Nikifa MkeWangu Asiolewe
JF-Expert Member
- Feb 26, 2024
- 6,739
- 13,833
Kama utahitaji kupinga hili basi wewe ni mbishi tu tangu kuzaliwa.
Ukabila nchi hii upo nje nje kabisa ni rahisi sana kukuta watu wa kabila moja wako zaidi 96% kuliko makabila mengine ikiwa tu Boss ni wa kabila husika.
Utafiti wangu mfupi nimebaini hili jambo lipo katika kila sehemu halafu sio Tanzania tu hata kwa wenzetu.
Ikitokea Boss akatimliwa basi Boss ataye kuja lazima atakuja na safu yake na ataanza kufukuza watu alio wakuta kwa style fulani fulani au kuwashusha vyeo pamoja na kuwapunguzia mishahala ili mradi tu waichukie kazi na kuacha alete wa kwakwe.
Hapa kuna kitengo cha wakina shomire nimekuja kugundua kati ya wafanyakzi 44 wa kitengo hicho ni 11 tu ndo sio kabila husika na la boss.
Ukienda kwa wakina shirima na shayo usiseme ukigeuka wakina mwamposa na mwandosya wao hata aibu hawana wamepangana kaka mtu na wadogo mtu kitengo kimoja(hapa nazungumzia ingekuwa shuleni basi mkuu wa shule,second na mtaaluma wote wawe wa tumbo moja).
Basi ukija kwangu wakina malendeja na masanja hali ni ile ile na makabila mengine ni vilevile.
Hali hii hadi makanisani hasa haya makanisa ya wajasiria mali njaa. Mambo ni yaleyale.
Vijana wengi wameumizwa sana.
Mwishoni mwa mwaka jana kuna Boss alifukuzwa kazi kwa kuendekeza U simba na yanga.Ilikuwa ukiwa simba basi usijionyeshe hadharani wewe na ushabiki wako na kilichofanya afukuzwe kazi aliwapa ruhusa mashabaki wote wa yanga kwenda kuangalia mpira akabaki na mashabiki wa simba wa siku hiyo hiki kitendo kiliwakera mashabiki wa simba hadi kwenda nae HR Ukiambatanisha na kero na tuhuma za nyuma za mambo hayahaya akafukuzwa kazi.Na ndiko tuendako nawaambieni ipo siku hili litakuwa kubwa pia.
Nadhani mmekwisha kuona kwenye msiba au sherehekuna madaftari ya simba na yanga na mbwembwe zingine za kijinga.(Nimeunganisha hili pia maana linafanana na ubaguzi wa kikabila tu)
Pia kuna hii tabia ya kuangalia usoni na kupeana kazi hii hadi kwenye teuzi huko majuu wizarani hii tabia ishaota matawi na kuzaa watoto hadi vitukuu. Imefikia wakati sasa hadi ualimu wanaajiri kwa kujuana huyu ni mtoto wa mjomba,dada,shangazi ama wa baba mdogo.
Muda sio mrefu tutawafikia kenya na kuwazidi mpo hapa. Sasa hivi hata kama CV yako imeshiba namna gani bila connection wewe kauze mayai mtaani tu hakuna atakaye jari hata kidogo na pengine Cv yako utaikuta jararani huko imetupiliwa mbali.
Hii hali ndo imetufikisha hapa kupata wataalumu wasio na weredi wowote kwani kazi wamepeana kwa kujuana au kwa rushwa.Wengi sana waapo mtaani wenye sifa kuliko waliomo maofisini.
Mfano mdogo tu nenda mahospital kuanzia mapokezi utakavyokuwa unajibiwa kana kwamba huyo anayekupatia huduma kalazamishwa kuisomea hiyo kazi ni very careless.,
Niliwahi kulazwa hospital fln kubwa (VIP) Asubuhi ile kuna mdada mfanya usafi anadeki kwenye chumba changu nami nimelala basi akiwa anaendelea na usafi Dr wangu akaingia na kuchafua pale.Baada ya Dr kutoka yule binti mfanya usafi alimfyonza na kisha kutoa maneno makali.
Ni kamwambia ujue hii kazi yako inategemea watu wachafue ndo ufanye usafi imagine kama pangekuwa pa safi siku zote hapa wewe ungeipata hii ajira? Hujui kwamba huyu Dr pengine anahudumia wagonjwa zaidi ya 100 na hapo ukute ana kipindi anaenda kufundisha?(Dr alikuwa ni profesa maana mara kadhaa alikuwa anakuja na wanafunzi wake kuniuliza maswali)
Nilijikaza kumwelewesha yule binti na mwisho ni kamwambia haya ndiyo madhara ya kupeana kazi kwa kujuana. Siku ukifanikiwa ukawa na kampuni yako usifanye makosa haya .
