Balozi Dkt. Kusiluka: Rais Samia anataka ufanisi wa Mashirika ya Nchini yawe na viwango vya kimataifa

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
3,452
13,070
f1ca70db-fe73-4c38-82c1-3011abbbfe8c.jpg
Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Kusiluka amesema ndoto ya Rais Samia Suluhu Hassan ni kuhakikisha nchi inakuwa na mashirika yenye ufanisi mkubwa na wa viwango vya kimataifa.

Hivyo, amewataka Wenyeviti wa Bodi na Watendaji Wakuu wa taasisi na Mashirika ya Umma kuhakikisha wanatekeleza kwa ukamilifu maagizo yaliyotolewa na Rais Samia.

Ametoa kauli hiyo Agosti 30, 2024 Jijini Arusha wakati akifunga kikao kazi cha viongozi hao kilichofanyika jijini humo tangu Agosti 27 hadi 30, 2024.
6254d9ee-083d-4098-9855-d41b9a930f5d.jpg

e5eb28db-e91e-4fd1-9836-5debbf57a3ee.jpg
“Serikali itayachukua maazimio yote yaliyokubaliwa na nawaahidi yatafanyiwa kazi, tutawasaidia kuhakikisha yanatekelezeka ili kutimiza ndoto ya Mhe. Rais Samia juu ya taasisi na mashirika ya umma,” amesema Balozi, Dkt. Kusiluka.

Amewataka viongozi wa taasisi na mashirika ya umma kujenga utamaduni wa kujifunza mbinu na mikakati mipya kutoka kwa mashirika yaliofanikiwa na kuitazama serikali kwa upana wake.

Naye, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Dkt. Tausi Mbaga Kida amesema wamewasilisha malengo na wanaamini watayasimamia malengo hayo ili kuweza kuhakikisha yale waliyojiwekea katika kusimamia na kuboresha utendaji kazi wa taasisi na mashirika ya umma yanaweza kufikiwa.
514ec4d9-0e2b-41f7-9f42-81d8b13b9e85.jpg
Kwa upande wake Msajili wa Hazina, Nehemiah Mchechu amesoma jumla ya maazimio sita yaliyoazimiwa na viongozi hao ikiwemo, Ushiriki katika Mpango wa Maendeleo wa Taifa 2050 na uandaaji wa mipango mkakati wa taasisi za umma; Utawala bora na mawasiliano ya umma pamoja na Usimamizi wa rasilimali watu, mafunzo na uendelezaji wa uongozi bora.

Maazimio mengini ni, Mikakati ya taasisi na mashirika ya umma kuwekeza nje ya Tanzania; Kuongeza uchangiaji na kupunguza utegemezi katika Mfuko Mkuu wa Taifa na kutekeleza kikamilifu maazimio yaliyotolewa kwenye kikao kilichopita ambayo hayajatekelezwa.

Akitoa neno la shukrani kwa niaba, Kamishna wa Bima Tanzania kutoka Mamlaka ya Usimamizi wa Bima Tanzania, Dkt. Baghayo Saqware amesema kuwa Wakuu wa Taasisi wamepokea maelekezo yote yaliyotolewa na viongozi na wanaahidi kuyatekeleza kwani wana hamu na mageuzi yanayotarajiwa.
 
Wanaongea tu bila vitendo. Mashirika kufanya vizuri yanahitaji mfumo mzuri wa serikali na sheria na haya yanahitaji katiba mpya inayoendana na wakati. Kwa mfumo wa sasa haitawezekana kwasababu mfumo wa sasa unaenda na matakwa ya mtu mmoja na sio mfumo
 
Back
Top Bottom