Aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Tabora mjini, Komanya Kitwala ahukumiwa kulipa fidia ya Tsh. milioni 80

Wajinga hao huyu kenge mi nilishafanya nae kazi akanidhulumu na hela yangu ni mpumbavu ,mjinga alipata nafasi ya kushauriwa akashupaza shingo.Imagine alishamweka ndani muuza chips kisa kamcheleshea kumuhudumia,alishawasweka ndani jamaa kisa birthday hizo ni case chache tu.Anavuna alichokipanda.
Duh, jamaa mbona alikua mtu WA hovyo
Alipataje hicho cheo mjinga huyu
 
MaDC wa Jiwe wameanza kuonja joto ya jiwe. Mahakama ya Hakimu Mkazi Tabora yatoa amri alipe milioni 80. Hizi Hela walipe wenyewe, sio serikali, serikali huwa haiwajibiki kwa mtu anayefanya jambo nje ya maelekezo ya kisheria
Screenshot_20221230-204922.jpg
 
Komanya Kitwala alikwenda nyumbani kwa mlalamikaji akiwa na Askari Polisi ambao aliwaamuru kumkamata na kumtesa, kisha kumuweka ndani katika Kituo Kikubwa cha Polisi Tabora mjini bila kuwa na kosa lolote, ambapo baadaye aliyekuwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora kwa wakati huo, ACP Safia Jongo aliagiza mlalamikaji Alexander Ntonge kuachiliwa huru kwa madai kulikuwa hakuna kosa lolote alilofanya.
Utanitambua mimi ni nani
 
Siku moja nilikutana naye Uhazili, nilipokuwa na majukumu maalum.

Alinikuta nahudumiwa kwa wakala pale nje. Nilikuwa naweka fedha kwenye simu.

Sasa kafika, kapitisha kono lake puup, ndani. Hela zangu zikamwagika. Kistaarabu, kulikoni brother? Kaniambia sogea watu wa Muhimu tuhudumiwe tuwahi kuihudumia jamii. Unanifahamu mimi nani?

Nilishikwa na hasira, nikachukua hela zake na kuzitoa nje. Nikasogeza na Million moja ikadondoka chini.

Bahati nzuri kwake, kijana huyo akatoka na kunituliza. Akachukua hela za Komanya na kwenda nazo ndani. Mimi nikahudumiwa na binti, nikamalizana.

Alisema atanitafuta. Nikamueleza namba yangu utachukua kwa huyu binti anayenihudumia.

Ukweli ni kuwa alinitafuta na alituma vijana wake wanifuate. Mh Sengati aliimaliza ishu kiutu uzima

Mpumbavu mno. Ana ubabe wa kipuuzi.
 
Siku moja nilikutana naye Uhazili, nilipokuwa na majukumu maalum.

Alinikuta nahudumiwa kwa wakala pale nje. Nilikuwa naweka fedha kwenye simu.

Sasa kafika, kapitisha kono lake puup, ndani. Hela zangu zikamwagika. Kistaarabu, kulikoni brother? Kaniambia sogea watu wa Muhimu tuhudumiwe tuwahi kuihudumia jamii. Unanifahamu mimi nani?

Nilishikwa na hasira, nikachukua hela zake na kuzitoa nje. Nikasogeza na Million moja ikadondoka chini.

Bahati nzuri kwake, kijana huyo akatoka na kunituliza. Akachukua hela za Komanya na kwenda nazo ndani. Mimi nikahudumiwa na binti, nikamalizana.

Alisema atanitafuta. Nikamueleza namba yangu utachukua kwa huyu binti anayenihudumia.

Ukweli ni kuwa alinitafuta na alituma vijana wake wanifuate. Mh Sengati aliimaliza ishu kiutu uzima

Mpumbavu mno. Ana ubabe wa kipuuzi.
Mungu alilikomboa taifa
 
Mungu alilikomboa taifa
Yule jamaa ni mpumbavu sana. Story ya huyo jamaa niliipata siku hiyo.

Jamaa kama vile ngozi yake ilipata changamoto kidogo. Nadhani anafanya kazi kama Chief Accountant, TUWASA.

Alimuomba amkopeshe hela. Jamaa kukataa ndiyo akamdhalilisha kupitia ngozi yake.

Ishu ilitulizwa ila jamaa alisue baada ya kunyang'anya uDC
 
Jamaa nimesoma nae UMBWE BOYS....kipindi naingia form ONE ye alikuwa form FIVE
Alikuwa ni kiranja wa ulinzi... Usiombe umetoroka one time kuingia mjini halafu ukawa hauja attend roll call...halafu yeye ndio kaandika majina ya watoro... Utadhani sio mwanafunzi jinsi alivyo kuwa anatoa adhabu...

Jamaa lilikuwa MBAVU halafu muonevu mbaya...

Amenikumbusha mbali kweli
 
Siku moja nilikutana naye Uhazili, nilipokuwa na majukumu maalum.

Alinikuta nahudumiwa kwa wakala pale nje. Nilikuwa naweka fedha kwenye simu.

Sasa kafika, kapitisha kono lake puup, ndani. Hela zangu zikamwagika. Kistaarabu, kulikoni brother? Kaniambia sogea watu wa Muhimu tuhudumiwe tuwahi kuihudumia jamii. Unanifahamu mimi nani?

Nilishikwa na hasira, nikachukua hela zake na kuzitoa nje. Nikasogeza na Million moja ikadondoka chini.

Bahati nzuri kwake, kijana huyo akatoka na kunituliza. Akachukua hela za Komanya na kwenda nazo ndani. Mimi nikahudumiwa na binti, nikamalizana.

Alisema atanitafuta. Nikamueleza namba yangu utachukua kwa huyu binti anayenihudumia.

Ukweli ni kuwa alinitafuta na alituma vijana wake wanifuate. Mh Sengati aliimaliza ishu kiutu uzima

Mpumbavu mno. Ana ubabe wa kipuuzi.
Chai...

Kauli za "Unanijua mi nani" hazikusikika kabisa enzi za Hayati JPM.
JamiiForums561838404.jpg


Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 
Jamaa nimesoma nae UMBWE BOYS....kipindi naingia form ONE ye alikuwa form FIVE
Alikuwa ni kiranja wa ulinzi... Usiombe umetoroka one time kuingia mjini halafu ukawa hauja attend roll call...halafu yeye ndio kaandika majina ya watoro... Utadhani sio mwanafunzi jinsi alivyo kuwa anatoa adhabu...

Jamaa lilikuwa MBAVU halafu muonevu mbaya...

Amenikumbusha mbali kweli
Umenikumbusha enzi hizo Vijana walikuwa watukutu balaa lakini Viranja Wakuu walikuwa miungu watu.

Yani wanafunzi mnahangaika na mauji shuleni lakini wao wanapata chai yao spesho wakiwa pamoja na Walimu.

Kimbembe sasa uingie kwenye 18 za Kiranja Mkuu ndipo utapoita maji mma.

Sent from my CPH2387 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom