Pre GE2025 Gambo aibua tuhuma za ufisadi wa mabilioni Arusha, Spika Tulia amwagiza Mchengerwa kuandaa ripoti iwasilishwe Bungeni

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Waufukweni

JF-Expert Member
May 16, 2024
2,498
7,065
Mbunge wa Arusha Mjini (CCM), Mrisho Gambo, amedai kuwepo kwa harufu ya upigaji fedha katika Ujenzi wa Jengo la Utawala Arusha. Akiwasilisha hoja yake leo, Jumatano Aprili 16, 2025, wakati akichangia hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kwa mwaka wa fedha 2025/26, Gambo amesema vipimo vya mradi huo vinatofautiana na vile vilivyopo kwenye orodha ya manunuzi ya vifaa (BOQ), jambo linaloashiria uwepo wa ubadhirifu wa fedha.

Gambo ameeleza kuwa jengo hilo lina gharama ya jumla ya Shilingi bilioni 9, kiasi alichokitaja kuwa kikubwa kuliko kawaida, akimtaka Waziri wa TAMISEMI, Mohamed Mchengerwa, kutuma timu maalum kufanya uchunguzi juu ya matumizi ya fedha hizo. Aidha, amesema kuwa kuna mkataba mwingine wa Shilingi bilioni 6.2 ambao pia una mapungufu, kwani baadhi ya vipengele vilivyoorodheshwa kwenye BOQ havijatekelezwa kama ilivyopangwa.

Mbunge huyo amesema kutokana na tofauti kati ya maandishi ya mkataba na utekelezaji halisi wa kazi, gharama za ujenzi zimeongezeka kwa zaidi ya Shilingi bilioni 8 bila maelezo ya kina. Amesisitiza kuwa ni muhimu kwa Serikali kuchukua hatua haraka ili kujiridhisha na kuhakikisha kuwa fedha za umma zinalindwa dhidi ya matumizi mabaya.


Kuhusu TARURA, Mrisho amezungumzia TSh. 3.4 bilioni ambazo amezitilia shaka na kutaka TSh. 1.6 bilioni zingeweza kutumika kumaliza kero zingine kwa Wananchi wa Arusha. Spika Tulia amtaka Waziri Mchengerwa kuandaa taarifa fupi ya tuhuma hizo ili kuiwasilisha mwishoni mwa bajeti yake ya Ujenzi wa jengo la Utawala.

Tuhuma hizo zimemuibua Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Tulia Ackson aliyemtaka Waziri wa Tamisemi, Mohammed Mchengerwa kufuatilia tuhuma hizo alizoziita ‘nzito’ na kuagiza kuja na ripoti fupi.

Mchengerwa akijibu baada ya mchango wa Gambo na maagizo ya spika amesema: "Nimelipokea jambo hilo na tutawasilisha taarifa hiyo wakati wa kuhitimisha. Hili la kusema fedha hii ingefanya hivi na siyo vile, ni vyema tukakumbushana kuwa mipango ya maendeleo, haipangwi na Tamisemi ila ni vikao maalumu katika mabaraza ya madiwani ambayo sisi sote ni wajumbe."
 
Mrisho Gambo aibu tuhuma nzito za wizi wa mabilioni ya fedha ujenzi wa jengo la Utawala la Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru iliyopo Wilayani Arumeru Mkoani Arusha, ambapo amsema gharama zake za jumla ni TSh. 9 bilioni na anadai kuwa gharama hivi ni kubwa kuliko kawaida na amemtaka Waziri Mchengerwa atume timu yake ikachunguze.

Ameongeza kuwa wameingia mkataba mwingine wa TSh. 6.2 bilioni lakini katika mkataba kilichoandikwa kwenye BOQ na kwenye utekelezaji ni tofauti ambayo zimeongeza gharama ambapo amesema kuna kunaziada zaidi ya TSh. 8 bilioni.

Kuhusu TARURA, Mrisho amezungumzia TSh. 3.4 bilioni ambazo amezitilia shaka na kutaka TSh. 1.6 bilioni zingeweza kutumika kumaliza kero zingine kwa Wananchi wa Arusha. Spika Tulia amtaka Waziri Mchengerwa kuandaa taarifa fupi ya tuhuma hizo ili kuiwasilisha mwishoni mwa bajeti yake ya Ujenzi wa jengo la Utawala.

Je? B264 za uchaguzi wa serikali za mitaa ambao ulikuwa kichekesho??
 
Mrisho Gambo aibu tuhuma nzito za wizi wa mabilioni ya fedha ujenzi wa jengo la Utawala la Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru iliyopo Wilayani Arumeru Mkoani Arusha, ambapo amsema gharama zake za jumla ni TSh. 9 bilioni na anadai kuwa gharama hivi ni kubwa kuliko kawaida na amemtaka Waziri Mchengerwa atume timu yake ikachunguze.

Ameongeza kuwa wameingia mkataba mwingine wa TSh. 6.2 bilioni lakini katika mkataba kilichoandikwa kwenye BOQ na kwenye utekelezaji ni tofauti ambayo zimeongeza gharama ambapo amesema kuna kunaziada zaidi ya TSh. 8 bilioni.

