Boniface Jacob na Godlisten Malissa Wafikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
118,489
220,124
Wamefunguliwa kesi ya Uchochezi na kuzua Taharuki

Kesi hiyo imefunguliwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi, Kisutu, Dar es Salaam.

Bado haijajulikana kama watapata dhamana au watapelekwa Segerea

Jopo la Mawakili wao likiongozwa na Peter Kibatala tayari lishafika Mahakamani hapo kusimamia utetezi.
Updates:
=======
Hatimaye wameachiwa kwa Dhamana

Screenshot_2024-05-06-15-34-05-1.png


Pia soma
- Mauaji ya Robert Mushi ndugu wa aliyekuwa Meya wa Ubungo Boniface Jacob polisi wanahusika?

- Kamanda Muliro: Malisa GJ, Boniface Jacob wakamatwe kwa tuhuma za kupotosha taarifa za kifo cha Robart Mushi

- Utata sakata la ndugu wa Boniface Jacob: Kupotea mpaka kukutwa mochwari ya polisi, Amana wapigilia msumari!

- Hatimaye Malissa na Boniface Jackob waachiwa kwa dhamana
 
Mfumo wa jinai haki (criminal justice system)wa Tanzania umezidi kuboreshwa kwa wadau kuwawezeshwa kwa mafunzo na ujuzi kwa wale wote waliopo ndani ya mfumo kufanya kazi wa weledi :

MAFUNZO YA HAKI JINAI KWA WAENDESHA MASHTAKA, WAPELELEZI YAHITIMISHWA​


MoroMachi24-1523-03-24.jpg

MoroMachi24-123-03-24.jpg

MoroMachi24-323-03-24.jpg

MoroMachi24-723-03-24.jpg

MoroMachi24-923-03-24.jpg

Na Faustine Kapama –Mahakama, Morogoro

Mafunzo ya siku 28 kuhusu Haki Jinai yaliyokuwa yanafanyika katika Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Morogoro mjini hapa kwa washiriki 250 ambao ni waendesha mashtaka na wapelelezi waliotoka taasisi mbalimbali nchini yamehitimishwa leo tarehe 24 Machi, 2023.

Naibu Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA) anayeshughulikia Mipango, Fedha na Utawala, Prof. Fatihiya Massawe amehitimisha mafunzo hayo yaliyokuwa yanatolewa kwa washiriki kutoka Ofisi ya Taifa ya Mashtaka, Jeshi la Polisi, Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori na Kitengo cha Kudhibiti Fedha Haramu.

Akizungumza katika hafla hiyo, Prof. Massawe aliwahimiza maafisa hao kuendelea kushirikiana wanapotekeleza majukumu yao kwani hatua hiyo itaharakisha upatikanaji wa utoaji haki kwa wananchi na kuboresha haki jinai.

"Mahakama inaamini sana katika ushirikiano na wadau wa mfumo wa haki jinai kwenye jukumu lake la kikatiba la utoaji haki na hili linaonekana kwenye Mpango Mkakati wa Mahakama (2020/21-204/25), hususani katika nguzo yake ya tatu.

Hivyo, nitoe rai kuwa muwe na ushirikiano wa dhati na Mahakama ili muweze kufanikisha jukumu la upatikanaji wa haki," alisisitiza.


Aidha, Prof. Massawe aliwaeleza kuwa mafunzo waliyopata yawe chachu ya utayari wa kutamani kujifunza kwa kusoma uamuzi mbalimbali unaotolewa na Mahakama ambao unaelekeza taratibu muhimu za kuzingatia katika upelelezi na uendeshaji wa mashtaka. Alisema kwa kufanya hivyo kutawawezesha kuendelea kuongeza ujuzi mpya utakaowawezesha kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazoweza kuibuka wakati wa upelelezi au uendeshaji wa mashtaka.

Awali, akimkaribisha mgeni rasmi kuongea na wahitimu wa mafunzo hayo, Kaimu Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Morogoro, Mhe. Livin Lyakinana alieleza kuwa Mahakama ya Tanzania inaendelea na utekelezaji wa Mpango Mkakati Awamu ya Pili (2020/21-2024/25 na inatekeleza mradi wa kuimarisha upatikanaji haki unaomlenga mwananchi.

Alisema mpango huo unatekeleza maeneo makuu matatu ya maboresho, ikiwemo uwajibikaji na usimamizi bora wa rasilimali, upatikanaji na utoaji haki kwa wananchi na kuimarisha imani ya wananchi na ushirikishwaji wa wadau.

