Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

20240430_102052.jpg

Hii kuchanika kwenye kona shida ni nini? ubora wa tofari au mvutano wa kuta?
 
View attachment 2977303
Hii kuchanika kwenye kona shida ni nini? ubora wa tofari au mvutano wa kuta?
Kuna sababu nyingi zinazopelekea kuta zinazounda kona kupata nyufa katika maungio na ili ujue sababu ya kutokea hiyo nyufa ni vizuri mtaalam akafika eneo la site akakagua vizuri.

Mtaalam itabidi aangalie pattern ya nyufa jinsi ilivyo ambapo itamsaidia kujua kama nyufa imesababishwa na vertical ama lateral movement (hapa sijui niitaje, mjongeo wima na mjongeo mlalo)

Wakati mwingine unakuta huo ufa haujafika mpaka kwenye kuta (non structural cracks), hivyo unatakiwa ukwangue hiyo powder, ukiona nyufa imefika na kwenye plaster, menya tena na hiyo plaster tararibu ili ujue kama ukuta nao umefikiwa na hiyo crack (structural crack) au lah. Fundi asiwe na haraka tu ya kuanza kutindua ukuta kwa sababu kule kutindua tu kunaweza kukaongeza tatizo zaidi
 
Katika ujenzi wa chemba za vyoo, hakikisha kuta zote nne za chemba zinajitegemea (usitumie ukuta wa nyumba kama moja ya kuta za chemba hata kama chemba ipo karibu na nyumba). Utafanya kuta zako ziloane kutokana na maji yanayopita kila mara katika chemba na kupelekea rangi/plaster kubanduka (ukuta kuoza)

Ramani, Makadirio au Ushauri kuhusu Ujenzi tuwasiliane
 
Katika uletaji wa tofali site, trip ya kwanza huwa zinakuja idadi kamili ili kusoma ramani ya site kama kuna mfatiliaji anayefatilia kuhesabu idadi au lah. Mfano kama umelipia tofali 3000 na kila trip gari ikawa inabeba tofali 300 maana yake gari italeta trip 10
Wakishagundua kwamba hamna mtu anayehesabu na wakati huo tofali zinatumika katika ujenzi, trip ya pili na kuendelea wanakuwa wanapunguza idadi(badala ya kubeba tofali 300, wanabeba hata pc 280)

Hasara = (300-280)pc x 9trip x Tsh 1,000 = Tsh 180,000/=

Hili sasa linakuwa ni dili la muuzaji (mahali ulipolipia) na dereva wa gari linaloleta tofali

Maboss wengi huwa wanahesabu trip tu, zikishatimia idadi ya trip wanaridhika


Ramani, Makadirio au Ushauri kuhusu Ujenzi tuwasiliane
 
Kipindi cha upepo mkali kama hichi, nyumba nyingi bati zake huezuliwa na upepo. Kama nyumba yako hujaweka fascia board, nyumba yako itakuwa katika risk kubwa ya kuezuliwa paa na upepo.

Fascia board ni zile mbao za 1×6,1x8, au 1×10 ambazo huwa zinapigiliwa kuzunguka paa la bati (ambapo mkingio wa maji (gutter) hupigiliwa)

Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
 
Wale ndugu zangu ambao makazi yenu yapo pembezoni mwa mto, njia pekee ya kukabiliana na hayo maji yasiweze kuathiri makazi yenu ambayo ni ya uhakika ni kutumia Gabions.

Gabions ni yale mawe meusi ambayo huwa yanapangwa pembezoni mwa mto, yanafungwa na wavu ambao haupati kutu (galvanized). Mawe meusi ni mazuri zaidi kwa sababu yenyewe hayafyonzi maji kama ilivyo kwa mawe mengine
 
Wale ndugu zangu ambao makazi yenu yapo pembezoni mwa mto, njia pekee ya kukabiliana na hayo maji yasiweze kuathiri makazi yenu ambayo ni ya uhakika ni kutumia Gabions.

