Blockchain; Mfumo uliokuja kuvuruga mifumo ya kibenki na ndio kisa hupigwa vita (decentalized system)

UBILUKO

Member
Sep 30, 2018
94
192
HELLO GUYS!
Baada ya kusubiri muda mrefu kidogo tukisubiri tuweze kuongezeka napenda kuwakumbusha kuwa hapa ni sehemu salama zaidi na mafunzo yote yatatolewa bure bila malipo yoyote na tutajitahidi kila siku kuleta angalau somo moja ili kufikia malengo ya kila mmoja kuweza kuelewa nini maana ya cryptocurrency,metaverse na nft. Mambo yote haya tutajifunza kwa lugha ya kiswahili na muda ukifika Basi tutakuwa na uwezo wa kujibu maswali ya kila mmoja kutoka na maswali ndani ya mada au nje ya mada yanayohusu cryptocurrency metaverse na nft


Kabla ya yote nipende kukiri kuwa humu ndani tumetofautiana level yaani Kuna watu ambao hawajui chochote ,wapo ambao wamefikia level fulani ( intermediate) na wapo ambao tayari wanaufahamu na wanafanya hii biashara bila shida yoyote hivyo sisi Kama mahosters wa haya masomo tunawakaribisha wote katika mijadala yote itakayoendelea hapa kwa kusaidiana ili angalau kila mtu awe na uelewa wa haya mambo

Na masomo yataanza mwanzo kabisa kwa kufundisha vitu vyote vya awali ambavyo mtu atatakiwa kuvijua kabla hajaingia moja kwa moja kwenye biashara hii ya cryptocurrency metaverse na nft na hatimaye hatua kwa hatua namna ambavyo anaweza kujiingiza katika biashara hii


Pia sisi Kama wawezeshaji wa mijadala hii hatujakamiliaka hivyo Kuna sehemu huenda hatutagusia either kwa kutokujua au kwa kusahau hivyo mtu yeyote atakayeona Kuna kitu ambacho anaweza kukiongezea katika mada zetu anaruhusiwa kuongezea kwa utaratibu wowote atakao ona unafaa na watu wa humu ndani wataweza kumuelewa

Kwa leo tutaanza na maana ya neno BLOCKCHAIN:

Je, BLOCKCHAIN ni nini?


Watu wengi wamekuwa wakisema kuwa BLOCKCHAIN ni sawa na Bitcoin kitu ambacho sio sahihi ! Yaani ni sawa na mtu aseme kuwa noti ya shilingi 10000 ni sawa na mtandao wa tigo,au Airtel au voda na vitu kama bank Western Union PayPal n.k kwa vyovyote atakuwa si sahihi kwa maana noti ya 10000 ni currency na hizo tigopesa, PayPal,bank ni njia za kutuma na kupokelea pesa hivyo Basi unavosema Bitcoin sio sawa na BLOCKCHAIN

Je, BLOCKCHAIN ni nini na Bitcoin ni nini?

BLOCKCHAIN ni njia/mfumo wa kutuma , kupokelea,kutunza taarifa mbalimbali yaweza kuwa ni taarifa za kifedha kwa maana ya miamala au taarifa za mikataba n.k

BLOCKCHAIN nikizungumzia upande wa transaction (miamala) Basi ni njia ya kupokea au kutuma pesa kidigital yaani mwanzo tulikuwa tukituma pesa au kufanya muamala ndani ya nchi au nje ya nchi kwa kutumia mifumo mbalimbali Kama vile bank,na pia ili mtu unayemtumia hizi pesa aweze kupokea lazima mtu Kati awepo yaani unatuma pesa inapitia mahali fulani wanaikagua then wanakata ada(fee) yao ndo wanaipeleka kwa muhusika na inaweza kuchukua siku tatu Hadi wiki kadhaa ili kumfikia mlengwa hasa Kama unatuma nje ya nchi,

So BLOCKCHAIN ilichokuja kufanya ni kufuta third part mfano bank na pesa itamfikia mlengwa direct bila kupita kwa mtu Kati hivyo kusaidia uharaka wa miamala yaani muamala ndani ya dak 1 uneshamfikia mlengwa popote pale alipo duniani, na faida nyingine ni kuwa fee(ada) ni ndogo yaani unaweza kutuma tzs 1 billion kwa ada ya tsh 3000 tu au pungufu lakini pia hii BLOCKCHAIN inasaidia Sana katika uwazi na kuepusha mtu kuibiwa au kupoteza pesa zake maana kila kitu kutakuwa recorded na hakuna mtu anaweza kufoji muamala maana pesa itaonekana imetoka block gani kwenda block ipi kwa mfumo wa chain .

