UTALII WA KILIMO: Hiki ni kitu nilichokishuhudia wakati natafuta fursa za Kilimo Mkoa wa Iringa

Kommando muuza madafu

JF-Expert Member
Aug 30, 2022
3,161
7,199
Habari za jioni wana JF.

Katika kutafuta fursa za kimaisha baada ya kustaafishwa rasmi na Trump πŸ˜ƒπŸ˜„πŸ˜πŸ˜€.

Niliwasiliana na jamaa yangu mmoja ambaye naye amestaafishwa na Trump ambaye alikuwa anafanya kazi kwenye shirika moja la Kilimo huko Iringa. Jamaa alinieleza fursa za Kilimo kwenye Kulima, kununua, kuchakata lakini pia kwenye uuzaji wa pembejeo za kilimo Mkoani Iringa.

Nikapanga safari ya kwenda Iringa ili nijionee mwenyewe fursa hizo kwenye mazao ya Mboga na Matunda pia na mazao ya Nafaka hususani Mahindi. Jamaa yangu akaniunganisha na maafisa Kilimo wa Serikali kwenye Wilaya za Kilolo, Mufindi na Iringa DC.

Nilianza safari ya kutoka Dar hadi Iringa. Tukapita Morogoro nika enjoy pale Mikumi kwa kuona wanyama angalau nipunguze mawazo ya Trump na kile alichotufanyia. Nikafurahia zaidi Iyovi na yale makona na namna kuna mito inapita karibu na barabara.

Safari ikaendelea hadi Ruahambuyuni na barabarani naona vitunguu vingi vikiwa vimepandwa mashambani lakini pia vijana wakiuza vitunguu barabarani wakiweka kwenye vindoo.

Kituo changu cha Kwanza.
Kituo changu cha kwanza kilikuwa Ruahambuyuni. Nilitafuta sehemu ya kulala kisha nikawasiliana na BWANA SHAMBA FARM. Yule Bwana Shamba wa Ruahambuyuni anayejishughulisha na uzalishaji wa miche ya mboga na matunda, uuzaji wa pembejeo za Kilimo pamoja na uzalishaji wa mazao ya mboga na matunda.

Itaendelea ikiambatana na picha.

====

Sehemu ya pili

Inaendelea sehemu 2.
Nilipolelewa na yule Bwana Shamba na akaanza kunipeleka kwenye eneo lake la Uzalishaji wa Miche.
View attachment 3236486

Ni kweli yule jamaa anaitendea haki taaluma yake ya Kilimo. Anazalisha miche ya mazao ya Mboga mboga kama Nyanya, Hoho, Pilipili mwendokasi n.k. Amekuwa msaada kwa wakulima wa eneo husika na binafsi nilijifunza kuwa uuzaji wa miche ya mboga na matunda ni fursa kubwa sana kwenye maeneo ya Ruahambuyuni na Iringa kwa ujumla. Mtaalamu yule ana duka lake la Pembejeo na anauzia wakulima wanotiririka mamia kwa mamia madawa na mbegu bora za mazao lakini pia anauza na mbolea.

Tunatoka hapo na kwenda shambani kwake ambapo analima mazao mbalimbali kama kitunguu, Hoho, Nyanya na Pilipili mwendokasi.

Pale Ruahambuyuni watu wanamaanisha na unaweza juta kwanini nilikuwa nangangania kuishi Dar huku nikifanya kazi badala ya kujiajiri kwenye Kilimo. Jamaa wana skimu yao ya umwagiliaji ambayo hutumia kumwagilia mashamba yao. Nimeona aina mbalimbali za pumpu mbalimbali zilizofungwa mtoni ambazo humwagilia maji umbali wa zaidi ya Kilomita 6 hadi 10.
View attachment 3236493
Mkulima aliyevuna Pilipili Mwendokasi akiwa na noti zake.πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€
 
Habari za jioni wana JF.

Katika kutafuta fursa za kimaisha baada ya kustaafishwa rasmi na Trump πŸ˜ƒπŸ˜„πŸ˜πŸ˜€.

