Tiba Asili wamjibu Dr Kigwangala

Cardinal06

JF-Expert Member
Jan 7, 2015
963
326
SIKU chache baada ya Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee, Dkt. Hamis Kigwangalla, kutoa tamko la kuwataka watoa huduma za tiba asili na mbadala, tamko hilo limepingwa na Jukwaa la Tiba Asilia na Mbadala Tanzania.
Katika tamko lake, Dkt. Kigwangalla alipiga marufuku matangazo yote yanayotolewa na Matabibu kwa ajili ya elimu kwa umma katika vyombo vya habari, mitandao ya kijamii, kuwasilisha nyaraka zote muhimu kuhusu huduma wanazotoa ndani ya siku 14.Pia Dkt. Kigwangalla aliwataka
Matabibu hao kuwasilisha nyaraka zote za kumiliki mashine zinazotumika kufanya uchunguzi wa tiba asili, mbadala na kulitaka Baraza la Tiba Asili na Mbadala, kupitia nyaraka zote ambazo zinahusu usajili wa watoa huduma, vituo na maduka ya dawa asili ndani ya siku 14 kuanzia Desemba 24 mwaka huu.
Dkt. Kigwangala alitoa tamko hilo siku chache baada ya kufanya ziara ya kushtukiza kwenye Kituo cha Tiba Asili na Mbadala cha Foreplan Clinic, kilichopo Ilala, Bungoni, kinachomilikiwa na Tabibu Juma Mwaka.
Baada ya kufanya ukaguzi kituoni hapo, alitoa siku saba kwa Baraza hilo kuchunguza huduma zinazotolewa katika kituo hicho ambacho Tabibu wake amejipatia umaarufu mkubwa kama mmoja wa Matabibu wa tiba mbadala kutokana na vipindi vyake vinavyoelezea tiba ya maradhi mbalimbali ya binadamu kwa kutumia tiba asilia.
Kutokana na tamko hilo, jana Matabibu wa tiba hizo kutoka mikoa mbalimbali nchini, walikutana Dar es Salaam na kulipinga kwa hoja ya viongozi wa Jukwaa la Tiba Asili Tanzania kutoshirikishwa.
Jukwaa hilo limewataka baadhi ya viongozi wa Serikali ya Awamu ya Tano, kutoichukulia dhana ya 'Hapa Kazi Tu' kufanya maamuzi yasiyofaa mbele ya jamii badala yake waangalie namna ya kutoa mwongozo kwa Matabibu kuhusu sheria ya utoaji elimu kwa jamii kupitia vyombo vya habari.
Nao wanachama wa Jukwaa hilo, waliitaka Serikali kuitambua tiba asili na mbadala kwani Watanzania wengi wamenufaika na dawa hizo.
Walisema yapo magonjwa mengi yanayowasumbua Watanzania ambao kwa muda mrefu wametumia tiba za kisasa hospitalini bila kupona lakini walipotumia tiba asili na mbadala, zimewasaidia na kupona.
Akitoa tamko la Jukwaa hilo, Katibu Mkuu wa Shirika la Dawa Asilia na Ulinzi wa Mazingira (TRAMEPRO), ambaye pia ni Mwenyekiti wa Jukwaa hilo, Bonaventura Mwalongo, alisema tamko la Wizara hiyo limelenga kudhoofisha nia njema ya utoaji huduma za tiba asili.
Aliwataka Matabibu wote wa tiba asili na mbadala, kuwa wavumilivu katika kipindi hiki akiwataka watoe ushirikiano wa hali na mali kwa viongozi wa taasisi zinazosimamia masuala ya tiba asili ngazi ya Taifa ili kupata mwafaka baina yao na Serikali.
"Kusiwe na matamko mengine zaidi ya hili, tamko la mtu mmoja mmoja linaweza kudhoofisha umoja tulionao hasa kwa kuzingatia kuwa, asilimia 60 ya Watanzania wanatumia tiba asili kupata tiba," alisema Mwalongo.
 
Waboreshe hospital Huduma ziwe bora zaidi wananchi hawataangalia tiba mbadala tena,
 
Chamsingi si kutoleana matamko au kutunishiana misuli. Wawasilishe hizo nyaraka na vifaa tiba vyao kama walivyotakiwa. Pili kuhusu swala la matangazo Sharia inasemaje? Watafsiri sheria inavyowataka na si kulalama tu kwa go.
 
IPO haja ya kutengeneza muswada maalum wa kupelekwa bungeni Juu ya taratibu na mipaka ya scientific doctors na traditions healers.
n.b
***
Ni vifaa gani ataruhusiwa kuwa navyo huyu traditions healers,
Ataruhusiwa kutibu mtu tu ,Mara baada ya tatizo husika kuthibitishwa na hospitali za serekali / kwa MTU huyu ni ruksa baadha ya tatizo kuonekana ni complicated.
 
Last edited:
Umenena mkuu!
 
Mtahisoma namba mwaka huu, hapa kazi tu. Mulitegemea namba hasome nani
 
Hizi tiba asili ni aina nyingine ya utaperi kuwataperi watu wenye ufinyu wa kufikiri..natamani natamani wangepigwa marufuku hata kuwepo nchini hawana tofauti na wapiga lamuli hawa..
 
Tatizo likiwa complicated liende kwa tiba asili???
 
Baba ndevu mtoto ndevu na mama pia ana ndevu.sasa kila mtu ndani ya familia ana ndevu.kibezi kwa kwenda mbele.
 
Baba ndevu mtoto ndevu na mama pia ana ndevu.sasa kila mtu ndani ya familia ana ndevu.kibezi kwa kwenda mbele.

Na hapo ndipo mara nyingi tunapopata mkwamo, wenye mamlaka wakigwaya katika hili dharau zitakita mizizi.
 
Cha msingi wakubaliane kutoa hizo Huduma lakin wawe na mipaka sio magonjwa yote wanayaweza hapana watibu wanayoweza ukuta mtu anaongea kuwa anatibu magonjwa 50 na kuendeea kitu ambacho akiwezekan we kuwa specialize kwenye magonjwa yote hayo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…