CHADEMA chama bora mwaka 2008: Tujifunze toka kwao

- Ni kama vile ambavyo sijaona sababu ya huu ubora wa Chadema unaosemwa hapa, ubora wa chama cha siasa ni kwenye kura za uchaguzi mkuu kwanza, mara ya mwisho uchaguzi wa taifa ulipofanyika CCM ilishinda kwa miaka mitano, sasa tupo kwenye wa tatu na CCM imekuwa ikishinda for the last 47 years, huo ndio ubora wa chama cha siasa.

- Kama kuna ubora wa the last three years, tutauona kwenye uchaguzi wa 2010, kwenye uchaguzi uliopita ni CUF ndio walioshika namba mbili sio Chadema, CCM ndio chama tawala kilichochaguliwa na wananchi wengi wa Tanzania for the last 47 years, we can talk kuhusu viongozxi wachache ndani ya chama chochote cha siasa bongo, lakini as far as CCM so far hao viongozi wachache hawajaathiri mtizamo mzima wa chama,

- Ukweli ni kwamba mijadala ya namna hii ndani ya hii forum ni very low, lakini hatuna njia ila kujibu tu, ingawa ni very low kwa taifa!

FMES, natofautiana sana na wewe katika mjadala huu. Pamoja na kutambua uwezo wako wa kujenga hoja na uwezo mzuri wa kuchagua maneno sahihi katika kuyapa maandiko yajo mvuto, katika mjadala huu, kwa mtazamo wangu umepwaya sana kimantiki.


Ni kweli kuwa uchaguzi mkuu wa mwisho ulifanyika mwaka 2005 na kwamba ndio rejea ya mwisho ya uchaguzi mkuu.Unachosahau katika siasa kuna maisha baada ya uchaguzi mkuu, mara nyingi huwa tunavisakama vyma vya upinzani kuwa ni vyama vya uchaguzi na kuwa havifiki vijijini leo CHADEMA inajitokeza inafanya kazi yake vizuri sana, ni vizuri tuka waunga mkono kwa minajili ya kukuza demokrasia Tanzania.


Kumbuka mjadala ni kutathmini kazi ya vyama vya siasa mwaka 2008, kwa chama cha upinzani kina kuwa na wajibu wa kujiimarisha(kimuundo na ki-uwenezi) na pia kuiwajibisha serekali pale ambapo inajikwaa, CHADEMA wametekeleza vizuri sana wajibu wao huu. Lazima tuwe tayari kupima ufanisi wa vyama wakati ambapo hamna uchaguzi mkuu, je umihimu wao katika ustawi wa taifa unakuwa umehairishwa mpaka kipindi cha uchaguzi mkuu?


Pia umesema mijadala kama hii ni milaaini na haina umihimu wa uzito wa kutosha kujadiliwa katika eneo hili na kwamba haina umuhimu kwa taifa!Naomba kutofautiana nawe hapa pia.Napinga hoja zako kwa mtazamo kwamba:
1. Hili ni jukwaa la siasa, si rahisi kuepuka mijadala ya taasisi zinazofanya siasa!

2. Nakubalina nawe kwamba tunapaswa kujadili maswala mazito ya kitaifa na kwamba tutangulize maslahi ya taifa mbele. kuanzisha mjadala huu ni sehemu ya kuetekeleza hoja hii. Naamini kuna umuhimu mkubwa sana wa kukuza vyama vya siasa ili kuweka mazingira mazuri ya ushindani wa kisiasa na ukuaji wa demokrasia nchini kwetu.

Haya maswala mazito unayotaka tujadili yanapaswa kupokelewa na taasisi imara za kisiasa ili yaweze kufanyiwa kazi. Ikiwa tuna taasisi dhaifu za kisiasa hata tujadili mambo mazito kiasi gani bado hakutakuwa na matokeo tarajiwa, hivyo ni sehemu muhimu sana ya maslahi ya taifa kukuza taasisi zetu za kisiasa.Kutambua mchango wao na kuvipongeza vinapofanya vema ni sehemu ya kuvikuza!

Tunaweza kuwa na mijadala mizito sana ya masuala mbalimbali lakini kama hatutajenga taasisi imara za kisiasa kuweza kusimamia masuala haya tutakuwa tunafurahisha genge, kujiumiza kihisia na kutotoa mchango wetu kwa taifa kama inavyopaswa.

Kama wanaharakati wa demokrasia na wazalendo wa nchi, sambamba na kujadili masuala mazito kama ulivyopendekeza(na ninakubaliana nawe), tunawajibu wa kutengeneza mazingira mazuri ya demokrasia na kuimarisha vyama vyetu.Kutambua na kuwapongeza pale wale wanapofanya vizuri ni sehemu ya kujenga taasisi imara za kisiasa ambazo zitaweza kubebea vizuri masuala mazito tunayoyajadili hapa.

