Ugonjwa wa bipolar unanisumbua, naombeni ushauri

Mdau tu

Member
Jun 8, 2024
13
12
Jamani m nmekua na ugonjwa Wa bipolar nimekua nikteseka nao naombeni ushauri kwa ambae amekuwa nao au mwenye kujua kuhusu uo ugonjwa
 
Ndugu zangu niliomba msaada juu ya ugonjwa Wa bipolar sikupata msaada sahihi naomba mwenye uelewa anisaidie kuhusu matibabu yake au namna ya kupata msaada kuutibu
 
Hospital ni sehemu sahihi,,,, ili kupata matibabu sahihi….
😇😇😇😇
 
Huu ugonjwa hauna tiba, japokuwa unaweza kutumia mood stabilizers, na dawa zingine, huu ugonjwa ni wakif-a-la sana nishawah kuwa na mwanamke ana mood swings na wenge la ajabu sijawah kuona, aisee pole sana mkuu you need therapy...
 
Jamani m nmekua na ugonjwa Wa bipolar nimekua nikteseka nao naombeni ushauri kwa ambae amekuwa nao au mwenye kujua kuhusu uo ugonjwa
136330845_207692251005964_3458388643877332178_n.jpg

SAIKOLOJIA: FAHAMU UGONJWA WA BIPOLAR DISORDER

Leo nimeleta somo kuhusu ugonjwa wa saikolojia unaofahamika kama Bipolar Disorder. Pengine wengi wetu neno ili au msamiati huu ni mpya kabisa kuusikia au wengi waliousikia lakini hawakuweza ingia kujifunza kuelewa Bipolar ndio ukoje.

Moja ya watu maarufu ambao wameripotiwa kuugua ugonjwa huu ni kama vile Chris Browm na na siku hizi za karibuni ndugu Kanye West.

Jambo ambalo naweza kukuhakikishia tu ndugu msomaji huu ugonjwa hupo sana kwa asilimia kubwa katika jamii yetu. Ingawa wengi watanzania kutokana na uamsho mdogo wa taaluma ya saikolojia hatujafahamu. Na umekuwa na madhara mengi sana kwa jamii yetu na kichochezi cha kuamsha uadui na majeraha ya nafsi baina ya familia, koo na hata nchi.

Siku zetu katika maisha haya, utendaji kazi wetu kuwa unaathiriwa kikubwa sana na hisia zetu ziwe hisia zakufurahi au hisia za huzuni, Hivyo kuwa na mood hasi basi utendaji na mienendo yetu nao unakuwa sio mzuri pia.

Ndio maana kuna msemo unasema usipende kufanya maamuzi makubwa ukiwa na furaha sana au uamuzi ukiwa na hasira.

TAFSIRI
Bipolar Disorder ndio ugonjwa gani huu?
Ni ugonjwa wa kiakili (kisaikolojia) ambapo huambatana na sifa ya mabadiliko ya makubwa ya kihisia yaani (mood) kusipokuwa kwa kawaida,
hasa kugusa utendaji wa mtu bidii na shughuli zake wakati mwingine unasababisha mtu kuwehuka (maniac) na kupatwa na Msongo au sonona (Depression).
Kutokana na namna ugonjwa huu unavyojitokeza inakuwa vigumu sana kama mwanasaikolojia au madaktari kumgundua mgonjwa wa bipolar sababu kuna wakati anatokea kuwa na dalili zote za depression na wakati mwingine kama kuwehuka au kuchizika kitabia iwe gadhabu, furaha au matamanio ya kingono.
Bipolar pia unaweza kujitokeza kwa mtu wa rika au umri wowote au jinsia yoyote pia.
Zipo namna ambazo Bipolar Disorder ujitokeza
Namna ya kwanza mtu anaweuka hadi wiki kihisia hadi wiki na kupelekea kulazwa kabisa hospitali.
Namna nyingine kuweuka na kupelekea kukosa mood kabisa.
Namna nyingine vyote kwa pamoja vina ambatana.

