Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 94,295
- 122,539
Gamboshi ni moja ya vijiji vilivyopo wilaya ya Bariadi, mkoani Simiyu. Kwa Wanyantuzu huko.
Kijiji hiki kinasifika kwa kuwa na wachawi wakali sana hadi baadhi ya watu kukiita kuwa ndo makao makuu ya wachawi na uchawi kwa kanda ya ziwa.
Kama video hii ya kwanza inavyoeleze, Gamboshi kipo kama kilometa 44 hivi kutoka Bariadi mjini.
Mimi natokea Ikungulyabashashi [hapo kwenye video dakika 1:56 sikia jinsi Ikungulyabashashi inavotamkwa], ambapo si mbali kivile na Gamboshi.
Gamboshi nimeshafika mara nyingi tu. Nina ndugu wengi tu huko. Habari na sifa za Gamboshi hekaya tu.
Hazina ukweli wowote. Kuna watu ukiwakuta wanaiongelea Gamboshi unaweza kudhani Gamboshi ni NYC.
Wapo ambao huwa wanadai huko Gamboshi kuna magorofa makali sana, kuna mabarabara mazuri kama ya Marekani, na mengineyo mengi mazuri lakini eti kwa wengine ambao sio wachawi hawawezi kuyaona.
Huo ni uongo. Gamboshi ni kijiji cha kawaida mno na hakina tofauti na vijiji vingine vya Tanzania.
Tatizo kubwa la Gamboshi ni ujinga tu. Na ndo maana hata maendeleo [kwa viwango vya Tanzania] ni madogo mno.
Kwa mfano, zahanati ipo lakini idadi ya watu wanaoenda kutibiwa hapo ni chache mno. Watu wakiumwa wanaenda kwa 'Nfumu' [Wasukuma wenzangu mtakua mnajua nfumu ni nini].
Shule ya msingi ipo, ya sekondari ipo, lakini ndo hivyo tena. Imani potofu zishawapotosha watu kiasi cha kutokuona umuhimu wa elimu ya darasani.
Halafu inadaiwa eti karibu kila mwana-Gamboshi ni mganga wa kienyeji
. Binafsi sidhani kama watu wapatao 4,000 waishio huko wanaweza karibu wote kuwa waganga/ wachawi.
Jionee mwenyewe mazingira ya Gamboshi na wasikie wasikie kwa masikio yako wana-Gamboshi.
Kijiji hiki kinasifika kwa kuwa na wachawi wakali sana hadi baadhi ya watu kukiita kuwa ndo makao makuu ya wachawi na uchawi kwa kanda ya ziwa.
Kama video hii ya kwanza inavyoeleze, Gamboshi kipo kama kilometa 44 hivi kutoka Bariadi mjini.
Mimi natokea Ikungulyabashashi [hapo kwenye video dakika 1:56 sikia jinsi Ikungulyabashashi inavotamkwa], ambapo si mbali kivile na Gamboshi.
Gamboshi nimeshafika mara nyingi tu. Nina ndugu wengi tu huko. Habari na sifa za Gamboshi hekaya tu.
Hazina ukweli wowote. Kuna watu ukiwakuta wanaiongelea Gamboshi unaweza kudhani Gamboshi ni NYC.
Wapo ambao huwa wanadai huko Gamboshi kuna magorofa makali sana, kuna mabarabara mazuri kama ya Marekani, na mengineyo mengi mazuri lakini eti kwa wengine ambao sio wachawi hawawezi kuyaona.
Huo ni uongo. Gamboshi ni kijiji cha kawaida mno na hakina tofauti na vijiji vingine vya Tanzania.
Tatizo kubwa la Gamboshi ni ujinga tu. Na ndo maana hata maendeleo [kwa viwango vya Tanzania] ni madogo mno.
Kwa mfano, zahanati ipo lakini idadi ya watu wanaoenda kutibiwa hapo ni chache mno. Watu wakiumwa wanaenda kwa 'Nfumu' [Wasukuma wenzangu mtakua mnajua nfumu ni nini].
Shule ya msingi ipo, ya sekondari ipo, lakini ndo hivyo tena. Imani potofu zishawapotosha watu kiasi cha kutokuona umuhimu wa elimu ya darasani.
Halafu inadaiwa eti karibu kila mwana-Gamboshi ni mganga wa kienyeji
Jionee mwenyewe mazingira ya Gamboshi na wasikie wasikie kwa masikio yako wana-Gamboshi.