Teknolojia inavyoharibu saikolojia na mfumo mzima wa akili za watoto

Gota8s

JF-Expert Member
Aug 4, 2014
201
189
Habari za wakati huu wanajamvi:

Mimi sijambo kabisa naendelea vizuri, na naamini kila mmoja wenu anaendelea vema.. lakini ikiwa kjna changamoto yoyote kiafya nawaombea nafuu ya mapema.

Pasipo kupoteza muda mwingi nadhani niende mona kwa mona kwenye mada.

Hapa nitazungumzia zaidi jinsi gani masuala ya Teknolojia yanavyoathiri moja kwa moja ufikiri wa watoto na matokeo yake mpaka wanapokuwa watu wazima.

Binafsi sijakulia kwenye mazingira yaliyoendelea. Namaanisha kuwa masuala ya TV na Games za watoto hayakuwepo hata kidogo. Nilichokifanya ni ile michezo ya kawaida ya watoto inayochezwa vijijini. Kuwinda, kucheza mpira, kombolela na mingine kama hiyo.

Ila katika ukubwa wangu nimepata nafasi ya kuishi na watoto ambao ndio wanapitia sasa nyakati za kuishi maisha ya kiteknolojia.

Watoto wanaojua ratiba za vipindi mbalimbali vya televisheni kwenye king'amuzi chao, watoto wanaojua kufuatilia tamthiliya na katuni mbali mbali, watoto wajuzi wa kutumia vyombo mbalimbali kama simu, tablet, laptop n.k.

Watoto wa aina hii ndio ninaowazungumzia.

Waandaaji wa Games na Movie za watoto sijawahi kujua lengo lao ni nini. Kuna namna huwa nafikiri huenda kuna mtego wanaoutega.

Fiction inayotumika inakuwa imepita upeo na fantansy huwa zinawekwa hata pasipokuwa na ulazima.

Kwa mfano badala ya movie na games hizo kuwasaidia watoto kujifunza kutatua matatizo wanayokumbana nayo, utakuta heros wa movie hizo au games wanapata changamoto halafu purposeless wanapata magics na wana-overcome hayo matatizo.

Nimekuwa nikifuatilia sana katuni mbalimbali na nimegundua kuwa watoto huwa wanaishi ulimwengu tofauti na tunaoishi.

Watoto wanapewa imani kuwa siku zote watakutana na bahati kila watakapopata shida. Kwa mfano kuna katuni inaitwa Rango, hii inanisikitisha sana endapo baadhi ya watoto watachukua mafundisho yake na kuyajengea imani.

Despicable me, Frozen, cindelela, Grinch, home, ben10, son of Bigfoot, Rio n.k.

Pia zile movie za Spiderman huwajengea taswira watoto kushindwa kutatua changamoto zao wenyewe kwa kuamini mambo yale.

Kuna dogo wa miaka kama tisa hivi huwa muda mwingi nipo nae, akiagizwa kufuata kitu dukani ataanza kujisemea mwenyewe kuwa angekuwa Sonic angetumia sekunde tu akawa amerejea, au hata angekuwa spiderman angedanda kwenye majumba halafu arushe nyuzi zake achukue akitakacho kisha arudi haraka.

Pia waandaaji wa movie na game hizi wanawajaza ujinga watoto kuwa Bunduki huweza kutatua shida zao, yaani hata kitendo cha kuua mtu kwa bunduki watoto wanakichukulia kama jambo la burudani.

Watoto wanashindwa kuelewa kiundani thamani ya utu kwa kuwa ni suala la kawaida kumuona ninja kwenye movie akinyata na kuua watu na wakati mwingine kuwafyeka kwa mapanga. Baada ya hapo ninja huondoka kuendelea na mission.

Watoto hawawezi kujua inakuwaje mtu akifa au akikutwa popote amekufa process zinakuwaje, taratibu za kisheria na za kipolisi, uchungu wanaokuwa nao ndugu waliofiwa, uharamu wa tukio lenyewe la kuua.

