Kuelekea 2025 Freeman Mbowe amtaka Mchungaji Peter Msigwa kumuomba radhi kwenye Magazeti na kulipa fidia ya Tsh. Bilioni 5 kwa kumkashifu na kumchafua jina

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Kwa kweli, this is the right way ku - deal na mtu huyu......

Na kwa ujumla mtu mwenye akili timamu anashindwa kumwekewa mchungaji huyu kuwa amepagawa na pepo la namna gani.....

Bila shaka hata huko CCM wanapata shida sana kumwelewa huyu mchungaji wa Kanisa anapokuwa anafyatua mdomo wake. Ma - CCM yameshajua ni tapeli fulani kama yule Mkongo - Kiboko cha wachawi.....

Haiwezekani kwa mtu mwenye maadili ya uchungaji wa Kanisa awe mzushi na muongo wa wazi kiasi hiki huku akiwa na uso mkavu kabisa anapokuwa anaoayuka udanganyifu wake...
 
Mbona hizi fidia ni kama zinatajwa tu kwenye mahakama lkn hazilipwi?

1. Bilioni 5 the late Membe toka kwa Musiba ....kimya.
2. Bilioni 5 za Masoud Kipanya toka kwa Mwijaku.....kimya.
3. Na sasa ni bilioni 5 za Mbowe toka kwa Msigwa.....
Kwani ulitaka wakilipwa wakujulishe?
 
Yeye ni kiongozi wa umma kama hataki kuitwa mwizi wakati kweli chama kinapokea ruzuku lakini hata ofisi hakina achane na siasa akakoroge mbege machame
Mbona yeye anamuita Samia mwizi?
Kama anamwita Samia mwizi na si mwizi kweli, basi Samia anayo haki na kila sababu ya kwenda mahakamani ili kudai jina lake lisafishwe, lakini kama hajaenda mahakamani, haimaanishi mwingine akiitwa mwizi wakati si kweli, asiende mahakamani.
 
Aliyosema Mchungaji ni mambo ambayo yanaonekana ni yeye tu bw.Mbowe aweze kujificha.chama anadai ni cha kidemokrasia lakini ni mara ya 5 anang'ang'ana kwenye kichwa lazima ana jambo lake.na kwa taarifa yenu sasa mbowe ndiye mwenye kukiongezea ccm pumzi tangu zamani na kwa sababu hii ccm itadumu sana hata mbowe atakapoirudia nchi.
Ulikisoma ulichokiandika na kukielewa kweli kabla ya kutuletea JF!!??
 
Mahakama inaenda kusikiliza madai ya Mwenyekiti kwamba amechafuliwa.

Hoja za msigwa zinapaswa kujibiwa na chama kupitia katibu mkuu kama ambavyo Lissu alipendekeza.
Ushahidi wa kuwa madai ya Msigwa ni uongo si utatolewa na upande wa Mbowe (KM Mnyika ataitwa kama shahidi), au ushahidi wa madai ya Msigwa kuwa ni kweli utatolewa na Msigwa (hapa napo KM Mnyika anaweza kuitwa kama shahidi kuthibitisha madai ya Msigwa kama ni kweli ama la, ndipo vielelezo vya ukweli au uongo kuwekwa hadharani na mwisho wa siku hoja zake Msigwa zinakuwa zimejibiwa mbele ya chombo ambacho uongo ni kosa kisheria).
 
Ushahidi wa kuwa madai ya Msigwa ni uongo si utatolewa na upande wa Mbowe (KM Mnyika ataitwa kama shahidi), au ushahidi wa madai ya Msigwa kuwa ni kweli utatolewa na Msigwa (hapa napo KM Mnyika anaweza kuitwa kama shahidi kuthibitisha madai ya Msigwa kama ni kweli ama la, ndipo vielelezo vya ukweli au uongo kuwekwa hadharani na mwisho wa siku hoja zake Msigwa zinakuwa zimejibiwa mbele ya chombo ambacho uongo ni kosa kisheria).
Lissu aliomba hoja za msigwa zijibiwe kabla hata ya sakata hili la kupelekana mahakamani, lakini Mnyika na ofisi yake hawakufanya hivyo.

Ngoja tuone labda huko mahakamani panaweza kuwa sehemu sahihi ya kumaliza utata huu.
 
Lissu aliomba hoja za msigwa zijibiwe kabla hata ya sakata hili la kupelekana mahakamani, lakini Mnyika na ofisi yake hawakufanya hivyo.

Ngoja tuone labda huko mahakamani panaweza kuwa sehemu sahihi ya kumaliza utata huu.
Kesi tamu sana hii, UTABIRI, ITAPELEKEA ANGUKO LA MWENYEKITI, STAY TUNES!
 
Yale yale kama ya kinana na Msigwa hadi akaomba poo... ndilo linaloenda kutokea... Msigwa fanya uungwana mapema kabla mambo hayajawa mambo... kuomba msamaha nayo ni heri, sijui kama unazo hizo billion tano, labda kama mpango ni kukufilisi hadi nyumba....
Huyu dingi ana matatizo
Anaropoka sana
Anatakiwa anyooshwe haswa
Hilo jopo la mawakili naomba mumnyooshe hii kenge
 
1 Kwamba anaiba pesa za chama kwa kutumia Mbowe Foundation
2. Amegeuza chama kuwa SACCOS yake
3. Chadema digital inamilikiwa na Mbowe kwa manufaa yake

My take: hilo nililitegemea and that is the right way to go!

