TP Mazembe waomba kufundishwa football management na Yanga

Wakati Simba Sc anachukua ubingwa 2017 mbele ya mgeni rasmi JPM, alifungwa mechi gani nyingine kwenye ligi tofauti na ile ya mwisho dhidi ya Kagera? Unadhani hapo nyuma alikuwa na unbeaten ngapi?

Nilisikia unasoma Chuo Kikuu ila kwa hizi akili, napata shida na ninaihurumia sana Tz.
Kumbe TPL iliwahi kuwa na idadi ya mechi 49 kwa misimu miwili (2016/2017) tu, na Makolokolo SC ikaweka rekodi ya unbeaten run? Kweli hata vichaa huona Watu timamu ni vichaa

Ubinadamu ni kazi/The humanity is a work.
 
Matusi hayo,Hamna hata nusu kikombe cha Africa wao wanacho,hamna hata uwanja wao wanao kisha waje kujifunza kwa mbumbumbu?
Football club nyingi za Africa zinazomilikiwa na mtu binafsi zina matumizi mabaya ya pesa. Hali hiyo hupelekea kuyumba kwa mmiliki wa timu na kuamua kuitelekeza kama ambavyo Mo amefanya mara kdhaa na baadae hurudi kwa mapenzi yake. Timu nyingi hazijiendeshi kitaasisi kiasi kwamba mmiliki akipitia changamoto na timu inakuwa kwenye changamoto kama ilivyokuwa kwa Moses Katumbi na Mazembe.

Yanga imepitia hali hizo pia. Mfadhili alipopitia misukosuko na timu ilipitia wakati mgumu sana mpaka alipopatikana GSM. Jambo zuri GSM alipata ushauri mzuri mapema wa namna ya kuzitumia pesa zake . Lakini wazo kuu likawa kufanya transformation wa namna ya kuendesha timu tofauti na utaratibu wa kijima uliozoeleka ambao haukuwa na faida kwa zaidi ya kuifanya kuwa ombaomba.

Kwenye eneo la kiuongozi Yanga imefanikiwa sana kuwa transformed. Na matokeo ya transformation hiyo ya uongozi yameonekana uwanjani hata kama timu haijachukua kombe.

Kunapokuwa na matokeo mazuri uwanjani lazima yataonekana tu. Kupitia mafanikio hayo imekuwa rahisi kwa Rais wa Yanga kuchaguliwa kuwa mwenyekiti wa vilabu baroni Africa. Mnafikiri imekuja kwa bahati tu? Hapana. Kuna jambo limefanyika. Iliwahi tokea wakati Simba ikifanya vizuri CEO wake Babra aliteuliwa kuwa mmoja wa wanakamati za CAF.

Mazembe wanahitaji transformation ya kuendesha timu kutoka kwenye kutegemea maamuzi ya mtu mmoja na kuwa na proper structure ya uongozi. Na hii itaisaidia Tp Mazembe kwa miaka mingi. Mazembe hawana mashabiki waliowasajiri kidigitali na kama wapo ni kwa idadi ndogo sana na hili wanalipitia pia Mamelodi, hili pia wanaweza kujifunza kutoka kwa Yanga kwa kuwa ndio timu iliyofanikiwa kwenye kipengele hicho kwa ukanda huu hata kama sio kwa kiwango kikubwa lakini mapato yanaonekana.

Mambo ni mengi ambayo Tp Mazembe wanaweza kudesa toka kwa Yanga ili waweze kujiendesha hapo baadae Moses Katumbi atakapokuwa hayupo. Na huenda desa hili likawanufaisha zaidi Mazembe kuliko Yanga yenyewe.

Mazembe ni kubwa kimafanikio kuliko Yanga kimataifa na kipesa huenda. Lakini hatuna uhakika kama ikitokea sheria ya Financial fair play ikaja Africa kama Mazembe, Yanga na timu nyingine zitaweza kujiendesha. Ndio maana kunahitajika Transformation mapema sana.
Inasemekana Nigeria walichukua desa la makao makau yao kutoka ramani ya Dodoma na haimaanishi Tanzania ilikuwa imefanikiwa kuliko Nigeria
 
kule champion leuge awamu hii hata wale waliotudhulumu tutawavunja ngoko na hata viuno wasisubutu kujaribu kutuzuia tena kwa dhuluma
Kule CAFCL hatukudhurumiwa ndugu, Yanga haina wapigaji wazuri wa penati na hiyo ndiyo sababu iliyotufanya tuishie robo.

Ni vyema viongozi wakafanya usajili wa maana ili CAFCL ijayo tutwae kombe kabisa
 
“Tumepokea ugeni mzito kutoka moja ya Klabu kubwa Barani Afrika, TP Mazembe ya DR Congo ambao wamevutiwa na namna Klabu yetu ya Yanga inavyoendeshwa hivyo wamekuja hapa Tanzania kujifunza mambo mbalimbali kwenye Mfumo wetu wa Mabadiliko ya Uendeshaji" Simon Patrick, Mkurugenzi wa Sheria wa Yanga SC.
---

Pia tutakuwa na makubaliano rasmi ya urafiki wa kushirikiana kati ya Klabu yetu ya Yanga na TP Mazembe ili kuweza kubadilisha ujuzi wa mambo mbalimbali ya kimpira yatakayoweza kuisaidia Klabu yetu.

Klabu kubwa kama TP Mazembe imesafiri kutoka DR Congo kuja hapa Jangwani kujifunza kwa kichwa chetu, Rais wetu Eng. Hersi Said halafu kuna watu wako nyumba ya 16 tu jirani hapo, wanapiga kelele kuwa hawana cha kujifunza kwa Yanga. Niwaambie tu, tutabeba Makombe hadi kila Mwanachama atakuwa anabeba la kuweka nyumbani kwake

#timuyawananchi
#daimambelenyumamwiko

Je Kuna ukweli kuwa Yanga ndio workshop ya soka hapa Afrika???
Wanafundishwa jinsi ya kutuma miamala kwa marefa
 
Nilikua Borgsburg naangalia mpira Wazambia na Wapopo walikuwepo nifurahi kuona wanaipa Heshima Yanga maana huku Dzonga walikua wanatudharau sana toka tumewakimbiza Mamelodi wametupa heshima yetu..
 
Goli la key 🔑. Lililochinjiwa baharini na V.A.R na referee akashindwa kuhakiki na kutoa haki🤔
Huyo huyo key 🔑alipopewa nafasi ya kwanza kwenye kupiga penati alimpasia tu Williams badala ya kushusha shuti la nguvu ili kurudisha goli lake alilodhurumiwa.

Tukubali tu Yanga hatuna wapigaji wazuri wa penati, viongozi wetu wafanye sajili za maana ili kuzlrekebisha kasoro zilizo tokea pale Pretoria zisijirudie kwa msimu ujao wa CAFCL.
 
Nilikua Borgsburg naangalia mpira Wazambia na Wapopo walikuwepo nifurahi kuona wanaipa Heshima Yanga maana huku Dzonga walikua wanatudharau sana toka tumewakimbiza Mamelodi wametupa heshima yetu..
Yanga ni kama maji mkuu
 
Back
Top Bottom