Leo hata bunge letu linapwaya kutokana na ubabe na uwiano mbaya baina ya wabunge na vyamba mbalimbali,kuwa na chama kimoja chenye nguvu kupindukia ni mazingira hatarishi kwa taifa. Ikiwa CHADEMA inatengeneza njia ya kurekebisha suala hili ni vyema tukawapongeza na kuhimiza wengine kufanya hivyo ili tuwe na siasa zenye afya zitakazochochea ustawi wa taifa letu kwa ujumla wake.

Lengo na kuanzisha mjadala huu msukumo wake si "Usimba na Uyanga" kama ulivyoainisha bali ni kutambua jitihada za CHADEMA katika ujenzi wa Demokarsia Tanzania. Niko tayari kujadli na kutafakari nawe kama kipo chama kilichofanya vyema zaidi ya CHADEMA mwaka 2008.

Asante
 
FMES
Niseme hivi: CCM are the worst party and which cannot be trusted; corrupt, etc. CHADEMA at least wametuonyesha kuwa they can play a game by putting the government of CCM naked (Which no party could do in my life time). Maybe we do not have any alternative, CHADEMA are still a young PARTY; we know this DEVIL CCM. Lakini ukweli ni kuwa if I was told to select which PARTY have done a good job in 2008; I 'll say BRAVO to CHADEMA; they just need to solve some of their consolidation problems!

Again 2008, CHADEMA did a best job which you and I will only dream; CCM are the worst PARTY! CCM inategemea siasa za AMANI na STABILITY otherwise they are a dead body!
 
Field Marshall Es,
Mkuu bado hujanipa Ubora wa chama CCM, hayo ya ushindi wa Uchaguzi yamepita miaka mitatu au umesahau hoja inasema mwaka 2008..
CCM kama chama kusema kweli hakikufanya kitu zaidi ya watu binafsi kusimama nje ya matakwa ya chama..
Binafsi nampongeza Kikwete kafanya mengi mazuri ambayo sikutegemea kabisa ikiwa ni pamoja na kurudisha haki ya waandishi, kupigana na Ufisadi akiungwa mkono na kina Mwakyembe, Mama Kilango, Sitta na baadhi ya wabunge na wastaafu ambao wameweza kusimama nje ya chama kwa maslahi ya Taifa... Pamoja na yote haya,Chadema kama chama wamejitahidi sana kuonyesha Ubora wa chama mwaka huu..
Hizo habari za mbunge wa Mbeya vijijini kujaza form jambo la kawaida kuliko ile ya mama meghji waziri mzima wa Fedha kuingizwa mkenge na Balali akapitisha malipo bila hata supporting document, kuna ujuha gani zaidi ya huo..Kisha basi huko vijijini hakimu wenyewe wangapi basi!.. unaweza kuta hakimu ni mmoja au wawili wakiondoka basi kila kiitu kimelala..

Mkuu, nadhani hoja hapa ni chama sio watu binafsi na tukianza kuweka list za watu walioboronga sidhani kama ukumbi huu utatosha..

Fair point.
swali Kikwete ni mwenyekiti wa DP? ama ni mwanachama wa chama gani? na nini maana ya chama if that is the case chadema imefanya nini kama chama tofauti na juhudi za wachache kabisa Mnyika ,zitto na Slaa tu?
 
Fair point.
swali Kikwete ni mwenyekiti wa DP? ama ni mwanachama wa chama gani? na nini maana ya chama if that is the case chadema imefanya nini kama chama tofauti na juhudi za wachache kabisa Mnyika ,zitto na Slaa tu?

Mkama nimeanisha Waliofanya CHADEMA katika mchango wangu wa kwanaa. Na Je wanaoyafanya wakina zito, wanafanyia kama watu binafsi au ni sehemu ya utekelezaji wa mipango ya chama kwa mwaka husika? Sehemu kubwa wanayofanya ni sehemu ya mikakati ya chama chao.
 
Huu mjadala unaweza kuwa mpana sana kutokana na watu kuwa na misimamo tofauti. Lakini kimsingi, unaweza kuufupisha wiapo utaamua kuchukulia ukweli wa mantiki ya mambo. Kuifananisha Chadema na CCM katika ubora ni upotofu. Chadema ni chama cha upinzani na CCM ni chama tawala, majukumu yao hawa hayafanani.
Kwa hiyo, kwa wanaoamini hivyo, wanaweza kusema kuwa kwa upande wa vyama vya upinzani, Chadema kimefanya vizuri mwaka huu. Lakini ni vigumu kuangalia kwa upande wa chama tawala kwa sababu kipo chenyewe tu, hakina wa kumlinganisha naye. Hapo sasa ndipo tunapolazimisha kukilinganiahs chama hicho na vyama vingine wakati hili haliswihi.
 
