Yanga heshima mbele Afrika, Sagrada yalala mara mbili

Daniel Mbega

JF-Expert Member
Mar 20, 2013
338
180
YangaMtibwa.jpg

MABINGWA wa soka Tanzania Bara, Yanga, leo wamewapa raha Watanzania baada ya kushinda kwa mabao 2-0 dhidi ya Sagrada Esparanca ya Angola katika mchezo wa kwanza wa raundi ya tatu ya Kombe la Shirikisho wakiwania kucheza hatua ya makundi.

Mechi hiyo iliyofanyika kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam imekuwa mwanzo mzuri kabla ya timu hizo kurudiana Mei 18 ambapo Yanga itakuwa inahitaji sare ili kusonga mbele.

Habari zaidi, soma hapa=> Yanga heshima mbele Afrika, Sagrada yalala mara mbili | Fikra Pevu
 
WAKIMATAIFA NI WAKIMATAIFA TU,mikia inawaumaaa naona leo mlivalia jezi za waangola
 
Wana jangwani wenzangu timu inatupa raha na kutembea kifua mbele lakini tujiulize kwa ukongwe wa timu yetu tulistahili kupata mafanikio zaidi ya haya.Hakuna mwana yanga asiejua kuwa mafanikio haya ya kucheza kandanda safi yusuf manji ana mchango mkubwa na hatuna budi kumshukuru kwa hili.
Zaidi ya gate collection na pesa ya udhamini wa TBL je club ina vyanzo gani vingine vya mapato kwa mwenye uelewa ningeomba anijuze nina kuwa na shaka na hali hii kwani siku manji akikaa pembeni je hali hii ya furaha itaendelea?khofu yangu ipo hapo na khasa nikitizama majirani zetu hali wanayopitia inanipa shaka.
Najaribu kuwaza kama mikakati madhubuti inakuwepo hata kwa kuuza gazeti la yanga imara walau wanachama na wapenzi wakaeleweshwa kuwa sio unanunua tu khabari bali unakuwa umechangia club muamko huo ukiwepo hata kwa kupata watu laki moja kwa wiki wenye uwezo wa kutoa 500 kununua gazeti kweli chanzo hiki hakifai?
Unaweza kujibu kuwa mbona gazeti lipo miaka mingi?sikatai ile je lipo kimaslahi ya timu au wajanja wachache?maana kwa watu laki takriban kwa mwezi mapato yasingepungua 200m je ndogo hizo?Najihisi vibaya jinsi timu yangu inavyo kuwa na fursa kama hii ya mtaji wa mashabiki kisha I nashindwa kuitumia.Wacha niishie hapa wachangiaji wengine nao wachangie.
 
Idadi kubwa ya washabiki ibadilike kuwa wanachama wanaolipa ya Shs elfu moja kwa mwezi. Hicho kitakuwa chanzo kizuri cha mapato.
 
Idadi kubwa ya washabiki ibadilike kuwa wanachama wanaolipa ya Shs elfu moja kwa mwezi. Hicho kitakuwa chanzo kizuri cha mapato.
Yaah!haya mambo kama tunapenda kuendelea kuwa na furaha inabidi nasi tushiriki hivi haiwezekani walau kuwa na tawi humu?na hilo la 1000 kubwa hilo club inakuwa na chanzo cha uhakika wa mapato hili ipo siku litatugharimu.
 
Back
Top Bottom