Sasa Kuna kitu gani kinatumwa humo kwenye BLOCKCHAIN?

Hapa ndo tunakuja kuisikia Bitcoin lakini Bitcoin sio sarafu pekee inayotumia mfumo huu Kuna sarafu(cryptocurrency) nyingi sana lakini Bitcoin ndo imejulikana Sana kwa sababu ya umaarufu wake yaani ni sawa na us dollar ya kimarekani mtu anaweza hisi ni kitu Cha tofauti kumbe dola ya kimarekani ni sawa tu na ilivyo Tanzania shillings,kwacha ya Malawi n.k lakini Dolla imekuwa maarufu sana kutokana na value yake Hali kadharika kwenye Bitcoin nayo imekuwa maarufu sana kutokana na value yake au popularity yake kuwa watu wengi wanaijua na wamejaribu kuitumia maeneo kadha wa kadha lakini Kuna lundo la sarafu (cryptocurrency) ambazo zote hizi hutumia mfumo huu wa BLOCKCHAIN katika kutuma na kupokea

miamala yake baadhi yake ni
Etherium
Solana
Bitcoin cash
Litecoin
Ripple
Binance coin
Stella
Avax
Usdt
Algo
Dogecoin
Shiba Inu
Matic
Mana n.k n.k hizi coin pia unaweza kuziona kupitia coinmarketcap ambapo utakuta zaidi ya coin 10000+ na zote hutumia mfumo wa BLOCKCHAIN katika kutuma na kupokea hio miamala

Nadhani kwa ufupi leo umeweza kuelewa maana ya BLOCKCHAIN na tofauti iliyopo na Bitcoin nakaribisha maswali na michango



Ahsante na jioni njema
 
Nimemkumbuka yule tapeli Ontario aliyekuja na mada hapa JF ikiandikwa

Forex: Biashara Yenye Utajiri Mkubwa Zaidi Duniani Ambayo Hakuna Benki Itataka Uijue.​


Kilichofuata Ni kilio Cha Mbwa mwizi
 
Nimemkumbuka yule tapeli Ontario aliyekuja na mada hapa JF ikiandikwa

Forex: Biashara Yenye Utajiri Mkubwa Zaidi Duniani Ambayo Hakuna Benki Itataka Uijue.​


Kilichofuata Ni kilio Cha Mbwa mwizi
Huyu Ontario ni Master, ana yule mwenzake mwingine nimemsahau jina, hawa wamezaliwa Tanzania kabla muda wao.
 
hata mashirika ya posta yaliweka bajeti kupinga mfumo wa barua pepe.

benki wanacho kasirika pale account ya mtu hipo kwenye server.alafu unaweza kwenda nchi yoyote na kutoa pesa bila kuamisha sijui benki hii kwenda hii.
tatu kutumiana pesa hakuna makato na hiki ndiko kinawachanganya.
 
HELLO GUYS!
Baada ya kusubiri muda mrefu kidogo tukisubiri tuweze kuongezeka napenda kuwakumbusha kuwa hapa ni sehemu salama zaidi na mafunzo yote yatatolewa bure bila malipo yoyote na tutajitahidi kila siku kuleta angalau somo moja ili kufikia malengo ya kila mmoja kuweza kuelewa nini maana ya cryptocurrency,metaverse na nft. Mambo yote haya tutajifunza kwa lugha ya kiswahili na muda ukifika Basi tutakuwa na uwezo wa kujibu maswali ya kila mmoja kutoka na maswali ndani ya mada au nje ya mada yanayohusu cryptocurrency metaverse na nft


Kabla ya yote nipende kukiri kuwa humu ndani tumetofautiana level yaani Kuna watu ambao hawajui chochote ,wapo ambao wamefikia level fulani ( intermediate) na wapo ambao tayari wanaufahamu na wanafanya hii biashara bila shida yoyote hivyo sisi Kama mahosters wa haya masomo tunawakaribisha wote katika mijadala yote itakayoendelea hapa kwa kusaidiana ili angalau kila mtu awe na uelewa wa haya mambo

Na masomo yataanza mwanzo kabisa kwa kufundisha vitu vyote vya awali ambavyo mtu atatakiwa kuvijua kabla hajaingia moja kwa moja kwenye biashara hii ya cryptocurrency metaverse na nft na hatimaye hatua kwa hatua namna ambavyo anaweza kujiingiza katika biashara hii


Pia sisi Kama wawezeshaji wa mijadala hii hatujakamiliaka hivyo Kuna sehemu huenda hatutagusia either kwa kutokujua au kwa kusahau hivyo mtu yeyote atakayeona Kuna kitu ambacho anaweza kukiongezea katika mada zetu anaruhusiwa kuongezea kwa utaratibu wowote atakao ona unafaa na watu wa humu ndani wataweza kumuelewa

Kwa leo tutaanza na maana ya neno BLOCKCHAIN:

Je, BLOCKCHAIN ni nini?


