Wazo la siku: Katiba bora ni nzuri, lakini vizuri zaidi ni uadilifu wa wasimamizi wa Katiba hiyo

Mathanzua

JF-Expert Member
Jan 4, 2017
17,285
22,948
Katiba Bora ni kitu muhimu, hilo halina mjadala na ubishi. Lakini mwisho wa siku kama wanaoisimamia hiyo 'Katiba Bora' ni wezi, wachumia matumbo, majitu yenye ubinafsi uliokithiri na wasiokuwa na uzalendo; basi Katiba bora yo yote huwa ni bure ghali.

Rais Magufuli, Rais wa tano wa Tanzania, alileta miradi mikubwa sana ya maendeleo katika muda miaka mitano kuliko Rais mwingine yoyote tangu nchi yetu ipate uhuru. Lakini hakutumia Katiba Mpya.

Rais Ibrahim Traore hivi sasa ndiye Rais bora kuliko wengine wote katika bara la Afrika. Lakini kipaumbele chake hakikuwa Katiba Mpya, bali *uthibiti wa wezi wa mali ya umma wa ndani na wa nje ya nchi yake." Mafanikio ya maendeleo nchini Burkina Faso hivi sasa yanaonekana kama ni miujuza, lakini hakuna muujiza wowote, yote anayoyafanya Rais Traore ni ya kibinadamu, na yote yanaigika.Viongozi wetu waige anayofanya Rais Traore,watakuwa wanatutendea haki na tutawapenda kama anavyopendwa Rais Ibrahim Traore na wananchi wake..Vinginevyo wataendelea kuwa maadui WA Watanzania.
 
Katiba Bora ni kitu muhimu, hilo halina mjadala na ubishi. Lakini mwisho wa siku kama wanaoisimamia hiyo 'Katiba Bora' ni wezi, wachumia matumbo, majitu yenye ubinafsi uliokithiri na wasiokuwa na uzalendo; basi Katiba bora yo yote huwa ni bure ghali.

Rais Magufuli, Rais wa tano wa Tanzania, alileta miradi mikubwa sana ya maendeleo katika muda miaka mitano kuliko Rais mwingine yoyote tangu nchi yetu ipate uhuru. Lakini hakutumia Katiba Mpya.

Rais Ibrahim Traore hivi sasa ndiye Rais bora kuliko wengine wote katika bara la Afrika. Lakini kipaumbele chake hakikuwa Katiba Mpya, bali *uthibiti wa wezi wa mali ya umma wa ndani na wa nje ya nchi yake. Mafanikio ya Maendeleo nchini Burkina Faso hivi sasa yanaonekana kama ni miujuza, lakini hakuna muujiza wowote, yote anayoyafanya Rais Traore ni ya kibinadamu, na yote yanaigika.Viongozi wetu waige anayofanya Rais Traore,watakuwa wanatutendea haki,tutawapenda kama anavyopendwa Rais Ibrahim Traore.Vinginevyo wataendelea kuwa maadui zetu
sie tuna chura kiziwi

#NoReformsNoElection
 
Hivi hawawezagi kuleta maendeleo huku wakifuata democracy?
Mkuu democracy is an illusion which has no relevance to development,ni utapeli wa wazungu..Common sense shows that clearly.Maendeleo ya Burkina Faso yanatisha,and there is no even mention of democracy.Wazungu wametuletea mbuzi kwenye gunia,let's wake up.
 
Mkuu democracy is an illusion which has no relevance to development,ni utapeli wa wazungu..Common sense shows that clearly.Maendeleo ya Burkina Faso yanatisha,and there is no even mention of democracy.Wazungu wametuletea mbuzi kwenye gunia,let's wake up.
Kwako wewe maendeleo ni nini mkuu
 
Uwezo wa Bungee au mahakama kumwajibisha Rais akiwa madarakani utamfanya Rais kuwa mtumishi na sio Boss!!mamlaka ya kikatiba ni muhimu mno Kwa mstakabali wa kesho ya taifa letu!
 
china ni nchi ya chama kimoja ila ndio inayokimbiza kiuchumi sasa hivi dunian,
Hata muwe madictator kiasi gani hamuwezi kuwafikia watu weupe toka lini ngozi nyeusi ikawa na akili ya maendeleo

Maendeleo hayaletwi na udictator bali huletwa na akili za uvumbuzi na ugunduzi
 
Hata muwe madictator kiasi gani hamuwezi kuwafikia watu weupe toka lini ngozi nyeusi ikawa na akili ya maendeleo