Gabions ni yale mawe meusi ambayo huwa yanapangwa pembezoni mwa mto, yanafungwa na wavu ambao haupati kutu (galvanized). Mawe meusi ni mazuri zaidi kwa sababu yenyewe hayafyonzi maji kama ilivyo kwa mawe mengine
Ni Njia nzuri sana hii ila aisee maji yakiwa mengi sana taratiiibu yanakula udongo unaoegemewa/shika hizo gabions na mwishowe taritiiibu zinaporomoka zenyewe dah nimeshuhudia hii sehemu nyingi sana. Kama mtu bado ana nguvu za fedha hata kama ni kidogo ni heri akatafuta eneo jingine zuri la kuishi.
 
Ni Njia nzuri sana hii ila aisee maji yakiwa mengi sana taratiiibu yanakula udongo unaoegemewa/shika hizo gabions na mwishowe taritiiibu zinaporomoka zenyewe dah nimeshuhudia hii sehemu nyingi sana. Kama mtu bado ana nguvu za fedha hata kama ni kidogo ni heri akatafuta eneo jingine zuri la kuishi.
Wanakosea namna ya kuziweka, mawe inatakiwa yapangwe katika namna ambayo mtu akitaka kuingia mtoni awe anashuka kama anavyochuka kwenye ngazi. Chunguza hata kwenye madaraja makubwa, utaona njia hii ndio inayotumika sana, kabla ya kupanga hayo mawe chini huwa inatangulia zege (nitawaletea picha baadae)
 
Wanakosea namna ya kuziweka, mawe inatakiwa yapangwe katika namna ambayo mtu akitaka kuingia mtoni awe anashuka kama anavyochuka kwenye ngazi. Chunguza hata kwenye madaraja makubwa, utaona njia hii ndio inayotumika sana, kabla ya kupanga hayo mawe chini huwa inatangulia zege (nitawaletea picha baadae)
ok sawa mtaalamu shukrani
 
Hechy Essy
Kuhusu kulaza au kusimamisha matofali kwenye ujenzi wa nyumba ya kawaida ghorofa 1 kipi ni sahihi?
Maana kuna wanaosema kuwa ukitumia nondo 4 za mm16 kwenye nguzo tofali unaweza kusimamisha na wala hamna shida.
Then kuna wanasema ukitumia nondo 6 za mm12 basi tofali ndo utazilaza, na wakati huohuo bado kuna wanaotumia nondo hizo 6 za mm 12 na bado tofali zinasimamishwa.
Nimeona ujenzi wa nyumba Uganda, Nigeria, Kenya mara nyingi tofali hawalazi tena basi za kwao ni hollow blocks, sasa najuliza kipi ni sahihi kiutaalamu.
Then kwa sasa kuna ujenzi ule wa pre casted slab ambapo unakuta kwenye slab wanapanga tu hollow blocks, then kuna mapande marefu ya zege wanayapanga, then kuna wire mesh inatandikwa au wanaweka tu kichanja cha nondo chache then wanamwaga zege, najiuliza ujenzi huo ni sahihi?
Niseme yoyote kwa yote binafsi naamini/nahisi ujenzi huo wooote nilioutaja hapo juu nia yao ni kupunguza gharama sasa je huo ujenzi kiutaalam ni sahihi au ndo baada ya miaka kadhaa kupita tutegemee majanga?
 
Plaster nzuri ni ile ambayo ukimwagia ukuta maji, ukuta unakauka bila kuchora alama za matofali. Kiujumla michoro ya tofali katika ukuta uliopigwa plaster hutokea pale ratio ya udongo uliotumika kujengea tofali ni kali kuzidi ratio ya udongo uliotumika kupigia plaster

Kitaalam udongo wa kujengea tofali tunatumia ratio ya 1:6 na udongo wa kupigia plaster tunatumia ratio ya 1:4 na 1:5 (ratio ya 1:4 inatumika kwenye kuta upande wa nje, na 1:5 upande wa ndani)

Ratio ya plaster inatakiwa iwe kali kuzidi ratio ya udongo uliotumika kujengea

Kwa mahitaji ya ramani, makadirio ya vifaa vya ujenzi tuwasiliane
weka mawasiliano na gharama zako zipoje
 