Watu wengi wamekuwa wakisema kuwa BLOCKCHAIN ni sawa na Bitcoin kitu ambacho sio sahihi ! Yaani ni sawa na mtu aseme kuwa noti ya shilingi 10000 ni sawa na mtandao wa tigo,au Airtel au voda na vitu kama bank Western Union PayPal n.k kwa vyovyote atakuwa si sahihi kwa maana noti ya 10000 ni currency na hizo tigopesa, PayPal,bank ni njia za kutuma na kupokelea pesa hivyo Basi unavosema Bitcoin sio sawa na BLOCKCHAIN

Je, BLOCKCHAIN ni nini na Bitcoin ni nini?

BLOCKCHAIN ni njia/mfumo wa kutuma , kupokelea,kutunza taarifa mbalimbali yaweza kuwa ni taarifa za kifedha kwa maana ya miamala au taarifa za mikataba n.k

BLOCKCHAIN nikizungumzia upande wa transaction (miamala) Basi ni njia ya kupokea au kutuma pesa kidigital yaani mwanzo tulikuwa tukituma pesa au kufanya muamala ndani ya nchi au nje ya nchi kwa kutumia mifumo mbalimbali Kama vile bank,na pia ili mtu unayemtumia hizi pesa aweze kupokea lazima mtu Kati awepo yaani unatuma pesa inapitia mahali fulani wanaikagua then wanakata ada(fee) yao ndo wanaipeleka kwa muhusika na inaweza kuchukua siku tatu Hadi wiki kadhaa ili kumfikia mlengwa hasa Kama unatuma nje ya nchi,

So BLOCKCHAIN ilichokuja kufanya ni kufuta third part mfano bank na pesa itamfikia mlengwa direct bila kupita kwa mtu Kati hivyo kusaidia uharaka wa miamala yaani muamala ndani ya dak 1 uneshamfikia mlengwa popote pale alipo duniani, na faida nyingine ni kuwa fee(ada) ni ndogo yaani unaweza kutuma tzs 1 billion kwa ada ya tsh 3000 tu au pungufu lakini pia hii BLOCKCHAIN inasaidia Sana katika uwazi na kuepusha mtu kuibiwa au kupoteza pesa zake maana kila kitu kutakuwa recorded na hakuna mtu anaweza kufoji muamala maana pesa itaonekana imetoka block gani kwenda block ipi kwa mfumo wa chain .

Sasa Kuna kitu gani kinatumwa humo kwenye BLOCKCHAIN?

Hapa ndo tunakuja kuisikia Bitcoin lakini Bitcoin sio sarafu pekee inayotumia mfumo huu Kuna sarafu(cryptocurrency) nyingi sana lakini Bitcoin ndo imejulikana Sana kwa sababu ya umaarufu wake yaani ni sawa na us dollar ya kimarekani mtu anaweza hisi ni kitu Cha tofauti kumbe dola ya kimarekani ni sawa tu na ilivyo Tanzania shillings,kwacha ya Malawi n.k lakini Dolla imekuwa maarufu sana kutokana na value yake Hali kadharika kwenye Bitcoin nayo imekuwa maarufu sana kutokana na value yake au popularity yake kuwa watu wengi wanaijua na wamejaribu kuitumia maeneo kadha wa kadha lakini Kuna lundo la sarafu (cryptocurrency) ambazo zote hizi hutumia mfumo huu wa BLOCKCHAIN katika kutuma na kupokea

miamala yake baadhi yake ni
Etherium
Solana
Bitcoin cash
Litecoin
Ripple
Binance coin
Stella
Avax
Usdt
Algo
Dogecoin
Shiba Inu
Matic
Mana n.k n.k hizi coin pia unaweza kuziona kupitia coinmarketcap ambapo utakuta zaidi ya coin 10000+ na zote hutumia mfumo wa BLOCKCHAIN katika kutuma na kupokea hio miamala

Nadhani kwa ufupi leo umeweza kuelewa maana ya BLOCKCHAIN na tofauti iliyopo na Bitcoin nakaribisha maswali na michango



Ahsante na jioni njema
Mkuu endelea kutoa hiyo elimu watu waamke usikatishwe tamaa
 
Something is better than nothing. Assume bei ifike $1000 per coin bado 0.48 utaziona ndogo?
Achana na ndoto za alinacha wewe...

Unategemea RENEC ifikie thamani ya dollar elfu moja kimchezomchezo.

BNB yenyewe pamoja na kuwa strong mpaka leo bado inacheza kwenye $300.
 
Back
Top Bottom