Bunge Lisilo Na Faida Kwa Watanzania Lijitafakari

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
17,838
44,793
Tukitaka kuwa wakweli kwa nafsi zetu, Bunge la Tanzania la sasa halina faida wala msaada kwa Watanzania. Nina hakika hata kama lisingekuwepo, hakuna ambacho kingebadilika. Hili ni Bunge ambalo chochote kinachopelekwa Bungeni na Serikali, lazima kitapitishwa kama kilivyo. Namna nyingine, tunaweza kusema ni Bunge la hasara. Wanakula kodi zetu lakini bila kuwa na msaada wowote. Hili ni Bunge kikaragosi cha Serikali. Na anayeupinga ukweli huu, basi atuwekee kumbukumbu hapa, ni jambo gani baya lilipelekwa na Serikali hii Bungeni, Bunge hili likalikataa au kulifanyia marekebisho makubwa ya msingi. Tuna mambo mabaya kabisa ama yaliyotendwa na Serikali au watendaji wa Serikali hii, yalipopelekwa Bungeni, yakaenda tu kupata muhuri wa Bunge:

1. MKATABA WA HOVYO WA IGA
Mkataba ule kwa mtu yeyote mwenye uelewa na mkweli, ni mkataba wa hovyo kabisa, kwa sababu ulikuwa unakiuka sheria za nchi, na ulikuwa unapora mamlaka ya nchi katika kuamua yale inayoyaona yana maslahi kwa Taifa. Taasisi mbalimbali, kuanzia chama cha wanasheria nchini, taasisi za dini, wasomi wabobezi, wote walilaani kwa sauti kubwa IGA ile ya hovyo, lakini Bunge liliusifia na kuupitisha kama ulivyo. Na lile kongwa bado nchi imelivaa kama maadui wa Taifa walivyokuwa wamepanga.

2. MABADILIKO YA SHERIA YA UCHAGUZI NA TUME YA UCHAGUZI
Ile sheria ni ya hovyo. Taasisi mbalimbali zilizotoa maoni, kuanzia taasisi za dini, vyama vya siasa, chama cha wanasheria nchini, n.k; wote walionesha sheria ile ni kiinimacho. Lakini Bunge liliipitisha hivyo hivyo. Yaani Rais anateua majaji, halafu majaji wanapendekeza wajumbe wa Tume ya Uchaguzi kwa Rais, halafu Rais anawateua wajumbe waliopendekezwa na watu aliowateua yeye. Hii ni kuwafanya watu wote hawana akili.

3. TAARIFA YA CAG ILIYOONESHA UFISADI MKUBWA.
Sote tunafahamu, kila mwaka kumepelekwa taarifa ya CAG inayoonesha ufisadi mkubwa ndani ya mamlaka za Serikali, lakini hakuna chochote ambacho Bunge lilifanya, tena kwa kiasi kikubwa, Spika akionesha kupinga kujadiliwa ufisadi huo mapema baada ya baadhi ya wabunge kutaka wawajadili mafisadi.

4. UFISADI WA KWENYE SUKARI
Mheshimiwa sana. Ndugu Mpina ameonesha kwa namna iliyo dhahiri kabisa, jinsi Bashe alivyotenda kinyume kabisa cha taratibu, kwa kinachoonekana kwaajili ya manufaa binafsi yake na aliowapa contracts, na amefanya hivyo kwa vielelezo vilivyo dhahiri kabisa, Lakini Spika na wabunge wake wasio na sifa ya kuitwa wabunge, waliishia kupiga tu kelele za kumshambulia bila ya kujibu hoja zake hata moja.

BUNGE KAMA HILI LINA FAIDA GANI? LINAMTUMIKIA NANI?
Bunge hili lipo kwaajili ya kulinda maslahi ya Taifa na umma au kuyaangamiza.

Bunge hili lisilo na msaada kwa Taifa, lijifunze kwa yanayotokea Kenya, watu wasiishi kwa kukariri, kuna siku yatawapata yanayowapata wabunge wa Kenye sasa hivi:














Mbunge Aliyeunga Mkono Ongezeko la Kodi, AAdhibiwa vikali na Waandamanaji.jpg


Waandamanaji wanakula chakula Kilichoandaliwa kwaajili ya aabunge.jpg


Waandamanaji waondoka na Siwa ya Bunge.jpg


Mabango ya waandamanji.jpg



Siku zote tunasema kuwa, Mwenye Hekima hujifunza Kutokana na Makosa Ya mwenzake. Lakini ukikosa hekima, akili na uelewa, yanayowatokea wenzako, unaamini ni ya kwao tu, hayawezi kukufikia wewe.