Niliwasiliana na jamaa yangu mmoja ambaye naye amestaafishwa na Trump ambaye alikuwa anafanya kazi kwenye shirika moja la Kilimo huko Iringa. Jamaa alinieleza fursa za Kilimo kwenye Kulima, kununua, kuchakata lakini pia kwenye uuzaji wa pembejeo za kilimo Mkoani Iringa.

Nikapanga safari ya kwenda Iringa ili nijionee mwenyewe fursa hizo kwenye mazao ya Mboga na Matunda pia na mazao ya Nafaka hususani Mahindi. Jamaa yangu akaniunganisha na maafisa Kilimo wa Serikali kwenye Wilaya za Kilolo, Mufindi na Iringa DC.

Nilianza safari ya kutoka Dar hadi Iringa. Tukapita Morogoro nika enjoy pale Mikumi kwa kuona wanyama angalau nipunguze mawazo ya Trump na kile alichotufanyia. Nikafurahia zaidi Iyovi na yale makona na namna kuna mito inapita karibu na barabara.

Safari ikaendelea hadi Ruahambuyuni na barabarani naona vitunguu vingi vikiwa vimepandwa mashambani lakini pia vijana wakiuza vitunguu barabarani wakiweka kwenye vindoo.

Kituo changu cha Kwanza.
Kituo changu cha kwanza kilikuwa Ruahambuyuni. Nilitafuta sehemu ya kulala kisha nikawasiliana na BWANA SHAMBA FARM. Yule Bwana Shamba wa Ruahambuyuni anayejishughulisha na uzalishaji wa miche ya mboga na matunda, uuzaji wa pembejeo za Kilimo pamoja na uzalishaji wa mazao ya mboga na matunda.

Itaendelea ikiambatana na picha.
Hizi Itaendelea kama za Trump!
 
Inaendelea sehemu 2.
Nilipolelewa na yule Bwana Shamba na akaanza kunipeleka kwenye eneo lake la Uzalishaji wa Miche.
IMG-20250214-WA0003.jpg


Ni kweli yule jamaa anaitendea haki taaluma yake ya Kilimo. Anazalisha miche ya mazao ya Mboga mboga kama Nyanya, Hoho, Pilipili mwendokasi n.k. Amekuwa msaada kwa wakulima wa eneo husika na binafsi nilijifunza kuwa uuzaji wa miche ya mboga na matunda ni fursa kubwa sana kwenye maeneo ya Ruahambuyuni na Iringa kwa ujumla. Mtaalamu yule ana duka lake la Pembejeo na anauzia wakulima wanotiririka mamia kwa mamia madawa na mbegu bora za mazao lakini pia anauza na mbolea.

Tunatoka hapo na kwenda shambani kwake ambapo analima mazao mbalimbali kama kitunguu, Hoho, Nyanya na Pilipili mwendokasi.

Pale Ruahambuyuni watu wanamaanisha na unaweza juta kwanini nilikuwa nangangania kuishi Dar huku nikifanya kazi badala ya kujiajiri kwenye Kilimo. Jamaa wana skimu yao ya umwagiliaji ambayo hutumia kumwagilia mashamba yao. Nimeona aina mbalimbali za pumpu mbalimbali zilizofungwa mtoni ambazo humwagilia maji umbali wa zaidi ya Kilomita 6 hadi 10.
1739443785086.jpg

Mkulima aliyevuna Pilipili Mwendokasi akiwa na noti zake.πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€

====

Sehemu ya tatu

Nitajitahidi niandike kifupi sana ili iishe yote.

Inaendelea.
Tukatoka Ruahambuyuni akanipeleka skimu za Umwagiliaji za Msosa pamoja na Ikula ambazo zipo katika Kata ya Ruahambuyuni. Huko watu wanalima kwa kwenda mbele na mzunguko wa Pesa ni mkubwa sana.