DALILI ZA KUATHIRIWA NA BIPOLAR DIS ORDER

Athari kitabia na mahusiano na wengine

Furaha feki ya kifani (Euphoric)
Ushawahi kukutana na mtu ambae sio rahisi kumuelewa mood yake. Yaani kuna siku mnakuwa vizuri tu mnaongea na kucheka na kufurahi (Euphoric) na kupanga mipango mingi tu yaani uchangamfu wa hali ya juu kama hautamuelewa au ukimuelewa utashangazwa jinsi halivyokuwa na furaha kweli.
Kuwehuka kiakili au kupatwa na sonona (Maniac and Depression)
Halafu muda huo huo au baadae mood imebadilika anakuwa na jazba au gadhabu na (si hasira) ya hata kudhuru au kumuumiza mwingine au kuwa/kupatwa na sonona au msongo mzito.
Mara nyingi kuwa haeleweki haeleweki katika maamuzi kutokana na mabadiliko ya mood mara kwa mara hivyo ni rahisi kuathiri mahusiano na mwenza au jamii ya watu wanaomzunguka.
*Kuwehuka kwa kuwa na furaha ya kifani (euphoric) kuchizika kuwa na gadhabu zisizoeleweka(maniac)wakati mwingine zikiambatana na ukatili na maamuzi mabaya au kupatwa na sonona (Msongo mzito).
Kuwa na hali ya juu ya kihisia za tendo la ndoa (Hypersexual)
Pia ugonjwa huu una tabia kuathiri utendaji wa mapenzi au hisia za mapenzi
Mara nyingi huathiri utendaji kwa hamu au ashiki kuzidi (hypersexual)
Mambo haya hujitokeza katika utendaji wa hisia za kimapenzi (tendo la ndoa)
Kutoridhika kabisa na tendo la ndoa kwahiyo kama mwenza wake anakuwa na changamoto sana kumridhisha.
Pia kama kujichua wakati mwingine kuzidi sana kwa tabia hiyo husababishwa na tatizo ili kama lipo katika utendaji kazi wa ubongo wako.
Mara chache pia huathiri matatizo ya nguvu za kiume
Kama ni watoto au vijana wadogo kupenda onesha ishara za kingono kwa watu wazima (kama tabia hizi hazikurithiwa au kujifunza kwa rafiki anao) unajikuta kama mzazi unajiuliza huyu binti yangu au kijana wangu tabia hizi nyingi kazipata wapi? Au kajifunzia wapi?

(Niombe radhi kwa tatizo lolote na kiuandishi na pia kutokana na misamiati mingine ya kitaaluma ambayo haijaweza kupata tafsiri nzuri inapotafsiriwa katika lugha ya Kiswahili ).
 
Sasa kwanini unajipachika vyeo ambavyo hata huna kabisa Vyeo navyo ( Dr Matola PhD) una cheo cha Dr una cheo cha PHD vyote hivyo ni vyeo feki badilisha hivyo vyeo ujiite jina lako tu Matola kuliko kujipachika vyeo feki Samahani kama nimekukwaza.
Wala hujanikwaza kwa sababu hujui hata umeandika nini.

Hakuna PHD bali kuna PhD, inashangaza mtu wa magumashi ya miti shamba unajiita Dr.
 
Wala hujanikwaza kwa sababu hujui hata umeandika nini.

Hakuna PHD bali kuna PhD, inashangaza mtu wa magumashi ya miti shamba unajiita Dr.
Nipe Maana ya neno Dr. na PHD? Mimi ni Doctor wa dawa za Mitishamba wewe ni nani?unayejipachika mavyeo feki mengi namna hiyo? huoni hata aibu kujipachika vyeo wakati hata huna hivyo vyeo!!!!!!!!!!!!!!!
 
