Japokuwa hujaeleza dalili za ugonjwa lakini nahisi ni African Swine Fever.
Ugojwa huu hauna tiba wala chanjo,unaua nguruwe wengi kwa wakati mmoja.
Ili kuokoa nguruwe wengine fanya yafuatayo:
Tafuta dawa iitwayo V-RID kwenye maduka ya dawa.
Ukipata changanya mls 4 au 5 za dawa kwa maji ya lita moja.
Wanyweshe nguruwe mls 2 za mchanganyiko huo kwa kila nguruwe (tumia syringe kuwanywesha)
Dawa iliyobaki wanyunyizie kwa pampu mwilini kisha nyunyizia kwenye banda wanalokaa.
Ukifanya hivyo unaweza kuwaokoa.