peno hasegawa
JF-Expert Member
- Feb 24, 2016
- 14,691
- 24,404
Watu saba wamefariki dunia na wengine 75 wamejeruhiwa katika ajali mbili tofauti zilizotokea wilayani Same. Ajali ya kwanza ilitokea majira ya saa saba usiku wa kuamkia leo katika maeneo ya Njoro na kuhusisha basi la Kampuni ya Osaka lililokuwa likielekea Dar es Salaam, ambapo ilisababisha kifo cha mtu mmoja na wengine 52 walijeruhiwa.
Ajali ya pili ilihusisha basi aina ya Costa la Kampuni ya Mkokota majira ya saa2 asubuhiya leo, ambalo lilipinduka katika kona za milima ya Ilamba, na kusababisha vifo vya watu sita na majeruhi 23. Waliofariki dunia katika ajali hiyo ni wanakwaya waliokuwa wakisafiri kutoka Chome kuelekea Ndolwa.
Mganga Mkuu wa Wilaya ya Same, Dkt. Alex Alexander, amesema kuwa majeruhi wa ajali ya kwanza walipokelewa hospitalini majira ya saa nane usiku, huku majeruhi wengine 23 pamoja na miili ya marehemu sita ikifikishwa hospitalini mchana wa leo.
View: https://youtu.be/D_2maGWZn4Y?si=_QUdY4lhQHgOjcfN
Ajali ya pili ilihusisha basi aina ya Costa la Kampuni ya Mkokota majira ya saa2 asubuhiya leo, ambalo lilipinduka katika kona za milima ya Ilamba, na kusababisha vifo vya watu sita na majeruhi 23. Waliofariki dunia katika ajali hiyo ni wanakwaya waliokuwa wakisafiri kutoka Chome kuelekea Ndolwa.
Mganga Mkuu wa Wilaya ya Same, Dkt. Alex Alexander, amesema kuwa majeruhi wa ajali ya kwanza walipokelewa hospitalini majira ya saa nane usiku, huku majeruhi wengine 23 pamoja na miili ya marehemu sita ikifikishwa hospitalini mchana wa leo.
View: https://youtu.be/D_2maGWZn4Y?si=_QUdY4lhQHgOjcfN