Huu mjadala unaweza kuwa mpana sana kutokana na watu kuwa na misimamo tofauti. Lakini kimsingi, unaweza kuufupisha wiapo utaamua kuchukulia ukweli wa mantiki ya mambo. Kuifananisha Chadema na CCM katika ubora ni upotofu. Chadema ni chama cha upinzani na CCM ni chama tawala, majukumu yao hawa hayafanani.
Kwa hiyo, kwa wanaoamini hivyo, wanaweza kusema kuwa kwa upande wa vyama vya upinzani, Chadema kimefanya vizuri mwaka huu. Lakini ni vigumu kuangalia kwa upande wa chama tawala kwa sababu kipo chenyewe tu, hakina wa kumlinganisha naye. Hapo sasa ndipo tunapolazimisha kukilinganiahs chama hicho na vyama vingine wakati hili haliswihi.

Ndugu inawezekana kama kuishindanisha CCM na vyama vingine? Suala ni mizania? Tuangalia uwezo wake kusimamia serekali? Usimamiaji wa ilani yao ya uchaguzi? shughuli na mikakati yake ya kisiasa? na maamuzi mbalimbali iliyofanya kisiasa? mathlani ushiriki wake katika mjadala wa muafaka? ushiriki wake katika uchaguzi wa Tarime na kadhalika
 
Mkama nimeanisha Waliofanya CHADEMA katika mchango wangu wa kwanaa. Na Je wanaoyafanya wakina zito, wanafanyia kama watu binafsi au ni sehemu ya utekelezaji wa mipango ya chama kwa mwaka husika? Sehemu kubwa wanayofanya ni sehemu ya mikakati ya chama chao.


Mkuu
mimi namemuuliza Mkandara homeboy swali hilohilo yeye amesema haoni ccm ilichofanya lakini wakati huo huo anawasifia watu binafsi akina mwakyembe,jk, seleli na akina anna sasa ndio nikauliza maana ya chma ni nini?
 
Ndugu inawezekana kama kuishindanisha CCM na vyama vingine? Suala ni mizania? Tuangalia uwezo wake kusimamia serekali? Usimamiaji wa ilani yao ya uchaguzi? shughuli na mikakati yake ya kisiasa? na maamuzi mbalimbali iliyofanya kisiasa? mathlani ushiriki wake katika mjadala wa muafaka? ushiriki wake katika uchaguzi wa Tarime na kadhalika

ishindanishe ccm na orange ama narc ya kenya.ama kile chama cha Mugabe ama cha Kagame ama kurunziza ama mzee mzima mseven.
 
A matter of opinion.. and even if this is the case... kuwa the least ulieoza katika kundi la samaki wabovu sio sababu yakusifiwa or more likely in this case kujisifu.
 
MkamaP,
nadhani Eric amekujibu vizuri labda mimi nifafanue zaidi.
Aloyafanya Kikwete ni kinyume cha matakwa ya wanachama au chama CCM.. Kuna watu wacheche sana wanaounga mkono Kikwete ktk maswala yote ikiwa ni pamoja na swala la Lowassa, kuvunja baraza la Mawaziri, Kuwapeleka mahakamani kina Jeetu, Mramba na Yona..Kila siku tunaona michango ya watu humu wakilaani kukamatwa kwa hao na wengine..
Kwa hiyo kama maswala haya yote yangepigiwa kura ndani ya chama Kikwete angeungana na watu wachache sana niliowataja hapo nyuma..

Wakati maswala yote yanayohusiana na Zitto pamoja na Dr. Slaa ni maswala ambayo kwanza yamepitishwa na chama mbali na kuwakilishwa na watajwa hao..kifupi mambo yote yaliyofanywa na Zitto, Dr. Slaa Mnyika na wengine yamepata baraka za chama na pengine sio watu waliokuwa nataarifa za awali isipokuwa wamependekezwa kusimamisha hoja Bungeni..Kumbuka tu Chadema ina wabunge watano (5) tu wa kuchaguliwa na kati yao wawili ni mfano mzuri wa nini wabunge wanatakiwa kusimamia..

Kisha swala hapa ni swala la mwaka hadi mwaka. Hili sio swala la Ushindani kama Simba na Yanga kiasi tuseme timu bora ni ile iliyochukua kombe! Hakuna mashindano ya mwaka.. labda hizo chaguzi ndogo nazo pia sio ubora wa chama..Tunazungumzia Ubora wa chama kulingana na mazuri waliyoyafanya kama chama mwaka 2008...
Kwa mfano, Ukitazama mapungufu yaliyoandika mkuu Kazi ndio kipimo cha Utu.. utagundua kwamba ni mapungufu ambayo yapo vyama vyote..Hakuna kasoro hata moja aliyoitaja ambayo huwezi kuikuta CCM, CUF, NCCR au vyama vinginevyo..
 
1.
MAONI YA MHARIRI

Kilichotokea Mbeya Vijijini kinaweza kuelezewa kwa maneno matatu tu: kilele cha uzembe. Kwa chama ambacho kinajaribu kujiweka katika nafasi ya kuwa mbadala wa chama tawala kushindwa kufuata taratibu rahisi na ambazo siyo ngeni kwao inaonesha ni kuchukulia kitu kiurahisi wakitegemea kuungwa mkono na wananchi. Tunajiuliza ni nani nani alikuwa msimamizi wa mchakato wa kumtafuta mgombea wa uchaguzi wa Chadema huko Mbeya?

