Hii tabia imekuwa sugu; mtu anaamua tu aje Dar kukusalimia na afikie kwako

Mkifa mitoto yenu inarudi mikoani kunyanyaswa......ndugu mliowaita wanoko hamuwataki wanachukua Mali zote ulizochuma....mke wa marehemu akishtaki,ndugu hutumia pesa za marehemu kushinda kesi....Hapo marehemu umelala kimya kaburini.Hii ndiyo dunia mkuu
Acha uoga wa kijinga. Mtu ashindwe kuishi maisha yake kwa kuhofia atakufa siku moja? Kuna ambaye hatokufa? Kama una mali unashindwa hata kuandaa wosia juu ya warithi wa mali zako?
 
Duuuh! nilirudi kijijini kwetu,nikakuta stori ya bibi mmoja,alienda kwa mwanae mjini,alinyanyasika Sana,hadi akaomba arudi kijijini kwenye maisha ya shida.Watu wa mjini msiwadharau watu wa kwenu,chakula tu au malazi ni nongwa...?
Anyway mnasubiriwa,mkifa mkazikwe huko vijijini,ambako wachimba kaburi mtawakuta haohao mnaowajandia,wasije makwenu.
 
Umeandika yote kwa usahihi lakini chanzo cha yote ni UMASIKINI NA BAJETI ULIYO NAYO ISIYONYUMBULIKA.

Mtu kuja kwako lazima atoe taarifa hili naunga hoja kwa 100% ndiyo mfumo wa maisha.

Lakini mtu anapokuja bila taarifa ameshakuja tayari, hatuangalii madhaifu ya kuja bila taarifa muda huo tunakabiliana na shida ya kuja kwake bila taarifa.

Mtu msitaarabu na mwenye uwezo na bajeti ya ziada ambaye hayana dhiki na umasikini, atamkaribisha mgeni atampeleka nyumbani, atampa maji,chakula na mengineyo, haijalishi utamlaza sebuleni, kwenye ukumbi wa nyumba, jikoni kwenye korido siku kwanza ipite.

Kukicha au ucku ule ule unamwambia nashukru umekuja lakini ulijisahau kuja bila kuniambia.

Kwangu hakuna nafasi kwa sasa ya kutunza mgeni hatakama nafasi ipo utatumia lugha ya kiutu.

Hivo utakaa hizi cku 3 kwa shida ili tutafute nauli urudi au kama una nauli ya kurudi itabidi urudi siku fulani.

Kama wote hamna nauli hilo sasa ni tatizo ambalo mtajadili kama familia wewe na ndugu zako huko alikotoka kuwa huku hakuna nafasi ya yeye kukaa na wote maisha ni magumu, uzeni mbuzi huko, kuku, bata, njiwa au gunia la mahindi mtume nauli arudi nyumbani.

KUMZIMIA MTU SIMU, KUMKIMBIA STAND NI DALILI ZA UBABAISHAJI, UJANJA UJANJA, UELEWA MDOGO NA UPUUZI.

Pokea simu mwambie ukweli bila kupepesa macho full stop.

Mwisho.

Umasikini ni kitu kibaya sana unaweza kuongozwa na umasikini huo ukahisi uko sahihi maamuzi yako kumbe tu ni umasikini.
 
Ninafikiria ni kwa jinsi gani ninaweza kuwa na roho ya kumtelekeza ndugu au rafiki yangu stendi??!!.... kwa jinsi nilivyokuzwa ni kuwa kutompokea kabisa kiasi cha kutompa hata hifadhi ya usiku mmoja ni dhambi kubwa na ikigundulika ni kesi nzito kuanzia kwa baba na mama mzazi. Tujitahidi tu kuwa wakarimu kwa wageni wetu bila kuchotwa sana na tamaduni za magharibi. Wewe mwache aje kisha mlaze hata bafuni kuliko kumtelekeza kabisa. Haya maisha hayana mjanja... mambo kama ajali, kesi mahakamani, magonjwa au jela yanaweza kubadili kabisa title yako na ukawa tegemezi kwa unaowatelekeza stendi.
 
