Wanasiasa hatutaki elimu ya bure tunataka elimu bora

WEKKI

JF-Expert Member
Feb 17, 2014
477
146
Katika kampeni za mwaka huu kuna jambo ambalo wanasiasa wamekuwa wakiwahadaa watanzania na watu wamegeuzwa mashabiki bila wao kujua. Wamesikika watu wakisema kuwa Tanzania inahitaji elimu ya bure. Maneno kama haya ni sawa kuyatamka kisiasa lakin sio sawa kiuhalisia.

Changamoto yetu kama taifa ni elimu iliyo BORA ambayo mtu akimaliza shule ya kata ubora wake uwe sawa na mtu alietoka St Mary's Feza,Tusiime,St Mthew n.k . ifike wakati kuwa mtu kwenda shule binafsi kma nilizotaja hapo liwe ni suala EXTRA na STAREHE kama vile ilivyo kununua bia kwenye kibanda cha Mangi na kunywa na kuwa sawa na aloenda Serena kunywa bia maana zote ni bia na ukizinywa utalewa.

Ni utoto kusema mtu asomeshwe bure mpaka chuo kikuu huku kichwani akawa amekaririshwa mitihani na mchango wake kwa ukuaji kiuchumi ukawa zero. Elimu yetu imeporomoka kwa kasi sana kwa sababu wanasiasa wanamini kuwa kujenga shule nyingi za sekondari na vyuo vingi vya elimu ya juu ni kupandisha thamani elimu yetu kumbe wanaidumaza huku sisi tukigeuzwa kama chapatti na kushangilia mambo bila kuyatafakari. Lengo sio upatikanaji wa elimu kwa watu wengi; lengo kubwa sasa liwe ubora wa hiyo elimu wanayopewa hao wanaomaliza ili wakiingia kwenye soko la ajira wapambane kisawasawa na washindani wetu kitaaluma.

Ni aibu kwa taifa hili kusema kuwa tunahitaji elimu BURE ambayo haina ubora wowote kitaifa na kimataifa. Elimu ambayo mwajiriwa anapata kigugumizi kukuajiri ;elimu ambayo watu hawafundishwi practise ila wanafundishwa theory. Elimu sasa isiwe quantity kwamba kila mmoja akasome ila elimu sasa ibadilishwe kuwa quality. Ni afadhali elimu ikawa quailty and free kuiliko kuwa quantiy and free.

Wanavyuo vya elimu ya juu wapatiwe msaada na wawezeshwe kwagharama a ada na malazi na kila stahiki bila kucheleweshwa.Ila wanachokisoma kiwe bora katika soko la ajira.Elimu ibadilishwe na kuleta watengeneza ajira na suio watafuta ajira maana elimu ya bure bila pahala pa kumwajiri mhitimu ni sawa na kulima kwenye lami. Kwa sababu hawa waakuwa mizigo kwa serikali na waaendelea kusema serikali haijaufania kitu.

My take, tupime sera za wanasiasa hawa kwa uhalisia na sio kwa ushabiki na mahaba ambayo yatakuja kutupoteza kwa miaka kumi ijayo. Sidhani kama tunataka elimu BURE ambayo sio BORA.

PIGANIA ELIMU BORA MWAKA HUU
 
#TeamMfumo watakuja baadae, japo sina imani na utendaji wa serikali kupitia sera zao majukwaani, lakini wanasiasa wetu wametudharau sana kutujazia ahadi za kupendeza bila kuwa na maelezo ya utekelezaji na Deadline ya lini tutakuwa wapi, huku ni kutufanya tutamani kuifikia kesho kama tumaini jipya lakini hatuna uhakika juu ya ubora wa hilo tumaini letu.
 
Katika kampeni za mwaka huu kuna jambo ambalo wanasiasa wamekuwa wakiwahadaa watanzania na watu wamegeuzwa mashabiki bila wao kujua. Wamesikika watu wakisema kuwa Tanzania inahitaji elimu ya bure. Maneno kama haya ni sawa kuyatamka kisiasa lakin sio sawa kiuhalisia.