Haya yanayotokea sasa kwa nchi nyingi za Afrika, yakianzia West Africa, ni hatua tu za maendeleo za mwanadamu. Huko Ulaya na America yalitokea sana miaka ya 1960 mpaka 1970, na leo hakuna mtawala anayewaburuza bali watawala wanalazimika kufuata matakwa ya umma. Kwa bahati mbaya watawala wa Arika bado wamelala, na kwa kuwa hawataki kubadilika, watasombwa na mafuriko.

Kwa bahati mbaya Watanzania wamelala, maana ukiangalia kwa umakini, kwa hakika yanayofanywa na Bunge la Tanzania ni hovyo maradufu ya yale yanayofanywa na Bunge la Kenya. Fikiria hawa wabunge wa Tanzania wangekuwa Kenya, wangefanywa nini!!

Mpaka sasa:

1. Polisi wamezidiwa nguvu, wamekimbia, waandamanaji wamelichukua gari la polisi.
2. Kaunti zote za Kenya zimeandamana.
3. Watu wanne wameuawa kwa risasi za polisi.
4. Waandamanaji wamevunja milango ya Bunge na kuingia ndani.
5. Wamebeba siwa, wamevunja nembo ya Bunge, wameondoka na vazi la spika.
6. Wamechoma moto ofisi ya Gavana wa Nairobi.
7. Wamechoma moto supermarket ya mbunge aliyeunga mkono mswada.
8. Wamempiga vibaya mbunge aliyeunga mkono mswada, mlinzi wake akakimbilia kanisani.
9. Wamezingira ikulu ndogo ya Rais ya Nakuru.
10. Waandamanaji wanasema kuwa mamlaka ya Bunge yapo mikononi mwao kwa sasa.
11. Spika na wabunge wote wamekimbia, bila hata ya kuahirisha bunge kama kanuni zinavyotaka.
 
Wapo watu wanateseka sana na Afrika. Soma Mada.

Eti wanaionea huruma. Wanaitakia maendeleo.?

Sasa kwa sababu hawawezi kujichotea kama ilivyokuwa zamani. Wanaanza kuzichafua nchi za Afrika mashariki kama ilivyokuwa kule Tunisia, Egypt etc kwa kufanya Uchochezi.

Wanataka kuweka vibaraka wao?

...yakitokea haya machafuko kwetu Tanzania, na mimi nita andamana kwenda kuwatafuta wachochezi na kuchukua siwa Ufipa.

mbunge-aliyeunga-mkono-ongezeko-la-kodi-aadhibiwa-vikali-na-waandamanaji-jpg.3026327

☝🏿❌
ngeu hizi🙌🏾😂😂😂
 
Wapo watu wanateseka sana na Afrika. Soma Mada.

Eti wanaionea huruma. Wanaitakia maendeleo.?

Sasa kwa sababu hawawezi kujichotea kama ilivyokuwa zamani. Wanaanza kuzichafua nchi za Afrika mashariki kama ilivyokuwa kule Tunisia, Egypt etc kwa kufanya Uchochezi.

Wanataka kuweka vibaraka wao?

...yakitokea haya machafuko kwetu Tanzania, na mimi nita andamana kwenda kuwatafuta wachochezi na kuchukua siwa Ufipa.
Acha ujingaujinga. Unajichoresha.Upo nyuma ya wakati umeushika wowowo.
 
Wapo watu wanateseka sana na Afrika. Soma Mada.

Eti wanaionea huruma. Wanaitakia maendeleo.?

Sasa kwa sababu hawawezi kujichotea kama ilivyokuwa zamani. Wanaanza kuzichafua nchi za Afrika mashariki kama ilivyokuwa kule Tunisia, Egypt etc kwa kufanya Uchochezi.

Wanataka kuweka vibaraka wao?

...yakitokea haya machafuko kwetu Tanzania, na mimi nita andamana kwenda kuwatafuta wachochezi na kuchukua siwa Ufipa.

mbunge-aliyeunga-mkono-ongezeko-la-kodi-aadhibiwa-vikali-na-waandamanaji-jpg.3026327


ngeu hizi

Unapoonekana ni punguani ni pale unapoandika vitu ambavyo havipo.

Hiyo Siwa ya ufipa ndiyo kitu gani?
 
Wapo watu wanateseka sana na Afrika. Soma Mada.

Eti wanaionea huruma. Wanaitakia maendeleo.?

