Arusha: Benki yatoa pikipiki 20 kwa Jeshi la Polisi, RC Makonda awakabidhi

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,925
12,204
Jeshi la Polisi mkoa wa Arusha leo Mei 16, 2024 limepokea msaada wa pikipiki 20 toka benki ya CRDB kwa ajili ya kuimarisha usalama wa raia na mali zao katika Mkoa huo.

Akikabidhi pikipiki hizo Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe; Paul Makonda amesema pikipiki hizo zimetolewa kwa Jeshi la Polisi ikiwa ni utekelezaji wa sehemu ya ahadi yake aliyoitoa hivi karibuni ya kutoa pikipiki hamsini kwa Jeshi la Polisi kwa ajili ya kuimarisha usalama katika Jiji la Arusha hasa kwa kuzingatia ni kitovu cha Utalii hapa Nchini.
WhatsApp Image 2024-05-16 at 17.40.35_cac7a54b.jpg
Mkuu huyo wa Mkoa amebainisha kuwa mbali na kutolewa kwa pikipiki hizo leo, amesema kabla ya kumaliza siku mia moja za Uongozi wake katika mkoa huo, atahakikisha anakamilisha ahadi yake aliyoitoa ya kutoa baiskeli mia moja, pikipiki hamsini na magari ishirini kwa Jeshi la Polisi.

Mheshimiwa Makonda amelitaka Jeshi la Polisi kuhakikisha linaimarisha usalama maeneo yote katika Mkoa huo ili uendelee kuwa shwari, na shughuli za utalii zifanyike kwa amani na utulivu.
WhatsApp Image 2024-05-16 at 17.40.36_d331a2ed.jpg

WhatsApp Image 2024-05-16 at 17.40.36_cec0412f.jpg

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo Bwana Abdulmajid Nsekela amesema suala la usalama ni jambo la muhimu hasa kipindi hiki ambacho idadi ya watalii imeongezeka mkoani humo hivyo benki hiyo ikaona ni vyema kusaidia vitendea kazi ambavyo vitarahisisha katika utendaji wa kazi.

Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha pamoja na kumshukuru Mkuu wa Mkoa na benki hiyo kwa msaada huo, amebainisha kuwa pikipiki hizo zitasaidia kufanya doria katika mitaa mbalimbali ili kutimiza dhamira ya Serikali ya kuona mkoa huo unakua shwari wakati wote.

Aidha SACP Masejo ametoa onyo kwa baadhi ya watu wachache wanaojihusisha na matukio ya uhalifu kuacha mara moja vitendo hivyo kwani Jeshi hilo limejipanga vyema kuhakikisha Mkoa huo unakua shwari na litaendelea kuchukua hatua za kisheria kwa watakaobainika kutenda uhalifu.
 
Back
Top Bottom