Changamoto yetu kama taifa ni elimu iliyo BORA ambayo mtu akimaliza shule ya kata ubora wake uwe sawa na mtu alietoka St Mary's Feza,Tusiime,St Mthew n.k . ifike wakati kuwa mtu kwenda shule binafsi kma nilizotaja hapo liwe ni suala EXTRA na STAREHE kama vile ilivyo kununua bia kwenye kibanda cha Mangi na kunywa na kuwa sawa na aloenda Serena kunywa bia maana zote ni bia na ukizinywa utalewa.

Ni utoto kusema mtu asomeshwe bure mpaka chuo kikuu huku kichwani akawa amekaririshwa mitihani na mchango wake kwa ukuaji kiuchumi ukawa zero. Elimu yetu imeporomoka kwa kasi sana kwa sababu wanasiasa wanamini kuwa kujenga shule nyingi za sekondari na vyuo vingi vya elimu ya juu ni kupandisha thamani elimu yetu kumbe wanaidumaza huku sisi tukigeuzwa kama chapatti na kushangilia mambo bila kuyatafakari. Lengo sio upatikanaji wa elimu kwa watu wengi; lengo kubwa sasa liwe ubora wa hiyo elimu wanayopewa hao wanaomaliza ili wakiingia kwenye soko la ajira wapambane kisawasawa na washindani wetu kitaaluma.

Ni aibu kwa taifa hili kusema kuwa tunahitaji elimu BURE ambayo haina ubora wowote kitaifa na kimataifa. Elimu ambayo mwajiriwa anapata kigugumizi kukuajiri ;elimu ambayo watu hawafundishwi practise ila wanafundishwa theory. Elimu sasa isiwe quantity kwamba kila mmoja akasome ila elimu sasa ibadilishwe kuwa quality. Ni afadhali elimu ikawa quailty and free kuiliko kuwa quantiy and free.

Wanavyuo vya elimu ya juu wapatiwe msaada na wawezeshwe kwagharama a ada na malazi na kila stahiki bila kucheleweshwa.Ila wanachokisoma kiwe bora katika soko la ajira.Elimu ibadilishwe na kuleta watengeneza ajira na suio watafuta ajira maana elimu ya bure bila pahala pa kumwajiri mhitimu ni sawa na kulima kwenye lami. Kwa sababu hawa waakuwa mizigo kwa serikali na waaendelea kusema serikali haijaufania kitu.

My take, tupime sera za wanasiasa hawa kwa uhalisia na sio kwa ushabiki na mahaba ambayo yatakuja kutupoteza kwa miaka kumi ijayo. Sidhani kama tunataka elimu BURE ambayo sio BORA.

PIGANIA ELIMU BORA MWAKA HUU

Mkuu politcis ni kama biashara nyingine yoyote ile unaangalia needs na wants za wateja hivyo politicians nao wameona mbali wakajua wakija na sera hizo zitawalipa! mzazi aliyejipanga vizuri na kwa kujua kabisa nini maana ya mzazi kuwa mtoto/watoto hatababaishwa na sera hizo maana atakuwa amejipanga kumsomesha wa/mtoto wake ingawa nakubaliana kuwa kuna watz hawana huo uwezo hivyo inabidi kuwa na alternative kwa ajili yao.

Ili elimu yetu iwe bora kuna kazi kubwa sana ya kufanya, hebu jaribu kufikiri shule zote za serikali ziwe kama fedha, marian, shaaban robert, mzizima, maua, rosemin unafikiri ni uwekezaji wa namna gani unahitajika? Lakini inawezekana kupanga ni kuchagua!

Leo hii UDSM haipo kwenye top 50 ya taasisi credible kama times education nia aibu sana!

Vyuo vyetu vinashindana kuwa enrolment kubwa!

JK aliwahi shauriwa kuwa huu wingi wa vyuo visivyo na ubora siyo afya kwa taifa letu yeye akajibu wacha viwe vingi tu suala la ubora ni baadae yaana mbele kwa mbele!

Ni vema kama mtu una uwezo ukamsomesha mwanao elimu nzuri kuliko kuliko kusubira hii elimu bure kwa wote! kumbuka jukum la kumhudumia mtoto wa kwako ni lako!