Hechy Essy
Kuhusu kulaza au kusimamisha matofali kwenye ujenzi wa nyumba ya kawaida ghorofa 1 kipi ni sahihi?
Maana kuna wanaosema kuwa ukitumia nondo 4 za mm16 kwenye nguzo tofali unaweza kusimamisha na wala hamna shida.
Then kuna wanasema ukitumia nondo 6 za mm12 basi tofali ndo utazilaza, na wakati huohuo bado kuna wanaotumia nondo hizo 6 za mm 12 na bado tofali zinasimamishwa.
Nimeona ujenzi wa nyumba Uganda, Nigeria, Kenya mara nyingi tofali hawalazi tena basi za kwao ni hollow blocks, sasa najuliza kipi ni sahihi kiutaalamu.
Then kwa sasa kuna ujenzi ule wa pre casted slab ambapo unakuta kwenye slab wanapanga tu hollow blocks, then kuna mapande marefu ya zege wanayapanga, then kuna wire mesh inatandikwa au wanaweka tu kichanja cha nondo chache then wanamwaga zege, najiuliza ujenzi huo ni sahihi?
Niseme yoyote kwa yote binafsi naamini/nahisi ujenzi huo wooote nilioutaja hapo juu nia yao ni kupunguza gharama sasa je huo ujenzi kiutaalam ni sahihi au ndo baada ya miaka kadhaa kupita tutegemee majanga?
Kulaza ama kusimamisha tofali inategemea na jengo lilidesigniwa namna gani (framed structure ama load bearing structure). Mfano yale majengo ya mjini ambayo unaona wanajenga tu nguzo,mkanda,slab, nguzo,mkanda,slab mpaka juu (ghorofa ya mwisho) yale uzito wake unabebwa na lile lifrem la zege unaloliona na kupelekwa moja kwa moja ardhini (slab>beam>column>footing>soil) hivyo kuta zake zote hazihusiki katika ubebaji wa mzigo badala yake zinakuwa na kazi ya kuziba tu uwazi au kufanya partition na ndio maana utaona tofali zake zinasimamishwa kuanzia floor ya kwanza mpaka mwisho na huwa zinajengwa mwishoni baada ya hilo lifrem kukamilika

Kwa hizi ghorofa za kawaida, mfumo wake wa ujenzi unafanya kuta nazo zihusike katika ubebaji wa mzigo ndio maana tofali zake zinalazwa (zege ya beam inamwagwa juu ya ukuta tofauti na ilivyo kwenye framed structure ambapo zege inakuwa supported na formwork na baada ya kufikia ukomavu kiasi flan, formwork inatolewa)

Kama jengo litakuwa limefanyiwa design ambayo kuta zake zitakuwa hazihusiki katika ubebaji wa mzigo basi hata ukisimamisha tofali inakuwa haina shida, lakini kama design ilikusudia kuta ziwe zinabeba mzigo halafu wewe ukawa umesimamisha hizo tofali maana yake kuna uwezekano mkubwa hizo kuta zikashindwa kubeba huo mzigo uliokusudiwa.
 
Kulaza ama kusimamisha tofali inategemea na jengo lilidesigniwa namna gani (framed structure ama load bearing structure). Mfano yale majengo ya mjini ambayo unaona wanajenga tu nguzo,mkanda,slab, nguzo,mkanda,slab mpaka juu (ghorofa ya mwisho) yale uzito wake unabebwa na lile lifrem la zege unaloliona na kupelekwa moja kwa moja ardhini (slab>beam>column>footing>soil) hivyo kuta zake zote hazihusiki katika ubebaji wa mzigo badala yake zinakuwa na kazi ya kuziba tu uwazi au kufanya partition na ndio maana utaona tofali zake zinasimamishwa kuanzia floor ya kwanza mpaka mwisho na huwa zinajengwa mwishoni baada ya hilo lifrem kukamilika

