UNHCR: Idadi ya wanaozamia Barani Ulaya na kufariki yaongezeka mara dufu

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Feb 7, 2022
2,775
6,592
image1170x530cropped.jpg

Zaidi ya wakimbizi, wahamiaji na waomba hifadhi 3,000 wamekufa au hawajulikani walipo kwa mwaka 2021 wakati wakijaribu kufika Ulaya kupitia Bahari ya Mediterranean na Bahari ya Atlantic.

Hayo yamebainishwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi (UNHCR) katika ripoti yake iliyotoka Aprili 29, 2022.

Ripoti hiyo inaonyesha idadi ya waliokufa ni kubwa katika miaka ya hivi karibuni.

Maelfu ya Waafrika wanatumia njia ndefu na hatari kufika Ulaya kila mwaka mara nyingi wakipitia Jangwa la Sahara na kuacha ufukwe wa Afrika Kaskazini wakiwa kwenye boti ndogo wakikimbia hali ngumu au kutafuta maisha bora.

Mwaka 2021, UNHCR iliripoti watu 3,077 walikufa au hawajulikani walipo hiyo ni karibu mara mbili ya idadi ya mwaka 2020.

UNHCR ilianza kutoa idadi mwaka 2019 na idadi ya watu wanaopoteza maisha inaongezeka kila mwaka.

Hadi sasa mwaka 2022 watu 553 wanaripotiwa kuwa wamekufa au hawajulikani walipo na kulingana na miaka iliyopita wengi wamekufa kwenye njia ya kati ya Mediterranean, data zinaonyesha.


Source: NEWS UN
 
Tunaambiwa kila siku na watawala wetu kuwa Bara letu limebarikiwa kila rasilimali na ni tajiri . Lakini cha kushangaza ni bara linaloongoza kwa kuhamwa duniani . why?.
Leo hii afrika ni bara linaloongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya wakimbizi . Why?.
Tizama nchi kama Ethiopia na Somalia ambazo wananchi wake wanazikimbia na kuzamia kila siku wanakamatwa kwenye malori wakizikimbia nchi zao . why?.
Cha kushangaza wengi wanakimbilia huko kwa wazungu ambako pia tunaaminishwa kuwa ni watu wabaya duniani . why?.
Hata blacks wenzetu waliofanikiwa kutoboa huko kwa wazungu tunawasikia wakilalamika kuwa wazungu ni watu wabaguzi sana . ila ukiwaambia kama mnabaguliwa basi rudini barani kwenu Africa . HAWATAKI KABISA . why ?.
🤔🤔🤔🏃🏃🏃🤔🤔🤔
 
... badala ya ...

UNHCR: Idadi ya wanaozamia Barani Ulaya na kufariki yaongezeka mara dufu

... would be more precise if read ...

UNHCR: Idadi ya wanaofariki wakizamia Barani Ulaya yaongezeka mara dufu

Muktadha sio kufariki baada ya kuzamia; bali kufariki wakizamia, kabla hawajaingia Ulaya.
 
Back
Top Bottom