Siku zote vitu vya bure lazima ubora uwe comromised kwa kiasi fulan!!!
 
infomania, WEKKI

..inawezekana kabisa shule za serikali zikawa na viwango sawa au hata kuzizidi shule za private kama Feza, Marian, etc.

..wakati mimi nasoma shule za serikali zilikuwa na viwango kuliko shule binafsi.

..tena wanafunzi tulikuwa tunaona FAHARI kwenda shule za serikali kuliko shule binafsi. kwanza ukienda shule ya serikali ulikuwa unaonekana kwamba umefaulu na unajiweza kimasomo.

..sasa wakati huo tulikuwa tunasoma bure kuanzia darasa la kwanza mpaka chuo kikuu. zaidi, tulikuwa tunapata mlo shuleni, tunapewa madaftari na vitabu vya kiada. yaani daftari likiisha unakwenda kwenye stoo ya shule kuchukua lingine jipya.

..ELIMU BURE NA YENYE VIWANGO INAWEZEKANA.

cc [B WEKKI[/B]
 
Last edited by a moderator:
infomania, WEKKI

..inawezekana kabisa shule za serikali zikawa na viwango sawa au hata kuzizidi shule za private kama Feza, Marian, etc.

..wakati mimi nasoma shule za serikali zilikuwa na viwango kuliko shule binafsi.

..tena wanafunzi tulikuwa tunaona FAHARI kwenda shule za serikali kuliko shule binafsi. kwanza ukienda shule ya serikali ulikuwa unaonekana kwamba umefaulu na unajiweza kimasomo.

..sasa wakati huo tulikuwa tunasoma bure kuanzia darasa la kwanza mpaka chuo kikuu. zaidi, tulikuwa tunapata mlo shuleni, tunapewa madaftari na vitabu vya kiada. yaani daftari likiisha unakwenda kwenye stoo ya shule kuchukua lingine jipya.

..ELIMU BURE NA YENYE VIWANGO INAWEZEKANA.

cc [B WEKKI[/B]

Mkuu hili linawezeka pale ambapo kuna political will na commitment ya hali ya juu sana! na vilevile pale ambapo kunakuwa na vipaumbele vichache! nina uhakika na philosophy hii ikifanyiwa kazi ELIMU BURE NA YENYE VIWANGO INAWEZEKANA binafsi nimesikitika sana na kushuka kwa elimu yetu yaan inafikia hatua serikali inadanganya wananchi kwa kushusha pass mark i.e. division 5 ili ionekane mwanafunzi kafaulu wakati nchi zinazojitambua kama china ina pass mark ya juu sana. Lakini serikali inafanya hivyo maana inajua kuna wananchi wajinga wanafurahi kuambiwa mwanao kapata division 5 maana angeambiwa zero ingekuwa nongwa, mzazi huyu hajiulizi je mtoto huyu atamudu vipi changamoto za ushindani zilizopo katika dunia ya sasa!
 
Kama huelewi uliza.

1. Magufuli aliyeibia michakato ya UKAWa, ndiye anayesema "elimu bure bila michango michango".


2. UKAWA WENYE SERA ZAO WAKO MAKINI NA WANAELEWA MAANA, UMUHIMU NA THAMANI YA ELIMU. HAWA WAMESEMA BAYANA, KWAMBA WATATOA ELIMU BURE ILI WATANZANIA WOTE WENYE UWEZO WA KUSOMA WAPATE ELIMU, LAKINI ELIMU HIYO ITAKUWA BORA NA SI BORA ELIMU KAMA ILIVYOFINYANGWA FINYANGWA NA CCM.

Mpaka hapa thread yako is totally irrelevant.
 
infomania, WEKKI

..inawezekana kabisa shule za serikali zikawa na viwango sawa au hata kuzizidi shule za private kama Feza, Marian, etc.

..wakati mimi nasoma shule za serikali zilikuwa na viwango kuliko shule binafsi.

..tena wanafunzi tulikuwa tunaona FAHARI kwenda shule za serikali kuliko shule binafsi. kwanza ukienda shule ya serikali ulikuwa unaonekana kwamba umefaulu na unajiweza kimasomo.

