Barua ya wazi kwa Sheikh Mziwanda na Dr. Sule: Acheni kutetea dhulma dhidi ya Watanzania wenzenu

Ukiipinga dola uwe sheikh uwe askofu basi wewe si mwenzetu.....
Hawa masheikh wamesahau kuwa:
1. Aliyesweka ndani masheikh wa Zanzibar ni rais muislamu, na mwenyekiti wa CCM wa wakati huo
2. Aliyewapa masheikh kesi za ugaidi huko Arusha ni rais muislamu, tena alikuwa mwenyekiti wa CCM
3. Aliyempiga risasi sheikh Ponda ikamjeruhi almanusra imtoe uhai ni rais muislamu, na alikuwa mwenyekiti wa CCM

Na aliyekuwa akipaza Sauti kuwatetea wote hawa ni CHADEMA. Hata kampeni za Urais za CHADEMA zilijikita katika kuwatetea hawa masheikh!
 
Ndugu Masheikh
Nimewajibika kuandika barua hii kuwaomba kwa unyenyekevu mkubwa ACHENI KUTETEA dhulma dhidi ya watanzania wenzenu ktk madhila yanayowakumba.

NIANZE NA SULE
Wakati wa sakata la Ngorongoro, Mwanamihadhara ndugu Sule aliandaa clip ambayo ilisambazwa katika makundi ya kijamii ikieleza kuwa wamasai waishio ngorongoro ni wakenya waliovamia maeneo hayo kutoka Kenya. Katika kauli hizo akajaribu kuwaaminisha watanzania kuwa hao wamasai walioko ngorngoro hawastahili kuonewa huruma pindi serikali ikijaribu kuwatoa kwa sababu ni Wakenya.
Kauli hii ilikuwa ni ya ajabu sana hasa ukizingatia kwanza ni uongo, maana wamasai walioko ngorongoro walihamishiwa hapo na serikali hiyohiyo ili kupisha uanzishwaji wa hifadhi ya Serengeti miaka ya 1960's. lakini ukiachilia mbali hilo ile ni kauli isiyo na chembe ya huruma kwa watanzania wenzetu waishio ngorongoro ambao, walikuwa wananyimwa kila aina ya haki za kiraia na utawala huu wa Samia ili kuwapa maisha magumu waondoke. Kusema uongo ni kinyume cha Agizo la Mwenyezi Mungu anayetaka watu waseme ukweli!
Hata hivyo ndugu Sule amekuwa akilalamikiwa na waislamu wenyewe kwa kulete mafundisho ambayo wao wanaita ni Shirki, kwa kutangaza pete za Majini kuwa eti zina msaada kwa watu kitu ambacho masheikh wenzie wamempnga vikali kuwa asilete SHIRKI katika dini.

KWA SHEIKH MZIWANDA
Ndugu Sheikh mziwanda, umesikika ukidai kuwa wanaotekana nchini ni CHADEMA wenyewe, na ukatoa mfano wa Clip ya Dr Slaa ya miaka takriban minne akizungumzia tukio la kutekana katika chama. Kinachonisikitisha unanasibisha matukio ya sasa kwa kusema kuwa ni CHADEMA wanafanyiana hayo.
Ndugu Mziwanda, Muogope ALLAH, Tafadhali sana ndugu yangu, Wewe mwenyewe umesema una listi ya watu zaidi ya 100 waliotekwa kipindi cha Magufuli, Je Ndugu mziwanda hao wote walitekwa na CHADEMA?- Mo Dewji alitekwa na CHADEMA?,Roma mkatoliki alitekwa na CHADEMA?, Azory Gwanda alipotezwa na CHADEMA?

Kwenye kauli yako ukasikika unasema kuwa kipindi cha Magufuli walipotea zaidi ya watu 100, ukahoji kuwa mbona hakukuwa na maandamano?- Kwa hiyo ndugu Mziwanda, unataka kutwambia kuwa kwa kuwa watu hawakuandamana kudai jambo fulani kipindi cha nyuma basi ni makosa watu hao kuandamana kutaka jambo fulani leo hata kesho?. Sisi tunapata mashaka ndugu Mziwanda kuwa unataka kuchomeka hisia za udini, unataka watu waone kuwa kwa kuwa mtawala wa sasa ni muislamu basi kila dai lolote la msingi ambalo raia wa nchi hii wanalo basi eti wanaweka presha kwa sababu rais ni muislamu. NDugu mziwanda hiki unachokifanya ni kibya mno, si chema na kwa kweli kinagawa watu kuliko kujenga!

MZIWANDA, wewe hujitokeza mara nyingi wananchi wanapokuwa na ishu na serikali yao, wewe husimama kuitetea serikali tena kwa kuwagawa waislamu wajitenge na madai ya msingi ya kitaifa. Ulifanya hivyo katika mimbari kutetea uuzwaji wa bandari, ukadai kuwa mama anashambuliwa kwa imani yake.
Leo Umma unataka kutumia haki zao za kikatiba kuandamana ili mauaji na utekwaji vikomeshwe, wewe unakuja na kuongea na waislamu eti wajitenge na mambo hayo. SHEIKH HIVI UNASIMAMIA HAKI AU UNAWALINDA WATAWALA?

