Chatanda apokea vyerehani 125 kutoka Ubalozi wa China, kuimarisha uchumi wa wanawake nchini

Ojuolegbha

JF-Expert Member
Sep 6, 2020
795
501
Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania UWT Mary Chatanda (MCC) ampokea Vyerehani 125 vilivyotolewa na Ubalozi wa China nchini Tanzania kwa lengo la kuimarisha uchumi wa wanawake nchini.

Akizungumza katika Hafla ya upokeaji wa Vyerehani hivyo Mwenyekiti Chatanda amesema vifaa hivyo vitaenda kuinua uchumi wa wanawake na kuwafanya wajitegemee kwa shughuli zao ikiwemo za kisiasa.

“Sote tunatambua kuwa, katika mapambano ya kuitafuta 50/50 moja ya nyenzo muhimu ya kumsaidia mwanamke kufika huko ni uchumi imara katika hili la kupewa vyerehani hivi ni chachu ya kumuongezea mwanamke kuwa na uchumi mzuri “Amesema Mwenyekiti Chatanda na kuongeza

“Uchumi wa mwanamke ukiimarika anaweza kufanya vizuri katika siasa na hata hata ya kijamii kwani inamuongezea kujiamini lakini pia anakuwa na uwezo wa kujisimamia pasipo kutegemea mahali popote na kuondokana na utumwa wa kipato”

Mwenyekiti Chatanda amesema ubalozi wa China kupitia all China women federation mmelitambua hilo na mmeamua kumuwezesha mwanamke kiuchumi kwa kugawa vyerehani na mashine za kutotolea vifaranga”

“Kipekee nachukua fursa hii Kuushukuru ubalozi wa China kwa kuikumbuka Jumuiya ya UWT kuwa kati ya wanufaika wa zawadi hizi, wanawake tuna jukumu la kuiendeleza miradi hii kwa ustadi mkubwa ili kuwa na uchumi imara na hatimaye tuweze kujisimamia na kujitegemea kijamii, kisiasa na kiuchumi.”

Aidha Chatanda amemshukuru Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. Dorothy Gwajima ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Baraza Kuu la UWT Taifa kwa kusimamia upatikanaji wa vyerehani na mashine za kutotolea vifaranga Kwa ajili ya Wanawake wajasiriamali wa Tanzania.

📍Dar es Salaam
🗓️29/4/2024


IMG-20240429-WA0046.jpg
IMG-20240429-WA0054.jpg
IMG-20240429-WA0051.jpg
IMG-20240429-WA0048.jpg
IMG-20240429-WA0052.jpg
IMG-20240429-WA0044.jpg
IMG-20240429-WA0049.jpg
IMG-20240429-WA0050.jpg
IMG-20240429-WA0047.jpg
IMG-20240429-WA0045.jpg
IMG-20240429-WA0053.jpg
 
CHATANDA APOKEA VYEREHANI 125 KUTOKA UBALOZI WA CHINA, KUIMARISHA UCHUMI WA WANAWAKE NCHINI

Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania UWT Mary Chatanda (MCC) ampokea Vyerehani 125 vilivyotolewa na Ubalozi wa China nchini Tanzania kwa lengo la kuimarisha uchumi wa wanawake nchini.

Akizungumza katika Hafla ya upokeaji wa Vyerehani hivyo Mwenyekiti Chatanda amesema vifaa hivyo vitaenda kuinua uchumi wa wanawake na kuwafanya wajitegemee kwa shughuli zao ikiwemo za kisiasa.

