SoC04 Majeshi ya Ulinzi na Usalama yaunde Sera na Mkakati maalumu wa ajira kwa jamii ya watu wenye ulemavu

Tanzania Tuitakayo competition threads

Alubati

JF-Expert Member
May 29, 2016
5,832
12,462
Ulemavu ni hali ya mtu kuwa na upungufu kimwili ambao hufanya iwe vigumu kufanya shughuli kulingana na mazingira yanayomzunguka. Kuna aina nyingi za ulemavu kama usikivu hafifu, ulemavu wa viungo vya nje ya mwili kama kama miguu, ulemavu wa ngozi,ulemavu wa kutoweka kutamka maneno, kushindwa kuona au uoni hafifu n.k.

Jamii hii ya watu wenye ulemavu imekuwa ikikosa fursa ta ushiriki kwenye mchakato wa kupata ajira kwenye vyombo vyetu vya ulinzi na usalama kama : Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Jeshi la Kujenga Taifa(JKT), Jeshi la polisi, Jeshi la Magereza,Jeshi la Zimamoto na Uokoaji,Jeshi la Uhamiaji na Usalama wa Taifa.

Ulemavu si ugonjwa ninapendekeza Tanzania tuitakayo iunde sera na mkakati kuhusu watu wenye ulemavu kwa kuwapatia nafasi maalumu za ajira kwenye majeshi yetu ya Ulinzi na Usalama hasa wali waliohitimu mafunzo katika vyuo vya ufundi stadi, Stashada na Shahada katika vyuo vya kati na vyuo vikuu katika taaluma ya fani mbalimbali kama Udaktari wa mifugo na binadamu, wataalamu wa Uchumi, Wahandisi mitambo, umeme, na miundombinu kama barabara, wataalamu wa kompyuta na mawasiliano,wataalamu wa nyuklia n.k.

Sera hii ya ajira kwa watu wenye ulemavu ijikite katika mafunzo maalumu ya kijeshi kulingana na aina ya ulemavu wa wahusika,na shughuli kiutendaji kwao zihusu katika kuhudumia jamii ya waTanzania katika kazi za kiofisi bila ya wao kuhusishwa katika operesheni za mapambano mstari wa mbele (frontline).

Nafahamu suala la utimamu wa mwili ni jambo la kuzingatia katika katika kutoa nafasi za ajira kwenye majeshi yetu ya Ulinzi na Usalama, lakini kupitia kuundwa sera na mkakati maalumu kuhusu ajira kwa watu wenye ulemavu kwenye majeshi yetu kunaweza kuleta tija na matokeo chanya kwakuwa watu hawa wana uwezo mkubwa kiutendaji katika fani mbalimbali. Pia itasaidia kuimarisha mahusiano baina ya majeshi yetu ya Ulinzi na Usalama na Jamii ya watu wenye ulemavu kwa kuwa kwa sasa ajira kwa watu wenye ulemavu katika majeshi yetu limekuwa ni jambo lisilowezekana.
 
Ulemavu ni hali ya mtu kuwa na upungufu kimwili ambao hufanya iwe vigumu kufanya shughuli kulingana na mazingira yanayomzunguka. Kuna aina nyingi za ulemavu kama usikivu hafifu, ulemavu wa viungo vya nje ya mwili kama kama miguu, ulemavu wa ngozi,ulemavu wa kutoweka kutamka maneno, kushindwa kuona au uoni hafifu n.k.

Jamii hii ya watu wenye ulemavu imekuwa ikikosa fursa ta ushiriki kwenye mchakato wa kupata ajira kwenye vyombo vyetu vya ulinzi na usalama kama : Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Jeshi la Kujenga Taifa(JKT), Jeshi la polisi, Jeshi la Magereza,Jeshi la Zimamoto na Uokoaji,Jeshi la Uhamiaji na Usalama wa Taifa.