Sheikh: Kwani mtume si alisema ukiona jambo baya/ovu liondoe kwa mkono wako, ukishindwa kemea uovu huo, na kama kukemea huwezi si mtume alisema chukia?- SASA WEWE unasimamia wapi katika hayo matatu kuhusiana na matendo ya kutekwa, kupotezwa na kuuawa watu?. Je hutaki watu waingie mitaani kukemea uovu huo unataka wafanyeje?. Umesema kuwa wakati wa Magufuli walipotea watu zaidi ya 100, LINI WEWE UMEWAHI KUKEMEA JAMBO HILO WAZIWAZI UMMA UKAKUSIKIA?

SHEIKH MZIWANDA SI KWA SABABU SAMIA NI MUISLAMU BASI UNAJARIBU KUMLINDA NA KUMKINGIA KIFUA KWA KILA KITU KIBAYA!.

Ndugu Mziwanda, Mwenyezi Mungu katika Qur'an anasema kuwa sema kweli hata kama ukweli huo "unakunyooshea kidole" wewe mwenyewe. Sasa kama mtu inabidi ujishuhudie ukweli hata kama ukweli huo uko dhidi yako kwa nini unamkingia Kifua Samia eti kwa sababu Samia ni muislamu mwenzako tu?.
Je umesahau Khalifa mmoja wa kiislamu amewahi kumpa haki Myahudi licha ya kuwa kuna shauri mbele yake lililetwa linalomhusu muislamu na myahudi. Kwa nini alimpa haki myahudi badala ya muislamu mwenzie?

NDUGU MZIWANDA: Umekuwa ukijaribu kuwatenga waislamu wasiungane na watanzania wenzao kwa hoja za :
1. Amani,
2. "Mbona wakati wa magufuli haikuwa hivi?"

Ningependa kukwambia tu kuwa wanaotekwa, kupotezwa na kuuawa siyo wakiristu tu bali hata waislamu pia. Mo Dewji ni muislamu, Mzee Ally kibao ni muislamu. Sasa kwa nini hutaki waislamu waungane na waislamu wenzao kupaza sauti kukataa udhalimu huu?

SHEIKH MZIWANDA: Napenda nikukumbushe tu kuwa ukizuia WENGI KUDAI HAKI basi mtu mmoja mmoja kwa siri au kwa dhahiri ataamua kuidai peke yake, Je unajua kitakachotokea pale mtu mmoja bila kushawishiwa na mwingine, au kwa kumshirikisha mwingine ataamua kulipa kisasi?.

SHEIKH tafadhali tetea haki ya watu, usitetee "ULUA" wa watawala!
Mziwanda Hovyo kabisa, anajipendekeza kwa Raisi kwa mgongo wa UDINI, Yeye kwake Samia hana baya!!!
 
Ndugu Masheikh
Nimewajibika kuandika barua hii kuwaomba kwa unyenyekevu mkubwa ACHENI KUTETEA dhulma dhidi ya watanzania wenzenu ktk madhila yanayowakumba.

NIANZE NA SULE
Wakati wa sakata la Ngorongoro, Mwanamihadhara ndugu Sule aliandaa clip ambayo ilisambazwa katika makundi ya kijamii ikieleza kuwa wamasai waishio ngorongoro ni wakenya waliovamia maeneo hayo kutoka Kenya. Katika kauli hizo akajaribu kuwaaminisha watanzania kuwa hao wamasai walioko ngorngoro hawastahili kuonewa huruma pindi serikali ikijaribu kuwatoa kwa sababu ni Wakenya.
Kauli hii ilikuwa ni ya ajabu sana hasa ukizingatia kwanza ni uongo, maana wamasai walioko ngorongoro walihamishiwa hapo na serikali hiyohiyo ili kupisha uanzishwaji wa hifadhi ya Serengeti miaka ya 1960's. lakini ukiachilia mbali hilo ile ni kauli isiyo na chembe ya huruma kwa watanzania wenzetu waishio ngorongoro ambao, walikuwa wananyimwa kila aina ya haki za kiraia na utawala huu wa Samia ili kuwapa maisha magumu waondoke. Kusema uongo ni kinyume cha Agizo la Mwenyezi Mungu anayetaka watu waseme ukweli!
Hata hivyo ndugu Sule amekuwa akilalamikiwa na waislamu wenyewe kwa kulete mafundisho ambayo wao wanaita ni Shirki, kwa kutangaza pete za Majini kuwa eti zina msaada kwa watu kitu ambacho masheikh wenzie wamempnga vikali kuwa asilete SHIRKI katika dini.

