Waziri Masauni: Rufaa ya kufungiwa kwa Kanisa haijaja kwangu (la Mchungaji "Kiboko ya Wachawi")

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,513
6,016

Waziri wa Mambo ya Ndani, Mhandisi Hamad Masauni ameulizwa juu ya kufungiwa kwa Kanisa la Christian Life Church linaloongozwa na Mchungaji Domique Kashoix Dibwe maarufu kwa jina la Kiboko ya Wachawi, lililopo Buza Kwa Lulenge, amesema rufaa ya kufungiwa kwa kanisa hilo haijafika mezani kwake, hivyo hawezi kuzungumza kwa urefu.

Barua ya kufungiwa kwa kanisa hilo ya Julai 25, 2024 iliyotolewa na Msajili wa Jumuiya za Kiraia imetaja sababu za kulifunga Kanisa hilo ni kwenda kinyume cha taratibu za usajili ikiwemo kuweka kutoza Tsh. 500,000 kupata huduma ya maombezi tofauti na Imani ya Kikristo na kinyume na Katiba pamoja na Kanuni za Kanisa lako, zinazotambuliwa rasmi na Ofisi ya Msajili wa Jumuiya.

Mengine ni kutoa mahubiri yanayodhalilisha watu madhabahuni.

Kutoa mahubiri chonganishi

Kuhamasisha waumini wa kanisa lake (Mchungaji Domique) kuua watu kwa dhana au tuhuma za uchawi/ushirikina.

Kutokana na hali hiyo, kwa barua hii, unajulishwa kuwa unatakiwa kufunga mara moja shughuli na huduma zote zinazotolewa katika Kanisa linaloendeshwa na Mchungaji Domique Kashoix Dibwe maarufu kwa jina la Kiboko ya Wachawi wakati taratibu nyingine za kisheria dhidi ya Kanisa la Christian Life Church zikiendelea. Utekelezaji wa maelekezo haya ufanyike kabla ya tarehe 28/07/2024.

Pia soma
~ Kufungiwa kwa kanisa la “Kiboko ya Wachawi” pongezi kwa Serikali
~ Waumini wa Mchungaji Domique Kashoix Dibwe, maarufu 'Kiboko ya Wachawi' wafurika Kanisani kusubiri ibada hata baada ya kanisa kufungwa
~ Serikali chukueni hatua za dharura na haraka dhidi ya Kiboko ya Wachawi kinachoendelea hapa buza mtalaumiwa
~ Serikali chukueni hatua za haraka dhidi ya Nabii Dominiki "Kiboko ya Wachawi"
 
Kiboko ya wachawi anahamishia huduma yake kwao Congo ,rufaa ya nini

USSR
 
Huyo ni tapeli kama matapeli wengine,sema hao wengine washajiweka karibu na viongozi
Wa nchi huku wakiendelea kufanya utapeli wao

Ova
 
Serikali iweke bodi ya kusimamia maswala yote ya kidini hapa nchini.

Ipitishwe pia na sheria yake.
 
Back
Top Bottom