Vugu-Vugu
JF-Expert Member
- Feb 24, 2017
- 1,219
- 1,378
Baada ya Ndugu Paul Makonda kuwekwa kando kwasababu ama ya makosa yake ya kiufundi au mbinu za wapinzani wake ndani ya CCM.
Nini kimemngo'a Paul Makonda?
Kwanza, Style yake ya vita isiyokwisha na waliotazamwa kama wapinzani wa JPM ilikuwa inakipasua chama vipande vipande.
Pili, Style yake ya kukusanya kero bila kueleza mafanikio ya Serikali ilikuwa inamjenga zaidi yeye binafsi kwa gharama ya kupunguza umaarufu wa Serikali na hata Chama hili lingefaa zaidi endapo tu yeye angekuwa Mgombea wa CCM 2025.
Tatu, Uwezo mdogo wa kutetea mafanikio ya awamu ya 6 hasa kwa kushindwa kuitambua awamu yenyewe kulipunguza sifa muhimu kuweza kuendelea kuwa msemaji Mkuu wa Chama.
===
Sasa mjadala ni mwana CCM gani anastahili kubeba jukumu hili hasa wakati huu mgumu kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu na ule wa Oktoba 2025.
Nimeona majina kadhaa yanatajwa kama Mhe John Mongela, Mhe Ali Happi, Mhe Amos Makala,Mhe Anthony Mtaka,Mhe David Kafulila, Heri James na hata Ndugu Martin Shigella.
Hata hivyo, Wote hawa hawatajwi kwa sifa za kwanini wataijenga CCM kuhimili ushindani wa kisiasa au kukubalika hasa nje ya CCM bali wanaelezwa kwa namna walivyo na uswahiba au connections na baadhi ya wazee wenye ushawishi mkubwa ndani ya CCM.
Naomba nianze kwa kuchambua sifa za mwenezi anaetakiwa kwa sasa kisha nichambue mmoja baada ya mwingine katika hawa wanaotajwatajwa;
1. Mwenezi lazima awe na uwezo kutetea mafanikio ya serikali ya CCM kwa hoja na takwimu.
2. Mwenezi lazima awe na uwezo wa kumtetea Rais Samia Suluhu Hassan kwa hoja za msingi na sio mapambio na ngonjera.
3. Mwenezi lazma awe na uwezo unaoendana na upeo wa vinara wa upinzani kama akina Tundu Lissu, Zitto Kabwe, John Heche, John Mnyika katika kujenga hoja waziwazi hata kama ni midahalo.
4. Mwenezi hapaswi kuwa mtu anayetazamwa kama mfuasi wa kambi fulani ndani ya CCM ili wanachama na viongozi wote wamsikilize na wawe na amani kufanya nae kazi kwa umoja wa chama hasa kuelekea 2025.
5. Mwenezi lazima awe na upeo kuweza kumudu na kusikilizwa na jamii ya social media na wasomi ambayo kuna watu wamejijengea himaya zenye ufuasi mkubwa na ni Muhimili mkubwa wa upinzani kuliko hata vyama vya upinzani kama ilivyo kwa Maria Sarungi, Kigogo na wengine wengi.
6. Mwenezi lazima awe ni mtu ambae umma unaweza kumsikiliza kwa kuwa na hoja zenye uzito na asichokwe kwa hoja zilezile (Charisma )
7. Mwenezi lazma awe mtu ambae anaweza kuongea na viongozi wa Serikali waone wanaongea na mtu anaejua Serikali hivyo wampe heshima bila kumuogopa na akiongea na watalaamu asidharaulike kwa kuonekana anapiga porojo za siasa tu.
8. Kwakuwa 45% ya wapigakura wote Tanzania ni vijana mwenezi lazima awe ni kijana msomi na mwelevu na mtu anayeichukia rushwa kwa maneno na matendo yake.
Hapa chini nafanya ranking kwa hoja hizi 8 Kwa majina haya 10 kwa Leo ambayo nadhani kama yatazingatiwa tutapata Mwenezi ambaye Wakati unamwitaji.
1. Ali Hapi 67%
2. David Kafulila 77%
3. Amos Makala 65%
4. John Mongela 65%
5. Martin Shigela 66%
7. Heri James 70%
8. Antony Mtaka 71%
9. Albert Chalamila 69%
10. Joketi Mwegelo 58%
Kila lenye heri chama Cha Mapinduzi,
Mungu ibariki CCM.