..sasa wakati huo tulikuwa tunasoma bure kuanzia darasa la kwanza mpaka chuo kikuu. zaidi, tulikuwa tunapata mlo shuleni, tunapewa madaftari na vitabu vya kiada. yaani daftari likiisha unakwenda kwenye stoo ya shule kuchukua lingine jipya.

..ELIMU BURE NA YENYE VIWANGO INAWEZEKANA.

cc [B WEKKI[/B]
linganisha idadi iliopo sasa na wakai ule na uakuja na majibu pia ambua kuwa kwa sasa nhi imehamia kwene ubepari ambapo mfumo wa elimu umebinafsishwa kiasi kwamba wale wanaosoma shule za binafsi wanaonekana kuwa wana uweo kuliko sisi mfagio na kidumu ubinafsishaji na kuleta wawekezaji katika elimu ndilo tatizo kubwa ila haujafikia kusema kuwa unahitaji elimu bure ambao sio bora kabisa katika mfumo huu
 
ukawa wanadai elimu iwe bure na ccm wanasema elimu iwe bure pia hawajawahi kuweka neno bure na bora mimi nimmesema tunahitaji elimu bure na ambayo ni bora
 
Katika kampeni za mwaka huu kuna jambo ambalo wanasiasa wamekuwa wakiwahadaa watanzania na watu wamegeuzwa mashabiki bila wao kujua. Wamesikika watu wakisema kuwa Tanzania inahitaji elimu ya bure. Maneno kama haya ni sawa kuyatamka kisiasa lakin sio sawa kiuhalisia.

Changamoto yetu kama taifa ni elimu iliyo BORA ambayo mtu akimaliza shule ya kata ubora wake uwe sawa na mtu alietoka St Mary's Feza,Tusiime,St Mthew n.k . ifike wakati kuwa mtu kwenda shule binafsi kma nilizotaja hapo liwe ni suala EXTRA na STAREHE kama vile ilivyo kununua bia kwenye kibanda cha Mangi na kunywa na kuwa sawa na aloenda Serena kunywa bia maana zote ni bia na ukizinywa utalewa.

Ni utoto kusema mtu asomeshwe bure mpaka chuo kikuu huku kichwani akawa amekaririshwa mitihani na mchango wake kwa ukuaji kiuchumi ukawa zero. Elimu yetu imeporomoka kwa kasi sana kwa sababu wanasiasa wanamini kuwa kujenga shule nyingi za sekondari na vyuo vingi vya elimu ya juu ni kupandisha thamani elimu yetu kumbe wanaidumaza huku sisi tukigeuzwa kama chapatti na kushangilia mambo bila kuyatafakari. Lengo sio upatikanaji wa elimu kwa watu wengi; lengo kubwa sasa liwe ubora wa hiyo elimu wanayopewa hao wanaomaliza ili wakiingia kwenye soko la ajira wapambane kisawasawa na washindani wetu kitaaluma.

Ni aibu kwa taifa hili kusema kuwa tunahitaji elimu BURE ambayo haina ubora wowote kitaifa na kimataifa. Elimu ambayo mwajiriwa anapata kigugumizi kukuajiri ;elimu ambayo watu hawafundishwi practise ila wanafundishwa theory. Elimu sasa isiwe quantity kwamba kila mmoja akasome ila elimu sasa ibadilishwe kuwa quality. Ni afadhali elimu ikawa quailty and free kuiliko kuwa quantiy and free.

Wanavyuo vya elimu ya juu wapatiwe msaada na wawezeshwe kwagharama a ada na malazi na kila stahiki bila kucheleweshwa.Ila wanachokisoma kiwe bora katika soko la ajira.Elimu ibadilishwe na kuleta watengeneza ajira na suio watafuta ajira maana elimu ya bure bila pahala pa kumwajiri mhitimu ni sawa na kulima kwenye lami. Kwa sababu hawa waakuwa mizigo kwa serikali na waaendelea kusema serikali haijaufania kitu.

My take, tupime sera za wanasiasa hawa kwa uhalisia na sio kwa ushabiki na mahaba ambayo yatakuja kutupoteza kwa miaka kumi ijayo. Sidhani kama tunataka elimu BURE ambayo sio BORA.