Je uongozi wa Taifa au Mkurugenzi wa mambo ya uchaguzi wa Chadema alishiriki vipi katika kufuatilia mchakato mzima wa kumteua na hatimaye kumpitisha mgombea wao? Je uongozi wa Taifa ulifuatilia kwa kiasi gani taratibu hasa ukizingatia kuwa viongozi wake tatu wa ngazi za juu ni wabunge au wamewahi kuwa wabunge?

Kama katika tovuti yao wao wenyewe wamesema sharti mojawapo la mgombea ni kuwa "awe amekula kiapo mbele ya Hakimu" na hakuna ushahidi wa mgombea mwingine yeyote kuapa kwa mtu mwingine isipokuwa hakimu iweje wadhanie kuwa wao Chadema watatengeneza taratibu zao wao wenyewe nje ya zile zilizokubalika na kutumika kwa muda huu wote? Angalau kama wangekuwa na mfano wa mgombea yeyote ambaye amewahi kupitishwa kugombea nafasi ya uongozi nje ya Hakimu labda wangekuwa na kesi.

Tunaamini hili ni doa linalofutika na ambalo linaweza kuwa nafasi ya wao kujichunguza zaidi na kujisahihisha zaidi. Wakati wa kulaumiana haupo lakini wakati wa kutengeneza umefika kwani hili ni kosa ambalo kama lingetokea kwenye chaguzi nyingi au kwenye uchaguzi mkuu kwa hakika lingekuwa na gharama kubwa mno. Gharama ambayo Chadema watailipa sasa hivi ni kutokuwa na mgombea wao, na hiyo ni gharama wanayostahili kuilipa kwa kufanya maamuzi ya kizembe.

Hata hivyo Chadema ikipenda na ikiacha maslahi yake inaweza kutumia nafasi hii kujijenga upya na kujirudishia imani kwa wananchi na wanachama wake. Baadhi ya hatua ambazo inapaswa kufanya ni hizi zifuatazo:

a. Chadema ichukue hatua za haraka na maramoja dhidi ya Shitambala, viongozi waliohusika na mchakato wa kumtafuta mgombea. Hatua hizo zapaswa kuwa kusimamishwa kwa muda, kutakiwa kuomba radhi n.k

b. Chadema ikubali kosa kuwa walifanya makosa kutofuata taratibu za uchaguzi nchini.

c. Bw. Shitambala kama alihujumu au kwa kujifanya "anajua sheria" aliamua kwenda nje ya sheria basi asipewe dhamana ya uongozi kwa muda fulani na kama ni kiongozi tayari asimamishwe au kupunguziwa madaraka yake.

d. Chadema iweke na kutangaza utaratibu wa kupattikana kwa wagombea wake hadharani na wahakikishe kuwa utaratibu huo unafuatwa nukta kwa nukta.

e. Chadema itangaze kumuunga mkono mgombea wa upinzani ambaye ana nafasi

f. Uongozi wa Chadema(TAIFA) kwa kuzingatia misingi ya demokrasia na kuhakikisha kuwa upinzani unashinda Mbeya vijijini watumie raslimali zao, vipaji na watu wao kumfanyia kampeni mgombea huyo wa upinzani pasipo masharti yeyote au kuendeleza kisasi kutokana na tofauti za kisiasa na vyama vingine huko nyuma.

Endapo hatua kama hizo zitachukuliwa wapinzani wanaweza kujiweka katika nafasi ya kushinda. Vinginevyo, wananchi wa Mbeya Vijijini wana haki na sababu ya kuongozwa na mtu ambaye anaheshimu sheria, na ambaye atawakilisha kweli maslahi yao. Kama mtu huyo hayuko upinzani basi upinzani haustahili kuchaguliwa ilimradi tu upinzani ushinde. Kufanya hivyo itakuwa ni kuchezea demokrasia na kuweka rehani hatima ya uwakilishi wa watu wa Mbeya vijijini kwenye Bunge la Jamhuri ya Muungano. Siyo tu chama sahihi lazima kishinde lakini hasa mgombea ambaye atawakilisha, kulinda, na kuyatunza maslahi ya watu wa Mbeya Vijijini lazima ashinde
.

2.
Interested Observer Re: CHADEMA chama bora mwaka 2008: Tujifunze toka kwao

FMES
Niseme hivi: CCM are the worst party and which cannot be trusted; corrupt, etc. CHADEMA at least wametuonyesha kuwa they can play a game by putting the government of CCM naked (Which no party could do in my life time). Maybe we do not have any alternative, CHADEMA are still a young PARTY; we know this DEVIL CCM. Lakini ukweli ni kuwa if I was told to select which PARTY have done a good job in 2008; I 'll say BRAVO to CHADEMA; they just need to solve some of their consolidation problems!