Nini kimemngo'a Paul Makonda?
Kwanza, Style yake ya vita isiyokwisha na waliotazamwa kama wapinzani wa JPM ilikuwa inakipasua chama vipande vipande.
Pili, Style yake ya kukusanya kero bila kueleza mafanikio ya Serikali ilikuwa inamjenga zaidi yeye binafsi kwa gharama ya kupunguza umaarufu wa Serikali na hata Chama hili lingefaa zaidi endapo tu yeye angekuwa Mgombea wa CCM 2025.
Tatu, Uwezo mdogo wa kutetea mafanikio ya awamu ya 6 hasa kwa kushindwa kuitambua awamu yenyewe kulipunguza sifa muhimu kuweza kuendelea kuwa msemaji Mkuu wa Chama.
===
Sasa mjadala ni mwana CCM gani anastahili kubeba jukumu hili hasa wakati huu mgumu kuelekea uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu na ule wa Oktoba 2025.
Nimeona majina kadhaa yanatajwa kama Mhe John Mongela, Mhe Ali Happi, Mhe Amos Makala,Mhe Anthony Mtaka,Mhe David Kafulila, Heri James na hata Ndugu Martin Shigella.
Hata hivyo, Wote hawa hawatajwi kwa sifa za kwanini wataijenga CCM kuhimili ushindani wa kisiasa au kukubalika hasa nje ya CCM bali wanaelezwa kwa namna walivyo na uswahiba au connections na baadhi ya wazee wenye ushawishi mkubwa ndani ya CCM.
Naomba nianze kwa kuchambua sifa za mwenezi anaetakiwa kwa sasa kisha nichambue mmoja baada ya mwingine katika hawa wanaotajwatajwa;
1. Mwenezi lazima awe na uwezo kutetea mafanikio ya serikali ya CCM kwa hoja na takwimu.
2. Mwenezi lazima awe na uwezo wa kumtetea Rais Samia Suluhu Hassan kwa hoja za msingi na sio mapambio na ngonjera.
3. Mwenezi lazma awe na uwezo unaoendana na upeo wa vinara wa upinzani kama akina Tundu Lissu, Zitto Kabwe, John Heche, John Mnyika katika kujenga hoja waziwazi hata kama ni midahalo.
4. Mwenezi hapaswi kuwa mtu anayetazamwa kama mfuasi wa kambi fulani ndani ya CCM ili wanachama na viongozi wote wamsikilize na wawe na amani kufanya nae kazi kwa umoja wa chama hasa kuelekea 2025.
5. Mwenezi lazima awe na upeo kuweza kumudu na kusikilizwa na jamii ya social media na wasomi ambayo kuna watu wamejijengea himaya zenye ufuasi mkubwa na ni Muhimili mkubwa wa upinzani kuliko hata vyama vya upinzani kama ilivyo kwa Maria Sarungi, Kigogo na wengine wengi.
6. Mwenezi lazima awe ni mtu ambae umma unaweza kumsikiliza kwa kuwa na hoja zenye uzito na asichokwe kwa hoja zilezile (Charisma )
7. Mwenezi lazma awe mtu ambae anaweza kuongea na viongozi wa Serikali waone wanaongea na mtu anaejua Serikali hivyo wampe heshima bila kumuogopa na akiongea na watalaamu asidharaulike kwa kuonekana anapiga porojo za siasa tu.
8. Kwakuwa 45% ya wapigakura wote Tanzania ni vijana mwenezi lazima awe ni kijana msomi na mwelevu na mtu anayeichukia rushwa kwa maneno na matendo yake.
Hapa chini nafanya ranking kwa hoja hizi 8 Kwa majina haya 10 kwa Leo ambayo nadhani kama yatazingatiwa tutapata Mwenezi ambaye Wakati unamwitaji.
1. Ali Hapi 67%
2. David Kafulila 77%
3. Amos Makala 65%
4. John Mongela 65%
5. Martin Shigela 66%
7. Heri James 70%
8. Antony Mtaka 71%
9. Albert Chalamila 69%
10. Joketi Mwegelo 58%
Kila lenye heri chama Cha Mapinduzi,
Mungu ibariki CCM.