Innocent Kirumbuyo
JF-Expert Member
- Jan 1, 2014
- 4,640
- 4,431
Hello
kwa miaka mitatu nipo hapa na niye nikiwapa vijana wenzangu ndugu zangu ABC za biashara ya viatu
Makala namba 1
Makala namba 2
Makala namba
Zote hizi zimebeba ushauri matumaini na nguvu ya kubadili maisha yako kama utafata ushauri ulitolewa huko
Leo nipo mbele yenu nikiwa nimebeba fursa nzuri kama kijana ukitumia vizuri aijalishi una elimu gani umetokea familia gani upo aje maisha yako yanabadilika kabisa
Uwajibika kujituma pasipo kuchoka hakika utafanikiwa
Baada ya safari ndefu ya kutimiza malengo yangu Sasa naona mwanga baada ya kufungua goli mjini nilipitia vipindi vizito sana biashara yangu aikwenda vizuri ikashuka sana
Nikaona naitaji mkopo kukuza biashara yangu nilichukuwa mikopo kwa marafiki na watu binafsi na kwenye tasisi za mikopo.
Kwa kweli kuchukuwa mkopo ilikuwa janga kubwa sana mkopo akufanya vema nikajikuta Nina deni zaidi ya milioni 10 alafu sina mzigo dukani sina mbele wa nyuma nilikuwa namawazo sana usiku silali kabisa.
Nikawaza niuze ilo eneo langu la biashara nilipe madeni ya watu niwe na amani kabisa nikaingiza eneo langu sokoni nikaita madalali kutafuta wateja nikakutana na kikwazo kikubwa mke wangu akagoma kabisa nisiuze eneo tupambane tu tutalipa madeni tu
Hapo Mimi nikajiona siwezi kabisa zaidi ya kuuza ilo eneo ukatokea tena mgogoro na mke wangu Mimi nataka kuuza eneo yeye ataki eneo liuzwe mwisho wa siku ilibidi nimsikilize mke wangu nisiuze eneo langu tuone ni njia gani nyingine tunaweza kufanya kuweza kulipa madeni ya watu na maisha kuendelea
Nilisoma vitabu sana niliomba ushauri watu wengi wengine nilikuwa natamani maisha yao ila wao waliponipa ukweli wa maisha yao nilichoka kabisa biashara ni vita kubwa sana ya kupata mafanikio
Niliendelea kupambana huku nikiwaza nini nifanye ili mambo yawe sawa huku watu wanaonidai wamenikalia kooni wanataka pesa zao nilipigia ndugu marafiki jamaa na yoyote kuomba pesa mawazo lakini niliambulia patupu
Ndio mwezi wa pili mke wangu akaja na wazo akaniambia kwanini nisiondoke nikapambane sehemu nyingine nimuache pale yeye na familia atapambana pale kwenye kipindi nikipambana paka mambo yatapokaa sawa niwe nawatumia pesa
Ilo wazo likawa gumu sana kwangu nikamuambia nitakuacha aje hapa madeni mengi hivi bila pesa yoyote sitakuwa na amani kabisa mke wangu akasema Mimi niende yeye atavumilia tu
Ndio nikaamua kuchukuwa hatua ya kumtafuta mtu nikamkodishia eneo langu la biashara kwa mwaka moja kwa masharti kuwa mke wangu atakuwa naye anakaa hapo kama mwajiriwa
Kwakweli jamaa akaubali akanipa pesa tuliokubaliana ile pesa kidogo nikapunguza pesa kidogo wale waliokuwa wananisumbua sana madeni yao nyingine kidogo nikampa wife nyingine nikafanya nauli ya kusafiri na kunisaidia safarini
Niliamua kuwa nitaenda dar es salaam kariakoo kuangalia fursa huko nikawasiliana na rafiki yangu mmoja niliyewai kuishi naye mwanza yeye alienda dar muda mrefu nikamuambia ukweli kabisa mzee Mimi nakuja kutafuta harakati hapo nakuomba unipokee jamaa naye bila iyana akakubali kuwa atanipokea
Tarehe 10 -3- mwaka huu nikapanda gari nakuja dar es salaam nikafika salama kabisa jamaa yangu akanipokea.