Again 2008, CHADEMA did a best job which you and I will only dream; CCM are the worst PARTY! CCM inategemea siasa za AMANI na STABILITY otherwise they are a dead body!

- Wakuu Eric Ongala na Interested Observer, naona mle darasa hapo juu, mimi siweki neno kabisaa.
 
Wacheni ndoto zenu za mchana,eti chama bora! hata haya hamna!

Kaka Kibinango, wenzako CHADEMA hawaoti ndoto za mchana bali wana mikakati na taratibu mafanikio ya utekelezaji wa mikakati yao unaonyesha mafanikio. Bandiko hili tu ni moja ya mifano ya mikakati bora ya CHADEMA. Nani alifikiria ama ameona chama chochote katika historia ya Tanzania baada ya TANU kikitoa mapitio kama haya katika siku ya mwaka mpya. Vilevile ni chama gani ama washabiki/wafuasi/ wanachama wa chama gani katika nchi yetu ambao wamewahi kuanzisha mijadala/mapitio kama haya yenye kulenga kujua mawazo ya watanzania kuhusu maendeleo ya chama chao kama wafanyavyo hawa jamaa wa CHADEMA.

Ndugu yangu kwa kuwa wewe ni mzanzibari na katika znz ur either with CCM ama against CCM translating to CUF, ni bora ukajiuliza ?
1. Hivi CCM na CUF wamefanya nini hata kuita mafanikio tangia mwaka 2005 ?
2. Je kati ya CCM, CUF ama CHADEMA ni chama gani kimeonyesha muelekeo wa kukua Kiasasi, Kisera ama Kiajenda tangia baada ya uchaguzi wa 2005 ?
3. Je ni chama gani kati ya CCM, CUF na CHADEMA kimeweza kuanzisha na kusimamia ajenda yoyite na ikawa ajenda ya kitaifa na ikawa na mvuto kwa watanzania walio wengi tangia uchaguzi wa 2005 ?

Tanzanianjema
 
- JF bwana kila tunapojaribu kuwa kwenye line na ishus za taifa, then yanakuja maneno ya Chadema kuwa bora, huku wamesahau kuwa sheria ndogo tu inayosema mgombea ubunge anatakiwa kuapishwa kwa hakimu, mgombea wao anaenda kujiapisha mwenyewe, so much kwa chama bora!

- Vyama vyote vya siasa nchini vimefanya kazi nzuri kwa taifa, sasa ni kuendeleza mshikamano wa kusimamia hoja nzito kitaifa bila kujali vyama na kukubaliana kutokubaliana kwenye hoja zingine, lakini ya ubora kwa chama kilichoshindwa kupata hata kura 15% nationwide kwenye uchaguzi wa rais, pamoja na kuburuza helikopta kila kona ya taifa letu, ni matusi makubwa sana kwenye wengine tusiokuwa wanachama wa Chadema hapa JF, it is about time sasa wakaondoa ukabila kwanza huko Chadema ili waweze kua current na sheria za taifa kwa vyama vya siasa nchini, hatupendi hii mijadala ya yanga na simba lakini mnatulzimisha wenyewe, tunakubali kuwa mko wengi sana humu JF, lakini it does not mean anything kihoja, maana ni uzito wa hoja na sio nani maarufu kati ya yanga na simba, au CCM na Chadema,

- Nia na madhumuni ya chama chochote cha siasa duniani ni kushinda uchaguzi mkuu wa taifa until then kujiita bora na maarufu ni kujidanganya na kuwadanganya wananchi bure, fanyeniu kazi ya wananchi ndio mtalipwa kwenye uchaguzi lakini sio kujipigia debe bila matokeo, kwenye hili ninaomba kukubali kutokubaliana, ila pole pole tusiburuzane kama magari mabovu!

Thanxs!

Kaka FMES

- Suala la maendeleo ya kidemokrasia ni suala la kitaifa. Kujadili kile kinachoonekana na baadhi ya watu kama mafanikio kwa chama kimojawapo kama CHADEMA ni moja ya hatua bora za kuboresha demokrasia yetu. Ni wazi ili kulinda, kutetea na kuimarisha demokrasia yetu ni lazima tuwe na chama ama vyama mbadala vyenye kuonyesha kukua kisera, kiajenda na kiasasi. CHADEMA imeonyesha hivyo na hakuna chama kingine kimeonyesha hivyo kuanzia mwaka 2005

- Katika demokrasia inayokuwa na wakati mwengine inayogandamizwa na ukiritimba wa chama kimoja kama ilivyo Tanzania, matokeo ya uchaguzi hayawezi kuwa kipimo cha ubora wa chama. Wote tunajua kuwa CCM inashinda kwa njia za halali na haramu pia. Lakini pia tunajua kuwa CCM inaendelea kuwa madarakani kutokana na advantage ya HISTORIA, Umiliki na matumizi mabaya ya vyombo vyetu vya dola, Ujinga wa wapiga kura walio wengi na UFISADI. Kwa mpenda nchi yake/mzalendo wa kweli yeyote, mafanikio yanayopatikana kutokana na njia hizi si mafanikio bora…

