CHADEMA kweli ni shwari au ni kauli za kisiasa tu ?

Nilisema kuwa jamaa alishindwa kupata uenyekiti UVCCM mkoa wa Dar-es-salaam sikusema Dodoma,amekuja kukanusha na kukubali kwa pamoja kuwa 'niligombea sikushindwa kwa vile jina lilikatwa sababu nilionekana mpinzani',sababu hiyo hakupewa na CCM ameitunga, walikatwa kina Malecela,Malima na Lowassa kwenye michakato ya namna hiyo hawakuambiwa wana chembe za upinzani.
Kitila hakuomba 2005 uenyekiti ilikuwa nyuma baada ya kuukosa uenyekiti wa mkoa wa Dar-es-salaam, akaenda NCCR na TLP, wewe ni mwandishi wa habari za utafiti ukipewa dondoo basi unachimba deep, kukusaidia wapi uanzie muulize Zitto Kabwe.

Jk ni mwenyekiti wa CCM sote tunamiini hivyo kama Ilivyo kwa Mbowe na Mbatia ni wenyeviti wa Taifa lakini sidhani kama wewe au mimi tunajua kadi namba zao kuthibitisha hilo.
John Komba ni mwanaccm au John Mnyika lakini mimi na wewe hatujui namba zao ila kuna ushahidi mwingi wa kimazingira kuthibitisha hoja hii.
vyama vyote vina regista ya wanachama wake ukienda huko utapata hadi kadi namba ya Kitila Mkumbo, alikuwa rais wetu wa UDSM kwa kauli hii ujue kuwa alikuwa mtu maarufu na anachofanya tulikifuatilia kwa makini.

Siasa inahitaji uvumilivu chama anachosema Tishio hivi(Chadema) ni nguvu na jasho la watu la miaka zaidi ya 14 hadi wamefika kwenye peak, kama kina Mtei au Mbowe wangekuwa nao wanabadilisha vyama kila mara leo tusingekuwa tunajadili Chadema wamefanya nini, 1995 Chadema walikuwa hawana mgombea wa urais na 2000 ilikuwa hakuna mtu na 2005 ilibidi Mbowe ajitose kufungua milango.

Ushauri kwa wanaoingia kwenye siasa kuwa kunahitaji uvumilivu na subira tusikimbilie kula bila kulima historia ipo na tutaitumia kuweka rekodi sawa pale zipopindishwa.

mimi bado naamini ukileta uthibitisho watu watakuelewa zaidi kuliko story zote hizi mwenzangu. Leta kadi namba au vinginevyo ili kuthibitisha usemi wako.
 
Spendi, vyama vyenye style ya OFISI KTK BRIEF CASE!!!!

Yaani mtu mmoja akisafiri, chama kimesafiri. Akisema, chama kimesema. Asipomtaka mtu, chama hakimtaki mtu huyo. Akilala, chama kimelala!!! Mnh, mola apishie mbali, akifa chama kimekufwa!!!!!!
 
Fikiria, ndio washachukua innji. Kisha wanaanza kutimuana ktk baraza la mawaziri!! ikulu hapatoshi!!!!!. Duh!!!!!!

kutimuana ni sehemu ya kazi ya kujenga, sio kama JK anayeogopa kuchukua hatua anaendelea kuwa na serikali ya watu wasioelewana na wasiofanya kazi yoyote, hadi serikali inaparalise na kila mtu, hata mtoto mdogo anagundua kuwa mambo hayaendi.

Viongozi wakichemsha wanafukuzwa! Huo ndio uongozi wa kuchukua maamuzi.

HEKO MBOWE kwa kazi nzuri.
 
Kitila ameshasema ukweli wake hapa.....kwa nini tunamng'ang'aniza uwongo?

Kama issue ni kuwa mfuasi wa Mrema, hiyo haiwezi kuwa hoja. hata hivyo, ameikubali, lakini hajasema alikuwa mwanachama NCCR-Mageuzi.

Watanzania wengi wenye akili nzuri waliokuwa watu wazima enzi za Mrema walimuunga mkono, siyo kwa sababu ya uzuri wake hasa, lakini sana sana kwa sbabu walichoshwa na ufisadi wa CCM na Mrema ndiye alionekana mtu jasiri aliyeweza kuthubutu kuwatikisa CCM.

Tusisahau pia kwamba enzi za kuvuma kwa Mrema ndizo zilikuwa za wananchi kwa mara ya kwanza tangu 1965 kujisikia huru kuwapinga watawala. Kama wewe hukuwa upande wa Mrema enzi hizo, sitashangaa kukusikia leo bado uko nyuma ya mafisadi.