"Kwa kawaida, Mahakama imekuwa ikishirikiana na wadau wa haki jinai katika majukwaa mengine yakiwemo vikao vya kamati za kusukuma mashauri.

Mafunzo haya yamefanyika lengo likiwa, (pamoja na mambo mengine) kupanua wigo wa azma ya Mahakama ya kushirikiana na wadau," alisema.

Akiwasilisha neno la shukrani kwa niaba ya washiriki wenzake,Wakili wa Serikali Sara Amandus alisema kuwa katika mafunzo hayo wamejifunda mada mbalimbali zikiwemo za kiuchunguzi, kuendesha mashtaka, utunzwaji wa vielelezo, ulinzi wa watoa taarifa na mashahidi, ushirikiano kwenye ukusanywaji wa ushahidi, urejeshwaji wa watuhumiwa, matumizi ya TEHAMA kuelekea Mahakama mtandao, hali ya mifumo na miundombinu pamoja na maadili katika uchunguzi na uendeshaji wa mashauri.

"Mafunzo haya yametuongezea weledi na motisha ya kufanya kazi kwa umakini, maadili pamoja na kuzingatia maendeleo ya sayansi na teknolojia katika uchunguzi na kuendesha kesi mahakamani.

Tunashukuru waandaaji, yaani Mahakama ya Tanzania pamoja na Chuo cha Uongozi wa Mahakama kwa kuandaa mafunzo haya," alisema.
Mwakilishi huyo alimhakikishia mgeni raismi kuwa wanaenda kuwa mabalozi wazuri na kuwapa elimu wale ambao hawajapata nafasi ya kushiriki mafunzo hayo.

Alitoa rai kuwa mafunzo hayo yawe endelevu kwani yanawaongezea ari ya kutekeleza majukumu yao.
Kabla ya kuhitimishwa mafunzo hayo, washiriki katika kundi la nne walipitishwa kwenye mada mbili, ikiwemo mikakati na mbinu za uendeshaji wa mashitaka na masuala ya kimaadili ya uchunguzi na mashtaka, zilizowasilishwa na Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Divisheni ya Biashara, Mhe. Awamu Mbagwa.

Akiwasilisha mada hizo, Mhe. Mbagwa aliwahimiza waendesha mashtaka kuandaa mashtaka kulinga na ushahidi uliokusanywa na wapelelezi na kuacha uzembe wanapoandaa na kuongoza mashahidi mahakakani.

Aliwaeleza washiriki hao wa mafunzo kuwa mchakato wa haki jinai hupitia hatua muhimu tatu, zikiwemo uchunguzi unaofanywa na wapelelezi, uendeshaji wa mashtaka unaofanywa na Ofisi ya Taifa ya Mashtaka na hatua ya kusikiliza na uamuzi inayofanywa na Mahakama.

“Ili haki ionekane imetendeka lazima hatua hizi zitekelezwe na watu watatu tofauti. Kila hatua ina umuhimu wake katika mnyororo mzima wa utoaji haki. Hatua zote hizi ni muhimu na lazima wanaohusika wafanye kazi yao vizuri. Tatizo huja pale mmoja kati ya hawa anapojiona siyo muhimu. Wote wanaumuhimu sawa, tukifanya hivyo tutawatendea haki wananchi,” alisema.

Aliwaeleza kuwa mahusiano kati ya wapelelezi na waendesha mashtaka yasiishie pale jalada linapowasilishwa Ofisi ya Taifa Mashtaka. Aliwahimiza maafisa hao kuendelea kushirikiana hadi shauli lililowasilishwa mahakamani litakapohitimishwa.

Kadhalika, Mhe. Mbagwa aliwasihi kuishi maadili wanapotekeleza majukumu yao, ikiwemo kutumia madaraka yao vibaya na kujiepusha na kufanya vitendo vya rushwa. “Haya madaraka ni dhamana. Kuna maisha baada ya hapa, nawaomba mzingatie maadili kwani ni muhimu katika mfumo wa utoaji haki,” alisisitiza.
Aliwashauli kujitahidi kadri inavyowezekana kutoshughulikia mashauri ambayo wanamaslahi nayo ili kuruhusu haki siyo tu itendeke bali pia ionekane imetendeka. Aidha, aliwahimiza wapelelezi kutunza siri na kutovujisha taarifa walizozikusanya kwa watu wasiohusika ili kulinda taswila yao wenyewe na taasisi wanazotoka.

