Benki ya I & M yawapiga mkwara mzito wadeni wake, kusambaza picha na madeni yao kama wakopeshaji mtandaoni

Replica

JF-Expert Member
Aug 28, 2017
1,507
8,132
Labda wameona wakopeshaji mtandaoni wamefanikiwa kwenye 'mkakati' wao wa kudai madeni. Binadamu huwa hatupendi kudhalilishwa hivyo na benki ya I & M wameamua kutumia mkakati huo huo kwa kuwatangaza wote wenye madeni sugu.

Hivi sheria inaruhusu kuanika taarifa za mtu binafsi kwa umma ama hawa wakenya wamepotoka? Na mchakato wa kukopa benki naamini una taratibu zake tofauti na mikopo ya mtandaoni ikiwemo kuweka dhamana, kwanini wasipambane na kuuza hizo dhamana!

Mbona NMB na CRDB huwa wanakubali matokeo ikitokea mikopo chechefu;)

=======

"Benki inapenda kuwataarifu wadaiwa wake pia kuwa, kukaidi taarifa hii kutachukuliwa kama kuridhia benki kuchukua hatua za ziada ikiwemo kutangaza jina lako na picha, kiasi unachodaiwa na/au kuchukua hatua Zaidi za kisheria dhidi ya mdaiwa, na/au wadhamini wa mikopo ili kuweza kurudisha pesa ulizokopa.

Benki ya I&M Bank Tanzania limited haitahusika na athari zozote zitakazotokana na matangazo ya taarifa za wadaiwa watakaokaidi taarifa /tangazo hili".


Mwananchi gazette
 
Kalipe deni la I & M ili na wengine wakakope na tujenge uchumi wa Taifa. Kuileta hapa hii taarifa ni kutafuta sympathies za KIJINGA tu
 
Kalipe deni la I & M ili na wengine wakakope na tujenge uchumi wa Taifa. Kuileta hapa hii taarifa ni kutafuta sympathies za KIJINGA tu
Mimi ni wale tuliamua kufanya 'mobile wallets' kama benki na tusioamini kwenye mikopo yenye riba za kuruka katika kujiinua kimaisha. Tujadili hoja iliyo ubaoni badala ya kunijadili mleta hoja..:)
 
Labda wameona wakopeshaji mtandaoni wamefanikiwa kwenye 'mkakati' wao wa kudai madeni. Binadamu huwa hatupendi kudhalilishwa hivyo na benki ya I & M wameamua kutumia mkakati huo huo kwa kuwatangaza wote wenye madeni sugu.

Hivi sheria inaruhusu kuanika taarifa za mtu binafsi kwa umma ama hawa wakenya wamepotoka? Na mchakato wa kukopa benki naamini una taratibu zake tofauti na mikopo ya mtandaoni ikiwemo kuweka dhamana, kwanini wasipambane na kuuza hizo dhamana!

Mbona NMB na CRDB huwa wanakubali matokeo ikitokea mikopo chechefu;)

=======

"Benki inapenda kuwataarifu wadaiwa wake pia kuwa, kukaidi taarifa hii kutachukuliwa kama kuridhia benki kuchukua hatua za ziada ikiwemo kutangaza jina lako na picha, kiasi unachodaiwa na/au kuchukua hatua Zaidi za kisheria dhidi ya mdaiwa, na/au wadhamini wa mikopo ili kuweza kurudisha pesa ulizokopa.

Benki ya I&M Bank Tanzania limited haitahusika na athari zozote zitakazotokana na matangazo ya taarifa za wadaiwa watakaokaidi taarifa /tangazo hili".


Mwananchi gazette
Nawafikia vipi hawa na mimi nikope?
 
Filisi dhamana, kama umetapeliwa dhamana nenda mahakamani. Kusema namdai Tsh na hii ndo picha yake ni kutishia nyau panya.
 
Filisi dhamana, kama umetapeliwa dhamana nenda mahakamani. Kusema namdai Tsh na hii ndo picha yake ni kutishia nyau panya.
Hapa ndio waliponishangaza, wanaiga wenzao wa mitandaoni ilihali taratibu ni tofauti.. wenyewe wana dhamana wenzao hawana japo nao wanakosea kutumia taarifa za watu vibaya..
 
  • Thanks
Reactions: Tsh
Hapa ndio waliponishangaza, wanaiga wenzao wa mitandaoni ilihali taratibu ni tofauti.. wenyewe wana dhamana wenzao hawana japo nao wanakosea kutumia taarifa za watu vibaya..
Unless kwenye list ya wadaiwa kuna wanasiasa na watu maarufu ambao kuanikwa hadhari ni hasara kwa shughuli zao.
 
Mimi ni wale tuliamua kufanya 'mobile wallets' kama benki na tusioamini kwenye mikopo yenye riba za kuruka katika kujiinua kimaisha. Tujadili hoja iliyo ubaoni badala ya kunijadili mleta hoja..:)
Leta hapa terms zenu za mkopo kati ya I & M Bank na wewe tuzione! Otherwise utakuwa unapiga vigelegele tu hapa
 
Back
Top Bottom