KWA SHEIKH MZIWANDA
Ndugu Sheikh mziwanda, umesikika ukidai kuwa wanaotekana nchini ni CHADEMA wenyewe, na ukatoa mfano wa Clip ya Dr Slaa ya miaka takriban minne akizungumzia tukio la kutekana katika chama. Kinachonisikitisha unanasibisha matukio ya sasa kwa kusema kuwa ni CHADEMA wanafanyiana hayo.
Ndugu Mziwanda, Muogope ALLAH, Tafadhali sana ndugu yangu, Wewe mwenyewe umesema una listi ya watu zaidi ya 100 waliotekwa kipindi cha Magufuli, Je Ndugu mziwanda hao wote walitekwa na CHADEMA?- Mo Dewji alitekwa na CHADEMA?,Roma mkatoliki alitekwa na CHADEMA?, Azory Gwanda alipotezwa na CHADEMA?

Kwenye kauli yako ukasikika unasema kuwa kipindi cha Magufuli walipotea zaidi ya watu 100, ukahoji kuwa mbona hakukuwa na maandamano?- Kwa hiyo ndugu Mziwanda, unataka kutwambia kuwa kwa kuwa watu hawakuandamana kudai jambo fulani kipindi cha nyuma basi ni makosa watu hao kuandamana kutaka jambo fulani leo hata kesho?. Sisi tunapata mashaka ndugu Mziwanda kuwa unataka kuchomeka hisia za udini, unataka watu waone kuwa kwa kuwa mtawala wa sasa ni muislamu basi kila dai lolote la msingi ambalo raia wa nchi hii wanalo basi eti wanaweka presha kwa sababu rais ni muislamu. NDugu mziwanda hiki unachokifanya ni kibya mno, si chema na kwa kweli kinagawa watu kuliko kujenga!

MZIWANDA, wewe hujitokeza mara nyingi wananchi wanapokuwa na ishu na serikali yao, wewe husimama kuitetea serikali tena kwa kuwagawa waislamu wajitenge na madai ya msingi ya kitaifa. Ulifanya hivyo katika mimbari kutetea uuzwaji wa bandari, ukadai kuwa mama anashambuliwa kwa imani yake.
Leo Umma unataka kutumia haki zao za kikatiba kuandamana ili mauaji na utekwaji vikomeshwe, wewe unakuja na kuongea na waislamu eti wajitenge na mambo hayo. SHEIKH HIVI UNASIMAMIA HAKI AU UNAWALINDA WATAWALA?

Sheikh: Kwani mtume si alisema ukiona jambo baya/ovu liondoe kwa mkono wako, ukishindwa kemea uovu huo, na kama kukemea huwezi si mtume alisema chukia?- SASA WEWE unasimamia wapi katika hayo matatu kuhusiana na matendo ya kutekwa, kupotezwa na kuuawa watu?. Je hutaki watu waingie mitaani kukemea uovu huo unataka wafanyeje?. Umesema kuwa wakati wa Magufuli walipotea watu zaidi ya 100, LINI WEWE UMEWAHI KUKEMEA JAMBO HILO WAZIWAZI UMMA UKAKUSIKIA?

SHEIKH MZIWANDA SI KWA SABABU SAMIA NI MUISLAMU BASI UNAJARIBU KUMLINDA NA KUMKINGIA KIFUA KWA KILA KITU KIBAYA!.

Ndugu Mziwanda, Mwenyezi Mungu katika Qur'an anasema kuwa sema kweli hata kama ukweli huo "unakunyooshea kidole" wewe mwenyewe. Sasa kama mtu inabidi ujishuhudie ukweli hata kama ukweli huo uko dhidi yako kwa nini unamkingia Kifua Samia eti kwa sababu Samia ni muislamu mwenzako tu?.
Je umesahau Khalifa mmoja wa kiislamu amewahi kumpa haki Myahudi licha ya kuwa kuna shauri mbele yake lililetwa linalomhusu muislamu na myahudi. Kwa nini alimpa haki myahudi badala ya muislamu mwenzie?

NDUGU MZIWANDA: Umekuwa ukijaribu kuwatenga waislamu wasiungane na watanzania wenzao kwa hoja za :
1. Amani,
2. "Mbona wakati wa magufuli haikuwa hivi?"

Ningependa kukwambia tu kuwa wanaotekwa, kupotezwa na kuuawa siyo wakiristu tu bali hata waislamu pia. Mo Dewji ni muislamu, Mzee Ally kibao ni muislamu. Sasa kwa nini hutaki waislamu waungane na waislamu wenzao kupaza sauti kukataa udhalimu huu?

SHEIKH MZIWANDA: Napenda nikukumbushe tu kuwa ukizuia WENGI KUDAI HAKI basi mtu mmoja mmoja kwa siri au kwa dhahiri ataamua kuidai peke yake, Je unajua kitakachotokea pale mtu mmoja bila kushawishiwa na mwingine, au kwa kumshirikisha mwingine ataamua kulipa kisasi?.

SHEIKH tafadhali tetea haki ya watu, usitetee k
Kuna sheikh na shehena. Hao uliowataja ni shehenas. Njaa si kitu kizuri
 
Mkuu umesahau,kwa Sinia moja la ubwabwa mashekh wanaweza kusaliti hata Imani yao???ukuwaona kanisani kwa Geordevie wakitoa ushuhuda???
 
Back
Top Bottom