Watoto wanawajua vema jinsi gani wa Vietnam wanavyokuwa wengi kwenye vita kisha wakipigwa risasi hata moja wanakufa nane watoto wameshamezeshwa hizi propaganda za wamarekani juu ya ugaidi wa waarabu na dini yao ya uislam.

Watoto wameshaaminishwa na movie kama za Koi mil gaya (ya kihindi) kuwa hata asipofanya juhudi za kitaaluma kujiweka sawa.. atatokewa na miujiza (jadu) na atamgusa kichwa kisha atakuwa genious na strong.

Mimi huwa nafikiri kuwa kizazi hiki cha watoto walio under 12 kwa sasa, na uwepo wa simu, tv, computer, n.k basi kuna wakati utafika sisi tutakaokuwa wazee tutayatazama maisha magumu sana ya watoto wetu.

Hii nimeanza kuiona jinsi ilivyoathiri hata masuala ya mapenzi kwa kuwateka dada zetu. Wale akina dada wanaofuatilia tamthiliya za kifilipino, za kihindi na kikorea, huwa wanaamini zile fantasy za mapenzi ndio maisha yenyewe. Wanaamini inabidi wakutane na vijana wa kiume mahandsome wenye sura laini wenye pesa zao kisha mapenzi yaende kwa mlolongo ule ule wanaouona kule.

Ndio maana hawa dada zetu walio wengi siku hizi kinachowakost ni kuwa mahusiano wanayoyatazamia kiuhalisia hawakutani nayo. Huishi wakiamini kuwa hawajampata mtu sahihi. Na akili inakuja kufunguka utu uzima ukishawafika.

Naamini wengi mna mengi ya kuongezea, kunirekebisha, kushauri au hata kuunga mkono.

Asanteni
 
Ukweli mchungu sana!

Kuanzia watoto mpaka dada zetu wanategemea wakiingia kwenye mahusiano au ndoa wakutane na mwanaume mcheshi, handsome, asiyejua kukasirika, hero na tajiri kama mwingizaji Fulani kwenye movie au tamthilia Fulani very romantic!

Mr. Right or Mr. Perfect so romantic indeed
 
Ukweli mchungu sana!

Kuanzia watoto mpaka dada zetu wanategemea wakiingia kwenye mahusiano au ndoa wakutane na mwanaume mcheshi, handsome, asiyejua kukasirika, hero na tajiri kama mwingizaji Fulani kwenye movie au tamthilia Fulani very romantic!

Mr. Right or Mr. Perfect so romantic indeed
Kila watakayekutana nae kwenye uhalisia watakuwa kaihisi kuna mambo hayajatimia
 
Naunga mkono hoja... suluhisho ni kupata watu wengi zaidi aina ya "ubungo kids" au katuni za Sarah mwanzoni mwa miaka ya 2000. Katuni hizi zina maudhui yanayoendana na mazingira yetu
Tatizo ndio hilo.. hata zikipatikana hatutaweza kushindana na soko la magharibi
 
Tuelewane sehem moja kila mtu aishi ulimwengu wake wewe unaona wanakosea na wao wnakuona wewe mshamba

Na huu ni mwanzo maana kizaz kinachokuja ni mwendo wa kutumia computer kweny kila kinachohusu maisha yako
 
Hakuna kinachoharibika , mtu Una miaka hamsini na wewe unajidai et mtu wa zamani haya walioishi miaka 200 before wao wasemeje ??? Au walioishi miaka 1000 before au BC,?? Kila kitu na zama zake , watu wanaishi kulingana na zama zao na huwez fanya reverse.....


Hata wewe watu wa walioishi miaka 400 nyuma wakiona lyfe lako watakushangaa na wewe pia utawaona washamba , kila kizazi kinajitune Tu kulingana na zama zake , wema wanakuwepo na wabaya wanakuwepo Maisha yanasonga mpak pale mshika Sheria yake atakapokuja .....