Kuhusu TARURA, Mrisho amezungumzia TSh. 3.4 bilioni ambazo amezitilia shaka na kutaka TSh. 1.6 bilioni zingeweza kutumika kumaliza kero zingine kwa Wananchi wa Arusha. Spika Tulia amtaka Waziri Mchengerwa kuandaa taarifa fupi ya tuhuma hizo ili kuiwasilisha mwishoni mwa bajeti yake ya Ujenzi wa jengo la Utawala.

Gambo huko TENGERU ni Jimbo la Arumeru, kunamuhusu nini?
 
Mrisho Gambo aibu tuhuma nzito za wizi wa mabilioni ya fedha ujenzi wa jengo la Utawala la Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru iliyopo Wilayani Arumeru Mkoani Arusha, ambapo amsema gharama zake za jumla ni TSh. 9 bilioni na anadai kuwa gharama hivi ni kubwa kuliko kawaida na amemtaka Waziri Mchengerwa atume timu yake ikachunguze.

Ameongeza kuwa wameingia mkataba mwingine wa TSh. 6.2 bilioni lakini katika mkataba kilichoandikwa kwenye BOQ na kwenye utekelezaji ni tofauti ambayo zimeongeza gharama ambapo amesema kuna kunaziada zaidi ya TSh. 8 bilioni.

Kuhusu TARURA, Mrisho amezungumzia TSh. 3.4 bilioni ambazo amezitilia shaka na kutaka TSh. 1.6 bilioni zingeweza kutumika kumaliza kero zingine kwa Wananchi wa Arusha. Spika Tulia amtaka Waziri Mchengerwa kuandaa taarifa fupi ya tuhuma hizo ili kuiwasilisha mwishoni mwa bajeti yake ya Ujenzi wa jengo la Utawala.

Chama cha Majizi
 
Gambo nyakati zimefika mwisho, amepiga fitna sana watu ili aonekane relevant kisiasa. Sasa kikombe kile kile anakinywea.

Nafsi za watu wengi zinalia, kilio kimefika machoni pa Mungu
 
Mbunge wa Arusha Mjini (CCM), Mrisho Gambo, amedai kuwepo kwa harufu ya upigaji fedha katika ujenzi wa jengo la utawala la Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru, lililopo Wilayani Arumeru, Mkoa wa Arusha. Akiwasilisha hoja yake leo, Jumatano Aprili 16, 2025, wakati akichangia hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) kwa mwaka wa fedha 2025/26, Gambo amesema vipimo vya mradi huo vinatofautiana na vile vilivyopo kwenye orodha ya manunuzi ya vifaa (BOQ), jambo linaloashiria uwepo wa ubadhirifu wa fedha.

Gambo ameeleza kuwa jengo hilo lina gharama ya jumla ya Shilingi bilioni 9, kiasi alichokitaja kuwa kikubwa kuliko kawaida, akimtaka Waziri wa TAMISEMI, Mohamed Mchengerwa, kutuma timu maalum kufanya uchunguzi juu ya matumizi ya fedha hizo. Aidha, amesema kuwa kuna mkataba mwingine wa Shilingi bilioni 6.2 ambao pia una mapungufu, kwani baadhi ya vipengele vilivyoorodheshwa kwenye BOQ havijatekelezwa kama ilivyopangwa.

Mbunge huyo amesema kutokana na tofauti kati ya maandishi ya mkataba na utekelezaji halisi wa kazi, gharama za ujenzi zimeongezeka kwa zaidi ya Shilingi bilioni 8 bila maelezo ya kina. Amesisitiza kuwa ni muhimu kwa Serikali kuchukua hatua haraka ili kujiridhisha na kuhakikisha kuwa fedha za umma zinalindwa dhidi ya matumizi mabaya.

Kuhusu TARURA, Mrisho amezungumzia TSh. 3.4 bilioni ambazo amezitilia shaka na kutaka TSh. 1.6 bilioni zingeweza kutumika kumaliza kero zingine kwa Wananchi wa Arusha. Spika Tulia amtaka Waziri Mchengerwa kuandaa taarifa fupi ya tuhuma hizo ili kuiwasilisha mwishoni mwa bajeti yake ya Ujenzi wa jengo la Utawala.

Tuhuma hizo zimemuibua Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Tulia Ackson aliyemtaka Waziri wa Tamisemi, Mohammed Mchengerwa kufuatilia tuhuma hizo alizoziita ‘nzito’ na kuagiza kuja na ripoti fupi.

Mchengerwa akijibu baada ya mchango wa Gambo na maagizo ya spika amesema: "Nimelipokea jambo hilo na tutawasilisha taarifa hiyo wakati wa kuhitimisha. Hili la kusema fedha hii ingefanya hivi na siyo vile, ni vyema tukakumbushana kuwa mipango ya maendeleo, haipangwi na Tamisemi ila ni vikao maalumu katika mabaraza ya madiwani ambayo sisi sote ni wajumbe."
Pia alishamsingizia Mkurugenzi wa Jiji la Arusha kwa ufisadi lakini akaachiwa na Mahakama. Wakati mwingine huyu Gambo huwa anaenda na mihemko na wivu pia.
 
Back
Top Bottom