“Sote tunatambua kuwa, katika mapambano ya kuitafuta 50/50 moja ya nyenzo muhimu ya kumsaidia mwanamke kufika huko ni uchumi imara katika hili la kupewa vyerehani hivi ni chachu ya kumuongezea mwanamke kuwa na uchumi mzuri “Amesema Mwenyekiti Chatanda na kuongeza

“Uchumi wa mwanamke ukiimarika anaweza kufanya vizuri katika siasa na hata hata ya kijamii kwani inamuongezea kujiamini lakini pia anakuwa na uwezo wa kujisimamia pasipo kutegemea mahali popote na kuondokana na utumwa wa kipato”

Mwenyekiti Chatanda amesema ubalozi wa China kupitia all China women federation mmelitambua hilo na mmeamua kumuwezesha mwanamke kiuchumi kwa kugawa vyerehani na mashine za kutotolea vifaranga”

“Kipekee nachukua fursa hii Kuushukuru ubalozi wa China kwa kuikumbuka Jumuiya ya UWT kuwa kati ya wanufaika wa zawadi hizi, wanawake tuna jukumu la kuiendeleza miradi hii kwa ustadi mkubwa ili kuwa na uchumi imara na hatimaye tuweze kujisimamia na kujitegemea kijamii, kisiasa na kiuchumi.”

Aidha Chatanda amemshukuru Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. Dorothy Gwajima ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji ya Baraza Kuu la UWT Taifa kwa kusimamia upatikanaji wa vyerehani na mashine za kutotolea vifaranga Kwa ajili ya Wanawake wajasiriamali wa Tanzania.


📍Dar es Salaam
🗓️29/4/2024
Kama siyo wazimu huu ni nini? Yaani, kama taifa mnasimama na kupiga makofi kwa kupewa misaada ya cherehani. Kama Wachina wameamua kutoa msaada kusaidia wanawake; kwanini wasiamue kujenga high school za wasichana za kisasa mbili ambazo zitawanufaisha zaidi ya watoto 125? Misaada mingine ni ya kijinga. Inanikumbusha miaka fulani nyuma huko mbeya kuna kiongozi (sijui alikuwa ni Chalamila wakati ule) alienda kupokea misaada ya matundu ya choo. Na ninakumbuka wakati Kikwete naye alipokea misaada ya baskeli kutoka China pale Ikulu.
 
Kama siyo wazimu huu ni nini? Yaani, kama taifa mnasimama na kupiga makofi kwa kupewa misaada ya cherehani. Kama Wachina wameamua kutoa msaada kusaidia wanawake; kwanini wasiamue kujenga high school za wasichana za kisasa mbili ambazo zitawanufaisha zaidi ya watoto 125? Misaada mingine ni ya kijinga. Inanikumbusha miaka fulani nyuma huko mbeya kuna kiongozi (sijui alikuwa ni Chalamila wakati ule) alienda kupokea misaada ya matundu ya choo. Na ninakumbuka wakati Kikwete naye alipokea misaada ya baskeli kutoka China pale Ikulu.
CCM imewaharibu sn watanzania
 
Bei ya juu sana ya cherehani cha mchina ni $100, bei zinaanzia $48 ila tuchukue kuwa hivyo ni vile vya bei ya juu sana. Kwa hiyo msaada huo ni kam $12,500 au Shilingi milioni 31 sawa na mashahara wa wabunge wawili tu.
Tunapiga na picha
 
Hii serikali inapenda vya bure. Ombaomba hawataki kabisa kuweka mikakati ya kujitegemea. Inaanzia juu kabisa kwenye huu utawala wa sasa.
 
Kama siyo wazimu huu ni nini? Yaani, kama taifa mnasimama na kupiga makofi kwa kupewa misaada ya cherehani. Kama Wachina wameamua kutoa msaada kusaidia wanawake; kwanini wasiamue kujenga high school za wasichana za kisasa mbili ambazo zitawanufaisha zaidi ya watoto 125? Misaada mingine ni ya kijinga. Inanikumbusha miaka fulani nyuma huko mbeya kuna kiongozi (sijui alikuwa ni Chalamila wakati ule) alienda kupokea misaada ya matundu ya choo. Na ninakumbuka wakati Kikwete naye alipokea misaada ya baskeli kutoka China pale Ikulu.
Hapo mchina anashiriki kutoa rushwa, uchaguzi umekaribia.
Na kuna kitu mchina anafaidika ujue, tenda zote kubwa za ujenzi nchi hii anapewa yeye
 
Back
Top Bottom