Wakulenga
Member
- Jul 1, 2015
- 77
- 134
Habari zenu members,
Leo nimetumia muda mrefu saana kuongea na kucheka na mke wangu(huaga nafanyaga hivo siku moja moja) maana huyu mwanamke hana utofauti na wanawake wengine kwahiyo naishi nae kwa akili saana.
Hivyo baada ya furaha ya muda ikabidi akili inikumbushe namna nilivompata huyu mwanamke na kumuoa baadae.
Ilikuwa mwaka 2012 wakati niko advance shule flani hivi nakumbuka ilikuwa kipindi cha kupokea wanafunzi wa form 5.
Bahati mzuri nilimuona jamaa mmoja hivi ambae nilisoma nae o-level nilikuwa sijuani nae saana ila kwa vile alinikumbuka ikabidi nimpokee, nikaenda nae room akatulia wakati wachakula cha mchana nikaenda kuchukua chakula nikala nae.
Siku iliyofuata tukaingia darasani mi nikamwambia yule chalii akomae tu palepale kwakuwa kulikuwa na kitanda ambacho hakina mtu so atalala tu.
Kweli chalii akalala pale na siku zikasonga, tukawa tunashare vitu yaan kama kuna kitu anakihitaji alafu mi sipo anafungua tu tranka langu anacheki kama kipo anachukua nami pia nacheki kwake kama kipo najichukulia.
Sasa siku moja katika pekuapekua kwenye tranka lake nikakutana na karatasi ya majina na namba za simu za watu aliosoma nao, alafu kwenye yale majina nikaona jina na msichana ambae alikuwa mtulivu mno shuleni ila nilimtangulia darasa moja.
Dah sikufikiria mzee nikachukua ile namba nikaandika kwenye karatasi nikaweka kweny tranka langu, siku iliyofuata nikaenda kuazima simu nikamcheki bahati mzuri akapatikana.
Nikaanza kushusha mistari ya kitoto, akanijibu kuwa ana mtu nikasema basi sawa isiwe shida ila akaniambia tuwe tu tunawasiliana nikajisemea tu mwenyewe huu mtego huenda hana mtu.
Basi tukawa tunawasiliana miaka miwili baadae akaniambia amekubali, duh nami nikawa nimeshajikanyaga sehem huko nikasema isiwe kesi haina shida twende tuishi.
Nikaenda nae manzi ila mim moyo wangu ulikuwa umerudi flani hivi sio kama mwanzo.
baada ya muda tukazinguana tukamwagana nikawa naendelea na maisha yangu ya chuo, nikimpigia simu tunaongea kawaida tu.
Baada ya muda manzi akapata post ya ajira akaniambia, nikamwambia sawa hongera, ooh baadae akanicheki tena akaniambia anaomba tuendelee nikamwambia haina shida maana nilishaona nina sehem yakuegemea.
Haikupita muda tukaoana mpaka leo hii niko nae nina miaka 7 kwenye ndoa.
Mimi sina ajira ila yeye ameajiriwa.
Hii siri sijawahi mwambia yy wala yule mshikaji na naamin sitakuja kuwaambia.
Na wewe kama hutojali tuambie huyo uliyefunga nae ndoa ulimpataje mpaka mkafunga ndoa na mna mda gani kwenye ndoa?
Leo nimetumia muda mrefu saana kuongea na kucheka na mke wangu(huaga nafanyaga hivo siku moja moja) maana huyu mwanamke hana utofauti na wanawake wengine kwahiyo naishi nae kwa akili saana.
Hivyo baada ya furaha ya muda ikabidi akili inikumbushe namna nilivompata huyu mwanamke na kumuoa baadae.
Ilikuwa mwaka 2012 wakati niko advance shule flani hivi nakumbuka ilikuwa kipindi cha kupokea wanafunzi wa form 5.
Bahati mzuri nilimuona jamaa mmoja hivi ambae nilisoma nae o-level nilikuwa sijuani nae saana ila kwa vile alinikumbuka ikabidi nimpokee, nikaenda nae room akatulia wakati wachakula cha mchana nikaenda kuchukua chakula nikala nae.
Siku iliyofuata tukaingia darasani mi nikamwambia yule chalii akomae tu palepale kwakuwa kulikuwa na kitanda ambacho hakina mtu so atalala tu.
Kweli chalii akalala pale na siku zikasonga, tukawa tunashare vitu yaan kama kuna kitu anakihitaji alafu mi sipo anafungua tu tranka langu anacheki kama kipo anachukua nami pia nacheki kwake kama kipo najichukulia.
Sasa siku moja katika pekuapekua kwenye tranka lake nikakutana na karatasi ya majina na namba za simu za watu aliosoma nao, alafu kwenye yale majina nikaona jina na msichana ambae alikuwa mtulivu mno shuleni ila nilimtangulia darasa moja.
Dah sikufikiria mzee nikachukua ile namba nikaandika kwenye karatasi nikaweka kweny tranka langu, siku iliyofuata nikaenda kuazima simu nikamcheki bahati mzuri akapatikana.
Nikaanza kushusha mistari ya kitoto, akanijibu kuwa ana mtu nikasema basi sawa isiwe shida ila akaniambia tuwe tu tunawasiliana nikajisemea tu mwenyewe huu mtego huenda hana mtu.
Basi tukawa tunawasiliana miaka miwili baadae akaniambia amekubali, duh nami nikawa nimeshajikanyaga sehem huko nikasema isiwe kesi haina shida twende tuishi.
Nikaenda nae manzi ila mim moyo wangu ulikuwa umerudi flani hivi sio kama mwanzo.
baada ya muda tukazinguana tukamwagana nikawa naendelea na maisha yangu ya chuo, nikimpigia simu tunaongea kawaida tu.
Baada ya muda manzi akapata post ya ajira akaniambia, nikamwambia sawa hongera, ooh baadae akanicheki tena akaniambia anaomba tuendelee nikamwambia haina shida maana nilishaona nina sehem yakuegemea.
Haikupita muda tukaoana mpaka leo hii niko nae nina miaka 7 kwenye ndoa.
Mimi sina ajira ila yeye ameajiriwa.
Hii siri sijawahi mwambia yy wala yule mshikaji na naamin sitakuja kuwaambia.
Na wewe kama hutojali tuambie huyo uliyefunga nae ndoa ulimpataje mpaka mkafunga ndoa na mna mda gani kwenye ndoa?