Uchina Wameunda Kamera Yenye Nguvu Zaidi Duniani, Ikinasa Taswira kutoka Anga za Juu

N'yadikwa

JF-Expert Member
Aug 10, 2014
7,405
10,878
Unaweza kusema headline iwe "Ni Uchina Tena"

Kamera za Ufukunyuzi Zenye Nguvu Zaidi Duniani zimetengenezwa na Wanasayansi wa China nchi hiyo ikiweka Viwango Vipya vya Upelelezi na Ufuatiliaji wa Kimataifa visivyomithirika.

Kamera hizi mpya zina uwezo wa kushinda viwango vya kimataifa vya kamera za ufuatiliaji na zinaweza kuchukua picha za hali ya juu kwa umbali wa kilomita nyingi hata katika hali ya hewa mbaya kutokea anga za juu yaani space.

Kamera hizi kwa mujibu wa Yahoo News hutumia teknolojia ya kisasa inayojulikana kama "single-photon detection" ambayo inaruhusu kuchukua picha za hali ya juu hata katika mazingira yenye mwanga mdogo. Hii inafanya kamera hizi kuwa bora zaidi kuliko zile zilizotumika hapo awali kutokea kwenye Satellite za Mawasiliano na za kipelelezi za hapo kabla.

Kwa sababu ya uwezo wake mkubwa kamera hizi zinaweza kutumika kwa ajili ya ufuatiliaji wa kijeshi, usalama wa mipaka na hata katika utafiti wa kiikolojia. Wataalamu wanasema kuwa teknolojia hii inaweza kuwa na matumizi mengi zaidi katika siku za usoni.

Uwezo wa Kamera hizi ni kunasa picha kwa saizi ya Milimita na zinaweza kuzoom na kuleta serial namba za Satellite nyingine anga za juu au ardhini kuzoom kwa karibu na kwa uangavu wa juu vitu vidogo sana hali inayowezesha na kuboresha zaidi upelelezi wao...
 

Attachments

  • images (11) (10).jpeg
    images (11) (10).jpeg
    12.3 KB · Views: 2
Unaweza kusema headline iwe "Ni Uchina Tena"

Kamera za Ufukunyuzi Zenye Nguvu Zaidi Duniani zimetengenezwa na Wanasayansi wa China nchi hiyo ikiweka Viwango Vipya vya Upelelezi na Ufuatiliaji wa Kimataifa visivyomithirika.

Kamera hizi mpya zina uwezo wa kushinda viwango vya kimataifa vya kamera za ufuatiliaji na zinaweza kuchukua picha za hali ya juu kwa umbali wa kilomita nyingi hata katika hali ya hewa mbaya kutokea anga za juu yaani space.

Kamera hizi kwa mujibu wa Yahoo News hutumia teknolojia ya kisasa inayojulikana kama "single-photon detection" ambayo inaruhusu kuchukua picha za hali ya juu hata katika mazingira yenye mwanga mdogo. Hii inafanya kamera hizi kuwa bora zaidi kuliko zile zilizotumika hapo awali kutokea kwenye Satellite za Mawasiliano na za kipelelezi za hapo kabla.

Kwa sababu ya uwezo wake mkubwa kamera hizi zinaweza kutumika kwa ajili ya ufuatiliaji wa kijeshi, usalama wa mipaka na hata katika utafiti wa kiikolojia. Wataalamu wanasema kuwa teknolojia hii inaweza kuwa na matumizi mengi zaidi katika siku za usoni.

Uwezo wa Kamera hizi ni kunasa picha kwa saizi ya Milimita na zinaweza kuzoom na kuleta serial namba za Satellite nyingine anga za juu au ardhini kuzoom kwa karibu na kwa uangavu wa juu vitu vidogo sana hali inayowezesha na kuboresha zaidi upelelezi wao...

