Watanzania tumekua Waapole sana! Mtu anatengeneza ARVs fake anatanua mtaani?

MAHANJU

JF-Expert Member
Aug 26, 2014
5,252
8,003
Hivi kweli jamani mtu anatengeza ARVs fake, anasambaza kwa maelfu ya Wanzania wanaoishi na VVU wanakunywa wakidhani ni dawa za kuwaongezea maisha! Is this serious? Hivi tunaelewa kasi ya ongezeko Virusi kwa mwili wa mwathirika asiyetumia dawa? Ni Watanzania Wangapi wamepoteza maisha kwa kutumia kutumia hizo ARVs zilizothibitika kua ni fake?



Hivi hili suala lingetokea kwenye nchi kama ya China au kwa majirani pale Rwanda hawa watu wangeendelea kuranda mitaani kweli? tena wengine viongozi?
Inaumiza inaumiza inaumiza mno. Hata kama Rais atumbue majipu lakini moja lakini hayawezi kufanana na haya majipu ya ARVs fake kamwe.


Sijui hii kesi imefikia wapi mpaka sasa, Sidhani kama kuna watu wameguswa na hili na kuumia zaidi ya wale ndugu waliopoteza ndugu zao kwa matumizi ya ARVS fake.




Hivi huyu mtanzania aliyeenda akakaa na kufikiria kutengeneza ARVs fake alifikiria nini? Huyu mtu anaamini kwamba kuna Mungu kweli? Anatengeneza unga sijui ni wa mihogo au mahindi akiaminisha watu kua ARVS kweli?
Kwakweli vyombo vyetu vya dola juu ya hili kuona wahusika wamatembea mitaani haviwatendei haki Watanzania.
 
Sisiemu madabidaaa daresalaaam. Kulindana kama kawa, jipu gumu alitumbuliki kama LUGUMI meeeen
Halafu hiyo familia ni kasheshe tupu,mama ndio mwanzilishi wa hayo mambo ya sijui Deci sijui upatu,watu wali lizwa sio mchezo miaka ile na haikuwapo kesi wala nini, ni watafutaji wasiojali matokeo ila kama desturi chama kina wanusuru.
 
Hela za kuzunguka Tz nzima kwa gari wafanya mchezo? Halafu wale wasanii wote waliokuwa wakimtangulia. Halafu, msambazaji ndiye meneja wake! Mambo mengine jamani tuache kuulizauliza kwani waweza jipatia msiba buure.
Sisiieem hakuna fisadi wala jipu. Jipu ni kwa wale mliojikita upande wa pili. Waliopewa fake hawakuwa upande wetu
 
Mwenyekiti wa Chama Chetu cha Majambazi mkoa hatumbuliwi hata tulie vipi,sijui kama hata tathmini ilifanyika ya madhara yatokanayo
 
Wanasema dawa za arvs hospital wanagawa bure inamaana hizo dawa feki yeye alikua anamuuzia nani?
 
Wanasema dawa za arvs hospital wanagawa bure inamaana hizo dawa feki yeye alikua anamuuzia nani?
Njia ni moja mkuu hupitia mahospitalini, Ispokua hua zinalipiwa na wafadhili moja kwa moja, Sasa kama wewe ni mzalishaji unapokea hayo mabilioni ya afadhili.Hapa pesa za wajanja waliziona ndo wakafungua kiwanda wakasaga unga wa mihogo wakapaki kama dawa pesa zikapigwa. Zakawa packed kama ARVs Wagonjwa wetu wakanywa wakifikiri na ARVs. Huu inawezekana ni mtandao mkubwa hata waganga wa mikoa watakua wanajua vizuri.
 
Hilo ni moja tu la kutisha na lina target specific group of people in our society.
Bomb lingine kubwa na maangamizi ni la ufutaji wa expiring dates na kupiga mihuri mipya ili bidhaa ziendelee kuuzwa madukani.
Amini usiamini hii ya kulishana sumu inamkumba kila mtu. Wakishindwa kufuta wanafanya re-bagging.
 
Kama hutaji wahusika kwa jina hii inabaki kuwa soga za kijiweni kama sio majungu kabisa.
 
Ramadhan Madabida, Mwenyekiti wa CCM mkoa wa Dar es salaam na swahiba wa Lowassa anatuhumiwa kuwa na kiwanda kinachofyatua dawa feki za kurefusha maisha kwa wagonjwa wa HIV, ARVs.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…