Kesho yake akaniunganisha na jamaa yake mmoja pale Mtandika ili anioneshe fursa ya Kilimo cha umwagiliaji katika Kijiji cha Mtandika pamoja na kule ndani ndani panaitwa Mgowelo na Nyanzwa. Mtandika wana skimu ya umwagiliaji na jamaa wamepiga kambi huko wanalima kwa kwenda mbele. Napemda kuwapongeza wale jamaa wa Kilolo kwani wamejitahidi kujenga skimu za umwagiliaji kwenye maeneo yasiyo na mvua nyingi. Kuna mradi mkubwa wa skimu wanaita ya Mgambalenga inaendelea pale Mtandika. Itawasaiaidia sana wakulima wa eneo lile. Baada ya kuona fursa kwenye Kilimo kwa kutumia skimu ya umwagiliaji Mrandika, safari iliendelea kwa pikipiki ya Bwana Shamba wa Pale Mtandika kwenda huko ndanindani kama unaenda Mpwapwa panaitwa Mgowelo na Nyanzwa.

Huko kuna wasukuma, wamasai na makabila wengine wakifuga mifugo pamoja na kulima mbegu za vitunguu. Hapa palinivutia sana kwani wana skimu za Umwagiliaji ambazo wakulima wanalima mboga mboga na matunda. Mzunguko wa pesa ni mkubwa japo pana changamoto ya umbali toka barabara kuu hadi huko ila pana maji na umeme na barabara inafikika vizuri kipindi chote cha mwaka.

Utalii wa Kilimo sasa.
Hapa ndipo pana msingi wa uzi wangu. Baada ya kumaliza kutoka nyanzwa ambapo kuna maeneo na ardhi wanauza tsh 30,000 hadi 50,000 kwa ekari Safari yangu iliendelea ya kupanda ymlima Kitonga hadi Ilula. Nilienda kutafuta sehemu ya kulala ili naingalie fursa katika mji wa Ilula na maeneo ya jirani.

Asububi yangu ilianza kwa kuwasiliana na Bwana Shamba wa Pale Ilula. Yule jamaa naye anauza miche ya mazao ya Mboga na matunda. Mji ule umechangamka sana. Akanipitisha kwenye maduka ya Pembejeo na tukafika hadi pale kwenye kiwanda cha kuchakata nyanya. Tukaenda soko la TASAF kuangalia uuzaji wa nyanya pale na ilpofika saa 7 akanipeleka Shamba moja kubwa wanaitwa farm for the Future.

Pale wanafanya Kilimo kilicho advance na wana program 3 muhimu ila kilichonifurahisha zaidi ni kituo chao cha Children farm.

Katika kituo hiko, wameanzisha mashamba ya mboga. Wamefuga samaki na mbuzi za maziwa pia wamefuga kuku za nyama na mayai. Kuna green house ambayo inazalisha mazao ya Mboga na matunda pia kuna jiko na ukumbi/Bwalo la chakula kwa ajili ya kuwafundisha watoto shughuli za kilimo na ufugaji wa Mbuzi za maziwa na Samaki.

Wasimamizi wa pale walinieleza kuwa huleta watoto toka vijiji mbalimbali na kuwafundisha kuhusu kilimo na ufugaji. Watafundishwa kuhusu kuku au samaki then wataenda kuvua samaki au kukusanya mayai ya kuku na kisha watoto kupika na kuyala pale. Kama ni Kilimo kwa kutumia green house na zile drip walizofungiwa na SAGCOT watafanya kwa vitendo nankuchuma mboga kisha kuzipika wenyewe na kuzila.
 
Habari za jioni wana JF.

Katika kutafuta fursa za kimaisha baada ya kustaafishwa rasmi na Trump πŸ˜ƒπŸ˜„πŸ˜πŸ˜€.

Niliwasiliana na jamaa yangu mmoja ambaye naye amestaafishwa na Trump ambaye alikuwa anafanya kazi kwenye shirika moja la Kilimo huko Iringa. Jamaa alinieleza fursa za Kilimo kwenye Kulima, kununua, kuchakata lakini pia kwenye uuzaji wa pembejeo za kilimo Mkoani Iringa.

Nikapanga safari ya kwenda Iringa ili nijionee mwenyewe fursa hizo kwenye mazao ya Mboga na Matunda pia na mazao ya Nafaka hususani Mahindi. Jamaa yangu akaniunganisha na maafisa Kilimo wa Serikali kwenye Wilaya za Kilolo, Mufindi na Iringa DC.

