho hivi Huwa anajuaje kwmaba nimepelekwa.pale,mda Fulani ikawa hivi na vile afu nikapigwa na hiki,nini kinamjulisha yote hayo kwenye mazingira ya kutekwa?

Pole yake.
Nilikwambia ndugu, akili huna, ukanibishia.
 
Level hiyo ya uoga wenzio walishaivuka.

Unatakiwa kusimama tu katika Kweli na HAKI,

Ulinzi wa Mungu ni dhahiri na unatosha.

Siku za Serikali dhalimu ya CCM zinahesabika.
How many you are mliovuka hiyo level? Mkiwa wachache hamuwezi kushinda na mtaishia kuumia.

Sawa yangu macho na maskio siwezi wabishia maana Kila mtu amezakiwa Kwa aina yake na Kwa lengo tofauti but Mimi siwezi fanya lengo ambalo sijazaliwa kwalo
 
Kati ya polisi 1000000 wanaostaafu ni 1 tu mwenye mafanikio kuendelea mbele hizi ni laana za watanzania Kwa hiyo wakati polisi CCM mnafanya haya mjue kabisa maisha yenu ni ya laana siku zote
Sidhani kama wanaotekeleza upuuzi na unyama huu ni polisi hawahawa tunaowajua na kuishi nao mitaani...

Vitendo hivi vinatekelezwa na vikosi maalumu (mjumuiko wa baadhi ya polisi wachache, UWT wachache, JWTZ wachache ambao hata wao kwa wao hawajuani bali hukutana kwenye kazi zao hizi chafu)...

Vikosi hivi siku zote vina kinga ya viongozi wakubwa (Rais, DGNS, IGP na wenye mamlaka wengine pamoja na matajiri wenye fedha chafu za wizi na ufisadi...

Na kama hamjui, viongozi wa serikali huiba au kufisadi fedha za umma kwa kuzipitishia kwa baadhi ya matajiri hawa waovu ili tu isiwe rahisi kuutambua wizi na ufisadi wa viongozi hawa...

Mfano rahisi na current kabisa, ni ufisadi wa Kwenye skendo ya sukari unaomhusisha Waziri Bashe (Kilimo), Waziri Mwigulu Nchemba (Fedha), Rais Samia Suluhu Hassan na mwanae Abdul, na Bodi ya Sukari kupitia kampuni fake zilizopewa tenda ya mabilioni kuingiza sukari kwa msamaha wa 53% ya kodi...

Hesabu zinaonesha kuwa zaidi ya TZS 700B zilizopaswa kuwa kodi ya serikali zimeingia kwenye mifuko ya watu. Mnadhani ni kina nani? Halafu chunguza sukari inauzwa shilingi ngapi hapa nchini. Ni ghali kuliko hata kabla ya kuingia kwa sukari hii iliyosamehewa kodi...!!

Kwa hiyo, lengo la vikosi hivi ni kulinda maslahi ya kisiasa ya hawa viongozi, kulinda utawala mwovu na biashara chafu za viongozi na watu wao hawa wenye kampuni tata...

Kuwaweka polisi wote kwenye kundi hili la utekaji, utesaji na mauaji ni kuwaonea.

Polisi hawa wa kawaida, walioko kazini kwa routine za kawaida nakuhakikishia kuwa hawajui lolote zaidi ya wao kufanya majukumu ya kila siku kwa kuzingatia kiapo cha askari...!
 
How many you are mliovuka hiyo level? Mkiwa wachache hamuwezi kushinda na mtaishia kuumia.

Sawa yangu macho na maskio siwezi wabishia maana Kila mtu amezakiwa Kwa aina yake na Kwa lengo tofauti but Mimi siwezi fanya lengo ambalo sijazaliwa kwalo
Siku yaja, utatoka Kupambana HAKI pale watakapoguswa uwapendao, mtoto, au wazazi utajua.
 
Back
Top Bottom