Mdau wa JamiiForums.com ameelezea wasiwasi wake juu ya kuongezeka kwa maambukizi ya ugonjwa wa UTI kwa wanawake.
Anahoji inakuwaje sababu kubwa inayotajwa kuwa ni uchafu ipate mashiko kwa nyakati hizi, kwani wanawake wa zamani ndio walikuwa wasafi zaidi kuliko hawa wa sasa?
Mdau huyu anashauri wataalam wa afya waingie upya maabara kuchunguza nini hasa chanzo halisi cha kuongezeka kwa maambukizi ya UTI. Kwake hoja ya kuwa ugonjwa huu unaweza kusababishwa na uchafu anaona kama haina mashiko.
Sayansi inasemaje juu ya hoja hizi za mdau?
Habari zenu wakuu
Hivi nmekua nikijiuliza sana ni hali ya hewa ndio inapelekea watu kuumwa sana sasahivi au ni nini??
Maana nmekua nikishuhudia watu wangi wakikohoa sana ambapo hali hii yakukohoa wengi wamekua wakieleza kua huwakuta sana ifikapo mida ya saa 12 jioni ambayo huwafanya hata washindwe kulala kwa kikohozi icho kikali.
Je, mabadiliko ya hali ya hewa yana mchango wowote katika kusababisha magonjwa?
Chanzo cha habari gazeti la the The Citizen la leo Machi 30, 2021.
Dunia ina mambo mengi sana na vichekesho vingi sana, Hawa Jamaa Polisi mara ya kwanza waliogopa kutangaza.
Hongereni Polisi kwa kutoa ukweli ingawa mmechelewa mlikuwa mnasoma upepo.
Leo, Machi 15, 2021 Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais wa Tanzania ameanza ziara mkoani Tanga na akiwa kwenye kiwanda kimojawapo alichozindua kinachoshughulika na matunda wilayani Korogwe, alipata nafasi ya kusalimu wananchi baada ya kuombwa na mkuu wa mkoa wa Tanga ambapo alianza na salamu kutoka kwa Rais Magufuli
"Kabla ya kuwapongeza niwasalimie salam za Rais anawasalimia, anasema tuendelee tuchape kazi, kipindi hiki tushikane tujenge mshikamano, tujenge upendo, tuchape kazi tulete tija kwa Taifa letu"
Baada ya salam hizo Mama Samia amewapongeza kwa kuwa na kiwanda kwani ni mkombozi.
Mwananchi Digital imeripoti kuwa katika bandari ya Dar es Salaam kuna malori (magari makubwa ya mizigo) yamekwama kwa siku kadhaa hivyo kusababisha madereva wa maroli kulala na kuamka hapo hadi kufikia siku nne, madereva hao wamedai kulala na kula kwenye magari yao na kuomba kujisadia katika vyoo vya ofisi za jirani kwa kuwa hapo bandarini hakuna vyoo.
Madereva hao wamedai chanzo cha uchelewashaji huo wa mizigo unatokana na ucheleweshwaji wa kupakua na kupakia mizigo na na ucheleweshwaji wa vibali vinavyoruhusu mizigo kusafirishwa.
TRA Wamekanusha Taarifa zilizoandikwa JamiiForums zilizodai Mtandao wao kusumbua.
Wamesema ni taarifa ya Uongo na Uzushi. Kwani imelenga kupotosha na kuleta taharuki miongoni mwa Walipa Kodi pamoja na kuidhalilisha taasisi na Watumishi wake.
Katika kipindi cha mwezi mzima, TRA haikuwa na Hitilafu yoyote.
TRA imewataka Waipa Kodi kuendelea kulipa kodi.
Wakuu hasa wale Wataalamu Wa Chemical na Hata Physics Kwa Ujumla nataka kupata Ufafanuzi hapa Kidogo!
Chupa zetu za Kuhifadhi Joto La Vinywaji au Vimiminika Kama Chai, Kahawa au Maji Moto Ndani Imegundulika Kuna Vidonge!! Naam Ni vidonge!
Video hii inasambaa Mtandaoni Kuhusu Hili Jambo!! TFDA na TBS Lipi Neno Lenu hapa?
Nawasilisha
Kuna madai kuwa Takukuru wameingia nyumbani kwa Kakoko leo ghafla na kumkuta na begi lenye $1,625,800 taslimu baada ya kusimamishwa kazi jana!
Haijulikani hizo alizichota lini, lakini kama ni kweli inawezekana alikuwa akizichota pole pole kwa muda mrefu kidogo na huenda sasa hivi ana 'vijisenti' vingi sana huko Jersey au Switzerland kama yule mzee.