Sasa kwanini unajipachika vyeo ambavyo hata huna kabisa Vyeo navyo ( Dr Matola PhD) una cheo cha Dr una cheo cha PHD vyote hivyo ni vyeo feki badilisha hivyo vyeo ujiite jina lako tu Matola kuliko kujipachika vyeo feki Samahani kama nimekukwaza.
Dr Matola PhD ina maanisha ni udaktari wa falsafa,sio udaktari wa binadamu,na ndo maana mwishoni kaandika phd(doctor of philosophy) huenda ndo alivyo

Ila chakushangaza sasa kwa huyu Dr Matola PhD uwezo wake uchambuzi na ung'amuzi wa mambo unaweza sema ni mtu wa darasa la tatu C,hana staha na wala cheo hich hakimlinganii

Nadhani huyu atakuwa ni mhuni fulani kaamua kujiita Dr.
 
Dr Matola PhD ina maanisha ni udaktari wa falsafa,sio udaktari wa binadamu,na ndo maana mwishoni kaandika phd(doctor of philosophy) huenda ndo alivyo

Ila chakushangaza sasa kwa huyu Dr Matola PhD uwezo wake uchambuzi na ung'amuzi wa mambo unaweza sema ni mtu wa darasa la tatu C,hana staha na wala cheo hich hakimlinganii

Nadhani huyu atakuwa ni mhuni fulani kaamua kujiita Dr.
Umezungumza Point jinsi anavyo jiweka na vyeo alivyojipachika havilingani kabisa. Kwa sababu majibu yake ni ya kihunihuni labda Tumuite Doctor wa falsafa za kihunihuni ndio cheo kinacho mfaa angelikuwa ni mtu mstaarabu angenijibu kwa ustaarabu. Kama nilivyomueleza mimi hata mimi nimemujibu kwa ustaarabu lakini yeye amenijibu kihunihuni. Hafai kuwa Daktari wa Falsafa.Huyu ni daktari wa kihunihuni ndio cheo chake.
 
Dr Matola PhD ina maanisha ni udaktari wa falsafa,sio udaktari wa binadamu,na ndo maana mwishoni kaandika phd(doctor of philosophy) huenda ndo alivyo

Ila chakushangaza sasa kwa huyu Dr Matola PhD uwezo wake uchambuzi na ung'amuzi wa mambo unaweza sema ni mtu wa darasa la tatu C,hana staha na wala cheo hich hakimlinganii

Nadhani huyu atakuwa ni mhuni fulani kaamua kujiita Dr.
Labda ndo babu tale huyo......
 
View attachment 3019131
SAIKOLOJIA: FAHAMU UGONJWA WA BIPOLAR DISORDER

Leo nimeleta somo kuhusu ugonjwa wa saikolojia unaofahamika kama Bipolar Disorder. Pengine wengi wetu neno ili au msamiati huu ni mpya kabisa kuusikia au wengi waliousikia lakini hawakuweza ingia kujifunza kuelewa Bipolar ndio ukoje.

Moja ya watu maarufu ambao wameripotiwa kuugua ugonjwa huu ni kama vile Chris Browm na na siku hizi za karibuni ndugu Kanye West.

Jambo ambalo naweza kukuhakikishia tu ndugu msomaji huu ugonjwa hupo sana kwa asilimia kubwa katika jamii yetu. Ingawa wengi watanzania kutokana na uamsho mdogo wa taaluma ya saikolojia hatujafahamu. Na umekuwa na madhara mengi sana kwa jamii yetu na kichochezi cha kuamsha uadui na majeraha ya nafsi baina ya familia, koo na hata nchi.

Siku zetu katika maisha haya, utendaji kazi wetu kuwa unaathiriwa kikubwa sana na hisia zetu ziwe hisia zakufurahi au hisia za huzuni, Hivyo kuwa na mood hasi basi utendaji na mienendo yetu nao unakuwa sio mzuri pia.

Ndio maana kuna msemo unasema usipende kufanya maamuzi makubwa ukiwa na furaha sana au uamuzi ukiwa na hasira.

