sembo
JF-Expert Member
- May 25, 2011
- 4,350
- 3,451
1. Aliyekua kocha na mchezaji wa mda mrefu wa Mtibwa Sugar, Mecky Mexime alijiunga na Kagera Sugar kwa ajili ya Msimu huu wa 2016/2017 kama Kocha Mkuu.. Nafasi yake ilichukuliwa na Salum Mayanga.
2. Katika Msimu huu, Mtibwa Sugar wameondokewa na wachezaji takribani 5 wa kikosi cha kwanza.
Wachezaji hao na timu walizokwenda ni
Shiza Kichuya, Ibrahim Mohamed na Mzamiru Yasini walisajiliwa Simba SC, Vicent Andrew aliyesajiliwa Yanga SC na Hussein Sharif aliyemfata Mecky.
3. Baadhi ya wachezaji walioletwa kuziba mapengo ya walioondoka ni
Rashid Mandawa toka Mwadui FC, Cassian Ponera toka Ndanda FC na Haruna Chanongo toka Stand United.
4. Matokeo ya wakata miwa hao wa Manungu ni haya hapa
20/08/2016: Mtibwa Sugar 0 - 1 Ruvu Shooting
27/08/2016: Mtibwa Sugar 2 - 1 Ndanda
03/09/2016: Maji Maji 1 - 2 Mtibwa Sugar
Ikumbukwe leo [11.09.2016] mida ya saa 10 jioni, Simba SC itakua inapambana na hawa jamaa.
Wito wangu kwa mashabiki na wanachama wa wenzangu wa Simba SC tujazane kwa wingi Shamba la Bibi, pia wale wazee wenzangu wa vibanda umiza tunatakiwa tuwahi siti zetu mapema maana hii mechi tunaimaliza "mapema sana".
SIMBA SPORTS CLUB, NGUVU MOJA.
2. Katika Msimu huu, Mtibwa Sugar wameondokewa na wachezaji takribani 5 wa kikosi cha kwanza.
Wachezaji hao na timu walizokwenda ni

Shiza Kichuya, Ibrahim Mohamed na Mzamiru Yasini walisajiliwa Simba SC, Vicent Andrew aliyesajiliwa Yanga SC na Hussein Sharif aliyemfata Mecky.
3. Baadhi ya wachezaji walioletwa kuziba mapengo ya walioondoka ni

Rashid Mandawa toka Mwadui FC, Cassian Ponera toka Ndanda FC na Haruna Chanongo toka Stand United.
4. Matokeo ya wakata miwa hao wa Manungu ni haya hapa
20/08/2016: Mtibwa Sugar 0 - 1 Ruvu Shooting
27/08/2016: Mtibwa Sugar 2 - 1 Ndanda
03/09/2016: Maji Maji 1 - 2 Mtibwa Sugar
Ikumbukwe leo [11.09.2016] mida ya saa 10 jioni, Simba SC itakua inapambana na hawa jamaa.
Wito wangu kwa mashabiki na wanachama wa wenzangu wa Simba SC tujazane kwa wingi Shamba la Bibi, pia wale wazee wenzangu wa vibanda umiza tunatakiwa tuwahi siti zetu mapema maana hii mechi tunaimaliza "mapema sana".
SIMBA SPORTS CLUB, NGUVU MOJA.