Nilianza safari ya kutoka Dar hadi Iringa. Tukapita Morogoro nika enjoy pale Mikumi kwa kuona wanyama angalau nipunguze mawazo ya Trump na kile alichotufanyia. Nikafurahia zaidi Iyovi na yale makona na namna kuna mito inapita karibu na barabara.

Safari ikaendelea hadi Ruahambuyuni na barabarani naona vitunguu vingi vikiwa vimepandwa mashambani lakini pia vijana wakiuza vitunguu barabarani wakiweka kwenye vindoo.

Kituo changu cha Kwanza.
Kituo changu cha kwanza kilikuwa Ruahambuyuni. Nilitafuta sehemu ya kulala kisha nikawasiliana na BWANA SHAMBA FARM. Yule Bwana Shamba wa Ruahambuyuni anayejishughulisha na uzalishaji wa miche ya mboga na matunda, uuzaji wa pembejeo za Kilimo pamoja na uzalishaji wa mazao ya mboga na matunda.

Itaendelea ikiambatana na picha.
Kuwa makini na matapeli wa ruaha mbuyuni .

Chunga uwekezani wako hapo
 
Inaendelea sehemu 2.
Nilipolelewa na yule Bwana Shamba na akaanza kunipeleka kwenye eneo lake la Uzalishaji wa Miche.
View attachment 3236486

Ni kweli yule jamaa anaitendea haki taaluma yake ya Kilimo. Anazalisha miche ya mazao ya Mboga mboga kama Nyanya, Hoho, Pilipili mwendokasi n.k. Amekuwa msaada kwa wakulima wa eneo husika na binafsi nilijifunza kuwa uuzaji wa miche ya mboga na matunda ni fursa kubwa sana kwenye maeneo ya Ruahambuyuni na Iringa kwa ujumla. Mtaalamu yule ana duka lake la Pembejeo na anauzia wakulima wanotiririka mamia kwa mamia madawa na mbegu bora za mazao lakini pia anauza na mbolea.

Tunatoka hapo na kwenda shambani kwake ambapo analima mazao mbalimbali kama kitunguu, Hoho, Nyanya na Pilipili mwendokasi.

Pale Ruahambuyuni watu wanamaanisha na unaweza juta kwanini nilikuwa nangangania kuishi Dar huku nikifanya kazi badala ya kujiajiri kwenye Kilimo. Jamaa wana skimu yao ya umwagiliaji ambayo hutumia kumwagilia mashamba yao. Nimeona aina mbalimbali za pumpu mbalimbali zilizofungwa mtoni ambazo humwagilia maji umbali wa zaidi ya Kilomita 6 hadi 10.
View attachment 3236493
Mkulima aliyevuna Pilipili Mwendokasi akiwa na noti zake.πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€
Kama haitaendelea ndo imeishia hapa na umeamua kuandika ulichokiandika ni dhahiri marekani walikuwa na mzigo mzito sana wenye less masirahi.
 
Habari za jioni wana JF.

Katika kutafuta fursa za kimaisha baada ya kustaafishwa rasmi na Trump πŸ˜ƒπŸ˜„πŸ˜πŸ˜€.

Niliwasiliana na jamaa yangu mmoja ambaye naye amestaafishwa na Trump ambaye alikuwa anafanya kazi kwenye shirika moja la Kilimo huko Iringa. Jamaa alinieleza fursa za Kilimo kwenye Kulima, kununua, kuchakata lakini pia kwenye uuzaji wa pembejeo za kilimo Mkoani Iringa.

Nikapanga safari ya kwenda Iringa ili nijionee mwenyewe fursa hizo kwenye mazao ya Mboga na Matunda pia na mazao ya Nafaka hususani Mahindi. Jamaa yangu akaniunganisha na maafisa Kilimo wa Serikali kwenye Wilaya za Kilolo, Mufindi na Iringa DC.