Maendeleo hayaletwi na udictator bali huletwa na akili za uvumbuzi na ugunduzi
maendeleo hayaletwi na democrasia bali yanaletwa na technologia, km ulivyosema uvumbuzi na ugunduzi kwenye nyanja zooote, kilimo, viwanda, yaan sayansi ndio kila kitu
 
maendeleo hayaletwi na democrasia bali yanaletwa na technologia, km ulivyosema uvumbuzi na ugunduzi kwenye nyanja zooote, kilimo, viwanda, yaan sayansi ndio kila kitu
Tukiacha maendeleo kando ambayo hayaletwi na democracy wala udictator

Wewe kati ya udictator na democracy unachagua nini?
 
km china ni udictor bas nachagua mfumo wa china,
Udictator wa ccm hadi saizi umetupeleka wapi waafrika mnatumia kisingizio cha maendeleo kutawala kimabavu wakati akili zenu kisoda

Mnategemea misaada na mikopo kuendesha nchi, kujitajirisha na kujineemesha na familia zenu huku mkiwaumiza wote wanaowapinga

Hao unaowataja hawategemei misaada wala mikopo kuendesha nchi zao, marekani Ina full democracy na bado ni taifa lenye nguvu duniani nyie miaka 60 sasa na udictator wenu hamna mlichonacho zaidi ya barabara za lami mnazoona kwenu ni maendeleo

Acheni watu wawe huru hayo maendeleo hata mkitawala miaka buku mtasema haiwatoshi
 
km china ni udictor bas nachagua mfumo wa china,
China kinachowapa maendeleo ni akili zao sio mfumo nje ya mfumo ni wagunduzi na wavumbuzi wa vitu vingi sana gundueni na nyie muendelee udictator sio suluhisho la umasikini wenu
 
Udictator wa ccm hadi saizi umetupeleka wapi waafrika mnatumia kisingizio cha maendeleo kutawala kimabavu wakati akili zenu kisoda

Mnategemea misaada na mikopo kuendesha nchi, kujitajirisha na kujineemesha na familia zenu huku mkiwaumiza wote wanaowapinga

Hao unaowataja hawategemei misaada wala mikopo kuendesha nchi zao, marekani Ina full democracy na bado ni taifa lenye nguvu duniani nyie miaka 60 sasa na udictator wenu hamna mlichonacho zaidi ya barabara za lami mnazoona kwenu ni maendeleo

Acheni watu wawe huru hayo maendeleo hata mkitawala miaka buku mtasema haiwatoshi
china hata uhuru ulionao hapa tanzania haupo lkn wanamaendeleo sana imezipita hata nchi za europe ambazo zimejengeka kwa kutumia rasilimali za africa km vile raw material, cheap labour, slaves, etc.
kwa hiyo kigezo cha maendeleo sio uhuru. ni technologia , unataka uhuru wa kufanya nini labda hata tanzania ukakosaa??
 
..Tanzania tayari tuna udikteta na udhalimu kuliko China lakini hatuna maendeleo. Ndio maana tunapendekeza tubadilishe muelekeo.
china ni nchi ya chama kimoja, hamna facebook, jamii forum, km unavyojimwambafai huku, wewe ujui china wewe, china hakuna hata mtu mmoja anaweza kukosoa serikali
 
china hata uhuru ulionao hapa tanzania haupo lkn wanamaendeleo sana imezipita hata nchi za europe ambazo zimejengeka kwa kutumia rasilimali za africa km vile raw material, cheap labour, slaves, etc.
kwa hiyo kigezo cha maendeleo sio uhuru. ni technologia , unataka uhuru wa kufanya nini labda hata tanzania ukakosaa??
Labda huelewi tu ila nimekwambia mfumo wa utawala sio kigezo cha maendeleo kwa watu weupe ila akili zao ndio zinafanya kazi za kimaendeleo

Tukija bongo wanatumia kigezo cha maendeleo kukandamiza wengine wanatumia nguvu nyiiingi akili kidogo

Kwanini tuumizane kwa udictator haliyakuwa hatuwezi kupata maendeleo kama ya watu weupe
 
Labda huelewi tu ila nimekwambia mfumo wa utawala sio kigezo cha maendeleo kwa watu weupe ila akili zao ndio zinafanya kazi za kimaendeleo

Tukija bongo wanatumia kigezo cha maendeleo kukandamiza wengine wanatumia nguvu nyiiingi akili kidogo

Kwanini tuumizane kwa udictator haliyakuwa hatuwezi kupata maendeleo kama ya watu weupe
kitu gani umevumbua au opportunity yeyote uliyoipata ukakosa uhuru wa kufanya hicho kitu? mentions
 
Back
Top Bottom