Vatican ni mfupa mgumu, wamekataa kusalimu amri kwa Wakomunisti wa China kwa miaka zaidi ya 70 sasa

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
49,615
72,474
Mpaka leo hii China bara hakuna uwakilishi wa rasmi wa Kanisa Katoliki la Roma, shughuli zao zinafanywa na "underground church" ambalo ni kanisa la mafichoni na lisilotambuliwa na serikali ya China. Kanisa Katoliki la Taiwan ndili linalotambulika rasmi kama kanisa la China japo serikali ya China inapinga sana suala hili.

Chanzo cha haya yoto ni Mgogoro mkubwa uliozuka baada ya mapinduzi ya wakomunisti ambapo Mao Zedong aliamuru taasisi zote za kijamii China kuendeshwa kwa maelekezo ya mkono wa serikali ikiwemo serikali kuwa inachagua au kufanya vetting hadi ya viongozi wa kidini. Wakatoliki wao waliambiwa zaidi wanatakiwa kumkana Papa kama kiongozi wao mkuu.

Hili jambo Wakatoliki walilikataa kabisa wakashindwa kuelewana na serikali ya China ikapelekea serikali kuanzisha kitu kinachoitwa Umoja wa Wakatoli wazalendo/Catholic Patriotic Association (CCPA) kama mbadala wa kanisa Katoliki. Kwenye hili kanisa Katoliki la serikali la Kichina makadinali na Maaskofu wake huwa wanateuliwa kwa muongozo wa serikali na hawamtambui Papa kama kiongozi wao mkuu.

Upande mwingine Vatican wao hawalitambui kanisa Katoliki la Kichina/CCPA bali wanalitambua lile lilo mafichoni ikiwemo papa kuteua Maaskofu na makadinali wake kwa siri. Huko China kuna Maaskofu wa papa lakini huwa hawatangazwi mpaka wanakufa! Kwa wale ambao siri zinavuja na kutiwa nguvuni na Serikali ya China huwa wananyooshwa kweli magerezani au kupotea.

Papa Francis aliyefariki alijaribu kuleta maelewano na serikali ya China ikashindikana baada ya kupata upinzani mkali kutoka ndani ya kanisa kwenye.
 
Mpaka leo hii China bara hakuna uwakilishi wa rasmi wa Kanisa Katoliki la Roma, shughuli zao zinafanywa na "underground church" ambalo ni kanisa la mafichoni na lisilotambuliwa na serikali ya China. Kanisa Katoliki la Taiwan ndili linalotambulika rasmi kama kanisa la China japo serikali ya China inapinga sana suala hili.

Chanzo cha haya yoto ni Mgogoro mkubwa uliozuka baada ya mapinduzi ya wakomunisti ambapo Mao Zedong aliamuru taasisi zote za kijamii China kuendeshwa kwa maelekezo ya mkono wa serikali ikiwemo serikali kuwa inachagua au kufanya vetting hadi ya viongozi wa kidini. Wakatoliki wao waliambiwa zaidi wanatakiwa kumkana Papa kama kiongozi wao mkuu.

Hili jambo Wakatoliki walilikataa kabisa wakashindwa kuelewana na serikali ya China ikapelekea serikali kuanzisha kitu kinachoitwa Umoja wa Wakatoli wazalendo/Catholic Patriotic Association (CCPA) kama mbadala wa kanisa Katoliki. Kwenye hili kanisa Katoliki la serikali la Kichina makadinali na Maaskofu wake huwa wanateuliwa kwa muongozo wa serikali na hawamtambui Papa kama kiongozi wao mkuu.

Upande mwingine Vatican wao hawalitambui kanisa Katoliki la Kichina/CCPA bali wanalitambua lile lilo mafichoni ikiwemo papa kuteua Maaskofu na makadinali wake kwa siri. Huko China kuna Maaskofu wa papa lakini huwa hawatangazwi mpaka wanakufa! Kwa wale ambao siri zinavuja na kutiwa nguvuni na Serikali ya China huwa wananyooshwa kweli magerezani au kupotea.

Papa Francis aliyefariki alijaribu kuleta maelewano na serikali ya China ikashindikana baada ya kupata upinzani mkali kutoka ndani ya kanisa kwenye.
China wapo sahihi sana. Laiti ungelijua wazungu kupitia haya makanisa wanavyotupiga aubwaarabu kupitia hii misikiti wanavyotupiga ungewasifu wachina. Pamoja na hivyo kuna makanisa ya kikatoliki mengi yasiyotambua utawala wa papa sema kwasababu hujui umeshikilia china. Unafikir kanisa katoliki la mashariki linamtqmbua Pope kama kiongoz mkuu?
 
Nafikiri mfupa mgumu ndio hao wakomunisti kwanza mkataba wa makubaliano kati yao na kanisa katoliki hawauzingatii,pili wamefunga maaksofu wao na hakuna kitu Vatican imeafanya, tatu papa ndie ana omba makubaliano yao na wao wakubali taratibu za Roma kitu ambacho mpaka sasa hawafanyi hii kitu ni serikali chache sana zina hizi guts dhidi ya kanisa katoliki
 
Pope Francis katika uhai wake alikuwa akiiomba serikali ya China itoe uhuru kamili kwa Vatican kuwa na mamlaka na kanisa katoliki huko China kitu ambacho mpaka anakufa hakuwahi kukishuhudia hata papa atakayekuja hii ndio hali atakayo kutana nayo.
 
China wapo sahihi sana. Laiti ungelijua wazungu kupitia haya makanisa wanavyotupiga aubwaarabu kupitia hii misikiti wanavyotupiga ungewasifu wachina. Pamoja na hivyo kuna makanisa ya kikatoliki mengi yasiyotambua utawala wa papa sema kwasababu hujui umeshikilia china. Unafikir kanisa katoliki la mashariki linamtqmbua Pope kama kiongoz mkuu?
I wish nipate elimu hapa, kanisa katoliki linatupigaje na misikiti nayo inatupigaje kupitia kwa Waarabu. Tafadhari naomba elimu kidogo ju ya jambo hilo ulilo raise
 
I wish nipate elimu hapa, kanisa katoliki linatupigaje na misikiti nayo inatupigaje kupitia kwa Waarabu. Tafadhari naomba elimu kidogo ju ya jambo hilo ulilo raise
Zote hizo ni taasisi za kijasusi za watu mzee stuka. Hatusemi kuwa hawafanyi kaz za Mungu. Wazee wamepenyeza huko agenda zao za kutosha. Kama uliona DPW ilivyodhupaliwa na wale wakulugwa. Haikuwa bure.
 
Back
Top Bottom