Nilianza safari ya kutoka Dar hadi Iringa. Tukapita Morogoro nika enjoy pale Mikumi kwa kuona wanyama angalau nipunguze mawazo ya Trump na kile alichotufanyia. Nikafurahia zaidi Iyovi na yale makona na namna kuna mito inapita karibu na barabara.

Safari ikaendelea hadi Ruahambuyuni na barabarani naona vitunguu vingi vikiwa vimepandwa mashambani lakini pia vijana wakiuza vitunguu barabarani wakiweka kwenye vindoo.

Kituo changu cha Kwanza.
Kituo changu cha kwanza kilikuwa Ruahambuyuni. Nilitafuta sehemu ya kulala kisha nikawasiliana na BWANA SHAMBA FARM. Yule Bwana Shamba wa Ruahambuyuni anayejishughulisha na uzalishaji wa miche ya mboga na matunda, uuzaji wa pembejeo za Kilimo pamoja na uzalishaji wa mazao ya mboga na matunda.

Itaendelea ikiambatana na picha.
Remain honorable always!
 
Nitajitahidi niandike kifupi sana ili iishe yote.

Inaendelea.
Tukatoka Ruahambuyuni akanipeleka skimu za Umwagiliaji za Msosa pamoja na Ikula ambazo zipo katika Kata ya Ruahambuyuni. Huko watu wanalima kwa kwenda mbele na mzunguko wa Pesa ni mkubwa sana.

Kesho yake akaniunganisha na jamaa yake mmoja pale Mtandika ili anioneshe fursa ya Kilimo cha umwagiliaji katika Kijiji cha Mtandika pamoja na kule ndani ndani panaitwa Mgowelo na Nyanzwa. Mtandika wana skimu ya umwagiliaji na jamaa wamepiga kambi huko wanalima kwa kwenda mbele. Napemda kuwapongeza wale jamaa wa Kilolo kwani wamejitahidi kujenga skimu za umwagiliaji kwenye maeneo yasiyo na mvua nyingi. Kuna mradi mkubwa wa skimu wanaita ya Mgambalenga inaendelea pale Mtandika. Itawasaiaidia sana wakulima wa eneo lile. Baada ya kuona fursa kwenye Kilimo kwa kutumia skimu ya umwagiliaji Mrandika, safari iliendelea kwa pikipiki ya Bwana Shamba wa Pale Mtandika kwenda huko ndanindani kama unaenda Mpwapwa panaitwa Mgowelo na Nyanzwa.

Huko kuna wasukuma, wamasai na makabila wengine wakifuga mifugo pamoja na kulima mbegu za vitunguu. Hapa palinivutia sana kwani wana skimu za Umwagiliaji ambazo wakulima wanalima mboga mboga na matunda. Mzunguko wa pesa ni mkubwa japo pana changamoto ya umbali toka barabara kuu hadi huko ila pana maji na umeme na barabara inafikika vizuri kipindi chote cha mwaka.

Utalii wa Kilimo sasa.
Hapa ndipo pana msingi wa uzi wangu. Baada ya kumaliza kutoka nyanzwa ambapo kuna maeneo na ardhi wanauza tsh 30,000 hadi 50,000 kwa ekari Safari yangu iliendelea ya kupanda ymlima Kitonga hadi Ilula. Nilienda kutafuta sehemu ya kulala ili naingalie fursa katika mji wa Ilula na maeneo ya jirani.

Asububi yangu ilianza kwa kuwasiliana na Bwana Shamba wa Pale Ilula. Yule jamaa naye anauza miche ya mazao ya Mboga na matunda. Mji ule umechangamka sana. Akanipitisha kwenye maduka ya Pembejeo na tukafika hadi pale kwenye kiwanda cha kuchakata nyanya. Tukaenda soko la TASAF kuangalia uuzaji wa nyanya pale na ilpofika saa 7 akanipeleka Shamba moja kubwa wanaitwa farm for the Future.

Pale wanafanya Kilimo kilicho advance na wana program 3 muhimu ila kilichonifurahisha zaidi ni kituo chao cha Children farm.

