Bunge la Marekani laidhinisha kitita cha $ billion 60 kwa Ukraine

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
38,269
47,492
Baada ya mkwamo wa muda mrefu uliochangiwa na baadhi ya wabunge wa Marekani wenye mahaba na Putin hatimaye bunge la Marekani limepitisha kifurushi kipya cha $billion 60 kwa vita vya Ukraine.

Msaada huu mpya kwa Ukraine unajiri baada ya mwaka mmoja na nusu tangu bunge lililokuwa likiongozwa na Democrats kupitisha msaada kwa vita vya Ukraine.

Ushindi wa Republicans mwaka jana katika bunge la Marekani uliweka mkwamo wa zaidi ya mwaka mmoja na nusu kwa Ukraine kupata msaada kutoka Marekani.

Hata hivyo spika mpya wa bunge la Marekani ameamua kuwapuuza wabunge wachache wa MAGA lakini wenye sauti kubwa ndani ya chama cha Republicans waliosababisha mkwamo huo na kuamua kupeleka miswada mitatu ya usalama katika bunge iliyopewa jina la "21st Century Peace through Strength Act" ambayo imepitishwa kwa wingi wa kura.
 
TikTok imeambiwa ihamie Marekani vinginevyo inafungiwa milele.

Pentagon wamesema wanasubiri tu Senate na Rais wakimaliza tu ndani ya siku 3 Ukraine anapata kila kitu
Tatizo la Ukraine si upungufu wa silaha tu bali pia ina upungufu mkubwa sana wa wapiganaji na ufisadi ndani ya jeshi lake ,japo nchi za Magharibi zinajaribu kuyafumbia macho.
Mwaka jana Ukraine na washirika wake walitumia zaidi ya $ 35bilion kuandaa Offenseve lakini ilifeli vibaya ndani ya miezi miwili tu na silaha nyinyi ziliharibiwa.
Na mbaya zaidi sasa hivi kila silaha ya kimagharibi ya ardhini inayo aminika kuwa ni bora imesha pekekwa nchini Ukraine na kufeli.
Zaidi zaidi watakao faidika ni makampuni ya kutengeneza silaha na wanasiasa mafisadi ndani ya Ukraine basi.
 
Lakini Ukraine wameshapoteza maeneo mengi sana mpaka sasa.
Lengo la Marekani ni Ukraine kutoangukia mikononi mwa Russia na kumzuia Putin kuhamasika kuvamia nchi ya NATO baada ya Ukraine.
 
Back
Top Bottom