Usikubali kuwa mtu wa kukumbukwa na marafiki wakiwa na shida tu, wewe sio choo

Mwanasayansi Kalivubha

JF-Expert Member
Feb 4, 2024
342
916
UKIONA WANAKUKUMBUKA TU WAKIWA NA SHIDA JUA UMUHIMU WAKO NI MDOGO KWENYE MAISHA YAO MENGINE 😔

Ukitafutwa kwenye shida tu tafasiri ni kuwa muda mwingi wakiwa na raha hutumia na wengine ila kwenye majanga ndio wanakukumbuka wewe na baada ya utatuzi unasahaulika tena, Wewe sio Choo.

Hata Choo huwa kinakumbukwa kusafishwa kisha ndio kinasahaulika mpaka mtu apate haja ndio anakumbuka tena umuhimu wa Choo, ila wewe hata salaam hawakupi na siku ukiona tu meseji yao au mwito wao moja kwa moja akilini unajiandaa kutatua shida, kwanini wakukumbuke nyakati ngumu tu?

Tena sifa ya watu hao kubwa ni kuificha pindi wewe ukiwa unawahitaji na hapo utasikia vizingizio vya kila namna kutoka kwao.

Sasa kuna mtu akiwa anatafutwa kwenye shida tu hivimba kichwa na kujiona yeye ndio kila kitu mjini 😄 Janjaruka acha ujinga huo kwani wengine hutafutwa kwenye raha ila wewe unatafutwa kwenye shida na hulipwi chochote.

Kataa kabisa kuwa mtu wa kutafutwa kwenye majanga na sio kwamba wewe ni mtatuzi mzuri la hasha bali wamkuona wewe ni mdhaifu kwenye kipengele hicho ndio maana usipomsaidia zaidi ya mara mbili hutafuta pengine dhaifu kwa sababu tayari anakuona umekuwa mjanja sasa 😊

Mwanasayansi Saul Kalivubha

Mitandaoni kwa jina la Fikia Ndoto Zako.

+255652134707
 
Bandiko zuri lakini Kuna upande Bado haujauona.

Unapoona unatafutwa sana na marafiki au watu mnaofahamiana kipindi wanapojipata wapo kwenye matatizo basi sio jambo baya, jua Kuna kitu kikubwa ndani yako ambacho hawawezi kukipata sehemu nyingine isipokuwa kwako, Kwa maana hiyo wewe ni muhimu sana kwenye maisha yao.

Baada ya kulijua Hilo sasa ni muda wako wakuanza kuwatumia pia na wao Kwa chochote walichokuwa nacho either ushawishi, fedha (uchumi), nafasi, ujuzi na mengine mengi kusogeza mambo yako maana wanadeni lako wanalotakiwa kulipa.

Be cleaver enough to make a mutual friendship.
 
Hii ipo applicable kwa madaktari.

imekuwa ni kawaida kupotezea namba ngeni au namba zinazo watafuta wakat wanaumwa tu au wana taka kuuliza issues za dawa na Pombe.

wengi bado wana amini madaktari wanasomeshwa bure, au wana lipwa mishahara na serikali.
hawa jiulizi mbona mfano kama ni mwalimu, muulize mbona we huamshwi saa tisa usiku umsaidie dogo kunyambulisha, au ngeli za nomino.
 
Huu uzi kwangu una ukweli %100 kuna jamaa anaitwa Robert sitamtaja jina la pili ila mngoni mweupe enzi hizo akiwa anataka kukopa mahali ananitafuta mimi yeye ni boss ila akiwa kwenye njema anaspendi na washkaji wa benki sitamsahau mbwa yule. Akisoma hii post yangu atajitambua maisha yamebadilika namimi sasa ni boss namiliki na mkwasa (na hapa ipo) Sasa hivi namuona pimbi tu.
 
Bandiko zuri lakini Kuna upande Bado haujauona.

Unapoona unatafutwa sana na marafiki au watu mnaofahamiana kipindi wanapojipata wapo kwenye matatizo basi sio jambo baya, jua Kuna kitu kikubwa ndani yako ambacho hawawezi kukipata sehemu nyingine isipokuwa kwako, Kwa maana hiyo wewe ni muhimu sana kwenye maisha yao.

Baada ya kulijua Hilo sasa ni muda wako wakuanza kuwatumia pia na wao Kwa chochote walichokuwa nacho either ushawishi, fedha (uchumi), nafasi, ujuzi na mengine mengi kusogeza mambo yako maana wanadeni lako wanalotakiwa kulipa.

Be cleaver enough to make a mutual friendship.
✍️
 
Back
Top Bottom