Ulemavu si ugonjwa ninapendekeza Tanzania tuitakayo iunde sera na mkakati kuhusu watu wenye ulemavu kwa kuwapatia nafasi maalumu za ajira kwenye majeshi yetu ya Ulinzi na Usalama hasa wali waliohitimu mafunzo katika vyuo vya ufundi stadi, Stashada na Shahada katika vyuo vya kati na vyuo vikuu katika taaluma ya fani mbalimbali kama Udaktari wa mifugo na binadamu, wataalamu wa Uchumi, Wahandisi mitambo, umeme, na miundombinu kama barabara, wataalamu wa kompyuta na mawasiliano,wataalamu wa nyuklia n.k.

Sera hii ya ajira kwa watu wenye ulemavu ijikite katika mafunzo maalumu ya kijeshi kulingana na aina ya ulemavu wa wahusika,na shughuli kiutendaji kwao zihusu katika kuhudumia jamii ya waTanzania katika kazi za kiofisi bila ya wao kuhusishwa katika operesheni za mapambano mstari wa mbele (frontline).

Nafahamu suala la utimamu wa mwili ni jambo la kuzingatia katika katika kutoa nafasi za ajira kwenye majeshi yetu ya Ulinzi na Usalama, lakini kupitia kuundwa sera na mkakati maalumu kuhusu ajira kwa watu wenye ulemavu kwenye majeshi yetu kunaweza kuleta tija na matokeo chanya kwakuwa watu hawa wana uwezo mkubwa kiutendaji katika fani mbalimbali. Pia itasaidia kuimarisha mahusiano baina ya majeshi yetu ya Ulinzi na Usalama na Jamii ya watu wenye ulemavu kwa kuwa kwa sasa ajira kwa watu wenye ulemavu katika majeshi yetu limekuwa ni jambo lisilowezekana.
Una akili sana, ila tatizo lako Upinde. Majeshi kazi Yao ya Msingi ni mapigano. Kilema gani atapigana.
 
Nafahamu suala la utimamu wa mwili ni jambo la kuzingatia katika katika kutoa nafasi za ajira kwenye majeshi yetu ya Ulinzi na Usalama,
Hapo ndipo penyewe. Acha liendelee kuajiri watu timamu kadri inavyowezekana. Kwa mahitaji maalumu ndipo wanaweza kumchukua mwananchi yeyote (mzima/mlemavu) kusaidia shughuli maalumu. Hiyo haikatai. Lakini pia wale wanaopatwa na ulemavu wakiwa jeshini ndipo wanaweza kupatiwa vitengo vinavyoendana na ulemavu wao.

Katika kuongeza uhusiano mwema na jamii ya walemavu, jeshi linaweza kuanzisha programu maalumu ya kuwasaidia labda kwa kujenga miundombinu wezeshi ili wapate huduma pasi na usumbufu katika maeneo ya umma na misaada mingine.
 
Hapo ndipo penyewe. Acha liendelee kuajiri watu timamu kadri inavyowezekana. Kwa mahitaji maalumu ndipo wanaweza kumchukua mwananchi yeyote (mzima/mlemavu) kusaidia shughuli maalumu. Hiyo haikatai. Lakini pia wale wanaopatwa na ulemavu wakiwa jeshini ndipo wanaweza kupatiwa vitengo vinavyoendana na ulemavu wao.

Katika kuongeza uhusiano mwema na jamii ya walemavu, jeshi linaweza kuanzisha programu maalumu ya kuwasaidia labda kwa kujenga miundombinu wezeshi ili wapate huduma pasi na usumbufu katika maeneo ya umma na misaada mingine.
Kwanini walemavu waonekane ni wati dhaifu wa kupewa msaada wakati wame hold degree zao kwenye fani mbalimbali?
 
Kwanini walemavu waonekane ni wati dhaifu wa kupewa msaada wakati wame hold degree zao kwenye fani mbalimbali?
Tatizo linaanza pale unapowaombea nafasi ya upendeleo jeshini, ambapo jeshini kila mtu ni sawa kwa cheo chake. Kuruti woote wanafanana si wa kike si wa kiume.

Italeta changamoto watakapopewa amri "Mwendo wa kunyakuaaaaaas, mbelee..." halafu wasiitii amri kisa ulemavu.

Lakini sijakataa Alubati kama kuna kazi maalumu inayomuhitaji mtu maalumu jeshi linaruhusiwa kumchukua yeyote na kumkataa yeyote kwa manufaa ya taifa kiujumla.
 