Huwa nakereka na mimimtu inayosema ooh kizazi cha sa hv , sjui ooh ni nini daah nitakujaga nizabe mtu kibao Mimi bas Tu ... Mtu mwenyewe ukute ana miaka 70 , sasa unajiuliza ina maana mfumo wa Maisha waliokuwa nao ulikuwa bora Sana, kama ulikuwa bora why watu wameshindwa kuumantain na wameamua kumove on , yeye mwenyewe amehama kwake ng'wang'omango na kwenda kuishi Kwa mwanae DSM .....
 
Hivi najiuliza, aliyetunga katuni za Kirikuu inamaana hakupata hela za kutosha kuendelea kutunga katuni nyingine Kama mfululizo wa katuni zake?

Au alipewa dau aache utunzi? Ili vizazi vyetu viendelee na umagharibi tangu wadogo?
Sababu beberu nae hakubali mtumwa wake ajitambue na ajikomboe ili aendelee kumkanyaga.
 
Hakuna kinachoharibika , mtu Una miaka hamsini na wewe unajidai et mtu wa zamani haya walioishi miaka 200 before wao wasemeje ??? Au walioishi miaka 1000 before au BC,?? Kila kitu na zama zake , watu wanaishi kulingana na zama zao na huwez fanya reverse.....


Hata wewe watu wa walioishi miaka 400 nyuma wakiona lyfe lako watakushangaa na wewe pia utawaona washamba , kila kizazi kinajitune Tu kulingana na zama zake , wema wanakuwepo na wabaya wanakuwepo Maisha yanasonga mpak pale mshika Sheria yake atakapokuja .....

Huwa nakereka na mimimtu inayosema ooh kizazi cha sa hv , sjui ooh ni nini daah nitakujaga nizabe mtu kibao Mimi bas Tu ... Mtu mwenyewe ukute ana miaka 70 , sasa unajiuliza ina maana mfumo wa Maisha waliokuwa nao ulikuwa bora Sana, kama ulikuwa bora why watu wameshindwa kuumantain na wameamua kumove on , yeye mwenyewe amehama kwake ng'wang'omango na kwenda kuishi Kwa mwanae DSM .....

Khaaaa...!!!

Nimeacha kukufananisha na dogo langu.
 
Hakuna kinachoharibika , mtu Una miaka hamsini na wewe unajidai et mtu wa zamani haya walioishi miaka 200 before wao wasemeje ??? Au walioishi miaka 1000 before au BC,?? Kila kitu na zama zake , watu wanaishi kulingana na zama zao na huwez fanya reverse.....


Hata wewe watu wa walioishi miaka 400 nyuma wakiona lyfe lako watakushangaa na wewe pia utawaona washamba , kila kizazi kinajitune Tu kulingana na zama zake , wema wanakuwepo na wabaya wanakuwepo Maisha yanasonga mpak pale mshika Sheria yake atakapokuja .....

Huwa nakereka na mimimtu inayosema ooh kizazi cha sa hv , sjui ooh ni nini daah nitakujaga nizabe mtu kibao Mimi bas Tu ... Mtu mwenyewe ukute ana miaka 70 , sasa unajiuliza ina maana mfumo wa Maisha waliokuwa nao ulikuwa bora Sana, kama ulikuwa bora why watu wameshindwa kuumantain na wameamua kumove on , yeye mwenyewe amehama kwake ng'wang'omango na kwenda kuishi Kwa mwanae DSM .....
Mkuu mbona jazba?
 
Hivi najiuliza, aliyetunga katuni za Kirikuu inamaana hakupata hela za kutosha kuendelea kutunga katuni nyingine Kama mfululizo wa katuni zake?

Au alipewa dau aache utunzi? Ili vizazi vyetu viendelee na umagharibi tangu wadogo?
Sababu beberu nae hakubali mtumwa wake ajitambue na ajikomboe ili aendelee kumkanyaga.
Katuni ile nayo sina imani nayo

Yaleyale.
 
Katuni ile nayo sina imani nayo

Yaleyale.

Angeweza kubadili maudhui ya uchawi na kuweka maudhui ya maisha ya mjini na vijijini. Namna ya kusaidia wazee, kujituma kijana, kujitegemea....

Eenheeeee umenipa akili, asante wazo limenijia. Acha niliandike.
 
Back
Top Bottom