Mshangazi dot com

JF-Expert Member
Nov 19, 2011
783
1,878
Jamii zetu za kiafrika zimeweka mzigo mkubwa sana kwa mwanaume.
Naomba kutambua mchango wenu na kuwapa maua yenu kama ishara ya shukrani.

Shukrani za dhati ziwaendee;

🌹 Wanaume wanaoweka juhudi katika kazi zao halali, wakifanya kwa uaminifu na kujituma ili kujenga maisha bora kwao na familia zao – pokeeni maua yenu.

🌹 Wanaume wanaopambana kuhudumia familia zao bila kuchoka na kulea watoto wao kwa mapenzi na maadili mema – pokeeni maua yenu, tunawashukuru.

🌹 Wanaume wanaoshikamana na marafiki zao kwa uaminifu, kusaidiana katika shida na raha, na kuwa nguzo ya kweli kwa wenzao – pokeeni maua yenu.

🌹 Wanaume waliotoka kwenye maisha magumu na wanapambana kila siku kuhakikisha vizazi vyao vinaishi maisha bora kuliko wao – pokeeni maua yenu, tunawashukuru sana.

🌹 Wanaume wanaopambana na changamoto za afya ya akili kimya kimya, wakitafuta suluhisho bila kukata tamaa – pokeeni maua yenu, tunawatambua na kuwathamini.

🌹 Wanaume waliowahi kupitia maumivu makali (kuachwa, kupoteza wapendwa, kufeli, kuumizwa) lakini bado walisimama tena na kusonga mbele – pokeeni maua yenu!

🌹 Wanaume wanaopambana na hali ngumu za maisha bila kulalamika na bado wanajitahidi kutokata tamaa na kutia wengine moyo – tunawashukuru, pokeeni maua yenu.

🌹 Wanaume wanaosimamia shughuli za kijamii; likitokea tatizo wao ndiyo mstari wa mbele kupambana (mwizi mtaani wamo, misiba, sherehe, n.k.) – pokeeni maua yenu na asanteni sana.

🌹 Wanaume wanaolea watoto wa wenza wao bila kuwabagua na kuhakikisha wanasimamia nafasi zao kama wazazi wenza – pokeeni maua yenu.

🌹 Wanaume wanaohakikisha wazazi wao na wale wa wenza wao wanatunzwa na kuheshimiwa – tunawashukuru, pokeeni maua yenu.

🌹 Wanaume wanaowapenda, kuwaheshimu, kuwalinda na kuwasaidia wenza wao – pokeeni maua yenu na asanteni sana.

🌹 Wanaume wanaopigania maslahi ya wananchi na wanajamii wenzao, kuhakikisha usawa na haki zinazingatiwa kwa kila mmoja – tunawashukuru sana, pokeeni maua yenu.


Leo ni siku yenu, hasa wale wanaume wanaojituma na hawapati "ASANTE" wanazostahili. Shukrani kwa yote mnayofanya na kutufanyia 💐✨.


Ongeza na wewe sababu za ziada za kuwapa maua yao wanaume wa shoka kwenye jamii na maisha yetu.

PS:

Wale mnaopwaya pwaya hii nyuzi haiwahusu, ila mnaweza kujifunza kutoka kwa wenzenu.
 
🌹 Wanaume wanaolea watoto wa wenza wao bila kuwabagua na kuhakikisha wanasimamia nafasi zao kama wazazi wenza – pokeeni maua yenu.
Kundi hili ni la wanaume wapumbavu ambao hawastahili pongezi, infact wanaidhalilisha jinsia ME.

How comes you become a step father? Have you failed to find yourself a woman that has kept herself pure for that long? Why are you opting to enter the conflicts that you were never part of before?

Before accepting being step father first you must know, you are a man that single mother would not date you if she did not have kids. The man who get her pregnant was her type not you. She is with you because her type left her for a better woman. Infact, she is dating you now because you're a fool.
 
Kundi hili ni la wanaume wapumbavu ambao hawastahili pongezi, infact wanaidhalilisha jinsia ME.

How comes you become a step father? Have you failed to find yourself a woman that has kept herself pure for that long? Why are you opting to enter the conflicts that you were never part of before?

Before accepting being step father first you must know, you are a man that single mother would not date you if she did not have kids. The man who get her pregnant was her type not you. She is with you because her type left her for a better woman. Infact, she is dating you now because you're a fool.
Wewe utakua wa alfu mbili
 
Wewe utakua wa alfu mbili
Hata kama ningekua wa 2000 ndio ingeondoa ukweli kwamba baba wa kambo wanatumika tu kimasilahi na wanawake?

Unataka madogo wa 2000 nao wakubaliane na umalaya wa wanawake kwa assertions zenu potofu za "kitanda hakizai haramu" . Kama baba mtoto amekufa iyo inaweza kueleweka ila kama yupo hai hapana kwa kweli.

Real man build his own family not joining another man's family. Keep your class, you are not made for left overs
 
Hata kama ningekua wa 2000 ndio ingeondoa ukweli kwamba baba wa kambo wanatumika tu kimasilahi na wanawake?

Unataka madogo wa 2000 nao wakubaliane na umalaya wa wanawake kwa assertions zenu potofu za "kitanda hakizai haramu" . Kama baba mtoto amekufa iyo inaweza kueleweka ila kama yupo hai hapana kwa kweli.

Real man build his own family not joining another man's family. Keep your class, you are not made for left overs
Usiseme hivyo Kijana! Usiseme hivyo Kabisa! Tema mate Chini.
 
Back
Top Bottom