Tatizo linaanza pale unapowaombea nafasi ya upendeleo jeshini, ambapo jeshini kila mtu ni sawa kwa cheo chake. Kuruti woote wanafanana si wa kike si wa kiume.

Italeta changamoto watakapopewa amri "Mwendo wa kunyakuaaaaaas, mbelee..." halafu wasiitii amri kisa ulemavu.

Lakini sijakataa Alubati kama kuna kazi maalumu inayomuhitaji mtu maalumu jeshi linaruhusiwa kumchukua yeyote na kumkataa yeyote kwa manufaa ya taifa kiujumla.
Thank you!
 
Ulemavu ni hali ya mtu kuwa na upungufu kimwili ambao hufanya iwe vigumu kufanya shughuli kulingana na mazingira yanayomzunguka. Kuna aina nyingi za ulemavu kama usikivu hafifu, ulemavu wa viungo vya nje ya mwili kama kama miguu, ulemavu wa ngozi,ulemavu wa kutoweka kutamka maneno, kushindwa kuona au uoni hafifu n.k.

Jamii hii ya watu wenye ulemavu imekuwa ikikosa fursa ta ushiriki kwenye mchakato wa kupata ajira kwenye vyombo vyetu vya ulinzi na usalama kama : Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ), Jeshi la Kujenga Taifa(JKT), Jeshi la polisi, Jeshi la Magereza,Jeshi la Zimamoto na Uokoaji,Jeshi la Uhamiaji na Usalama wa Taifa.

Ulemavu si ugonjwa ninapendekeza Tanzania tuitakayo iunde sera na mkakati kuhusu watu wenye ulemavu kwa kuwapatia nafasi maalumu za ajira kwenye majeshi yetu ya Ulinzi na Usalama hasa wali waliohitimu mafunzo katika vyuo vya ufundi stadi, Stashada na Shahada katika vyuo vya kati na vyuo vikuu katika taaluma ya fani mbalimbali kama Udaktari wa mifugo na binadamu, wataalamu wa Uchumi, Wahandisi mitambo, umeme, na miundombinu kama barabara, wataalamu wa kompyuta na mawasiliano,wataalamu wa nyuklia n.k.

Sera hii ya ajira kwa watu wenye ulemavu ijikite katika mafunzo maalumu ya kijeshi kulingana na aina ya ulemavu wa wahusika,na shughuli kiutendaji kwao zihusu katika kuhudumia jamii ya waTanzania katika kazi za kiofisi bila ya wao kuhusishwa katika operesheni za mapambano mstari wa mbele (frontline).

Nafahamu suala la utimamu wa mwili ni jambo la kuzingatia katika katika kutoa nafasi za ajira kwenye majeshi yetu ya Ulinzi na Usalama, lakini kupitia kuundwa sera na mkakati maalumu kuhusu ajira kwa watu wenye ulemavu kwenye majeshi yetu kunaweza kuleta tija na matokeo chanya kwakuwa watu hawa wana uwezo mkubwa kiutendaji katika fani mbalimbali. Pia itasaidia kuimarisha mahusiano baina ya majeshi yetu ya Ulinzi na Usalama na Jamii ya watu wenye ulemavu kwa kuwa kwa sasa ajira kwa watu wenye ulemavu katika majeshi yetu limekuwa ni jambo lisilowezekana.
Daah hiyoo ni ngumu saana. Hata kama tunatafuta usawa katika nchi
 
Daah hiyoo ni ngumu saana. Hata kama tunatafuta usawa katika nchi
Ndio Tanzania tuitakayo hakuna lisilowezekana kwasababu hata waajiriwa kwenye majeshi yetu ya ulinzi na usalama wanafanya kazi katika fani mbalimbali , hawapigani tu. Hivyo hata hawa watu wenye ulemavu ambao wamehitimu vyuo katika fani mbali mbali wanaweza kuajiriwa na kufanya kazi kiofisi na field kwa wahandisi.
Sera hiyo inakuwa na sheria za kuwalinda.
Pia hawatahusika na operesheni za mstari wa mbele ( mapambano).
 
