Mbangaizaji wa Taifa
JF-Expert Member
- Dec 25, 2024
- 468
- 806
TATHMINI FUPI PRESS YA WENJE:
1. Waandishi wa Habari wamemuonyesha Wenje kwamba wamechoka kusikia uongo wake. Maswali aliyoulizwa Wenje katika Taaluma ya Sheria kwenye hatua za Dodoso (Cross Examination) tunasema yanalenga kufanya Impeachment kwa Shahidi. Wenje amefanyiwa Impeachment kwa public, Waandishi wa Habari wameuonyesha umma kwamba usimwamini binadamu huyo tena!
2. Psychology ya Waandishi na Wahariri wa Tanzania imekaa mkao wa kumpokea LISSU kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA na hivyo, wameonyesha kukasirika tabia za Wenje anapomchafua Lissu kwa namna yoyote ile. Wanahabari wameuliza maswali ambayo yanampinga kabisa Wenje na kumtetea Lissu, Lema na wengine. Yaani Waandishi wamesimama kama Mawakili wa Utetezi kuhakikisha porojo za Wenje hazileti madhara kwa Lissu dhidi ya umma. Wamefanya kazi ya ku- Dilute na ku- neutralize madhara yoyote ambayo Wenje alikusudia kuyaelekeza kwa LISSU na timu yake kwa kuwachafua kwa Umma.
3. Press ya Wenje imejijibu yenyewe palepale. Maswali ya Waandishi yameharibu shutuma zote na kugeuza kibao Wenje ameonekana ni Galasa, Punguani na Mzushi wa kiwango cha BWEGE. Haihitaji sana Lissu au Lema kuita press kumjibu Wenje. Amejimaliza mwenyewe.
4. Waandishi wameonyesha ushupavu kuwa wao ni sehemu ya jamii na wanaijua jamii inayohusiana na Press ya Wenje. Wamefanya tafiti za kutosha, wanajua kila kitu kuhusu maisha ya CHADEMA na mambo yake. Kwahiyo kila sentensi iliyotamkwa na Wenje kwa upotofu, wameinyoosha na kumkanusha kwa FACTS.
5. Press ya leo ya WENJE imempa Aibu Kuu yeye na MBOWE kwa pamoja. Ameonekana kabisa amepangwa na kutumwa, kugeuza maneno ya kuwaondoa Watu kwenye uelewa wa kawaida kuhusu ushindani wa kisiasa na Demokrasia kati ya LISSU vs MBOWE, HECHE vs WENJE; badala yake wakaubatiza ushindani huo jina baya la kwamba ni mwendelezo wa Njama, fitna, uhalifu, uhaini na ushenzi wa kufanya MAPINDUZI ya Uongozi wa CHADEMA mwaka 2021/22. Jambo ambalo kila mtu mwenye akili analikataa, Waandishi wamelikataa na kulipigia maswali mazito ambayo Wenje amepoteana kuyajibu. Kwa Press hii, Wenje ameshuka kutoka kuwa na alama 0% na kuangukia -1% (negative one).
6. Director wa Movie ya Wenje kutengeneza uongo wa 'Mapinduzi' ni mtu mwenye akili ndogo. Ameandika vibaya script, halafu mchezaji wa scene ni kilaza bwege ameharibu kabisa; mwisho Mkanda umeungua na picha zimeharibika. Badala ya Bongo Movie, imekuwa BONGO MAVI Series za Mawinga. Wameangukia aibu.
7. Aibu hii ya Wenje na Mbowe ni matokeo ya kushindana na Sheria ya Asili (Law of nature). Majira na Nyakati vimefanywa na MUNGU, na yeye huibua karama na vipawa kwa wakati na mahitaji yake kadiri anavyotaka kuihudumia Jamii. Mbowe huyu wa 2025 anataka awe na kibali kwa jamii kama yule Mbowe wa 2005-2018.
HUO MUUJIZA UMEFUNGWA, hatafanikiwa. Huu ni wakati wa TUNDU LISSU, Mungu amempa kibali na ukubalifu kwa jamii kadiri inavyompendeza yeye. Hata Lissu hizi sifa za sasa sio za kudumu, wataibuka Wapinzani wengine. Mbowe ends up being a Political Reject of the recent Tanzania Politics.
Wahenga wa kizungu waliwahi kusema, "Nature is a home to stay, not a place to visit." Ukipambana na nature utaumia tu.
Wenje ni kilaza cha makamo!
Ni kilaza kilichochelewa kugundulika.
Wenje, ntobi na yeriko ni vilaza viandamizi.
Over!