- Si kweli kabisa kuwa vyama vyote Tanzania vimefanya kazi nzuri kwa Taifa. Kuna vyama vimekuwa vikifanya mambo ambayo yanaendelea kubomoa nguzo za utaifa wetu na hivyo kuhatarisaha usalama na hatima ya nchi yetu. Siasa za kugawanya wananchi kidini, kikabila, kitabaka na hata kiasili zinazofanywa na baadhi ya vyama(kama mikakati ya kichama) ni siasa za kuvunja nchi. Kulinda na hata wakati mwengine kutetea UFISADI na MAFISADI eti kwa maslahi ya Taifa/chama ni uvunjaji wa Taifa.

Kuhusu kuwa “as far as CCM so far hao viongozi wachache hawajaathiri mtizamo mzima wa chama”

Unajua wazi kuwa hii sio kweli. Maovu ya viongozi walio wengi ndani ya CCM yamevuruga kabisa mtizamo mzima wa CCM. Inawezekana bado haujaathiri taswira ya chama ambayo ni kuenelea kushika madaraka kwa namna yoyote ile lakini hilo ni suala la muda tu kujionyesha…Hata hao wanaojidai kukemea uovu/ufisadi ndani ya CCM wamesema wazi kuwa wanafanya hivyo kwa ajili ya kulinda utawala wa CCM badala ya kuacha hayo yanasemwa na kina “Zitto” wakiwa na maana upinzani. Hapo bado utasema kuwa hiki ni chama bora? Labda ni bora kwa wadau wa tabaka tawala ambao nao pia wameaanza kukemea maovu ili kulinda nafasi/maslahi yao lakini kamwe bora kwa taifa wala watanzania kwa ujumla

Tanzanianjema
 
3.Uchaguzi wa wabunge wa kuteuliwa ushirikishe wanachama wote na hizo nafasi watu wasigombee kwa kupigiwa kura ndani ya chama ktk vikao vya juu na si kama sasa kwa uteuzi unavyofanywa na kikundi cha watu,Hili sina hakika katiba yao inasema nini na kama ndiyo katiba inavyosema basi nitaomba wanachadema mfanyie marekebisho katiba ili kutoa wigo wa demokrasia zaidi ktk kuwapata wabunge wa kuteuliwa ili kusitokee manung'uniko ya ubinafsi na upendeleo ktk uchaguzi kama ilivyowahi tokea awali.
4.washirikisheni wanachama kupitia vikao halali ktk maamuzi yanayohusu mikopo ,mapato na matumizi yake kama vile utumiaji wa helicopter wkt wa chaguzi ili kuepuka kuwabebesha mzigo wanachama wa kulipa deni bila ya kuwashirikisha ktk mchakato mzima wa kukopa na matumizi hapo awali na kuja kuwashirikisha ktk kulipa deni tu.
5.Inapotokea kiongozi wa juu anakikopesha chama wanachama washirikishwe na wakubali kukopeshwa na wanapokubali kiongozi aliyekopesha asiwe muamuzi mkuu wa utumiaji wa kile alichokikopesha ili kuwe na uhakiki na kuepusha wanachama kulipa kile ambacho wameambiwa kimekopeshwa chama na kutumiwa bila ya uhakiki wa hali juu na mkopeshaji huyo huyo ambaye bado ni kiongozi hapa kuna conflict of interest hasa inapotokea mkopeshaji ndiyo huyo huyo mtumiaji au mwenye mamlaka ya kuidhinisha utumiaji.
6.Kwani uongozi wa juu unaamua wao pekee yao kutoungana na vyama vingine upinzani kama walivyokubaliana awali ,kwanini wasirikishwe wanachama wote ktk ishu kama hii ili kuweka ushirikishwaji wa wananchama ktk maamuzi makubwa kama haya.

Ndugu yangu Kazi Ndiyo Kipimo Cha Utu

Umetoa mawazo mazuri lakini nadahni swali lako kuhus uteuzi wa wabunge wa viti maalumu ni vizuri ukaangalia katiba ya CHADEMA. Nijuavyo mimi ni kuwa suala hilo walishalijadili sana ndani ya chama na hata kufanya mabadiliko ya katiba kuhusiana na hilo….

Kuhusu maamuzi ya matumizi na mikopo sidhani kama kuhusisha wanachama wote inawezekana na kama feasible. Kuna baadhi ya majukumu ya kiutendaji yanapasa kushughulikiwa na sekretariati kwa ajili ya ufanisi. Wanachama wanakuwa na nafasi ya kuchagua viongozi na kupitisha sera na kwa kupitia viongozi waliowachagua ndio wanapaswa kuhusika katika utekelezaji wa sera na maazimio yaliyoptishwa na viongozi waliowachagua…

Nakubaliana nawe kabisa suala la kupanua wigo wa ushirikiano wa vyama hadi kwa wanachama. Itakuwa vizuri kama hivi vyama vitakuwa vinafanya mikutano ya pamoja. Hii itasaidia sana kujenga kuaminiana kati ya vyama hivi kuliko kuacha hili kwa viongozi pekee ambao ni ama hawaaminiani ama wanaoneana wivu…..