Sasa kwa sababu hawawezi kujichotea kama ilivyokuwa zamani. Wanaanza kuzichafua nchi za Afrika mashariki kama ilivyokuwa kule Tunisia, Egypt etc kwa kufanya Uchochezi.

Wanataka kuweka vibaraka wao?

...yakitokea haya machafuko kwetu Tanzania, na mimi nita andamana kwenda kuwatafuta wachochezi na kuchukua siwa Ufipa.

mbunge-aliyeunga-mkono-ongezeko-la-kodi-aadhibiwa-vikali-na-waandamanaji-jpg.3026327

☝🏿❌
ngeu hizi🙌🏾😂😂😂
Sasa Ufipa kuna Siwa, kama siyo upumbavu ni kitu gani sasa umeandika.
 
Kila Mara naandika hapa, kama ingekua tunafanya biashara, hiki kitengo Cha bunge tungeachana na hiyo biashara kabisa. Kukuangalia pesa tunapoteza Kwa bunge na tunachokipata, having uwiano kabisa. Ni zaidi ya hasara.

Bora tungekua na kikosi Cha watu walioajiriwa, wabobevu wa Sheria, utawala na kusimamia mipango. Hao ndio wawe na jukumu la kuishsuri, kusimamia na kupitia mambo ya kitaalam yanayohusu Sheria. Uwakilishi wa wananchi utapitia madiwani huko ngazi za wilaya, tawala za mikoa na kufikia hii tume.

Hawa jamaa wataomba kazi kulingana na sifa na watalipwa mishahara.

Tuachane na Hawa watu wasiokatwa hata makato ya kutuma 20k Kwa mitandao ya simu. Wanawakilisha maslahi yao zaidi na sio wananchi Tena.
 
Bunge letu limepoteza ile heshima ya kuitwa Bunge tukufu. Sasa hivi asilimia kubwa kama si yote, wanawaza hela afanye mambo yake na familia yake.

Hawezi kupinga chochote, kisicho na maslahi na wananchi. Yuko pale kwa aliyemuingiza Bungeni. Kuanzia spika mpaka huyo mbunge wa daraja la pili, viti maalum.

Leo hii hata wewe unayesoma hapa, ukiwa tu na connection, unaingia Bungeni. Watu wa hivi, ndiyo tuwategemee kwa fikra kubwa tunajidanganya.

Viti maalum VIFUTWE, wanawake sasa tunaweza kusimama na mwanaume, jimboni na kutangaza sera na kushinda. Hii viti maalum ni kirusi wao kila kitu ndiyo, hawana msaada.

Wao hawakatwi kodi, wana hasara gani kupitisha kila kitu, kinachomkandamiza mwananchi. Bunge hili, ni kufuga wavivu, wanalipwa bure, wananenepeana hovyo. Tunataka Bunge lenye tija si hili la kupeana kama zawadi.
 
Hatushangai sana kwa uduni wa Bunge la sasa.

Bunge hili la sasa, halina faida yoyote kwa yeyote,

Bunge bandia

Hili Bunge la sasa, uwezo wake unaishia kujadili vitu vidogo vidogo visivyo na tija wala faida kubwa kwa nchi na kwa wananchi

Je, ni halali wahalifu wa kupora haki za wananchi za kuwachagua wawakilishi wao kupitia boksi la kura, kufanya maamuzi juu ya rasilimali za Taifa?

Mwizi haachi asili yake. Hawa waliopo bungeni ni majizi ya haki za wananchi. Mtu mwizi tangu lini akafanya maamuzi ya kuzuia mali zisiibiwe. Mwizi anachotafuta ni faida binafsi.

Hawana uchungu wowote kwa sababu asili yao ni kuiba,

Hawa wabunge wevi wa haki za wananchi za kuwapata wawakilishi wao, ambao wameendeleza uovu wao kama vile tuhuma za rushwa dhidi yao zilivyo, wakatuingiza kwenye mkataba fedhuli, tuwafanye nini
Tanzania sio ya Vibaraka wa mabeberu, na masaliti kama ilivyo CHADEMA
 
Hakika nakubaliana nawe. CCM ina utajiri mkubwa sana wa watu wapumbavu, wajinga, wanafiki, mafisadi na watu waongo waliojaa hadaa na wasio na uzalendo kwa Taifa hata chembe.
Kama ilivyo CHADEMA. Imejaa vibaraka wa mabeberu, masaliti, waasi, magaidi, wauaji, wachochezi na waongo.

Wewe mwenyewe ni mamluki na ni mkoloni tu anayejinasibu Utanzania. Mpuuzi tu anayetawaliwa na fikra na mawazo ya Mkoloni.
 
Back
Top Bottom