Una akili sana, ila tatizo lako Upinde. Majeshi kazi Yao ya Msingi ni mapigano. Kilema gani atapigana.
Pamoja na hayo lakini wanashughulika na kazi mbali mbali za kiraia kama uhandisi, udaktari na kadharika, hivyo hawa walemavu watakuwa na kazi za kiofisi zaidi si mapambano .
Zingatia walemavu wengine ni wa ngozi ,usikivu hafifu n.k. hivyo eanaweza fanya kazi kwa ufanisi.
Hivyo tunahitaji Tanzania yenye mabadiliko na mtazamo chanya kuhusu jamii ya watu wenye ulemavu kupata fursa ya ajira kwenye majeshi yetu ya ulinzi na usalama.
 
Pamoja na hayo lakini wanashughulika na kazi mbali mbali za kiraia kama uhandisi, udaktari na kadharika, hivyo hawa walemavu watakuwa na kazi za kiofisi zaidi si mapambano .
Zingatia walemavu wengine ni wa ngozi ,usikivu hafifu n.k. hivyo eanaweza fanya kazi kwa ufanisi.
Hivyo tunahitaji Tanzania yenye mabadiliko na mtazamo chanya kuhusu jamii ya watu wenye ulemavu kupata fursa ya ajira kwenye majeshi yetu ya ulinzi na usalama.
Jeshi haliajiri Bali linaandikisha wapiganaji. Hata uwe ofisini inapotokea ukapigane inatakiwa uende front
 
Umeshawahi kufanya utafiti kujua ni nchi gani duniani ambayo majeshi yake yana walemavu?
Mkuu maswala ya jeshi ni habari nyingine.
 
Umeshawahi kufanya utafiti kujua ni nchi gani duniani ambayo majeshi yake yana walemavu?
Mkuu maswala ya jeshi ni habari nyingine.
M
Jeshi haliajiri Bali linaandikisha wapiganaji. Hata uwe ofisini inapotokea ukapigane inatakiwa uende front
Soma tangazo la jeshi la polisi lipo humu wameandikaje kichwa cha habari, neno kuandikisha ni siasa tu,hiyo ni ajira.
 
Umeshawahi kufanya utafiti kujua ni nchi gani duniani ambayo majeshi yake yana walemavu?
Mkuu maswala ya jeshi ni habari nyingine.
Jeshi la marekani lina kitu kinaitwa American with Disabilitilities Act (ADA) . Linaruhusu walemavu kulitumikia jeshi katika mazingira fulani kama ambavyo nimeainisha kwenye andiko langu pia.
Hivyo Tanzania tuitakayo inahitaji mabadiliko na kuunda sera zitakazo wapa nafasi watu wenye ulemavu kutumikia majeshi ya ulinzi na usalama.
 
Hakuna option Askari mmoja awe na risk kubwa mwingine awe na risk kidogo halafu wafanane malipo
LAkini umeangalia majeshi katika muktadha wa mapigano pekee,majeshi ya ulinzi na usalama nimemaanisha majeshi yote kuanzia jeshi la Polisi,Magereza, Uhamiaje, Zimamoto na Uokoaji n.k.
Pia nimesema ni sera na mkakati maalumu ambao watu wenye ulemavu katika ngazi ya elimu fulani ( rejea kwenye andiko) .
Wapewe nafasi ya ajira katika Majeshi yetu ya ulinzi na usalama.
Kuhusu mshahara na malipo hiyo ni mada nyingine, wao wanafanya kazi kulingana na sifa na taaluma zao hivyo watalipa kulingana na sifa zao kielimu.kama mlemavu ni mhandisi atalipwa mshahara kama muhandisi na si kwa sababu ya ulemavu alio nao.
 
Haliwezekani
Haliwezekani
Hakuna jambo lisilowezekana ikiandaliwa sera na mikakati yakinifu kuhusu ajira kwa watu wenye ulemavu kwenye majeshi yetu ya ulinzi na usalama.tunahitaji kuruhusu mabadiliko ya fikra kuhusu watu wenye ulemavu Tanzania ijayo
 
Back
Top Bottom