Mheshimiwa.

Sijasema kuwa ni ubaya kuhama vyama nimetoa mfano wa Mtemvu Abbas ni mbunge wa Temeke alianza Tadea 1992 akaenda UMD,NCCR,CUF na hatimaye CCM,Mtikila yuko DP na Ndesamburo yuko Chadema toka mwanzoni, James Mbatia hajabadilisha vyama kama Kitila.

mjadala wa Kitila umekuja baada ya mmoja wa wapenzi wa Chadema kusema kuwa Wangwe alikuwa NCCR na aliwasumbua huko. nikamjibu kwa kusema kuwa kwani Kitila Mkumbo alikuwa NCCR na TLP anasumbua?

Ni demokrasia kila mtu kuhamia chama anachokitaka hata iwe kila mwezi ila utulivu na subira vinahitajika sana kwenye siasa hata kwenye kazi za kawaida unaenda kwenye interview na kusema kuwa ndani ya miaka miwili umebadili kazi kumi, unawapa nafasi ya kukunyima kazi wakiamini utawakimbia kama ulivyokimbia huko kwingine.

somo hili litawasaidia wengi sana wanaopania kuingia kwenye ulingo wa kiasia kuwa kunahitajia uvumilivu na subira na tuwekeze sana kuliko kutegemea kuvuna, leo hii Mtemvu anaingia kundi la wanasiasa walizuunguka kwenye vyama vingi labda akifuatiwa na Kitila inaweza kuwa ni ishara ya kuonesha juhudi zao za kutaka mambo yaende vizuri ndani ya nchi yetu.

Kubwa jinga samahani sana kwa hili na wala sina maslahi na Wangwe ila haki lazima itendeke hata Saddam Hussein waliotaka kumuua waliweka mazingira ya kuhalalisha mauaji yao kama kumpeleka mahakamani wakati wamesha muhukumu.

naomba nishie hapa sitamjadaili zaidi RAIS wetu wa Daruso lakini kuyakimbia haya ndio baadae mtakuja kusema kuwa 'alikuwa mzigo' au alikuwa mvuta bangi au alikuwa ...... wa kisiasa.
 
Mheshimiwa.

Sijasema kuwa ni ubaya kuhama vyama nimetoa mfano wa Mtemvu Abbas ni mbunge wa Temeke alianza Tadea 1992 akaenda UMD,NCCR,CUF na hatimaye CCM,Mtikila yuko DP na Ndesamburo yuko Chadema toka mwanzoni, James Mbatia hajabadilisha vyama kama Kitila.

mjadala wa Kitila umekuja baada ya mmoja wa wapenzi wa Chadema kusema kuwa Wangwe alikuwa NCCR na aliwasumbua huko. nikamjibu kwa kusema kuwa kwani Kitila Mkumbo alikuwa NCCR na TLP anasumbua?

Ni demokrasia kila mtu kuhamia chama anachokitaka hata iwe kila mwezi ila utulivu na subira vinahitajika sana kwenye siasa hata kwenye kazi za kawaida unaenda kwenye interview na kusema kuwa ndani ya miaka miwili umebadili kazi kumi, unawapa nafasi ya kukunyima kazi wakiamini utawakimbia kama ulivyokimbia huko kwingine.

somo hili litawasaidia wengi sana wanaopania kuingia kwenye ulingo wa kiasia kuwa kunahitajia uvumilivu na subira na tuwekeze sana kuliko kutegemea kuvuna, leo hii Mtemvu anaingia kundi la wanasiasa walizuunguka kwenye vyama vingi labda akifuatiwa na Kitila inaweza kuwa ni ishara ya kuonesha juhudi zao za kutaka mambo yaende vizuri ndani ya nchi yetu.

Kubwa jinga samahani sana kwa hili na wala sina maslahi na Wangwe ila haki lazima itendeke hata Saddam Hussein waliotaka kumuua waliweka mazingira ya kuhalalisha mauaji yao kama kumpeleka mahakamani wakati wamesha muhukumu.

naomba nishie hapa sitamjadaili zaidi RAIS wetu wa Daruso lakini kuyakimbia haya ndio baadae mtakuja kusema kuwa 'alikuwa mzigo' au alikuwa mvuta bangi au alikuwa ...... wa kisiasa.

Ungeweka ushahidi usingekuwa na sababu ya kuandika kitabu kizima. Watu hapa wakiona ushahidi huwa wanakubali. Sasa wewe unaeleza mengi lakini ushahidi hakuna na ndio maana bado watu wanakuuliza ushahidi wa madai yako hapa.
 
