CCM Kwanini mnataka Makamanda Edward Lowassa, Freeman Mbowe Na Frederick Sumaye Wajiuzulu Siasa?

Mkuu kilichozuiwa siyo mikutano ya siasa ila ni zile movement za nchi nzima,majimboni mnaruhusiwa kujiachia kwa raha zenu.Kuhusu hao wazee wetu wala hawatutishi,tunachotamani ni kuona upinzani ulio imara na kutoa matumaini kwa taifa,siyo njaa na kiu ya madaraka.
Ifike mahali mtu aone upinzani unaoweza kutawala na uliojiandaa kwa hilo siyo hizi habari za eti madaraka kwanza mengine yatajulikana mbele ya safari.Tumechoshwa na viongozi wala rushwa,wakwepa kodi,na wachumia tumbo.
NB,kumbuka ruzuku ni fedha za watanzania zifanye kile zinapaswa kufanya.

f600023cbd13ba2f09c77cd9fbc20338.jpg
ogopa nyumbu kushikwa pabaya
 
Hakika threads za kuwataka Makamanda wa Chadema kina Mbowe , Lowassa Na Sumaye Wajiuzulu zimeongezeka .Sielewi Kwa nini CCM inataka wajiuzulu.Binafsi najua ni Woga wa CCM Kwa Viongozi hao.Kuthibitisha hilo CCM imediriki kuzuia mikutano ya vyama vya siasa lakini CCM inafanya mikutano ya Hadhara.Maendeleo ya Nchi hii yamepatikana huku Chama/Vyama vikifanya mikutano ya hadhara lakini awamu hii inayowata kina Mbowe, Lowassa Na Sumaye waache Siasa inadai eti maendeleo hayapatikani kama kuna mikutano ya Vyama kumbe ni kuuogopa Upinzani.
Hebu tuletewe ambapo CCM wanataka hao''makamanda ''waache siasa,kwani bado wako CCM kwa kipi CCM iwaogope hao ambao walikuwa CCM wakakimbia baada ya kukosa madaraka na hawana cha maana hadi CCM iwahofie,isiwahofie walipokuwa nao waje leo wawahofie wakati wanacheza ligi ya mchangani?
 
Hakika threads za kuwataka Makamanda wa Chadema kina Mbowe , Lowassa Na Sumaye Wajiuzulu zimeongezeka .Sielewi Kwa nini CCM inataka wajiuzulu.Binafsi najua ni Woga wa CCM Kwa Viongozi hao.Kuthibitisha hilo CCM imediriki kuzuia mikutano ya vyama vya siasa lakini CCM inafanya mikutano ya Hadhara.Maendeleo ya Nchi hii yamepatikana huku Chama/Vyama vikifanya mikutano ya hadhara lakini awamu hii inayowata kina Mbowe, Lowassa Na Sumaye waache Siasa inadai eti maendeleo hayapatikani kama kuna mikutano ya Vyama kumbe ni kuuogopa Upinzani.
Angalau Leo umekiri maendeleo yamepatkana. Ile kauli ya ccm haijafamya kitu kwa miaka 50 umeifuta rasmi, ukiwa muongo jitahid usisahau
 
Back
Top Bottom