Mkurugenzi wa TAKUKURU akanusha madai haya
Hayawi Hayawi sasa yamekuwa, ilianza kama kamchezo kakuigiza kutokupeana support za kupostiana kati ya Rayvan na wasanii wenzake wawasafi lakini utetezi ukawa mwingi, Ikafuata mama yake Boss wa Rayvan kumkatia Behewa Rayvan huko Instagram yaan Mama Dangote kumunfollow Rayvan.
Zikaja Event zote kubwa za wasafi Ikiwepo EP ya FOA kutopostiwa na kijana huyo Shaban Mwakyusa Almaarufu kama Rayvan na Leo hii kaamua kukata Behewa kwenye Bio yake na kuondoa Taarifa iliyokuwa ikimtambulisha kama msanii wawasafi.
Inasemekana Rayvanny kaondoka Wasafi. Hii ni kweli?
Picha ambayo baadhi ya watu wanadai kuwa inamuonyesha raisi wa Urusi Vladimir Putin akitoa mafunzo kwa wapigania uhuru kusini mwa Afrika ilisambaa na kutumiwa na baadhi ya watu kuhalalisha kuwa nchi za kiafrika zinapaswa kuunga mkono Urusi katika vita vya Ukraine.
Picha hiyo ilisambazwa sana mtandaoni baada ya kuchapiswa katika blogu za Zibwabwe mwishoni mwa mwaka 2018, machapisho hayo yalidai yanamuonyesha Putin katika mafunzo ya kijeshi ya Tanzania kwaajili ya harakati za kupigania uhuru katika nchi za Afrika mwaka 1973.
Chama cha siasa kilijulikano kama Umoja Party (UP) kimeomba usajili wa muda. Chama hicho tayari kimewasilisha maombi ya usajili wa muda ili kuanza kutafuta wadhamini kwa lengo la kupata usajili wa kudumu. Maswali yalikuwa mengi kuhusu nani hasa mwanzilishi wa chama hicho.
Hii ndio taarifa mpya iliyotufikia kwenye Jumatatu hii ya Pasaka , Kwamba Mheshimiwa Juma Raibu aliyekuwa Meya wa Manispaa ya Moshi Mkoani Kilimanjaro , kabla ya kung'olewa hivi karibuni , ameanza kampeni kabambe ya kuondoa miundo mbinu yote aliyojitolea akiwa madarakani .
Wakati wa madaraka yake alisaidia kutengeneza miundo mbinu ya maji kwenye uwanja wa Mandela uliopo Kata ya Pasua , ili kusaidia vijana wanaotumia uwanja huo , Sasa baada ya kung'olewa kwenye Umeya naye akaamua Kama Mmbwai basi iwe Mmbwai tu , kang'oa miundo mbinu yote ya maji aliyosaidia .
Zipo Taarifa kwamba anapanga kung'oa mabati yote aliyosaidia kwenye mashule mbalimbali pamoja na Zahanati .
Akijibu tuhuma hizo, Juma Raibu amesema: “Siwezi ondoa misaada...
Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam nchini Tanzania imewatangazia kuanzia kesho Alhamisi bodaboda na bajaji zote hazitaruhusiwa kuingia katikati ya Jiji hilo.
Kumekuwa na madai ya kwamba wasanii walioambatana na Rais Samia Suluhu katika safari ya Royal Tour walikuwa wakilipwa Tsh. Milioni 3 ya kitanzania kama pesa yao ya kujikumu kwa siku nzima kwa siku zote walizokuwepo nchini Marekani.
Watumiaji mitandao ya kijamii bado wanauliza kama Rihana na Asap Rocky huenda wameachana baada ya chapisho la mmoja wa mashabiki wa muziki kuchapisha kuwa Rihana na Asap wameachana na kupelekea kusambaa sehemu mbalimbali duniani.
Zimesambaa picha za Darasa chakavu lililojengwa kwa udongo katika mitandao mbalimbali. Baadhi ya wanaharakati wakidai kuwa darasa hilo ni la Shule ya msingi Litingi, kijiji cha Litingi, kata ya Nyangao, jimbo la Mtama.
Ukweli upoje?
Picha iliyosambaa mitandaoni ikidai kuwa ni darasa la Shule ya msingi Litingi, kijiji cha Litingi, kata ya Nyangao, jimbo la Mtama
Kumeibuka dondoo kuwa Viongozi wa CHADEMA walio nje ya nchi Tundu Lissu na Godbless Lema wanatajwa kuwemo kwenye Vikao vya Baraza kuu la Chadema vitakavyofanyika 11/5/2022 Nchini Tanzania.
Aidha, inadaiwa pia wawili hao mpaka sasa wanazo tiketi mikononi mwao kwa ajili ya kuanza safari za kurejea nchini na kuhudhuria vikao vya chama chao.
Je kuna ukweli hapa?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.