benzemah
JF-Expert Member
- Nov 19, 2014
- 1,533
- 3,187
WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Dk Ashatu Kijaji amezitaka taasisi zote za serikali zinazohusika na ukaguzi na udhibiti kuacha kufungia biashara na viwanda, kwani kufanya hivyo ni kusimamisha uchumi wa nchi.
Kijaji alisema katika maonesho ya wafanyabiashara yaliyoandaliwa na
Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (Brela) jijini Dar es Salaam.
“Naomba nisisitize kwa mamlaka zote za serikali za udhibiti ziendelee kuruhusu biashara zifanye kazi hata kama kuna jambo hatukubaliani kati yetu wakati tunashughulikia jambo lile hatuna sababu ya kusitisha kusimamisha shughuli za biashara, ni kusimamisha uchumi wa nchi.
“Kwa hiyo ni muhimu sana tunapoelekea kuhitimisha utekelezaji wetu wa dira yetu ya maendeleo ya mwaka 2025 tusisitishe shughuli yoyote ya kiuchumi kwa jambo lolote lile, kwani mazungumzo ni msingi wa sisi kuwa na uchumi imara, " alisema
Kijaji alisema katika maonesho ya wafanyabiashara yaliyoandaliwa na
Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (Brela) jijini Dar es Salaam.
“Naomba nisisitize kwa mamlaka zote za serikali za udhibiti ziendelee kuruhusu biashara zifanye kazi hata kama kuna jambo hatukubaliani kati yetu wakati tunashughulikia jambo lile hatuna sababu ya kusitisha kusimamisha shughuli za biashara, ni kusimamisha uchumi wa nchi.
“Kwa hiyo ni muhimu sana tunapoelekea kuhitimisha utekelezaji wetu wa dira yetu ya maendeleo ya mwaka 2025 tusisitishe shughuli yoyote ya kiuchumi kwa jambo lolote lile, kwani mazungumzo ni msingi wa sisi kuwa na uchumi imara, " alisema