=====


Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe amempa siku tano aliyekuwa mwenyekiti wa CHADEMA Kanda ya Nyassa, Mchungaji Peter Msigwa, kuomba radhi, asipfanya hivyo ajiandae kulipa kulipa fidia ya shilingi bilioni 5 Mahakamani kutokana na madai ya kumkashifu na kuharibu chapa yake kutokana na matamshi ya Msigwa yaliyotolewa hadharani baada ya kuhamia Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Katika barua (notisi ya madai) iliyotolewa Septemba 2, 2024 ikiwa na sahihi ya tarehe 4 Septemba, 2024, mawakili wa Mbowe ambao ni Hekima Mwasipu na wenzake kutoka Matwiga Law Chambers, Msigwa anadaiwa kutoa matamshi ya uongo na kumchafua Mbowe mbele ya umma.

“Msigwa alitumia majukwaa ya mikutano, vyombo vya habari, na hata mitandao ya kijamii kutoa madai ya kumkashifu mteja wetu,” ameleza Wakili Mwasipu.

Imeelezwa kuwa Msigwa alidai kuwa Mbowe ameanzisha "Mbowe Foundation," na anatumia chama cha CHADEMA kwa manufaa yake binafsi. Katika moja ya mikutano yake, Msigwa alinukuliwa akisema, "Mwenyekiti wa CHADEMA amegeuza chama kuwa SACCOS, fedha za chama zinaishia kwenye taasisi binafsi na si kwenye akaunti za chama.”

Mawakili wa Mbowe wameeleza kuwa matamshi hayo yameathiri sifa ya Mbowe ndani na nje ya Tanzania, hasa kutokana na nafasi zake mbalimbali kimataifa, ikiwa ni pamoja na kuwa Naibu Mwenyekiti wa Umoja wa Vyama vya Kidemokrasia vya Afrika (DUA).

“Mteja wetu anaona maneno yote yanayozungumzwa na kunukuliwa hapo juu katika maana yake ya asili, muktadha na misemo kuwa ni kashfa, dharau na kudhuru sio tu sifa yake binafsi bali pia kwa familia yake yote, marafiki, taaluma (Siasa), Jumuiya ya Biashara, Jumuiya ya Kidini, marafiki na rika. Maneno haya si chochote lakini ushahidi dhahiri wa nia mbaya dhidi ya mteja wetu”, imeelezwa na mawakili.

Mbali na hilo, Msigwa alidai kuwa CHADEMA Digital ambayo ni huduma ya usajili wa wanachama, inamilikiwa na kampuni binafsi na kwamba Mbowe anatumia fedha za chama kwa manufaa binafsi.

“Hali hii imeleta hasara kubwa kwa mteja wetu kwani sifa yake ya kiongozi wa kisiasa, mfanyabiashara na mwanafamilia imeathirika sana,” alisema Mwasipu.

Kwa mujibu wa notisi hiyo, Msigwa anatakiwa kuomba radhi kupitia machapisho katika magazeti mawili; moja lenye kuweza kufikia nchi nzima na lingine ambalo linaweza kuwafikia watu walau wa kanda, na kulipa fidia ya Shilingi bilioni 5, la sivyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa.

Pia soma
View attachment 3088571View attachment 3088572View attachment 3088573View attachment 3088574View attachment 3088575View attachment 3088576View attachment 3088577
Imeandikwa kitaalamu kabisa.
 
Lissu aliomba hoja za msigwa zijibiwe kabla hata ya sakata hili la kupelekana mahakamani, lakini Mnyika na ofisi yake hawakufanya hivyo.

Ngoja tuone labda huko mahakamani panaweza kuwa sehemu sahihi ya kumaliza utata huu.
Mnyika na ofisi yake wanawajibika kujibu hoja zinazoelekezwa CHADEMA tu na si kwa mtu binafsi - tena kwa utaratibu rasmi wa kiutendaji, si kwenye majukwaa ya kisiasa. Itakuwa kituko Mnyika akikurupuka kuja hadharani na mafaili ya chama kujibu porojo zinazoenezwa na Msigwa mitaani kumhusu Mbowe. Katibu Mkuu makini wa chama kikuu cha upinzani hawezi kuwa zoba kiasi hicho.

Msigwa kamsema Mbowe, hivyo Mbowe ndiye mjibu hoja. Na ndio keshajibu hivyo kwa kudai msamaha au Bilioni 5, period. Anasubiri majibu ya Msigwa.
 
Mbowe kama kuambiwa ukweli kidogo tu anakimbilia mahakamani badala ajibu hoja na kujisafisha je siku akiwa Rais ataweza kuvumilia maneno? Au ndo atapeleka kila mwananchi mahakamani na ikiwezekana kuwa mtekaji pia
Sasa si ukweli utajulikana mahakamani mara hii mnasema Mbowe akiwa rais
 
Back
Top Bottom