Lo! Ngoja tuwasubiri Sultani wa kijani waje wajitetee kwa matusi. Lakini yote kwa yote hakuna tofauti kati ya Sulatani (Mwarabu) na Sultani (Mweusi) tena huyu wa sasa aweza kuwa mbaya zaidi maana tunafanana kwa rangi hivyo ajifanya kondoo kati yetu huku akitutafuna kama chui.
Sent using Jamii Forums mobile app
Katika kuhalalisha Machafuko na uvamizi ( Mapinduzi) kwa Zanzibar imekuwa ni kawaida kwa viongozi wa Serikali ya CCM na baadhi ya viongozi wa makanisa , kulaumu usultani na Sultani mwenyewe wa Zanzibar kwa dhuluma na shida walizofanyiwa wananchi hasa waafrika na huyu Sultani.
Hata Waziri Lukuvi alipokuwa kanisani alitoa matamshi ya kumpinga Sultani na uislamu.
Ningependa kwa faida ya vizazi vijavyo , Serikali ya CCM na hayo makanisa yanayojifanya kulaumu usultani , waorodheshe machafu yaliyofanywa na huyu Sultani Jemshid na kuyapeleka ICC , ili kumshitaki. Hapo tutaona ukweli uko wapi.
Sultani bado yuhai na anaishi Uingereza'
Isiwe ni njia ya kudanganyana na kuletewa propaganda zisizo na mashiko katika kuziba machafu yaliyofanywa na yanayofanywa na hizi tawala za CCM[/QUOTE)
Wanahalalisha uovu wao kwa kuwatahadharisha na kuuaminisha umma kuwa matatizo waliyoyasababisha wao hawahusiki.Mchawi ndiyo analia zaidi msibani ili asishakiwe.
Tudai Katiba ya wananchi kabla hatujachelewa zaidi.
Kila unachokiona Zanzibar kimefanywa na Sultani,Ubaya mkubwa ni kujifanya zanzibar ni nchi yake na huku yeye alikuwa mwarabu.
Sent using Jamii Forums mobile app
It is sundayKila unachokiona Zanzibar kimefanywa na Sultani,
Miti ya Sultani
Miembe,Minazi ilitoka India ikaletwa kupandwa Zanzibar kwa niaba ya Sultani
Nyumba za Sultani
Sultani alileta mafundi kutoka India ili waje waijenge Zamzibar
Usafiri bora kwa raia
Sultani alianzisha usafiri wa Reli kutoka Mji Mkongwe mpaka BuBuBu,
Umeme kwa kila mwananchi
Sultani aliweka Magenerator Makibwa,Zanzibar ikawa nchi ya mwanzo kuwa na Umeme katika Afrika Mashariki na Kati
Biashara huria
Zanzibar ilikuwa kama unavyoiona Dubai sasa hivi,hii iliwavutia wageni wengi kuja kuishi Zanzibar,wakiwemo Warabu,Wahindi Waajemi,Wazaramo,Wamakonde nk
Elimu Bora
Zanzibar ilikuwa inafata mfumo wa Elimu kutoka Uingereza,mitihani ilikiwa inatoka Oxford,moja katika chuo Bora duniani..
Ali Hasan Mwinyi,Aboud Jumbe Mwinyi hawa ni moja kati ya wageni waliofaidika na Elimu ya Zanzibar..
Kwa yote hayo aliyoyafanya Sultani kwanini nchi isiwe yake?Je baada ya Sultani kuondolewa,waliomuondoa waliweza kuendeleza aliyoanzisha..?
Je Zazibar chini ya Sultan CCM,Uchumi,Elimu,maendeleo ya kijamii nk yakoje??..
🤣🤣T
It is sunday
Green devils are still on bed
Hold on.
Unadhani Sultani wa Kijani wana muda huo?ICC ipo , kama Sultani mwarabu alifanya mabaya na wakamshitaki kwani bado yuko hai. Na wafunguwe kesi kama alivyoshitakiwa Charles Taylor na wengine, vinginevyo wasimseme kwa ubaya bure
Huenda kama Dubai au nyuma kidogo ya Dubai.
Mbali kutokea wapi? Oman Au Mtambwe?
Udakta wa Lumumba akili za kisamvu Nani anauthamini? Mwanasiasa mwenye akili hawezi kutoa maneno ya kitoto kama hayo, tena ETI Katibu mkuu wa Chama? Hata Mwenyekiti wa kitongoji kwa tiketi ya NLD hawezi kutoa uharo huo.'...Kuna Sultan Chama chake kina Mbunge mmoja Nchi nzima lakin katengeneza ramani kichwani kwake Kuwa Mwakani anakamata dola...'- Dkt Bashiru
Ma Sultan wamepanga kuungana kuondoa Madarakani Serikali ya Kizalendo ya Wananchi Na Wanyonge wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Wanazungumzia Utawala wa Sultan, na sio dini ya Kiislamu! Mbona unachanganya mambo?! Unataka kuniambia Watanzania wanaosema bora Mkoloni angeendelea kuwepo hawa nao wanazungumzia uwepo wa Ukristo?Mtu mweusi alisha laaniwa kabisa. Leo hii watu wanasimama na kutetea ukoloni. Kweli. Siku zote nasema hizi dini zimetupumbaza uwezo wa kufikiri. Kuna watu wanaamini mwarabu ndo Mungu wao. Shame on you.