Mi sisemi hivyo lakini najua muda si mrefu kuna watu wakiingia humu watasema ni kwa kuwa tu si mchaga!

Wakuu,

Demokrasia ya nchi, chama au club husimamia katiba ya nchi hiyo, chama hicho au club husika.

Kwa kawaida inakuwa siyo busara kuweka njia ya kuingia bila ya kuwapo njia ya kutokea.

Mimi si mwanachama wa CHADEMA wala sijui katiba ya chama hicho inasemaje. Lakini, naamini hatua ya Bwana Wangwe kusimamishwa uongozi ni hatua ya kwanza.

Kusimamishwa uongozi si kufukuzwa uongozi. Kwa hiyo nafikiri hatua itakayofuatia ni hatua hiyo kufikishwa kwenye mkutano mkuu wa wanaongozwa, wenye chama na hao ndio watakaoamua kama wanathibitisha kusimamishwa kiongozi wao na kumfukuza kazi au watatengua kusimamishwa huko na wamwache aendelee kuwaongoza.

Kila likundi kina sheria zake za kufuatwa au kuvunjwa. JF hali kadhalika. Mara ngapi humu watu wamefungiwa na kufunguliwa? Mbona hatukusema JF ni kikundi cha wajinga?

Sheria tunazojiwekea mara zote zinakuwa msumeno. Zinakata huku na huko.
 
hivi kweli mnafikiri ccm itaondolewa madarakani na vyama vya upinzani,labda miaka kumi na tano ijayo.watanzania waliowengi naweza kusema 90% hajajua kuwa maisha yao iliyaboreshwa ni lazima pawe na uongozi imara na uliobora,wengi wanapiga kura bila kujua kwa nini wanapiga kura.

Je ni uongozi upi ambao unauongelea kwa ni imara na ulio bora na maisha ya Watanzania wengi wapi ambayo yameboreshwa?

Je una uhakika ya kwamba wengi wanapiga kura bila ya kujua kwa nini wanapiga kura ama wanapiga kuchagua yule wanayemuona anafaa kwa wakati huo.?

chadema wamemsimamisha Chacha kwa madai kwamba anakiuka maadili waungwana mnaamua kulalamika sana hili jambo ati linaua upinzani...

Kwa nini mazuri yote ambayo Upinzani unafanya kujijenga mayachukulia kama mawazo 'negative'? Chenge pamoja na kashfa za Ufisadi aliporudi katika Baraza la Mawaziri mlifurahia, hakusikitika kama ambavyo mnafanya sasa?

CHADEMA ni shamba lenye miche inayochipua na katu hatutokubali kuyaacha magugu yamee na kukua na miche bora! tunategemea mavuno mema kwa kile tulichokipanda na si vinginevyo!
 
Wapinzani wa chadema mnanichekesha sana. Hivi nyie mnayaamini vipi maneno ya Wangwe?
Si kafukuzwa na chama? kwani kafukuzwa na Mbowe? mbona wengi uelewa ni mdogo?
Wangwe kafukuzwa na Chama. Na kwa sababu mdomo tu ni mali yake na haukufukuzwa ana mamlaka nao kuutumia kwa jinsi aonavyo yeye.
Mwisho bado naamini Chadema itabaki imara bila Wangwe.
Lakini ccm inayoogopa kuwafukuza mafisadi eti kwa kukiokoa chama, wataishia kuiporomosha Danganyika yetu.
 
huku kweli kusafisha maana sasa mtakuwa weupe kiasi ambacho hamchaguliki. au hamuuziki



ndugu zetu siasa si lelemama, sasa nnategemea mtafahamu wananchi watanzania wako makini ktk kuchagua nani awakilishe taifa.


hivi ikiwa mmeshindwa kuvumiliana na kuekana sawa kwa haya madogo ingekuwaje mbowea angekuwa rais na wange waziri mkuu ?

nnaamini mzee wa wapuki na kikundi chake hawana sifa za uongozi ni watu wanaoongoza kwa kutumia hisia badala ya maaarifa, poleni sana

wazee wengi wa chama chenu walikihama tukazungumza hapa mkajidai ooh ccm imewanunua. tumehonga mapesa.

oo makamba kachaguliwa ili awanunuwe wapinzani, sasa semeni na huyu tumemnunua.

nyinyi wenzetu kwanza kubalini bado ni wadogo nakwa kukusaidieni 2010 tutakuwekeni benchi nyote na kisha mtajifunza siasa huko nje maana kupata hivyo vijiruzuku kidogo tu mshaanza kuvutana mashati na kutofautiana kiasi hicho


kufa kwa chadema ni faida kwa ustawi wa demokrasia

Kikwete akiwa Raisi na Lowasa Waziri Mkuu kilitokea nini baada ya Mtendaji Mkuu wa Serikali kuvurunda...