PIGANIA ELIMU BORA MWAKA HUU

Binafsi nakupongeza Wekki kwa mada nzuri. Nakubaliana nawe na sentensi /summary yako "PIGANIA ELIMU BORA MWAKA HUU". Ndugu yangu nikiamua hasa kuainisha matatizo na uozo katika sekta ya elimu ya nchi hii basi naweza kutunga kitabu kizima bila ya kutosheleza. Lakini kwa ufupi tu ni kuna ukweli usiopingika ya kuwa UBORA wa kiwango cha elimu yetu umekuwa ukiporomoka kadiri siku zinaposonga. Tunashindwa na hata jirani zetu kenya na uganda!! Baada ya Zaidi ya miaka 50 ya Uhuru bado tuna shule ambazo wanafunzi wanakaa chini hawana madawati. Bado tuna wanafunzi wanaosoma chini ya miti na si angalau kwenye mabanda ya shule!!! Sote tunaona jinsi walimu wetu walivyo na hali duni kimaisha. Shule zetu nyingi hazina maabara na iwapo zina maabara basi zinakosa vifaa kwa ajili ya elimu kwa vitendo. Matatizo ni mengi mno. HITIMISHO: Hali hii imesababishwa na jinsi ambavyo sisi raia wa nchi hii tunavyowapa madaraka viongozi wa CCM katika chaguzi zote zilizopita. Ni dhahiri ya kwamba CCM na serikali zake zimeshindwa kutatulia matatizo katika sekta ya elimu yetu. Saa ya mabadiliko ni sasa. PIGANIA ELIMU BORA MWAKA HUU.
 
linganisha idadi iliopo sasa na wakai ule na uakuja na majibu pia ambua kuwa kwa sasa nhi imehamia kwene ubepari ambapo mfumo wa elimu umebinafsishwa kiasi kwamba wale wanaosoma shule za binafsi wanaonekana kuwa wana uweo kuliko sisi mfagio na kidumu ubinafsishaji na kuleta wawekezaji katika elimu ndilo tatizo kubwa ila haujafikia kusema kuwa unahitaji elimu bure ambao sio bora kabisa katika mfumo huu

..nakubaliana na wewe kuhusu changamoto zilizopo.

..kuhusu UBEPARI nadhani hicho ni kisingizio tu. Bepari mkubwa duniani, usa, anatoa elimu bure ktk shule za serikali mpaka darasa la 12.

..sasa wagombea uraisi wa usa wanapendekeza elimu bure ktk community colleges na wengine hata vyuo vikuu.

..ushauri wangu ni kwamba tusiwasikilize wale wanaodai kwamba ubepari maana yake ni kila mtu na lwake na serikali haitoi huduma yoyote kwa jamii.

..kuhusu idadi kubwa tuliyonayo, tunapaswa kuzalisha zaidi kuliko wazee wetu wa enzi za mkoloni na mwalimu nyerere.

..tukizalisha zaidi, tutalipa kodi zaidi na serikali itakuwa na uwezo wa kutoa huduma nyingi zaidi na bora zaidi.

..mwisho, tunachimba dhahabu,tanzanite, chuma, makaa ya mawe, na gesi. Rasilimali zote hizi lazima mapato yake yaelekezwe kwenye sekta ya elimu.

..unajua ukisoma chuo kimoja na watu wa Botswana utaona tofauti yao na sisi Watanzania. Wenzetu wanatumia madini yao kusomesha vijana wao.

..ELIMU BORA NA YENYE VIWANGO INAWEZEKANA.

CC Nyani Ngabu
 
Last edited by a moderator:
Nimeshasema humu jukwaanihakuna kitu cha bure. Tunachokitaka ni mfumo utakaomwezesha kila mtu kuwa na fursa ya kupata elimu bora. Haya mambo ya bure ni kiinimacho ambacho pia kinawafanya baadhi ya wazazi kubweteka na kufikiria kuwa wanaweza kuzaa idadi yoyote ya watoto kwa vile gharama za elimu ni 'bure'!
 
we kweli kizibo nani kataja uvyama hapa?? ndo shida yetu wabongo mambo serious mnaleta uvyama huu unaofanya ni undorobo wewe
 
Back
Top Bottom