KUSOMA ZAIDI, Gonga hapo chini:View attachment 3247007
World's Most Powerful Spy Camera...
Wakati Wachina wakipiga hatua kubwa zaidi katika kufanya Utafiti, Ubunifu, Uvumbuzi na Ugunduzi Mpya katika maendeleo ya Sayansi na Teknolojia, sisi waTanzania kazi yetu imebaki katika Kusifu na Kuabudu Watawala.

Yaani hovyo kabisa!
 
wachina genius sana yani wanaakili sana

nmeona engineers wa kichina walivyonyoosha hii barabara ya tazara airport gongomboto ni hatari .
Wanatumia rula maalum ambayo inafanya kazi usiku ikitumia vitochi maalum vinavyotoa mionzi mikali ndo maana unaona road limenyooka fyaaa
 
Ooh, ok.
Nikadhani wanatuletea tecno ambazo ukipiga angani unaweza kuzoom visivyoonekana huko space.
 
Wakati Wachina wakipiga hatua kubwa zaidi katika kufanya Utafiti, Ubunifu, Uvumbuzi na Ugunduzi Mpya katika maendeleo ya Sayansi na Teknolojia, sisi waTanzania kazi yetu imebaki katika Kusifu na Kuabudu Watawala.

Yaani hovyo kabisa!
Weeeee
Ukibuni kigar tu figisu kibao
 
wachina genius sana yani wanaakili sana

nmeona engineers wa kichina walivyonyoosha hii barabara ya tazara airport gongomboto ni hatari .
Kipimo cha ubora ulinganishe daraja la Tanzanite(wakorea)na Mwalimu Nyerere(wachina),hiyo ya bongo la mboto unalinganisha na wakandarasi wetu au?
 
Unaweza kusema headline iwe "Ni Uchina Tena"

Kamera za Ufukunyuzi Zenye Nguvu Zaidi Duniani zimetengenezwa na Wanasayansi wa China nchi hiyo ikiweka Viwango Vipya vya Upelelezi na Ufuatiliaji wa Kimataifa visivyomithirika.

Kamera hizi mpya zina uwezo wa kushinda viwango vya kimataifa vya kamera za ufuatiliaji na zinaweza kuchukua picha za hali ya juu kwa umbali wa kilomita nyingi hata katika hali ya hewa mbaya kutokea anga za juu yaani space.

Kamera hizi kwa mujibu wa Yahoo News hutumia teknolojia ya kisasa inayojulikana kama "single-photon detection" ambayo inaruhusu kuchukua picha za hali ya juu hata katika mazingira yenye mwanga mdogo. Hii inafanya kamera hizi kuwa bora zaidi kuliko zile zilizotumika hapo awali kutokea kwenye Satellite za Mawasiliano na za kipelelezi za hapo kabla.

Kwa sababu ya uwezo wake mkubwa kamera hizi zinaweza kutumika kwa ajili ya ufuatiliaji wa kijeshi, usalama wa mipaka na hata katika utafiti wa kiikolojia. Wataalamu wanasema kuwa teknolojia hii inaweza kuwa na matumizi mengi zaidi katika siku za usoni.

Uwezo wa Kamera hizi ni kunasa picha kwa saizi ya Milimita na zinaweza kuzoom na kuleta serial namba za Satellite nyingine anga za juu au ardhini kuzoom kwa karibu na kwa uangavu wa juu vitu vidogo sana hali inayowezesha na kuboresha zaidi upelelezi wao...

KUSOMA ZAIDI, Gonga hapo chini:View attachment 3247007
World's Most Powerful Spy Camera...

= visivyomithilika.

Hivi hizi R na L tatizo siyo midomoni tu, hata vidoleni?
 
= visivyomithilika.

Hivi hizi R na L tatizo siyo midomoni tu, hata vidoleni?
Mama za siku nyingi. Kumbe upo? Kimya sana. Imetokea kwa bahati mbaya tu, mi sikusomea ujinga, tazama maandiko yangu humu utagundua ni balozi mzuri wa Kiswahili Sanifu. Sorry kwa kosa hilo dogo la kiuandishi.
 
Back
Top Bottom