Utafiti wa Simbachawene,ni maandalizi ya watumishi kupungunzwa makazini au ongezeko la mishahara!!?

RESILIENT KATO

JF-Expert Member
Aug 21, 2024
1,434
2,698
Kuna Kila dalili la anguko la uchumi wa Dunia Hadi sasa,Kuna dalili za mabenki kufilisika huko tuendako,je tunaandaliwa kisaikilojia!!?

Au ni Ile mbinu ya jk enzi zile ambayo dokta anaeozea mahabusu aliishtukia kipindi kile!!?

Wajuvi mje mjazie nyama hapa!
 
Utafiti wa kijinga tu huo. Yaani wanategemea mtumishi wa umma mwenye akili timamu afanye kazi kwa moyo, halafu mwisho wa mwezi analipwa mshahara mbuzi!

Na wakati huo huo Mbunge anayetakiwa kujua tu kusoma na kuandika, analipwa mamilioni ya shilingi kila mwezi, hata asipochangia chochote!!
 
Utafiti wa kijinga tu huo. Yaani wanategemea mtumishi wa umma mwenye akili timamu afanye kazi kwa moyo, halafu mwisho wa mwezi analipwa mshahara mbuzi!

Na wakati huo huo Mbunge anayetakiwa kujua tu kusoma na kuandika, analipwa mamilioni ya shilingi kila mwezi, hata asipochangia chochote!!
Mtu yeyote ambaye hana majibu ya mambo magumu hutafuta kisingizo Ili apate pa kujishika...Wafanyakazi wataachaje kuwa mizigo kama hujawaongezea mishahara yenye kuleta maana siyo kiini macho Kwa Miaka kumi? Wataachaje kuwa mizigo kama wanaowaongoza wengi wao hawajui wanawaongoza kwenda wapi Ili iweje zaidi ya kutaka kutukuzwa na kusifiwa?

Hali ya mfanyakazi wa Tanzania ni ngumu mno aelewe hilo kwanza kabla ya kuanza kupeleka lawama Kwa watu waliokosa matumaini na hasa nyakati hizi za chaguzi. Anatakaje kwamfano? Wafanyakazi waipigie serikali ya CCM kura ya hapana ama? Yeye mfaidika miaka yote hiyo Leo anataka kukifarakanisha chama chetu na wapiga kura ama, Ili hali yeye ndiye anatakiwa awe na hayo majibu ya kwanini?
 
Wahisani wanapoanza kujitoa Kwa nchi zetu,kila mtu afe kivyake ni rasmi vita vya kiuchumi vitaua mabenki yetu!
Kwakua na ma benki yenyewe yaliegemea Kwa wale ambao wanawategemea wafadhili badala ya kujenga uchumi wa watu wa kawaida...Mpaka waite maji ma!
 
Back
Top Bottom