CCM kuwa na mbegu kama hizi ndio zinachangia uchafu wa Chama kwa kukumbatia Uozo! Kujisafisha ni wajibu kabla ya aibu ya harufu mbaya kukukumba!
 
wenyeviti wa vyama vingi vya upinzani ni kama miungu ukitaka ukione cha moto wakosoe, hivyo demokrasi ni ndogo ndiyo maana CCM itaendelea kongoza tu. Demokrasi ndani ya CCM IPO JUU na jamaa wanaweza kukosoana kwa kiasi kikubwa kulinganisha upinzani.
huo ni mtazamo wangu tu
 
wenyeviti wa vyama vingi vya upinzani ni kama miungu ukitaka ukione cha moto wakosoe, hivyo demokrasi ni ndogo ndiyo maana CCM itaendelea kongoza tu. Demokrasi ndani ya CCM IPO JUU na jamaa wanaweza kukosoana kwa kiasi kikubwa kulinganisha upinzani.
huo ni mtazamo wangu tu

mmmmmmmhhhhhh unasema kweli?:oops:
 
Masaa machache baada ya Kamati Kuu ya Chadema kufanya uamuzi wa kumsimamisha aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho Bw. Chacha Wangwe (Tarime) KLHN ilipata fursa ya kuzungumza kwa kirefu na wahusika wote wakuu.

Mahojiano yangu na Bw. Tundu Lissu (Mkurugenzi wa Katiba na Sheria wa Chadema na Wakili wa Mahakama Kuu ya Tanzania) yalielezea kwa kirefu ni kwanini Chadema walifikia uamuzi huo na nini kilichojiri. Mara baada ya kuzungumza na Lissu nilipata pia nafasi ya kuzungumza kwa kirefu na Bw. Chacha Wangwe kuhusu kufungiwa kwake na zaidi ya yote kuhusu madai yaliyoainishwa dhidi yake kwenye Tamko la Kamati Kuu hiyo.

Mahojiano hayo ambayo yamechukua karibu saa nzima yatarushwa kwenye KLH News exclusive kesho ili kila mtu aweze kufanya uamuzi wake yeye mwenyewe baada ya kuwasikia.

We bring the news, from the news makers!

Yanapatina sehemu gani? kwenye Klh news? napata tabu kuyapata.
 
Mwkjj,
Kwa mara nyingine tena hongera kuwa mstari wa mbele katika kupambanua mchele na pumba. Tunayasubiri kwa makini.
 
Ungeweka ushahidi usingekuwa na sababu ya kuandika kitabu kizima. Watu hapa wakiona ushahidi huwa wanakubali. Sasa wewe unaeleza mengi lakini ushahidi hakuna na ndio maana bado watu wanakuuliza ushahidi wa madai yako hapa.

Sio wote wanaelewa darasani, nimetoa darasa na wenye kuelewa wamelewa ni mwaka 2000 ndio alikwenda TLP,muulize Zitto Kabwe labda utamuelewa.

Nitumie email yako nikwambie jina analotumia Mbowe kwenye mtandao kama tulivyokubaliana.
 
Masaa machache baada ya Kamati Kuu ya Chadema kufanya uamuzi wa kumsimamisha aliyekuwa Makamu Mwenyekiti wa Chama hicho Bw. Chacha Wangwe (Tarime) KLHN ilipata fursa ya kuzungumza kwa kirefu na wahusika wote wakuu.

Mahojiano yangu na Bw. Tundu Lissu (Mkurugenzi wa Katiba na Sheria wa Chadema na Wakili wa Mahakama Kuu ya Tanzania) yalielezea kwa kirefu ni kwanini Chadema walifikia uamuzi huo na nini kilichojiri. Mara baada ya kuzungumza na Lissu nilipata pia nafasi ya kuzungumza kwa kirefu na Bw. Chacha Wangwe kuhusu kufungiwa kwake na zaidi ya yote kuhusu madai yaliyoainishwa dhidi yake kwenye Tamko la Kamati Kuu hiyo.

Mahojiano hayo ambayo yamechukua karibu saa nzima yatarushwa kwenye KLH News exclusive kesho ili kila mtu aweze kufanya uamuzi wake yeye mwenyewe baada ya kuwasikia.

We bring the news, from the news makers!

Any summary?
 
Kwa wale mlioko US na sehemu nyingine ambazo mtakuwa macho nitarusha mahojiano yangu na Tundu na Wangwe kuanzia saa nne kamili EST nikiwa natangaza "live"..
 
Back
Top Bottom