Tanzanianjema
 
Fair point.
swali Kikwete ni mwenyekiti wa DP? ama ni mwanachama wa chama gani? na nini maana ya chama if that is the case chadema imefanya nini kama chama tofauti na juhudi za wachache kabisa Mnyika ,zitto na Slaa tu?

Ndugu yangu MkamaP…

Ingekuwa Kikwete amefanya aliyoyafanya kwa nia njema kwa Tanzania na sio katika jitihada za kuokoa chama chake nap engine urais wake basi hiyo ingekuwa credit. Lakini ukweli sio hivyo…

Pili utokana na ukweli kuwa mwenendo mzima wa kashfa za UFISADI zinaonyesha kuwa kumekuwa na juhudi kubwa nadni ya chama na hata katika maamuzi ya vikao vya chama cha CCM kujaribu kulinda wahusika na kwa kuwa ufisadi umetumika katika jitihada za kuendeleza utawala wa CCM nchini, ni wazi CCM kama chama hakiwezi kupata sifa yoyote nzuri katika suala zima la mapambano dhidi ya UFISADI…

Kulinganisha CCM na ORANGE MOVEMENT ama NARC na CCM ni kuchemsha. NARC na baadae Orange Movement zinashabihiana na jitihada za upinzani kung’oa chama fisadi pamoja na mfumo fisadi uliojengwa na KANU na baadae PNU ambacho kihistoria ndio kinapaswa kulinganishwa CCM….Nakubaliana nawe na kuhusisha CCM na kile chama cha Mugabe (ZANU-PF) ama mzee mzima mseven (NRM)…..

Tanzanianjema
 
Sitaki kulinganisha mwizi na mwuaji na kutafuta nani ana nafuu kwa vile wote ni adui wa maendeleo ya jamii. Baada ya madudu ya Mbeya, I have minimal respect for CHADEMA, na hasa wanaposita kukubali kuwa wamefanya 愚蠢. Ningewaelewa endapo wangekubali mapema kuwa waliteleza kisheria na kuanza kumsaidia mgombea wa chama kingine ambaye wanakaribiana kisera, lakini wanapopinga uamuzi unaoonyesha kuwa wamekiuka sheria ambayo iko wazi kabisa kuhusu "magistrate" ninaowaona kuwa hawa nao ni wale wale tu. Sheria ya zamani ya mahakama ilikuwa ina nafasi ya wao kujitetea, lakini kwa vile kuna sheria mpya ambayo wananakiwa wawe wanaijua, hapo ndipo nina-question uwezo wao.

Kwa sasa nadhani kuwa sheria ya mgombea binafsi ndiyo pekee itakayotusaidia kuondokana na tatizo hili la vyama.
 
Kaka Kibinango, wenzako CHADEMA hawaoti ndoto za mchana bali wana mikakati na taratibu mafanikio ya utekelezaji wa mikakati yao unaonyesha mafanikio. Bandiko hili tu ni moja ya mifano ya mikakati bora ya CHADEMA. Nani alifikiria ama ameona chama chochote katika historia ya Tanzania baada ya TANU kikitoa mapitio kama haya katika siku ya mwaka mpya. Vilevile ni chama gani ama washabiki/wafuasi/ wanachama wa chama gani katika nchi yetu ambao wamewahi kuanzisha mijadala/mapitio kama haya yenye kulenga kujua mawazo ya watanzania kuhusu maendeleo ya chama chao kama wafanyavyo hawa jamaa wa CHADEMA.

Ndugu yangu kwa kuwa wewe ni mzanzibari na katika znz ur either with CCM ama against CCM translating to CUF, ni bora ukajiuliza ?
1. Hivi CCM na CUF wamefanya nini hata kuita mafanikio tangia mwaka 2005 ?
2. Je kati ya CCM, CUF ama CHADEMA ni chama gani kimeonyesha muelekeo wa kukua Kiasasi, Kisera ama Kiajenda tangia baada ya uchaguzi wa 2005 ?
3. Je ni chama gani kati ya CCM, CUF na CHADEMA kimeweza kuanzisha na kusimamia ajenda yoyite na ikawa ajenda ya kitaifa na ikawa na mvuto kwa watanzania walio wengi tangia uchaguzi wa 2005 ?