Kwa hizi ghorofa za kawaida, mfumo wake wa ujenzi unafanya kuta nazo zihusike katika ubebaji wa mzigo ndio maana tofali zake zinalazwa (zege ya beam inamwagwa juu ya ukuta tofauti na ilivyo kwenye framed structure ambapo zege inakuwa supported na formwork na baada ya kufikia ukomavu kiasi flan, formwork inatolewa)

Kama jengo litakuwa limefanyiwa design ambayo kuta zake zitakuwa hazihusiki katika ubebaji wa mzigo basi hata ukisimamisha tofali inakuwa haina shida, lakini kama design ilikusudia kuta ziwe zinabeba mzigo halafu wewe ukawa umesimamisha hizo tofali maana yake kuna uwezekano mkubwa hizo kuta zikashindwa kubeba huo mzigo uliokusudiwa.
Shukrani Eng. kwa kushare utaalamu wako kwa hiyo inawezekana jengo let say residential G+1 kufanyiwa design kuwa nondo za 12mmm ndo zitumike kwenye nguzo badala ya 16mm?
 
Shukrani Eng. kwa kushare utaalamu wako kwa hiyo inawezekana jengo let say residential G+1 kufanyiwa design kuwa nondo za 12mmm ndo zitumike kwenye nguzo badala ya 16mm?
Inategemea na kiasi cha uzito utakaobebwa na nguzo, lakini yote kwa yote nguzo ni vizuri minimum size ya nondo ikaanzia 16mm japo kuwa mahesabu yanaweza yakaifanya nondo ya 12mm nayo ikapass kutokana na ushirikiano wa kuta na nguzo katika ubebaji wa mzigo
 
Mimi huwa namjibu mtu kulingana na namna alivyouliza...kwani wangapi huko juu wameuliza maswali kwa lengo la kutaka kujua na nimewajibu tu vizuri? Mtu anayeuliza kwa lengo la kutaka kujua anauliza namna hiyo? We umekuja kwa lengo la kubishana, kwamba uonekane we ni mjuzi zaidi kuliko wengine. Endelea tu na nyuzi zako bro, mimi nipo hapa kibiashara sijaja kubishana na watu, atakayeuliza kistaarabu nitamjibu kistaarabu pia (mimi ni mtu mmoja peace sana, sipendagi kujibizana na watu kwa sababu ambazo hazina msingi)
Tafadhali jibu swali la aliyekuuliza. Jibu lako litatusaidia hata sisi tunaotarajia kujenga karibuni.
Kama hujui ni bora ukasema hujui kuliko kujificha kwa kumshambulia muuliza swali
 
Umeshawahi kuona dirisha la aluminium lina vitundu vidogo katika ubao wake wa chini kwa nje?

Vile vitundu watu huwa wanaviweka makusudi ili maji ya mvua yanapoingia kwenye ule mfereji wa dirisha, maji yaweze kutoka nje kupitia hivyo vitundu

Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
 
Katika upauaji wa nyumba, matumizi ya wall plate (nadhani kwa Kiswahili huwa tunaziita mtambaa wa Panya, kiufupi wall plate ni mbao ambazo zinalazwa kiubapa juu ya kuta katika zoezi la upauaji, mara nyingi huwa tunatumia mbao za 2 by 4) husaidia kutawanya mzigo wa paa kuzunguka kuta zote (line load).

Usipoweka mbao za wall plate, utafanya mzigo wa paa katika kuta uwe unajikusanya sehemu moja (point load) na hivyo kuta zako zitakuwa katika hatari ya kupata nyufa hasa katika sehemu ambazo mbao za tie beam zinaegemea

Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
 
Saruji ikihifadhiwa vizuri, inaweza kudumu kwa muda wa miezi mitatu tangu siku ilipotengenezwa. Usije ukajichanganya ukanunua mifuko yako ya saruji na kuiweka store ili uje uitumie huko mbeleni, unaweza ukakuta mifuko yote imeshaganda na kuwa mawe


Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
 
Mbao za fascia board ni vizuri ukaziranda zote huko huko hardware unaponunulia ili kupata muonekano mzuri wa paa lako baada ya kukamilika

Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
 
Back
Top Bottom