Pre GE2025 DSM Chalamila: Kariakoo ni eneo la biashara siyo sehemu ya kufanyia mikutano ya hadhara

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

The Watchman

JF-Expert Member
Nov 7, 2023
1,140
1,944
Serikali imeeleza sababu za kukamatwa kwa Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), John Heche, katika eneo la Kariakoo, jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila, amesema Heche amekamatwa kutokana na kuendesha mkutano katika eneo lisiloruhusiwa kisheria.

Chalamila amesema ni muhimu wanasiasa kuheshimu taratibu za kufanya mikutano ya hadhara na kwamba sheria itachukua mkondo wake kwa yeyote atakayekiuka.

Aidha, Chalamila amezungumzia tetesi za kuwapo kwa kundi la watu wanaopanga kufanya maandamano tarehe 24 mwezi huu, akisisitiza kuwa vyombo vya ulinzi na usalama vimejipanga kuhakikisha amani inadumishwa. Ametoa wito kwa wananchi kufuata sheria na kuepuka kushiriki katika mikusanyiko isiyo halali.

Serikali imesisitiza kuwa haitafumbia macho vitendo vyovyote vinavyoweza kuhatarisha utulivu wa nchi.
Your browser is not able to display this video.

 
Hawa vegetables hapa walikua wanafanyia wapi?ukishafanya kazi yaiteuzi tu tayari lazima unakua na walakini by default
 

Attachments

  • Screenshot_20250422_213531_Chrome.jpg
    229.8 KB · Views: 1
Wamwachie tu huyo jamaa labda hakujua

Kumweka ndani heche ni kumpa kiki tu
 
well done RC,

we jitu ropokaji litoke tarime huko lije kufanya fujo eneo la biashara dar es salaam,

that's completely nonsense πŸ’
 

CCM hawakufanyia hapo?
 
well done RC,

we jitu ropokaji litoke tarime huko lije kufanya fujo eneo la biashara dar es salaam,

that's completely nonsense πŸ’
Wangemwachia tu jioni ya leo

It was wrong kwenda kariakoo, lakini hao jamaa wana shida za upeo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…