Acha uoga wa kijinga. Mtu ashindwe kuishi maisha yake kwa kuhofia atakufa siku moja? Kuna ambaye hatokufa? Kama una mali unashindwa hata kuandaa wosia juu ya warithi wa mali zako?
Kinacholeta shida ni umaskini. Watu wengi wa mji ni maskini sana kiasi kwamba wanachokipata hakitoshelezi hata kwa familia zao tu. Pia utakuta baba, mama na watoto wanaishi chumba kimoja. Yaani balaa.
 
Ninafikiria ni kwa jinsi gani ninaweza kuwa na roho ya kumtelekeza ndugu au rafiki yangu stendi??!!.... kwa jinsi nilivyokuzwa ni kuwa kutompokea kabisa kiasi cha kutompa hata hifadhi ya usiku mmoja ni dhambi kubwa na ikigundulika ni kesi nzito kuanzia kwa baba na mama mzazi. Tujitahidi tu kuwa wakarimu kwa wageni wetu bila kuchotwa sana na tamaduni za magharibi. Wewe mwache aje kisha mlaze hata bafuni kuliko kumtelekeza kabisa. Haya maisha hayana mjanja... mambo kama ajali, kesi mahakamani, magonjwa au jela yanaweza kubadili kabisa title yako na ukawa tegemezi kwa unaowatelekeza stendi.
Semina nzuri, ili angalau hayo yawezekane basi hebu tumia nafasi yako kumwomba asikubali kila jambo analopelekewa mezani maana wanamharibia na matokeo yake maisha yanakuwa magumu mwisho tunakimbiana mjini
Screenshot_20231101_173957_Samsung Internet.jpg
 
Hii tabia imekuwa sugu. Yaani mtu anakaa tu na halmashauri ya kichwa chake anaamua kuwa nimpigie jamaa yangu yupo Dar nikafikie kwake.

Mi nipo zangu home jana inaingiza simu ya Abouu. Ananiuliza maisha vipi namwambia safi tunalisongesha. Maneno maneno mengi mwisho anasema nipo Dar nataka nije kwako nielekeze. Nikamuuliza wakati unapanga kuja ulinishirikisha? Unaamua tu kuja kwangu hata hujanitaarifu.

Jamaa ame mind kawaambia watu nimemkataa. Ninyi wa Mikoani mnadhani huku ni kama kwenu huko ambako hamna ratiba maalum. Mnajiamulia tu.

Mwaka juzi nlimwacha mtu stand kwa upuuzi kama huo. Kakaa zake Mbwinde mwisho kaamua kuja town a anipigia simu kuwa yupo Dar anataka aje home. Nlimwambia tu kuwa sipo home na familia tumesafiri.

Akaanza kuomba basi nimpatie pesa ya sehemu ya kulala anisubiri. Nilimwambia mwezi mzima sitokuwa home. Akataka nimtumie nauli. Nlizima na simu kabisa. Huu ni wendawazimu.

Halafu tukiwaakaribisha mnaenda kutusema kijijini kuwa huku tunaishi maisha mazuri sana hatuwajali watu wa vijijini. Mnaenda kutuponda sana kijijini kuwa tunatumia pesa vibaya.
Tusameheni wakuu...

Siku nyingine tukitaka kuja huko Daslaam tutatoa taarifa mapema.

Saint Anne
 
Jam

Jamaa mbona una hasira dhidi ya ndugu zako wallikufanya nini mpaka unawaitia Mijitu?

Mkuu Jaribu kuwa Mnyenyekevu basi.

Hao unaowadharau ipo siku utawakumbuka na hutawaona.

Kama huwezi kumsaidia mtu basi achana naye ila usimpe majina mabaya eti Mijitu.....Itakuwa wewe Kweli Umeolewa maana hizo hasira tu sio kidogo.
Jamaa amezingua sana....ila msamehe bure tu, hajui atendalo.
 