Tusipokuwa na umoja na kutanguliza maslahi ya Taifa kwanza ipo siku hali itakuwa mbaya sana na tutakuwa tumechelewa mno kuliko sasa.
Ukabila nchi hii upo nje nje kabisa ni rahisi sana kukuta watu wa kabila moja wako zaidi 96% kuliko makabila mengine ikiwa tu Boss ni wa kabila husika.
Utafiti wangu mfupi nimebaini hili jambo lipo katika kila sehemu halafu sio Tanzania tu hata kwa wenzetu.
Ikitokea Boss akatimliwa basi Boss ataye kuja lazima atakuja na safu yake na ataanza kufukuza watu alio wakuta kwa style fulani fulani au kuwashusha vyeo pamoja na kuwapunguzia mishahala ili mradi tu waichukie kazi na kuacha alete wa kwakwe.
Hapa kuna kitengo cha wakina shomire nimekuja kugundua kati ya wafanyakzi 44 wa kitengo hicho ni 11 tu ndo sio kabila husika na la boss.
Ukienda kwa wakina shirima na shayo usiseme ukigeuka wakina mwamposa na mwandosya wao hata aibu hawana wamepangana kaka mtu na wadogo mtu kitengo kimoja(hapa nazungumzia ingekuwa shuleni basi mkuu wa shule,second na mtaaluma wote wawe wa tumbo moja).
Basi ukija kwangu wakina malendeja na masanja hali ni ile ile na makabila mengine ni vilevile.
Hali hii hadi makanisani hasa haya makanisa ya wajasiria mali njaa. Mambo ni yaleyale.
Vijana wengi wameumizwa sana.
Mwishoni mwa mwaka jana kuna Boss alifukuzwa kazi kwa kuendekeza U simba na yanga.Ilikuwa ukiwa simba basi usijionyeshe hadharani wewe na ushabiki wako na kilichofanya afukuzwe kazi aliwapa ruhusa mashabaki wote wa yanga kwenda kuangalia mpira akabaki na mashabiki wa simba wa siku hiyo hiki kitendo kiliwakera mashabiki wa simba hadi kwenda nae HR Ukiambatanisha na kero na tuhuma za nyuma za mambo hayahaya akafukuzwa kazi.Na ndiko tuendako nawaambieni ipo siku hili litakuwa kubwa pia.
Nadhani mmekwisha kuona kwenye msiba au sherehekuna madaftari ya simba na yanga na mbwembwe zingine za kijinga.(Nimeunganisha hili pia maana linafanana na ubaguzi wa kikabila tu)
Pia kuna hii tabia ya kuangalia usoni na kupeana kazi hii hadi kwenye teuzi huko majuu wizarani hii tabia ishaota matawi na kuzaa watoto hadi vitukuu. Imefikia wakati sasa hadi ualimu wanaajiri kwa kujuana huyu ni mtoto wa mjomba,dada,shangazi ama wa baba mdogo.
Muda sio mrefu tutawafikia kenya na kuwazidi mpo hapa. Sasa hivi hata kama CV yako imeshiba namna gani bila connection wewe kauze mayai mtaani tu hakuna atakaye jari hata kidogo na pengine Cv yako utaikuta jararani huko imetupiliwa mbali.
Hii hali ndo imetufikisha hapa kupata wataalumu wasio na weredi wowote kwani kazi wamepeana kwa kujuana au kwa rushwa.Wengi sana waapo mtaani wenye sifa kuliko waliomo maofisini.
Mfano mdogo tu nenda mahospital kuanzia mapokezi utakavyokuwa unajibiwa kana kwamba huyo anayekupatia huduma kalazamishwa kuisomea hiyo kazi ni very careless.,
Niliwahi kulazwa hospital fln kubwa (VIP) Asubuhi ile kuna mdada mfanya usafi anadeki kwenye chumba changu nami nimelala basi akiwa anaendelea na usafi Dr wangu akaingia na kuchafua pale.Baada ya Dr kutoka yule binti mfanya usafi alimfyonza na kisha kutoa maneno makali.
Ni kamwambia ujue hii kazi yako inategemea watu wachafue ndo ufanye usafi imagine kama pangekuwa pa safi siku zote hapa wewe ungeipata hii ajira? Hujui kwamba huyu Dr pengine anahudumia wagonjwa zaidi ya 100 na hapo ukute ana kipindi anaenda kufundisha?(Dr alikuwa ni profesa maana mara kadhaa alikuwa anakuja na wanafunzi wake kuniuliza maswali)
Nilijikaza kumwelewesha yule binti na mwisho ni kamwambia haya ndiyo madhara ya kupeana kazi kwa kujuana. Siku ukifanikiwa ukawa na kampuni yako usifanye makosa haya .
Tusipokuwa na umoja na kutanguliza maslahi ya Taifa kwanza ipo siku hali itakuwa mbaya sana na tutakuwa tumechelewa mno kuliko sasa.