Kesho yake nikaenda Kariakoo nikazunguka sana kuangalia maeneo mbalimbali kutafuta na watu niowafahamu waliopo huku na kutazama fursa ni kitu ambacho nitaweza kufanya nipate pesa
Kwa kweli kariakoo kuna fursa kubwa sana ndio nikapata wazo la kuwa agent kusaidia watu kuwanunulia viatu kwa bei halali ya mchina anayo wauzia na kuwatumia mikoani.
Hapo ndio niligundua watu wanauziwa vitu bei ya juu sana tofauti watu wanapigwa sana hapa Mimi ndio nikawasaidia kuchukuwa kwa mchina kwa bei halali na kuwauzia kwa bei halali kabisa
Nilifungua group WhatsApp nikawapigia simu wafanya biashara ninaowafahamu ambao najua wanaagiza bidhaa zao dar es salaam nikawaambia naweza kuwasaidia kuwanunulia bidhaa kwa bei halali kabisa na kuwatumia kwa uaminifu mkubwa watu wengi walikuwa wanawasiwasi sana ila nikawaomba kama awatojali niwaweke kwenye group langu wataona bidhaa wakakubaliana na Mimi.
Niliwaweka kwenye group nikaaza juhudi kubwa sana za kutafuta wachina na wahindi na watu wanao uza bidhaa zao kwa jumla naongea nao wanitumia sampo na Mimi naziweka kwenye group langu
Nilivyoweka watu wengi walishangaa sana wakaona mbona Mimi bei ipo chini sana tofauti na wao walivyozoe kununua ndio watu wakawa wananipa oda ndogo ndogo nikawa nawatumia kwa uaminifu mkubwa
Watu walivyopata bidhaa zao kwa bei nzuri wakawambia na wengine kila siku nikawa napata wateja wapya oda zikaongeza sana kwa kipindi kifupi
Kwa kweli Sasa hivi nimefanikiwa kupunguza deni langu pakubwa na muda mchache sana toka milioni 12 paka muda huu nadaiwa milioni 5 tu nadhani mwezi wa Saba nitakuwa nimeshamaliza kabisa ili deni
Namshukuru Mungu Sasa hivi mambo siyo mabaya kila siku naona ndoto zangu zinaenda kutimia natuma vitu vingi ila zaidi natuma viatu
Ushauri wangu kwa vijana wenzangu mafanikio siyo jambo rahisi inaitaji uwajibikaji wa hali ya juu kutokukata tamaa ata ukipitia magumu mengi usife moyo pambana tu
Hapo nimeandika machache sana yapo mengi sana
Nakaribisha ushauri maoni na watu wanotaka konecation ya kupata bidhaa kwa wachina kwa bei ya jumla kabisa
Ata ukitaka nikuunganishe na mchina moja kwa moja nakusaidia bure kabisa
Ukitaka viatu vyotevyote kwa bei ya jumla kabisa nakusaidia
Asante sana
Baadhi ya Mikopo niliyokuwa nachukuwa
kwa miaka mitatu nipo hapa na niye nikiwapa vijana wenzangu ndugu zangu ABC za biashara ya viatu
Makala namba 1
Biashara ya viatu inaweza kukutajirisha
Hello Natumaini mnaendelea vyema na harakati za kutafuta maisha nimeona leo niwaibie siri jinsi hii biashara ya sandals na viatu inaweza kukutajirisha kwa haraka. Historia Mimi kwa majina ya kuzaliwa naitwa Innocent kirumbuyo nimezaliwa Kilimanjaro katika hospital marubeneti miaka mingi...