Katika kituo hiko, wameanzisha mashamba ya mboga. Wamefuga samaki na mbuzi za maziwa pia wamefuga kuku za nyama na mayai. Kuna green house ambayo inazalisha mazao ya Mboga na matunda pia kuna jiko na ukumbi/Bwalo la chakula kwa ajili ya kuwafundisha watoto shughuli za kilimo na ufugaji wa Mbuzi za maziwa na Samaki.

Wasimamizi wa pale walinieleza kuwa huleta watoto toka vijiji mbalimbali na kuwafundisha kuhusu kilimo na ufugaji. Watafundishwa kuhusu kuku au samaki then wataenda kuvua samaki au kukusanya mayai ya kuku na kisha watoto kupika na kuyala pale. Kama ni Kilimo kwa kutumia green house na zile drip walizofungiwa na SAGCOT watafanya kwa vitendo nankuchuma mboga kisha kuzipika wenyewe na kuzila.

====

Sehemu ya nne

Inaendelea:
Pale farm for the Future pia wanaprogarm ya Young Mothers. Katika program hiyo, husapoti mabinti waliozalishwa na kutelekezwa na wenza wao au kukatishwa masomo tokana na kupata ujauzito.

Mabinti hao husapotiwa kwa kupewa elimu ya Kilimo, Ufugaji na ujasiliamali kisha hupewa mitaji kama ya mbuzi au mashamba au vifaa vya ujasiliamali na kusimamiwa ili waweze kujisimamia wenyewe kiuchumi.

Shamba hilo lililo chini ya taasisi fulani ya kidini toka nje ya nchi wana mradi wa shamba ambapo hulima mbegu za mahindi kwa ajili ya SEEDCO lakini pia wamepanda karanga mwitu, viazi na Alizeti. Jamaa wana Advance technology nami niliona mengi wa mara ya kwanza kwenye maisha yangu.

HOLISTIC FARMING.
Nimechoka nitaendelea kesho.
View attachment 3236560
 

Attachments

  • VID-20250210-WA0002.mp4
    2.6 MB
Daaa...hii kustaafishwa imenchekesha sana mwanangu!
Koo mmekula ridandasi
Habari za jioni wana JF.

Katika kutafuta fursa za kimaisha baada ya kustaafishwa rasmi na Trump πŸ˜ƒπŸ˜„πŸ˜πŸ˜€.

Niliwasiliana na jamaa yangu mmoja ambaye naye amestaafishwa na Trump ambaye alikuwa anafanya kazi kwenye shirika moja la Kilimo huko Iringa. Jamaa alinieleza fursa za Kilimo kwenye Kulima, kununua, kuchakata lakini pia kwenye uuzaji wa pembejeo za kilimo Mkoani Iringa.

Nikapanga safari ya kwenda Iringa ili nijionee mwenyewe fursa hizo kwenye mazao ya Mboga na Matunda pia na mazao ya Nafaka hususani Mahindi. Jamaa yangu akaniunganisha na maafisa Kilimo wa Serikali kwenye Wilaya za Kilolo, Mufindi na Iringa DC.

Nilianza safari ya kutoka Dar hadi Iringa. Tukapita Morogoro nika enjoy pale Mikumi kwa kuona wanyama angalau nipunguze mawazo ya Trump na kile alichotufanyia. Nikafurahia zaidi Iyovi na yale makona na namna kuna mito inapita karibu na barabara.

Safari ikaendelea hadi Ruahambuyuni na barabarani naona vitunguu vingi vikiwa vimepandwa mashambani lakini pia vijana wakiuza vitunguu barabarani wakiweka kwenye vindoo.

Kituo changu cha Kwanza.
Kituo changu cha kwanza kilikuwa Ruahambuyuni. Nilitafuta sehemu ya kulala kisha nikawasiliana na BWANA SHAMBA FARM. Yule Bwana Shamba wa Ruahambuyuni anayejishughulisha na uzalishaji wa miche ya mboga na matunda, uuzaji wa pembejeo za Kilimo pamoja na uzalishaji wa mazao ya mboga na matunda.

Itaendelea ikiambatana na picha.
 
Back
Top Bottom