Kwa kipindi cha wiki nne, washiriki hao wa mafunzo walipitishwa kwenye mada mbalimbali na walipata nafasi ya kubadilishana uzoefu kuhusu utendaji kazi wao wa kila siku, ikiwemo changamoto zinazotokana na kukua kwa teknoloji na kubadilika kwa mbinu za uhalkifu na wahalifu.
Kuandaliwa kwa mafunzo hayo ni sehemu ya utekelezaji wa maboresho ya Mahakama ambayo yanatekelezwa kupitia Mpango Mkakati wake wa miaka mitano (2021-203/2024) na ni utekelezaji pia wa Sera ya Mafunzo ya Taifa 2003 pamoja na Sera ya Mafunzo ya kimahakama 2019.

Mafunzo hayo yaliyofadhiliwa Benki ya Dunia World Bank kupitia mradi wa maboresho awamu ya pili yaliandaliwa na Mahakama ya Tanzania kwa kushirikiana na IJA.

View: https://m.youtube.com/watch?v=syayKwpcxj4&pp=ygUTSnVkaWNpYXJ5IFRhbnphbmlhIA%3D%3D 2017 Tanzania is prioritizing judicial modernization and justice service delivery by expanding court services throughout the country to reach underserved areas long denied access to courts as well as implementing changes to the way the court and its officers do business in an effort to decrease delays. The work is supported by the World Bank’s fund for the poorest, IDA, and is aimed at making sure that justice services like courts reach communities who need them the most. http://ida.worldbank.org/

Yalifunguliwa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Morogoro, Mhe. Paul Ngwembe tarehe 27 Februari, 2023.

Akizungumza wakati anafungua mafunzo hayo, Mhe. Ngwembe aliwahimiza waendesha mashtaka na wapelelezi hao kutekeleza majukumu yao kikamilifu kwa vile Mahakama haiwezi kufanya maajabu, ikiwemo kumtia hatiani mhalifu kwa kuletewa shahidi dhaifu.
Alisema jamii huwa haiielewi Mahakama pale inapomwachia mtuhumiwa aliyekamatwa na wananchi wakishuhudia akitenda kosa. Aliwaeleza washiriki hao wa mafunzo kuwa katika mazingira hayo, chombo kinacholaumiwa ni Mahakama, jambo ambalo halipendezi mbele ya macho ya jamii.


“Lakini Mahakama ifanye nini kama hakuna ushahidi wa kuweza kumhusisha mtuhumiwa na uhalifu anaotuhumiwa nao? Kama upande wa mashtaka umeshindwa kuleta mashahidi wa msingi, Mahakama ifanye miujiza gani? Lakini pia, upande wa mashtaka utaendesha vipi shauri kama upelelezi haukufanywa kama inavyotakiwa? Mwisho wa yote, mchakato mzima wa haki jinai utakuwa kituko mbele ya jamii,” alisema
Source : Judiciary.go.tz
 
Wamefunguliwa kesi ya Uchochezi na kuzua Taharuki

Kesi hiyo imefunguliwa kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi, Kisutu, Dar es Salaam.

Bado haijajulikana kama watapata dhamana au watapelekwa Segerea

Amezua Tena taharuki, amempatia Mjane nyumba ya kisasa ya kuishi.
 
Mfumo wa jinai haki (criminal justice system)wa Tanzania umezidi kuboreshwa kwa wadau kuwawezeshwa kwa mafunzo na ujuzi kwa wale wote waliopo ndani ya mfumo kufanya kazi wa weledi :

MAFUNZO YA HAKI JINAI KWA WAENDESHA MASHTAKA, WAPELELEZI YAHITIMISHWA​

24-03-2023 0
MoroMachi24-1523-03-24.jpg

MoroMachi24-123-03-24.jpg

MoroMachi24-323-03-24.jpg

MoroMachi24-723-03-24.jpg

MoroMachi24-923-03-24.jpg


Na Faustine Kapama –Mahakama, Morogoro

Mafunzo ya siku 28 kuhusu Haki Jinai yaliyokuwa yanafanyika katika Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Morogoro mjini hapa kwa washiriki 250 ambao ni waendesha mashtaka na wapelelezi waliotoka taasisi mbalimbali nchini yamehitimishwa leo tarehe 24 Machi, 2023.

Naibu Mkuu wa Chuo cha Uongozi wa Mahakama Lushoto (IJA) anayeshughulikia Mipango, Fedha na Utawala, Prof. Fatihiya Massawe amehitimisha mafunzo hayo yaliyokuwa yanatolewa kwa washiriki kutoka Ofisi ya Taifa ya Mashtaka, Jeshi la Polisi, Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori na Kitengo cha Kudhibiti Fedha Haramu.