www.jamiiforums.com
Utajiri uliojificha kwenye viatu vya mtumba
Hello Natumaini ni wazima wa afya mwaka jana mwezi kama huu niliandika uzi kwenye jukwaa ili kuhusu biashara ya viatu https://www.jamiiforums.com/index.php?threads/1790275/ Kwa kweli nawashukuru sana mlipokea ile biashara kwa mikono miwili na watu walinipongeza sana wengine kupitia ule uzi...
www.jamiiforums.com
SoC02 - Jinsi biashara ya viatu inavyonitoa mavumbini
Hello Mimi ni ndugu yenu innocent kirumbuyo kwa miaka miwili nimekuwa nikiweka story biashara ya viatu 1) Biashara ya viatu inaweza kukutajirisha 2) Utajiri uliojificha kwenye viatu vya mtumba Nafarijika sana kwa kupokea maoni mengi na mawazo jinsi watu walivyo badili mitazamo yao na maisha...
www.jamiiforums.com
Zote hizi zimebeba ushauri matumaini na nguvu ya kubadili maisha yako kama utafata ushauri ulitolewa huko
Leo nipo mbele yenu nikiwa nimebeba fursa nzuri kama kijana ukitumia vizuri aijalishi una elimu gani umetokea familia gani upo aje maisha yako yanabadilika kabisa
Uwajibika kujituma pasipo kuchoka hakika utafanikiwa
Baada ya safari ndefu ya kutimiza malengo yangu Sasa naona mwanga baada ya kufungua goli mjini nilipitia vipindi vizito sana biashara yangu aikwenda vizuri ikashuka sana
Nikaona naitaji mkopo kukuza biashara yangu nilichukuwa mikopo kwa marafiki na watu binafsi na kwenye tasisi za mikopo.
Kwa kweli kuchukuwa mkopo ilikuwa janga kubwa sana mkopo akufanya vema nikajikuta Nina deni zaidi ya milioni 10 alafu sina mzigo dukani sina mbele wa nyuma nilikuwa namawazo sana usiku silali kabisa.
Nikawaza niuze ilo eneo langu la biashara nilipe madeni ya watu niwe na amani kabisa nikaingiza eneo langu sokoni nikaita madalali kutafuta wateja nikakutana na kikwazo kikubwa mke wangu akagoma kabisa nisiuze eneo tupambane tu tutalipa madeni tu
Hapo Mimi nikajiona siwezi kabisa zaidi ya kuuza ilo eneo ukatokea tena mgogoro na mke wangu Mimi nataka kuuza eneo yeye ataki eneo liuzwe mwisho wa siku ilibidi nimsikilize mke wangu nisiuze eneo langu tuone ni njia gani nyingine tunaweza kufanya kuweza kulipa madeni ya watu na maisha kuendelea
Nilisoma vitabu sana niliomba ushauri watu wengi wengine nilikuwa natamani maisha yao ila wao waliponipa ukweli wa maisha yao nilichoka kabisa biashara ni vita kubwa sana ya kupata mafanikio
Niliendelea kupambana huku nikiwaza nini nifanye ili mambo yawe sawa huku watu wanaonidai wamenikalia kooni wanataka pesa zao nilipigia ndugu marafiki jamaa na yoyote kuomba pesa mawazo lakini niliambulia patupu
Ndio mwezi wa pili mke wangu akaja na wazo akaniambia kwanini nisiondoke nikapambane sehemu nyingine nimuache pale yeye na familia atapambana pale kwenye kipindi nikipambana paka mambo yatapokaa sawa niwe nawatumia pesa
Ilo wazo likawa gumu sana kwangu nikamuambia nitakuacha aje hapa madeni mengi hivi bila pesa yoyote sitakuwa na amani kabisa mke wangu akasema Mimi niende yeye atavumilia tu
Ndio nikaamua kuchukuwa hatua ya kumtafuta mtu nikamkodishia eneo langu la biashara kwa mwaka moja kwa masharti kuwa mke wangu atakuwa naye anakaa hapo kama mwajiriwa
Kwakweli jamaa akaubali akanipa pesa tuliokubaliana ile pesa kidogo nikapunguza pesa kidogo wale waliokuwa wananisumbua sana madeni yao nyingine kidogo nikampa wife nyingine nikafanya nauli ya kusafiri na kunisaidia safarini
Niliamua kuwa nitaenda dar es salaam kariakoo kuangalia fursa huko nikawasiliana na rafiki yangu mmoja niliyewai kuishi naye mwanza yeye alienda dar muda mrefu nikamuambia ukweli kabisa mzee Mimi nakuja kutafuta harakati hapo nakuomba unipokee jamaa naye bila iyana akakubali kuwa atanipokea
Tarehe 10 -3- mwaka huu nikapanda gari nakuja dar es salaam nikafika salama kabisa jamaa yangu akanipokea.