TAFSIRI
Bipolar Disorder ndio ugonjwa gani huu?
Ni ugonjwa wa kiakili (kisaikolojia) ambapo huambatana na sifa ya mabadiliko ya makubwa ya kihisia yaani (mood) kusipokuwa kwa kawaida,
hasa kugusa utendaji wa mtu bidii na shughuli zake wakati mwingine unasababisha mtu kuwehuka (maniac) na kupatwa na Msongo au sonona (Depression).
Kutokana na namna ugonjwa huu unavyojitokeza inakuwa vigumu sana kama mwanasaikolojia au madaktari kumgundua mgonjwa wa bipolar sababu kuna wakati anatokea kuwa na dalili zote za depression na wakati mwingine kama kuwehuka au kuchizika kitabia iwe gadhabu, furaha au matamanio ya kingono.
Bipolar pia unaweza kujitokeza kwa mtu wa rika au umri wowote au jinsia yoyote pia.
Zipo namna ambazo Bipolar Disorder ujitokeza
Namna ya kwanza mtu anaweuka hadi wiki kihisia hadi wiki na kupelekea kulazwa kabisa hospitali.
Namna nyingine kuweuka na kupelekea kukosa mood kabisa.
Namna nyingine vyote kwa pamoja vina ambatana.

DALILI ZA KUATHIRIWA NA BIPOLAR DIS ORDER

Athari kitabia na mahusiano na wengine

Furaha feki ya kifani (Euphoric)
Ushawahi kukutana na mtu ambae sio rahisi kumuelewa mood yake. Yaani kuna siku mnakuwa vizuri tu mnaongea na kucheka na kufurahi (Euphoric) na kupanga mipango mingi tu yaani uchangamfu wa hali ya juu kama hautamuelewa au ukimuelewa utashangazwa jinsi halivyokuwa na furaha kweli.
Kuwehuka kiakili au kupatwa na sonona (Maniac and Depression)
Halafu muda huo huo au baadae mood imebadilika anakuwa na jazba au gadhabu na (si hasira) ya hata kudhuru au kumuumiza mwingine au kuwa/kupatwa na sonona au msongo mzito.
Mara nyingi kuwa haeleweki haeleweki katika maamuzi kutokana na mabadiliko ya mood mara kwa mara hivyo ni rahisi kuathiri mahusiano na mwenza au jamii ya watu wanaomzunguka.
*Kuwehuka kwa kuwa na furaha ya kifani (euphoric) kuchizika kuwa na gadhabu zisizoeleweka(maniac)wakati mwingine zikiambatana na ukatili na maamuzi mabaya au kupatwa na sonona (Msongo mzito).
Kuwa na hali ya juu ya kihisia za tendo la ndoa (Hypersexual)
Pia ugonjwa huu una tabia kuathiri utendaji wa mapenzi au hisia za mapenzi
Mara nyingi huathiri utendaji kwa hamu au ashiki kuzidi (hypersexual)
Mambo haya hujitokeza katika utendaji wa hisia za kimapenzi (tendo la ndoa)
Kutoridhika kabisa na tendo la ndoa kwahiyo kama mwenza wake anakuwa na changamoto sana kumridhisha.
Pia kama kujichua wakati mwingine kuzidi sana kwa tabia hiyo husababishwa na tatizo ili kama lipo katika utendaji kazi wa ubongo wako.
Mara chache pia huathiri matatizo ya nguvu za kiume
Kama ni watoto au vijana wadogo kupenda onesha ishara za kingono kwa watu wazima (kama tabia hizi hazikurithiwa au kujifunza kwa rafiki anao) unajikuta kama mzazi unajiuliza huyu binti yangu au kijana wangu tabia hizi nyingi kazipata wapi? Au kajifunzia wapi?

(Niombe radhi kwa tatizo lolote na kiuandishi na pia kutokana na misamiati mingine ya kitaaluma ambayo haijaweza kupata tafsiri nzuri inapotafsiriwa katika lugha ya Kiswahili ).
Shukurani mkuu.
 
Back
Top Bottom