Akizungumza katika hafla hiyo, Prof. Massawe aliwahimiza maafisa hao kuendelea kushirikiana wanapotekeleza majukumu yao kwani hatua hiyo itaharakisha upatikanaji wa utoaji haki kwa wananchi na kuboresha haki jinai.

"Mahakama inaamini sana katika ushirikiano na wadau wa mfumo wa haki jinai kwenye jukumu lake la kikatiba la utoaji haki na hili linaonekana kwenye Mpango Mkakati wa Mahakama (2020/21-204/25), hususani katika nguzo yake ya tatu.

Hivyo, nitoe rai kuwa muwe na ushirikiano wa dhati na Mahakama ili muweze kufanikisha jukumu la upatikanaji wa haki," alisisitiza.


Aidha, Prof. Massawe aliwaeleza kuwa mafunzo waliyopata yawe chachu ya utayari wa kutamani kujifunza kwa kusoma uamuzi mbalimbali unaotolewa na Mahakama ambao unaelekeza taratibu muhimu za kuzingatia katika upelelezi na uendeshaji wa mashtaka. Alisema kwa kufanya hivyo kutawawezesha kuendelea kuongeza ujuzi mpya utakaowawezesha kukabiliana na changamoto mbalimbali zinazoweza kuibuka wakati wa upelelezi au uendeshaji wa mashtaka.

Awali, akimkaribisha mgeni rasmi kuongea na wahitimu wa mafunzo hayo, Kaimu Naibu Msajili wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Morogoro, Mhe. Livin Lyakinana alieleza kuwa Mahakama ya Tanzania inaendelea na utekelezaji wa Mpango Mkakati Awamu ya Pili (2020/21-2024/25 na inatekeleza mradi wa kuimarisha upatikanaji haki unaomlenga mwananchi.


Alisema mpango huo unatekeleza maeneo makuu matatu ya maboresho, ikiwemo uwajibikaji na usimamizi bora wa rasilimali, upatikanaji na utoaji haki kwa wananchi na kuimarisha imani ya wananchi na ushirikishwaji wa wadau.


"Kwa kawaida, Mahakama imekuwa ikishirikiana na wadau wa haki jinai katika majukwaa mengine yakiwemo vikao vya kamati za kusukuma mashauri.

Mafunzo haya yamefanyika lengo likiwa, (pamoja na mambo mengine) kupanua wigo wa azma ya Mahakama ya kushirikiana na wadau," alisema.


Akiwasilisha neno la shukrani kwa niaba ya washiriki wenzake,Wakili wa Serikali Sara Amandus alisema kuwa katika mafunzo hayo wamejifunda mada mbalimbali zikiwemo za kiuchunguzi, kuendesha mashtaka, utunzwaji wa vielelezo, ulinzi wa watoa taarifa na mashahidi, ushirikiano kwenye ukusanywaji wa ushahidi, urejeshwaji wa watuhumiwa, matumizi ya TEHAMA kuelekea Mahakama mtandao, hali ya mifumo na miundombinu pamoja na maadili katika uchunguzi na uendeshaji wa mashauri.


"Mafunzo haya yametuongezea weledi na motisha ya kufanya kazi kwa umakini, maadili pamoja na kuzingatia maendeleo ya sayansi na teknolojia katika uchunguzi na kuendesha kesi mahakamani.

Tunashukuru waandaaji, yaani Mahakama ya Tanzania pamoja na Chuo cha Uongozi wa Mahakama kwa kuandaa mafunzo haya," alisema.
Mwakilishi huyo alimhakikishia mgeni raismi kuwa wanaenda kuwa mabalozi wazuri na kuwapa elimu wale ambao hawajapata nafasi ya kushiriki mafunzo hayo.

Alitoa rai kuwa mafunzo hayo yawe endelevu kwani yanawaongezea ari ya kutekeleza majukumu yao.
Kabla ya kuhitimishwa mafunzo hayo, washiriki katika kundi la nne walipitishwa kwenye mada mbili, ikiwemo mikakati na mbinu za uendeshaji wa mashitaka na masuala ya kimaadili ya uchunguzi na mashtaka, zilizowasilishwa na Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Divisheni ya Biashara, Mhe. Awamu Mbagwa.

Akiwasilisha mada hizo, Mhe. Mbagwa aliwahimiza waendesha mashtaka kuandaa mashtaka kulinga na ushahidi uliokusanywa na wapelelezi na kuacha uzembe wanapoandaa na kuongoza mashahidi mahakakani.