Tanzanianjema
Kwa madudu waliyofanya Mbeya vijijini(ambayo wamefanya mwaka huohuo wa 2008) inakuwa ngumu kwangu kuunga mkono kuwa CHADEMA ni chama bora kwa mwaka 2008,wameonesha ni jinsi gani viongozi wao(ambao ndo injini ya chama) wasivyo makini...Halafu ikumbukwe kuwa ndani ya JF kuna members ambao ni wanachama wa CCM,CHADEMA,CUF,SAU,DP,NCCR nk(pia kuna members ambao si wanachama bali wanavutiwa na sera za mojawapo kati ya vyama hivyo) na kwa hali hii mjadala huu nategemea utakuwa mrefu mno jamani,kama CHADEMA ni chama bora ama la ni jukumu la wananchi kuamua na si kuleta suala hili hapa la nini kimefanywa na CHADEMA kwa mwaka 2008,hii inanikumbusha ule msemo wa 'mwamba ngoma huvutia kwake(ingawa ndani ya JF 'we dare to talk openly'),so tuachane na mambo ya kukipigia debe(ndani ya JF) chama chochote kwamba kimefanya vizuri kwa mwakwa 2008,tuwachie watanzania waamue wenyewe kwa kuangalia nini kimefanywa na chama kipi then hapo mtu mwenyewe kwa utashi wake ndo atajua kipi ni chama bora kwake kwa mwaka 2008...Mbarikiwe sana
 
Kwa madudu waliyofanya Mbeya vijijini(ambayo wamefanya mwaka huohuo wa 2008) inakuwa ngumu kwangu kuunga mkono kuwa CHADEMA ni chama bora kwa mwaka 2008,wameonesha ni jinsi gani viongozi wao(ambao ndo injini ya chama) wasivyo makini...Halafu ikumbukwe kuwa ndani ya JF kuna members ambao ni wanachama wa CCM,CHADEMA,CUF,SAU,DP,NCCR nk(pia kuna members ambao si wanachama bali wanavutiwa na sera za mojawapo kati ya vyama hivyo) na kwa hali hii mjadala huu nategemea utakuwa mrefu mno jamani,kama CHADEMA ni chama bora ama la ni jukumu la wananchi kuamua na si kuleta suala hili hapa la nini kimefanywa na CHADEMA kwa mwaka 2008,hii inanikumbusha ule msemo wa 'mwamba ngoma huvutia kwake(ingawa ndani ya JF 'we dare to talk openly'),so tuachane na mambo ya kukipigia debe(ndani ya JF) chama chochote kwamba kimefanya vizuri kwa mwakwa 2008,tuwachie watanzania waamue wenyewe kwa kuangalia nini kimefanywa na chama kipi then hapo mtu mwenyewe kwa utashi wake ndo atajua kipi ni chama bora kwake kwa mwaka 2008...Mbarikiwe sana

- Mkuu Tanzanianjema, naona kabla sikaujibu hapa Mkulu Balatanda, ameniwahi na kukupa darasa zito sana, kwamba tuache uyanga na simba maana taifa linadidimia hata ubingwa wa EAC tu unatushinda lakini tunalilia yanga ohhh simba,

- CCM ooha Chadema, taifa linakwenda chini mkuu kuna hoja muhimu za taifa sasa hivi badala ya hizi nyepesi nyepesi!, hivi umesikia kwua kuna wanafunzi wengi wamepasi primary lakini hawana shule za kwenda form one?
 
MFES,
CCM ooha Chadema, taifa linakwenda chini mkuu kuna hoja muhimu za taifa sasa hivi badala ya hizi nyepesi nyepesi!, hivi umesikia kwua kuna wanafunzi wengi wamepasi primary lakini hawana shule za kwenda form one?
Mkuu haya ndiyo maneno na ndio sababu hasa nikitazama madudu kama haya nasema CCM mwaka 2008 haikufanya kitu kwani ni sera zao ndizo zimeshindwa kuangalia hayo..Sasa kwa mabaya yote ya CCM au vyama vingine hatuna haja ya kuorodhesha isipokuwa tunatumia kumbukumbu zetu za mwaka huo kujaribu kuchanganua mazuri na chama gani kimetuonyesha mwamko mkubwa kwa maslahi ya Taifa..Kwa hiyo kipimo chetu kinazingatia maslahi ya Taifa zaidi ya matatizo ya chama kuweza kukipunguzia hadhi kwa kutazama maslahi ya Taifa nina hakika hata Popular vote kwa mwaka 2008 Chadema wanaweza kabisa kuchukua nafasi ya kwanza..

Nitarudia kusema hivi Kikwete kama rais ameyafanya mengi mazuri isipokuwa yote kayafanya kwa jina la taifa..kwani Ni huo huyo Kikwete anapovaa magwanda ya Kijani kama mwenyekiti ameweza kuwatetea viongozi wa chama chake aliowachisha maradaka serikalini..na vikao vyote vya NEC CCM wamewabeba mafisadi ambao wamebaki na maradaka ndani ya Chama CCM. Vita kubwa ya mwaka 2008 ilikuwa MAFISADI na Chadema walikuwa mstari wa mbele kusimamisha swala hili mbele iwe bungeni, magazetini, vikao na mikutanoni..CCM kama chama imeendelea kuwabeba wahusika nadhani ipo haja ya kusema CCM hawakusimamia maslahi ya Taifa..
 
Back
Top Bottom