Kesho yake nikaenda Kariakoo nikazunguka sana kuangalia maeneo mbalimbali kutafuta na watu niowafahamu waliopo huku na kutazama fursa ni kitu ambacho nitaweza kufanya nipate pesa
Kwa kweli kariakoo kuna fursa kubwa sana ndio nikapata wazo la kuwa agent kusaidia watu kuwanunulia viatu kwa bei halali ya mchina anayo wauzia na kuwatumia mikoani.
Hapo ndio niligundua watu wanauziwa vitu bei ya juu sana tofauti watu wanapigwa sana hapa Mimi ndio nikawasaidia kuchukuwa kwa mchina kwa bei halali na kuwauzia kwa bei halali kabisa
Nilifungua group WhatsApp nikawapigia simu wafanya biashara ninaowafahamu ambao najua wanaagiza bidhaa zao dar es salaam nikawaambia naweza kuwasaidia kuwanunulia bidhaa kwa bei halali kabisa na kuwatumia kwa uaminifu mkubwa watu wengi walikuwa wanawasiwasi sana ila nikawaomba kama awatojali niwaweke kwenye group langu wataona bidhaa wakakubaliana na Mimi.
Niliwaweka kwenye group nikaaza juhudi kubwa sana za kutafuta wachina na wahindi na watu wanao uza bidhaa zao kwa jumla naongea nao wanitumia sampo na Mimi naziweka kwenye group langu
Nilivyoweka watu wengi walishangaa sana wakaona mbona Mimi bei ipo chini sana tofauti na wao walivyozoe kununua ndio watu wakawa wananipa oda ndogo ndogo nikawa nawatumia kwa uaminifu mkubwa
Watu walivyopata bidhaa zao kwa bei nzuri wakawambia na wengine kila siku nikawa napata wateja wapya oda zikaongeza sana kwa kipindi kifupi
Kwa kweli Sasa hivi nimefanikiwa kupunguza deni langu pakubwa na muda mchache sana toka milioni 12 paka muda huu nadaiwa milioni 5 tu nadhani mwezi wa Saba nitakuwa nimeshamaliza kabisa ili deni
Namshukuru Mungu Sasa hivi mambo siyo mabaya kila siku naona ndoto zangu zinaenda kutimia natuma vitu vingi ila zaidi natuma viatu
Ushauri wangu kwa vijana wenzangu mafanikio siyo jambo rahisi inaitaji uwajibikaji wa hali ya juu kutokukata tamaa ata ukipitia magumu mengi usife moyo pambana tu
Hapo nimeandika machache sana yapo mengi sana
Nakaribisha ushauri maoni na watu wanotaka konecation ya kupata bidhaa kwa wachina kwa bei ya jumla kabisa
Ata ukitaka nikuunganishe na mchina moja kwa moja nakusaidia bure kabisa
Ukitaka viatu vyotevyote kwa bei ya jumla kabisa nakusaidia
Asante sana
Baadhi ya Mikopo niliyokuwa nachukuwa