Aliwaeleza washiriki hao wa mafunzo kuwa mchakato wa haki jinai hupitia hatua muhimu tatu, zikiwemo uchunguzi unaofanywa na wapelelezi, uendeshaji wa mashtaka unaofanywa na Ofisi ya Taifa ya Mashtaka na hatua ya kusikiliza na uamuzi inayofanywa na Mahakama.

“Ili haki ionekane imetendeka lazima hatua hizi zitekelezwe na watu watatu tofauti. Kila hatua ina umuhimu wake katika mnyororo mzima wa utoaji haki. Hatua zote hizi ni muhimu na lazima wanaohusika wafanye kazi yao vizuri. Tatizo huja pale mmoja kati ya hawa anapojiona siyo muhimu. Wote wanaumuhimu sawa, tukifanya hivyo tutawatendea haki wananchi,” alisema.

Aliwaeleza kuwa mahusiano kati ya wapelelezi na waendesha mashtaka yasiishie pale jalada linapowasilishwa Ofisi ya Taifa Mashtaka. Aliwahimiza maafisa hao kuendelea kushirikiana hadi shauli lililowasilishwa mahakamani litakapohitimishwa.

Kadhalika, Mhe. Mbagwa aliwasihi kuishi maadili wanapotekeleza majukumu yao, ikiwemo kutumia madaraka yao vibaya na kujiepusha na kufanya vitendo vya rushwa. “Haya madaraka ni dhamana. Kuna maisha baada ya hapa, nawaomba mzingatie maadili kwani ni muhimu katika mfumo wa utoaji haki,” alisisitiza.
Aliwashauli kujitahidi kadri inavyowezekana kutoshughulikia mashauri ambayo wanamaslahi nayo ili kuruhusu haki siyo tu itendeke bali pia ionekane imetendeka. Aidha, aliwahimiza wapelelezi kutunza siri na kutovujisha taarifa walizozikusanya kwa watu wasiohusika ili kulinda taswila yao wenyewe na taasisi wanazotoka.

Kwa kipindi cha wiki nne, washiriki hao wa mafunzo walipitishwa kwenye mada mbalimbali na walipata nafasi ya kubadilishana uzoefu kuhusu utendaji kazi wao wa kila siku, ikiwemo changamoto zinazotokana na kukua kwa teknoloji na kubadilika kwa mbinu za uhalkifu na wahalifu.
Kuandaliwa kwa mafunzo hayo ni sehemu ya utekelezaji wa maboresho ya Mahakama ambayo yanatekelezwa kupitia Mpango Mkakati wake wa miaka mitano (2021-203/2024) na ni utekelezaji pia wa Sera ya Mafunzo ya Taifa 2003 pamoja na Sera ya Mafunzo ya kimahakama 2019.

Mafunzo hayo yaliyofadhiliwa Benki ya Dunia World Bank kupitia mradi wa maboresho awamu ya pili yaliandaliwa na Mahakama ya Tanzania kwa kushirikiana na IJA.

Yalifunguliwa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Morogoro, Mhe. Paul Ngwembe tarehe 27 Februari, 2023.

Akizungumza wakati anafungua mafunzo hayo, Mhe. Ngwembe aliwahimiza waendesha mashtaka na wapelelezi hao kutekeleza majukumu yao kikamilifu kwa vile Mahakama haiwezi kufanya maajabu, ikiwemo kumtia hatiani mhalifu kwa kuletewa shahidi dhaifu.
Alisema jamii huwa haiielewi Mahakama pale inapomwachia mtuhumiwa aliyekamatwa na wananchi wakishuhudia akitenda kosa. Aliwaeleza washiriki hao wa mafunzo kuwa katika mazingira hayo, chombo kinacholaumiwa ni Mahakama, jambo ambalo halipendezi mbele ya macho ya jamii.


“Lakini Mahakama ifanye nini kama hakuna ushahidi wa kuweza kumhusisha mtuhumiwa na uhalifu anaotuhumiwa nao? Kama upande wa mashtaka umeshindwa kuleta mashahidi wa msingi, Mahakama ifanye miujiza gani? Lakini pia, upande wa mashtaka utaendesha vipi shauri kama upelelezi haukufanywa kama inavyotakiwa? Mwisho wa yote, mchakato mzima wa haki jinai utakuwa kituko mbele ya jamii,” alisema
Source : Judiciary.go.tz
Hapa hakuna aliyeelewa hata mmoja zaidi ya watu kuvuta posho pekee
 
Back
Top Bottom