Wanaofeli kidato cha pili,wafuatiliwe kama wanafunzi wengine

Mayo clinic

Member
Sep 1, 2022
23
22
Yamekuwepo mazoea mabaya sana ya kutowafuatilia wanafunzi wanaoshindwa katika mitihani ya upimaji ya kidato cha pili.Yaani mtoto na mzazi wanaamua wenyewe kama iwe mwisho wa kusoma au arudie darasa.kunakuwa hakuna ulazima tena.
Hali hii imejengeka na kuwa mazoea kiasi kwamba hakuna anaejali.Matokeo Yake ni kwamba kumekuwa na ongezeko la watoto mitaani ambao hawana mwelekeo wowote.
Serikali ni vizuri ikaingilia Kati na kukemea hali hii, kabla haijaota mizizi na watu wote wajue kuwa mtihani wa kidato cha pili,si hitimisho la kuendelea au kutoendelea na shule.
 
Yaani mtoto anashindwa kupata D kwenye masomo mawili au C ya somo moja tu kati ya tisa, hapo lazima wazazi wadau wengine wachanganyikiwe kidogo.

Siku hizi za elimu bila malipo mtoto anarudia mara moja tu, akifeli mara ya pili anapitishwa hivyo hivyo na box lake kichwani.

Na ndio hizo division zero za form 4 zisizokuwa na shaka.
 
Yaani mtoto anashindwa kupata D kwenye masomo mawili au C ya somo moja tu kati ya tisa, hapo lazima wazazi wadau wengine wachanganyikiwe kidogo.

Siku hizi za elimu bila malipo mtoto anarudia mara moja tu, akifeli mara ya pili anapitishwa hivyo hivyo na box lake kichwani.

Na ndio hizo division zero za form 4 zisizokuwa na shaka.
Angalau aendelee kuwa bize huko shuleni wakati umri unaongezeka,labda anaweza kuja kuwa na cha kufanya ktk jamii.Tuendelee kuwapa nafasi
 
Angalau aendelee kuwa bize huko shuleni wakati umri unaongezeka,labda anaweza kuja kuwa na cha kufanya ktk jamii.Tuendelee kuwapa nafasi
Na kwa zama hizi mtoto asipoenda shule basi ametaka mwenyewe tu,
serikali kwa nafasi yake imejitahidi kufungua fursa hata wale waliodrop kwa sababu mbalimbali kurudi shule kupita mpango wa SEQUIP.

Hawa wanaofeli upimaji wa kidato cha pili kwa kweli tuwaache waende shule kukua tu.
 
Back
Top Bottom