Hii tabia imekuwa sugu. Yaani mtu anakaa tu na halmashauri ya kichwa chake anaamua kuwa nimpigie jamaa yangu yupo Dar nikafikie kwake.

Mi nipo zangu home jana inaingiza simu ya Abouu. Ananiuliza maisha vipi namwambia safi tunalisongesha. Maneno maneno mengi mwisho anasema nipo Dar nataka nije kwako nielekeze. Nikamuuliza wakati unapanga kuja ulinishirikisha? Unaamua tu kuja kwangu hata hujanitaarifu.

Jamaa ame mind kawaambia watu nimemkataa. Ninyi wa Mikoani mnadhani huku ni kama kwenu huko ambako hamna ratiba maalum. Mnajiamulia tu.

Mwaka juzi nlimwacha mtu stand kwa upuuzi kama huo. Kakaa zake Mbwinde mwisho kaamua kuja town a anipigia simu kuwa yupo Dar anataka aje home. Nlimwambia tu kuwa sipo home na familia tumesafiri.

Akaanza kuomba basi nimpatie pesa ya sehemu ya kulala anisubiri. Nilimwambia mwezi mzima sitokuwa home. Akataka nimtumie nauli. Nlizima na simu kabisa. Huu ni wendawazimu.

Halafu tukiwaakaribisha mnaenda kutusema kijijini kuwa huku tunaishi maisha mazuri sana hatuwajali watu wa vijijini. Mnaenda kutuponda sana kijijini kuwa tunatumia pesa vibaya.
Siku watakapoamua kukusafirisha hao ndio wachimba kaburi wagawa chakula kwenye msiba wako be humble brother..
 
Mbaya zaidi MTU akishakaa kwako siku akiondoka huko anakofikia Ni kumsema mkeo vibaya.

Mara jamaa kaolewa maana yule mke Ni mvivu. Mke mchoyo, mke anadharau n.k

Kumbukeni mke wangu Ni pambo la nyumba yangu, sio MTU wa kusonga ugali kwa ajili ya mijitu ya kijijini.

Mke wangu ashindwe kunilisha vipaja vya kuku kisa Kuna mgeni au mke wangu asiwe na Uhuru wa kujiachia nyumbani kwake kisa mgeni!

Kwendreni huko.
Kama anakubana kwanini usimtimue..

Umaskini ni janga.
 
Hii tabia imekuwa sugu. Yaani mtu anakaa tu na halmashauri ya kichwa chake anaamua kuwa nimpigie jamaa yangu yupo Dar nikafikie kwake.

Mi nipo zangu home jana inaingiza simu ya Abouu. Ananiuliza maisha vipi namwambia safi tunalisongesha. Maneno maneno mengi mwisho anasema nipo Dar nataka nije kwako nielekeze. Nikamuuliza wakati unapanga kuja ulinishirikisha? Unaamua tu kuja kwangu hata hujanitaarifu.

Jamaa ame mind kawaambia watu nimemkataa. Ninyi wa Mikoani mnadhani huku ni kama kwenu huko ambako hamna ratiba maalum. Mnajiamulia tu.

Mwaka juzi nlimwacha mtu stand kwa upuuzi kama huo. Kakaa zake Mbwinde mwisho kaamua kuja town a anipigia simu kuwa yupo Dar anataka aje home. Nlimwambia tu kuwa sipo home na familia tumesafiri.

Akaanza kuomba basi nimpatie pesa ya sehemu ya kulala anisubiri. Nilimwambia mwezi mzima sitokuwa home. Akataka nimtumie nauli. Nlizima na simu kabisa. Huu ni wendawazimu.

Halafu tukiwaakaribisha mnaenda kutusema kijijini kuwa huku tunaishi maisha mazuri sana hatuwajali watu wa vijijini. Mnaenda kutuponda sana kijijini kuwa tunatumia pesa vibaya.
Mkuu usikimbie majukumu 😅😅..
Mpokee tu, kama mlivyokuwa mnaishi vizuri huko kijijini ishini vizuri tu na huko Mjini!
 
Back
Top Bottom